Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 24

Unaweza Kufikia Miradi Yako ya Kiroho

Unaweza Kufikia Miradi Yako ya Kiroho

“Tusiache kufanya mema, kwa maana kwa wakati wenye kufaa tutavuna kama hatuchoke kabisa.”​—GAL. 6:9.

WIMBO 84 Niko Tayari Kusaidia!

KIFUPI YA HABARI a

1. Watu wengi walishindwa kufanya nini?

 ULISHAKAJIWEKEA muradi fulani wa kiroho, lakini unashindwa kuufikia? b Kama ni vile, ujue kama hauko weye peke. Kwa mufano, Philip alijiwekea muradi wa kufanya sala zake zikuwe muzuri zaidi na kukuwa nasali mara mingi. Lakini, ilikuwa nguvu kwake kupata wakati wa kusali. Erika alijiwekea muradi wa kufika mbele ku mikutano ya mahubiri; lakini, alikuwa tu anafika nyuma karibu ku kila mukutano. Tomáš, mwenye alijikaza kusoma Biblia yote, anasema hivi: “Sikukuwa tu napenda kusoma Biblia. Nilipima kuisoma mara tatu, lakini kila mara nilikuwa naishia tu ku kitabu ya Mambo ya Walawi.”

2. Juu ya nini haupaswe kuvunjika moyo kama haufikie muradi fulani wa kiroho?

2 Kama uko na muradi wenye ulijiwekea hivi karibuni, lakini hauyaufikia, tafazali, usivunjike moyo. Inaombaka wakati na bidii ili kufikia hata muradi wa mwepesi. Vile ungali unapenda kuufikia, ile inaonyesha kama unasamini uhusiano wako na Yehova na kama unapenda kumupatia jambo ya muzuri sana. Yehova anasamini bidii yako. Kusema kweli, hatazamie umupatie jambo yenye inapita uwezo wako. (Zb. 103:14; Mik. 6:8) Kwa hiyo, unapaswa kujiwekea muradi wenye unapatana na uwezo wako. Kisha kufanya vile, unaweza kufanya nini juu uufikie? Tuzungumuzie mapendekezo fulani.

INAOMBA KUWA NA HAMU

Umuombe yehova akupatie hamu zaidi (Ona fungu ya 3-4)

3. Juu ya nini inaomba kuwa na hamu?

3 Kama tuko na hamu, tunaweza kufikia miradi yetu ya kiroho. Mutu mwenye iko na hamu ao mwenye anapendaka sana muradi wake anajikazaka na anapendaka sana kuufikia. Hamu inaweza kulinganishwa na upepo wenye uko nasukuma mashua ili ifike kwenye iko naenda. Kama ule upepo unaendelea kuisukuma, kiongozi anaweza kufika kwenye iko naenda. Na kama upepo ni wa nguvu, anaweza hata kufika mbele ya wakati. Vilevile, kama tuko na hamu, tunaweza kufikia miradi yetu. Ndugu David, wa mu El Salvador, anasema hivi: “Kama uko na hamu, utajikaza sana. Hautaruhusu kitu yoyote ikuzuie kufikia muradi wako.” Sasa, unaweza kufanya nini ili ukuwe na hamu zaidi?

4. Tunaweza kumuomba Yehova nini? (Wafilipi 2:13) (Ona pia picha.)

4 Umuombe Yehova akupatie hamu zaidi. Kupitia roho yake takatifu, Yehova anaweza kukusaidia ili ufikie muradi wako. (Soma Wafilipi 2:13.) Wakati fulani, tunajiwekeaka muradi juu tunajua kama tunapaswa kufanya vile; na ni muzuri kufanya vile. Lakini, pengine tunaweza kukosa kabisa hamu ya kuufikia. Ile njo ilimufikiaka dada Norina wa mu Uganda. Alijiwekeaka muradi wa kuongoza funzo ya Biblia hata kama hakukuwa na hamu ya kuufikia juu aliwaza kama hakukuwa mwalimu muzuri. Nini njo ilimusaidia? Anasema hivi: “Kila siku nilianza kumuomba Yehova anisaidie nipende sana kuongoza funzo ya Biblia. Juu ya kutenda kulingana na sala zangu, nilijikaza kufanya ufundi wangu wa kufundisha ukuwe muzuri zaidi. Kisha miezi fulani, nilianza kupenda sana kuongoza funzo ya Biblia. Mu ule mwaka, nilianza kuongoza mafunzo ya Biblia mbili.”

5. Tunapaswa kufikiri sana juu ya mambo gani ili tukuwe na hamu zaidi ya kufikia muradi wetu?

5 Ufikiri sana juu ya mambo yenye Yehova alishakakufanyia. (Zb. 143:5) Mutume Paulo alifikiri sana juu ya fazili zenye hazistahiliwe zenye Yehova alimuonyesha, na ile ilimuchochea amutumikie sana. (1 Ko. 15:9, 10; 1 Ti. 1:12-14) Vilevile, kadiri unafikiri sana juu ya mambo yote yenye Yehova alishakakufanyia, ni vile utakuwa na hamu zaidi ya kufikia muradi wako. (Zb. 116:12) Ona mambo yenye ilimusaidia dada Honduras afikie muradi wake wa kuwa painia wa kawaida. Anasema hivi: “Nilifikiri sana juu ya namna Yehova ananipendaka. Alinisaidia nikuwe kati ya watu wake. Ananihangaikiaka na kunilinda. Kufikiri sana mu ile njia kulifanya nimupende sana Yehova na nipende sana kufikia muradi wangu.”   

6. Ni jambo gani ingine yenye inaweza kutusaidia tukuwe na hamu zaidi ya kufikia muradi wetu?

6 Ukaze akili juu ya baraka zenye utapata wakati unafikia muradi wako. Erika, mwenye tulishataya, alijiwekea muradi wa kufika mbele ku mikutano ya mahubiri. Ona mambo yenye ilimusaidia. Anasema hivi: “Nilifikia kuelewa kama juu nilikuwa nafika nyuma ku mikutano ya mahubiri, nilikuwa nakosa mambo mingi. Lakini, kufika mbele kungenisaidia nisalimie ndugu na dada zangu na nipitishe wakati pamoya nao. Ningekuwa pia na nafasi ya kusikiliza mapendekezo yenye ingenisaidia nifurahie mahubiri na kufanya namna yangu ya kuhubiri ikuwe muzuri zaidi.” Erika alikaza akili juu ya baraka zenye angepata kama anafika mbele ku mikutano ya mahubiri, na ile njo ilimusaidia afikie muradi wake. Unapaswa kukaza akili juu ya baraka gani? Kama muradi wako ni wa kusoma Biblia ao kusali, fikiria namna ile inaweza kufanya urafiki wako na Yehova ukuwe nguvu zaidi. (Zb. 145:18, 19) Kama muradi wako ni wa kukomalisha sifa fulani ya kiroho, kaza akili juu ya namna ile itafanya uhusiano wako na wengine ukuwe muzuri zaidi. (Kol. 3:14) Unawaza nini kama unafanya liste ya sababu zenye zinafanya upende kufikia muradi wako? Kila mara ukuwe nachunguza ile liste. Tomáš, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Wakati nafikiria sababu zenye zinafanya nipende sana kufikia muradi fulani, najikazaka sana ili niufikie.”

7. Nini njo ilisaidia Julio na bibi yake wafikie muradi wao?

7 Upitishe wakati pamoya na wale wenye watakuchochea kufikia muradi wako. (Mez. 13:20) Ona mambo yenye ilisaidia Julio na bibi yake wafikie muradi wa kupanua utumishi wao. Julio anasema hivi: “Tulichagua marafiki wenye walitutia moyo ili tufikie muradi wetu, na tulikuwa nazungumuza nao juu ya ule muradi. Wengi kati yao walikuwa walishafikia miradi sawa ile. Kwa hiyo, walitupatia mapendekezo yenye ilitusaidia. Walikuwa pia natuuliza kwenye miradi yetu inafikia na kututia moyo wakati ni lazima.”

WAKATI HATUNA HAMU

Ujikaze kufikia muradi wako (Ona fungu ya 8)

8. Nini inaweza kutokea kama tunajikaza kufikia muradi wetu wakati tu tuko na hamu ya kufanya vile? (Ona pia picha.)

8 Lakini, kusema kweli, wakati fulani inawezekana tusikuwe na hamu ya kufikia muradi wetu. Ile inamaanisha kama hatupaswe kuendelea kujikaza? Hapana. Kwa mufano: Upepo wa nguvu unaweza kusukuma mashua iende. Lakini, wakati fulani upepo unakuwaka wa nguvu na wakati ingine hapana, na kuko wakati wenye haukuwake tu. Je, ile inaweza kufanya kiongozi wa mashua asiendelee na safari yake? Hapana. Kwa mufano, mashua fulani zinatembezwaka na motere na zingine zinatembezwaka na makasia. Kiongozi wa mashua anaweza kutumia motere ao makasia juu mashua yake iende. Hamu iko sawa vile upepo, wakati fulani, tunaweza kuwa na hamu sana na wakati ingine hapana. Wakati fulani tunaweza kukosa kabisa hamu ya kufikia muradi wetu. Kwa hiyo, kama tuko najikaza kufikia muradi wetu juu tu tuko na hamu, pengine hatutaufikiaka. Lakini, sawa vile tu kiongozi wa mashua anatafutaka njia zingine juu afike kwenye iko naenda, tunaweza pia kujikaza kufikia muradi wetu hata kama hatuna hamu ya kufanya vile. Kusema kweli, haiko mwepesi; lakini kama tunaufikia, tutakuwa na furaha. Mbele tuzungumuzie mambo yenye tunaweza kufanya, tuone kwanza ulizo yenye tunaweza kujiuliza.

9. Ni mubaya kujikaza kufikia muradi hata kama hatuna hamu ya kufanya vile? Fasiria.

9 Yehova anapenda tumutumikie kwa furaha na kwa kupenda. (Zb. 100:2; 2 Ko. 9:7) Sasa, tunapaswa kujikaza kufikia muradi wetu hata kama hatujisikie kufanya vile? Fikiria mufano wa mutume Paulo. Alisema hivi: “Ninapiga-piga mwili wangu na kuuongoza kama mutumwa.” (1 Ko. 9:25-27) Hata kama wakati fulani Paulo hakukuwa na hamu ya kufanya mambo yenye Yehova alimuomba, alijikaza kuifanya. Yehova alikubali utumishi wake? Ndiyo! Na alimupatia zawabu juu ya bidii yake.​—2 Ti. 4:7, 8.

10. Tutapata nini kama tunajikaza kufikia muradi wetu hata kama hatuna hamu ya kufanya vile?

10 Vilevile, Yehova anafurahiaka wakati tunajikaza kufikia muradi wetu hata kama hatuna hamu ya kufanya vile. Juu anajua kama kila mara hatufanyake mambo fulani juu tunaipenda, anafurahiaka wakati anaona tunaifanya juu tunamupenda. Sawa vile tu alimubariki Paulo, atatubariki pia juu ya bidii yetu. (Zb. 126:5) Na wakati tunaona namna Yehova iko natubariki, ile inaweza kufanya tuanze hata kupenda sana kufikia miradi yetu. Dada Lucyna wa mu Pologne anasema hivi: “Wakati fulani, sipendake kuenda mu mahubiri, zaidi sana kama nilishachoka. Lakini, nakuwaka na furaha sana kisha kuhubiri.” Tuzungumuzie basi mambo yenye tunaweza kufanya kama hatuna hamu ya kufikia miradi yetu.

11. Tunaweza kufanya nini juu Yehova atusaidie kukomalisha sifa ya kujizuia?

11 Umuombe Yehova akupatie sifa ya kujizuia. Mutu mwenye kuwa na sifa ya kujizuia anakuwaka na uwezo wa kuongoza hisia na matendo yake. Mara mingi, ile sifa inaletaka wazo ya kuepuka kufanya mambo ya mubaya yenye moyo wa mutu unapenda afanye. Lakini, inaomba pia kuwa na ile sifa ili kufanya mambo ya muzuri, zaidi sana kama kazi yenye tutafanya ni ya nguvu ao kama hatuna hamu ya kuifanya. Tusisahau kama kujizuia ni sifa ya maana na ni sehemu ya tunda ya roho. Kwa hiyo, umuombe Yehova akupatie roho yake takatifu ili uikomalishe. (Lu. 11:13; Gal. 5:22, 23) David, mwenye tulishataya, alionyesha namna sala ilimusaidia. Alipenda kufanya funzo yake ya pekee kwa ukawaida. Anasema hivi: “Nilikuwa namuomba Yehova anisaidie nikomalishe sifa ya kujizuia. Kwa musaada wake, nilianza kuwa na proramu ya muzuri ya funzo na niliiheshimia.”

12. Kanuni yenye kuwa mu Muhubiri 11:4 inahusiana namna gani na miradi ya kiroho?

12 Usichunge mupaka hali ikuwe muzuri sana. Mu hii dunia, pengine ile haitawezekana. Kwa hiyo, kama tuko nachunga hali ikuwe muzuri sana, pengine hatutawezaka kufikia miradi yetu. (Soma Muhubiri 11:4.) Ndugu Dayniel anasema hivi: “Haiwezekane hata kidogo hali ikuwe muzuri sana. Kwa hiyo, hatupaswe kuchunga, inaomba tu kuanza.” Ndugu Paul wa mu Uganda anaonyesha sababu ingine yenye inapaswa kutuchochea tusicheleweshe mambo; anasema hivi: “Wakati tunaanza kufanya jambo fulani ijapokuwa hali ya nguvu, tunamupatia Yehova jambo fulani yenye itafanya atubariki.”​—Mal. 3:10.

13. Juu ya nini ni muzuri kuanza na miradi ya kidogo-kidogo?

13 Uanze na miradi ya kidogo-kidogo. Wakati fulani, tunaweza kukosa hamu ya kufikia muradi kama unaonekana sawa vile ni wa nguvu sana. Kama ile njo hali yako, unawaza nini kama unagawanya ule muradi mu sehemu kidogo-kidogo? Kama muradi wako ni wa kukomalisha sifa fulani, hauone kama ni muzuri uionyeshe mu njia za kidogo-kidogo? Na kama muradi wako ni wa kusoma Biblia yote, unawaza namna gani kama unapanga kuisoma mu wakati kidogo-kidogo? Tomáš, mwenye tulishataya, alikuwa anashindwa kufikia muradi wake wa kusoma Biblia yote mu mwaka moya. Anasema hivi: “Nilitambua kama nilikuwa naisoma mu mwendo wa haraka sana. Kwa hiyo, niliamua kupima tena. Lakini, mara hiyo, nilipanga kusoma mistari fulani ya sura kila siku na kuitafakari. Ile ilifanya nianze kupenda kusoma.” Juu Tomáš’ alianza kupenda kusoma Biblia, alianza kuisoma kwa wakati murefu zaidi. Ku mwisho, alisoma Biblia yote. c

USIVUNJIKE MOYO KAMA UNAKUTANA NA VIZUIZI

14. Tunaweza kukutana na vizuizi gani?

14 Jambo ya kuhuzunisha, hata tukuwe na hamu namna gani ao tujikaze namna gani tunaweza tu kukutana na vizuizi. Kwa mufano, “matukio yenye hayatazamiwe” inaweza kutukulia wakati wenye tungetumia ili kufikia muradi wetu. (Muh. 9:11) Tunaweza kupata magumu yenye inaweza kutuvunja moyo na kupuguza nguvu yetu. (Mez. 24:10) Juu hatukamilike, tunaweza kufanya makosa yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu sana kwetu kufikia muradi wetu. (Ro. 7:23) Ao tunaweza tu kuchoka. (Mt. 26:43) Tunaweza kufanya nini ili tupambane na vizuizi?

15. Kama tunakutana na kizuizi, ile inaonyesha kama tumeshindwa? Fasiria. (Zaburi 145:14)

15 Kama unakutana na kizuizi, ile haionyeshe kama umeshindwa. Biblia inasema kama tunaweza kupata magumu tena na tena. Lakini, inaonyesha pia wazi kama tunaweza tena kufikia muradi wetu, zaidi sana kama Yehova anatusaidia. (Soma Zaburi 145:14.) Ndugu Philip, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Hata kama nashindwa mara ngapi, sikazake akili juu ya ile, lakini najikazaka kujua ni mara ngapi nilishajikaza ili kufikia tena ule muradi.” David, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Najikazaka kuona vizuizi kuwa nafasi ya kumuonyesha Yehova kama namupenda sana.” Kama unaendelea kujikaza kufikia muradi wako hata kama ni nguvu kufanya vile, unamuonyesha Yehova kama unapenda kumufurahisha. Wazia namna Yehova atafurahi wakati anaona tuko naendelea kujikaza kufikia muradi wetu!

16. Unaweza kufanya nini kama unakutana na kizuizi?

16 Ujifunze mambo fulani kupitia kizuizi yenye unakutana nayo. Unaweza kufikiria mambo yenye ilifanya ile kizuizi itokee na kisha ujiulize hivi: ‘Naweza kufanya nini juu ile isitokee tena?’ (Mez. 27:12) Lakini wakati fulani, kama uko nashindwa kufikia muradi fulani, pengine ni juu haupatane na uwezo wako. Kama ni vile, uufikirie tena ili kuona kama unaweza kuufikia. d Kama haufikie muradi wenye haupatane na uwezo wako, usiwaze kama Yehova ataona kuwa unashindwa.​—2 Ko. 8:12.

17. Juu ya nini haupaswe kusahau miradi yenye ulishakafikia?

17 Usisahau miradi yenye ulishakafikia. Biblia inasema kama “Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu.” (Ebr. 6:10) Na weye usisahau miradi yenye ulishakafikia, sawa vile kukomalisha urafiki wako pamoya na Yehova, kuambia wengine juu yake, ao kubatizwa. Sawa vile tu ulijikazaka kufikia miradi yako ya kiroho zamani, unaweza pia kujikaza kufikia miradi yako ya sasa.​—Flp. 3:16.

Ujikaze kuona namna yehova iko nakusaidia wakati uko najikaza kufikia miradi yako (Ona fungu ya 18)

18. Unapaswa kukumbuka nini wakati uko najikaza kufikia muradi wako? (Ona pia picha.)

18 Kwa musaada wa Yehova, unaweza kuwa na furaha ya kufikia muradi wako sawa vile tu viongozi wengi wa mashua wanakuwaka na furaha wakati wanafika kwenye wako naenda. Vilevile, kila mara ujikaze kuona namna Yehova iko nakusaidia, na ile itafanya ukuwe na furaha wakati uko najikaza kufikia miradi yako. (2 Ko. 4:7) Kama hauvunjike moyo, utapata baraka mingi hata zaidi.​—Gal. 6:9.

WIMBO 126 Ukuwe Macho, Usimame Imara, Ukuwe na Nguvu

a Mara mingi, tengenezo ya Yehova inatutiaka moyo tujiwekee miradi ya kiroho. Sasa, tunaweza kufanya nini kama tulishajiwekea muradi fulani wa kiroho, lakini tunashindwa kuufikia? Hii habari itazungumuzia mapendekezo mbalimbali juu ya namna tunaweza kufikia miradi yetu.

b MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Muradi wa kiroho ni jambo yoyote yenye tunaweza kufanya ili tumutumikie Yehova kwa ukamili na kumufurahisha. Kwa mufano, unaweza kujiwekea muradi wa kukomalisha sifa fulani ya Kikristo ao kufanya jambo fulani ili umuabudu Yehova muzuri zaidi, sawa vile kusoma Biblia, kufanya funzo ya pekee, ao kuhubiri.

c Ona kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, uku. 10-11, fu. 4.

d Juu ya kupata habari zaidi, soma habari “Uwe na Matarajio Yenye Usawaziko, na Uwe Mwenye Shangwe,” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2008.