Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 21

WIMBO 107 Tuonyeshe Upendo Kama Mungu

Namna ya Kupata Mutu Mwenye Anaweza Kuwa Bibi ao Bwana Muzuri

Namna ya Kupata Mutu Mwenye Anaweza Kuwa Bibi ao Bwana Muzuri

“Ni nani anaweza kupata bibi mwenye uwezo? Samani yake inapita sana samani ya marijani.”MEZ. 31:10.

WAZO KUBWA

Kanuni za Biblia zenye zinaweza kusaidia Mukristo apate mutu mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri na namna wengine mu kutaniko wanaweza kutegemeza Mukristo mwenye angependa kufunga ndoa.

1-2. (a) Mukristo mwenye hayaoa ao kuolewa anapaswa kufikiria nini mbele ya kuanzisha urafiki wa kimapenzi? (b) “Urafiki wa kimapenzi” maana yake nini? (Ona “Mafasirio ya Maneno Fulani.”)

 UNAPENDA kuoa ao kuolewa? Hata kama haiombe mutu afunge ndoa juu akuwe na furaha, Wakristo wengi wenye hawayafunga ndoa, ikuwe ni watu wazima ao vijana, wanatazamia kupata mutu mwenye wanaweza kufunga naye ndoa. Lakini mbele ya kuanzisha urafiki wa kimapenzi unapaswa kuwa na hali ya muzuri ya kiroho, unapaswa kujijua muzuri, na unapaswa kuwa na uwezo wa kutimiza mahitaji ya kimwili ya familia yako. a (1 Ko. 7:36) Kama unatimiza ile mambo, inawezekana ukuwe na ndoa yenye furaha.

2 Lakini haikuwake mwepesi kupata bibi ao bwana muzuri. (Mez. 31:10) Na hata kama unapata mutu mwenye ungependa kujua muzuri zaidi, inaweza kuwa nguvu kuanzisha naye urafiki wa kimapenzi. b Mu hii habari, tutazungumuzia mambo yenye inaweza kusaidia Wakristo wenye hawayafunga ndoa wapate mutu mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri na waanzishe urafiki wa kimapenzi. Tutaona pia namna wengine mu kutaniko wanaweza kutegemeza wale wenye wanapenda kuoa ao kuolewa.

KUPATA MUTU MWENYE ANAWEZA KUWA BIBI AO BWANA MUZURI

3. Mukristo mwenye hayafunga ndoa anapaswa kufikiria nini wakati iko natafuta mutu mwenye atakuwa bibi ao bwana yake?

3 Kama unapenda kuoa ao kuolewa, mbele ya kuanzisha urafiki wa kimapenzi ni muzuri ujue ni bibi ao bwana wa namna gani njo uko natafuta. Kama haufanye vile unaweza kuacha mutu mwenye anaweza kuwa bibi oa bwana muzuri kwako, na kuanzisha urafiki wa kimapenzi na mutu mwenye hakufae. Kwa kweli, mutu mwenye tunapenda akuwe bibi ao bwana yetu anapaswa kuwa Mukristo mwenye kubatizwa. (1 Ko. 7:39) Lakini haiko kila Mukristo mwenye kubatizwa njo anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri kwako. Kwa hiyo ujiulize hivi: ‘Niko na miradi gani mu maisha? Na naweza kupenda bibi ao bwana yangu akuwe na sifa gani? Niko mwenye usawaziko wakati ninafikiria namna bibi ao bwana yangu anapaswa kuwa?’

4. Wakristo fulani wanaambiaka Yehova nini mu sala?

4 Kama unapenda kuoa ao kuolewa, ni wazi kama umesali juu ya ile jambo. (Flp. 4:6) Kusema kweli Yehova haahidi mutu yeyote kama atamupatia bibi ao bwana. Lakini anahangaikia mahitaji yako na namna uko najisikia, na anaweza kukusaidia wakati uko natafuta mutu mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri. Kwa hiyo uendelee kumuambia namna uko najisikia na mambo yenye unapenda. (Zb. 62:8) Umuombe akusaidie ukuwe muvumilivu na ukuwe na hekima. (Yak. 1:5) Ndugu John, c mwenye hayaoa wa mu inchi ya Amerika, anaeleza mambo yenye anaambiaka Yehova mu sala. Anasema hivi: “Namuambiaka Yehova sifa zenye ninapenda bibi yangu akuwe nazo, ninasali juu nipate nafasi za kukutana na mutu mwenye anaweza kuwa bibi yangu. Namuomba Yehova anisaidie nikomalishe sifa zenye zitanisaidia nikuwe bwana muzuri.” Tanya, dada wa Sri Lanka, anasema hivi: “Wakati niko natafuta mutu mwenye anaweza kuwa bwana yangu namuomba Yehova anisaidie niendelee kuwa muaminifu, niendelee kuwa na mawazo yenye kufaa, na niendelee kuwa na furaha.” Hata kama haupate mutu mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana yako kwa sasa, Yehova anaahidi kama ataendelea kuhangaikia mahitaji yako ya kimwili na kukusaidia ujisikie kuwa unapendwa na kuhangaikiwa.—Zb. 55:22.

5. Wakristo wenye hawayafunga ndoa wako na nafasi gani za kukutana na mutu mwenye anamupenda Yehova? (1 Wakorinto 15:58) (Ona pia picha.)

5 Biblia inatutia moyo tukuwe na “mambo mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.” (Soma 1 Wakorinto 15:58.) Kama unaendelea kuwa na mambo mengi ya kufanya mu kazi ya Yehova na kupitisha wakati na ndugu na dada tofauti-tofauti utatiwa moyo. Lakini pia utapata nafasi ya kukutana na ndugu na dada wenye hawayafunga ndoa kama weye, na wenye wako pia naweka utumishi wao kwa Yehova pa nafasi ya kwanza. Na wakati uko nafanya yako yote ili kumufurahisha Yehova, utapata furaha ya kweli.

Kama unaendelea kuwa na mambo mengi ya kufanya mu kazi ya Yehova na kupitisha wakati na Wakristo tofauti-tofauti unaweza kukutana na wengine wenye wanapenda pia kufunga ndoa (Ona fungu ya 5)


6. Wakati Wakristo wenye hawayafunga ndoa wako natafuta bibi ao bwana, wanapaswa kukumbuka nini?

6 Lakini ukuwe muangalifu: Usiache muradi wako wa kutafuta bibi ao bwana ikuwe jambo ya maana zaidi mu maisha yako. (Flp. 1:10) Haiko kufunga ndoa ao kubakia bila kufunga ndoa njo kunaletaka furaha ya kweli. Furaha ya kweli inategemea uhusiano wako pamoya na Yehova. (Mt. 5:3) Na wakati hauyaoa ao kuolewa, unaweza kuwa na uhuru zaidi wa kupanua utumishi wako. (1 Ko. 7:32, 33) Tumia muzuri hii wakati yenye uko nayo. Jessica, dada wa Amerika mwenye aliolewa na iko na miaka karibu 40, anasema hivi: “Niliendelea kuwa na bidii mu utumishi wangu na ile ilinisaidia nitosheke na hali yangu hata kama nilikuwa napenda kuolewa.”

KAMATA WAKATI WA KUMUJUA MUZURI

7. Juu ya nini ni jambo ya hekima kukamata wakati wa kujua mutu muzuri mbele ya kumuambia kama unamufarahia? (Mezali 13:16)

7 Utafanya nini kama unaona kuwa ndugu ao dada fulani anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri kwako? Unapaswa kumuambia mara moja kama unamufurahia? Biblia inasema kama mutu mwenye hekima anatafuta ujuzi mbele ya kutenda. (Soma Mezali 13:16.) Kwa hiyo ni jambo ya hekima utafute kujua ule mutu muzuri zaidi kwa wakati fulani mbele ya kumuambia kama unamufurahia, lakini ufanye vile bila yeye kujua. Aschwin ndugu wa mu inchi ya Hollande anasema hivi: “Hisia za mapenzi zinakuyaka haraka sana na zinaweza pia kuisha haraka sana. Kwa hiyo kama unakamata wakati wa kujua mutu muzuri hautaanzisha urafiki wa kimapenzi kwa kutegemea tu namna unajisikia ile wakati.” Zaidi ya ile kama unakamata wakati wa kujua mutu muzuri unaweza kutambua kama hatakuwa bibi ao bwana muzuri kwako.

8. Namna gani Mukristo mwenye hayafunga ndoa anaweza kuchunguza mutu mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana yake? (Ona pia picha.)

8 Ku mikutano ya Kikristo ao wakati munakutana na ndugu na dada ili kujifurahisha, unaweza kutambua mambo fulani juu ya hali ya kiroho ya ule mutu, utu wake, na mwenendo wake. Marafiki wake ni nani? Anaongeaka kuhusu mambo gani? (Lu. 6:45) Miradi yake inapatana na miradi yako? Unaweza kuzungumuza na wazee wa mu kutaniko yake ao na Wakristo wenye kukomaa kiroho wenye wanamujua muzuri. (Mez. 20:18) Unaweza kuuliza kuhusu sifa zake na namna yake ya kuwa. (Rut. 2:11) Wakati uko nachunguza ule ndugu ao dada, usifanye ajisikie mubaya, usijiingize mu mambo yake ya kipekee, na usimufuate-fuate fasi yote.

Mbele ya kuambia mutu kama unamupenda umuchunguze kwa wakati fulani bila kumuambia kitu (Ona fungu ya 7-8)


9. Mbele ya kuambia ndugu ao dada kama unamufarahia unapaswa kuwa hakika na mambo gani?

9 Unapaswa kuchunguza mutu kwa muda gani mbele ya kumuambia kama unamufurahia? Kama mwanzo-mwanzo tu unaambia mutu kama unamufurahia anaweza kuwaza kama unakamataka maamuzi bila kufikiri kwa uangalifu. (Mez. 29:20) Lakini kama unakamata tena wakati murefu sana mbele ya kumuambia, ule mutu anaweza kuona kama uko mutu wa kusita-sita, zaidi sana kama alitambua kuwa unapendezwa naye. (Muh. 11:4) Kumbuka kama mbele ya kuzungumuza na mutu haiko lazima ukuwe hakika kabisa kama mutaoana. Lakini unapaswa kuwa hakika kama uko tayari kwa ajili ya ndoa, na kama ule mutu anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri kwako.

10. Unapaswa kufanya nini ikiwa unatambua kuwa Mukristo fulani anapendezwa na weye lakini weye haupendezwe naye?

10 Sasa utafanya nini kama unatambua kuwa mutu fulani anapendezwa na weye? Kama weye haupendezwe naye uonyeshe vile waziwazi kupitia matendo yako. Haiko muzuri kufanya mutu awaze kama inawezekana muanzishe uhusiano fulani, lakini weye hauwaze vile.—1 Ko. 10:24; Efe. 4:25.

11. Mu inchi zenye watu wa familia ao marafiki njo wanatafutianaka mutu wa kuoana naye, ni mambo gani njo wanapaswa kufikiria?

11 Mu inchi fulani ni wazazi ao watu wazima njo wanachagulia watu wa mu familia yao mutu wa kuoana naye. Mu inchi zingine watu wa familia ao marafiki njo wanatafutia mutu mwenye hayafungu ndoa Mukristo mwenye anaweza kuoana naye, na kisha wanakamata mipango juu ule mwanaume na ule mwanamuke wakutane ili waone ikiwa wanapatana. Ikiwa wanakuomba ukutanishe ndugu na dada ili waanzishe urafiki wa kimapenzi ao ili waoane, fikiria ikiwa ule ndugu iko natafuta dada wa namna gani na ule dada iko natafuta ndugu wa namna gani, na wote wawili wako na lazima ya nini. Kwa mufano ikiwa ndugu njo uko natafutia dada mwenye anaweza kuwa bibi muzuri kwake, wakati utapata ule dada tafuta kujua utu wake, sifa zake, na zaidi sana hali yake ya kiroho. Na kama ni dada njo uko natafutia, ufanye vilevile. Urafiki pamoya na Yehova njo jambo ya maana zaidi kuliko makuta, masomo yenye mutu alisoma, ao hali ya mutu ya maisha. Lakini, kumbuka kama ule ndugu na ule dada njo wanapaswa kukamata uamuzi wa mwisho, ikiwa wataoana ao hapana.—Gal. 6:5.

KUANZISHA URAFIKI WA KIMAPENZI

12. Kama unapenda kuanzisha urafiki wa kimapenzi na mutu fulani unaweza kumuambia namna gani?

12 Kama unapenda kuanzisha urafiki wa kimapenzi pamoya na mutu fulani, unapaswa kumuambia namna gani kama unamufurahia? d Unaweza kufanya mipango ili kuzungumuza na ule mutu fasi kwenye kuwa watu wengi ao ku telefone. Sema waziwazi nia yako. (1 Ko. 14:9) Kama ni lazima, patia ule mutu wakati wa kufikiri mbele akujibie. (Mez. 15:28) Kama mutu hapendi kuanzisha urafiki wa kimapenzi uheshimie uamuzi wake.

13. Unaweza kufanya nini kama mutu fulani anakuambia kama anapendezwa na weye? (Wakolosai 4:6)

13 Sasa utafanya nini kama mutu anakuambia kuwa anapendezwa na weye? Inawezekana iliomba ule mutu ajikaze sana juu azungumuze na weye. Kwa hiyo, umujibie kwa upole na kwa heshima. (Soma Wakolosai 4:6.) Kama uko na lazima ya wakati ya kuwaza juu ya kuamua ikiwa utaanza urafiki wa kimapenzi ao hapana, umuambie. Lakini usikawie sana mbele ya kumujibia. (Mez. 13:12) Kama haupendi kuanzisha urafiki wa kimapenzi, umuambie kwa upole na waziwazi. Ona vile Hans, ndugu wa Austria alifanya wakati dada fulani alimuambia kama anapendezwa naye: “Nilimuambia uamuzi wangu kwa upole lakini waziwazi. Nilimujibia palepale juu sikupenda akuwe na tumaini kama kunaweza kuwa jambo fulani kati yetu. Na kuanzia pale nilikuwa muangalifu juu nisiseme ao kufanya mambo yenye inaweza kufanya afikiri kama nimebadilisha uamuzi wangu.” Lakini, kama na weye unapenda kuanzisha urafiki wa kimapenzi na ule mutu, umuambie waziwazi namna unajisikia na mambo yenye unatazamia kwake. Mambo yenye kila mutu anatazamia kwa mwenzake inaweza kuwa tofauti, kwa sababu ya desturi ao mambo ingine.

NAMNA GANI WENGINE WANAWEZA KUTEGEMEZA WAKRISTO WENYE HAWAYAOA AO KUOLEWA?

14. Namna gani tunaweza kutegemeza kupitia maneno yetu Wakristo wenye hawayafunga ndoa?

14 Namna gani tunaweza kutegemeza Wakristo wenye wanapenda kufunga ndoa? Njia moya ya kufanya vile ni kuwa waangalifu juu ya mambo yenye tunasema. (Efe. 4:29) Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nafanyaka mizaha yenye inaweza kuumiza wenye wanapenda kufunga ndoa? Wakati ninaona ndugu mwenye hayaoa na dada mwenye hayaolewa wako nazungumuza, nawazaka kama wanapendana?’ (1 Ti. 5:13) Hatupaswe kufanya ndugu ao dada ajisikie kuwa anakosa jambo fulani juu tu hayaoa ao kuolewa. Hans, mwenye tulishazungumuzia anasema hivi: “Ndugu fulani wanasemaka ‘Juu ya nini hauyafunga ndoa? Hauko tena kijana.’ Maneno ya vile inafanyaka Mukristo mwenye hayafunga ndoa ajisikie kuwa haiko wa maana na inaweza kuwa sawa vile tuko namukaza aoe ao aolewe.” Inaweza kuwa muzuri kama tunatafuta nafasi ya kupongeza ndugu na dada wenye hawayafunga ndoa!—1 Te. 5:11.

15. (a) Kulingana na Waroma 15:2, tunapaswa kufikiria nini mbele ya kusaidia mutu apate mutu mwenye anaweza kufunga naye ndoa? (Ona pia picha.) (b) Ni mambo gani ulifurahia mu video?

15 Sasa tutafanya nini kama tunawaza kama inaweza kuwa muzuri ndugu na dada fulani waoane? Biblia inatuambia tufikirie mawazo ya wengine. (Soma Waroma 15:2.) Wakristo wengi wenye hawayafunga ndoa hawapendake wengine wawapendekeze kwa ndugu ao dada fulani mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana yao, na tunapaswa kuheshimia uamuzi wao. (2 Te. 3:11) Wengine wanaweza kufurahi kama tunawasaidia, lakini hatupaswe kufanya vile kama hawatuombe tuwasaidie. e (Mez. 3:27) Wamoja wanapendelea tufanye vile kwa njia yenye haiko ya waziwazi. Lydia, dada mwenye hayaolewa wa mu inchi ya Alemanye anasema hivi: “Unaweza kualika ule ndugu na ule dada mu kikundi ya watu wengi na kufanya mipango ili ule ndugu na ule dada wakutane na uwaache waamue juu ya jambo yenye watafanya kisha pale.”

Wakristo wenye hawayafunga ndoa wanaweza kupata nafasi ya kukutana na Wakristo wengine wenye hawayafunga ndoa mu kikundi ya watu wengi (Ona fungu ya 15)


16. Wakristo wenye hawayafunga ndoa wanapaswa kukumbuka nini?

16 Ikuwe tulishafunga ndoa ao hapana tunaweza kuwa na maisha ya muzuri na yenye furaha! (Zb. 128:1) Kwa hiyo, kama unapenda kufunga ndoa lakini hauyapata mutu, uendelee kukazia akili utumishi wako kwa Yehova. Dada Sin Yi wa mu inchi ya Macao anasema hivi: “Wakati wenye unapitisha weye peke bila kuwa na bibi ao bwana, haiko kitu ukiilinganisha na wakati murefu wenye utapitisha na bibi ao bwana yako mu Paradiso. Furahia hii wakati yenye uko nayo leo, na uitumie muzuri.” Sasa itakuwa namna gani kama ulishapata Mukristo mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri kwako na mulishaanzisha urafiki wa kimapenzi? Mu habari yenye kufuata tutazungumuzia mambo yenye munaweza kufanya ili kipindi ya urafiki wa kimapenzi iwasaidie kukamata maamuzi ya muzuri.

WIMBO 137 Wanamuke Wenye Imani

b MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mu hii habari maneno kuanzisha “urafiki wa kimapenzi” inamaanisha kipindi yenye mwanaume na mwanamuke wanachukua ili kujuana muzuri juu ya kuamua ikiwa wanaweza kuoana. Mu inchi fulani, wanaitaka ile kipindi kuchumbiana ao kipindi ya kujuana muzuri. Urafiki wa kimapenzi unaanza wakati mwanaume na mwanamuke wanakubaliana waziwazi kama wanapendana na unaendelea mupaka wakati wanaamua ikiwa wataoana ao kuvunja urafiki wao.

c Majina fulani imebadilishwa.

d Mu desturi fulani, kwa ukawaida ndugu njo anaombaka dada waanzishe urafiki wa kimapenzi, lakini dada anaweza kuamua kuzungumuza na ndugu juu ya kumuomba waanzishe urafiki wa kimapenzi. (Rut. 3:1-13) Ili kupata habari zaidi ona habari “Vijana Huuliza . . . Nitamwambiaje Jinsi Ninavyohisi?” mu Amuka! ya tarehe 22, Mwezi wa 10, 2004.