Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 28

Faida ya Kuendelea Kumuogopa Mungu

Faida ya Kuendelea Kumuogopa Mungu

“Mutu mwenye kutembea katika unyoofu wake anamuogopa Yehova.”​—MEZ. 14:2.

WIMBO 122 Tukuwe na Nguvu na Tusitikisike!

KIFUPI YA HABARI a

1-2. Namna gani hali yetu inafanana na hali ya Loti?

 TUKO najisikia sawa vile Loti wakati tunaona mwenendo mubaya wa watu leo. “Alihuzunishwa sana na mwenendo mupotovu wa bila haya wa watu wenye kuvunja sheria” juu alijua kama Baba yetu wa mbinguni anachukia mwenendo mubaya. (2 Pe. 2:7, 8) Juu alimuogopa Mungu na kumupenda, Loti alichukia mwenendo mubaya wa watu wenye aliishi nao. Siye pia, tuko naishi na watu wenye kuwa na mwenendo mubaya. Hata vile, tunaweza kuendelea kuwa na mwenendo safi kama tunamupenda Mungu na kumuogopa mu njia yenye kufaa.​—Mez. 14:2.

2 Yehova anatusaidia kufanya vile kupitia kitia-moyo yenye tunapata mu kitabu ya Mezali. Wakristo wote, ni kusema, wanaume na wanamuke, vijana na wazee, wanaweza kabisa kupata faida kwa kuchunguza mashauri ya hekima yenye kuwa mu ile kitabu.

KUMUOGOPA MUNGU KUNATULINDA

Wakati tuko ku kazi, tunapaswa kuepuka marafiki wabaya na kuepuka kufanya mambo yenye inaweza kumuhuzunisha Yehova (Ona fungu ya 3)

3. Kulingana na Mezali 17:3, ni sababu gani kubwa yenye inapaswa kutuchochea kulinda moyo wetu? (Ona pia picha.)

3 Sababu kubwa yenye inapaswa kutuchochea kulinda moyo wetu wa mufano ni juu Yehova anauchunguzaka, ni kusema, haangaliake tu vile tunaonekana kwa inje, lakini anaangaliaka vile tuko kabisa kwa ndani. (Soma Mezali 17:3.) Atatupenda kama tunaendelea kufikiria mashauri yake yenye inaweza kutusaidia kuishi milele. (Yoh. 4:14) Kama tunafanya vile, hatutaacha mwenendo mubaya wa watu wa mu hii dunia na uongo wa Shetani na wa watu wake ituharibishe. (1 Yo. 5:18, 19) Kadiri tunamukaribia Yehova zaidi ni vile tutamupenda na kumuheshimia sana. Juu hatupendi kumuhuzunisha Baba yetu, tutachukia hata kukuwa na mawazo ya kufanya zambi. Wakati tunajaribiwa kufanya jambo ya mubaya, tutajiuliza hivi, ‘Namna gani naweza kumuhuzunisha kimakusudi Yehova mwenye ananipendaka sana?’​—1 Yo. 4:9, 10.

4. Namna gani kumuogopa Yehova kulilinda dada moya?

4 Marta, dada wa mu Kroasia mwenye alijaribiwa kufanya uasherati, anasema hivi: “Ilikuwa nguvu kwangu kukamata uamuzi wa muzuri na kupiganisha tamaa ya kufanya jambo ya mubaya. Lakini kumuogopa Yehova kulinilinda.” b Namna gani? Marta alisema kama alifikiri sana juu ya matokeo yenye uamuzi wa mubaya ungemuletea. Tunaweza pia kufanya vile; juu kama hatufanye vile, tutamuhuzunisha Yehova na tutashindwa kumuabudu milele.​—Mwa. 6:5, 6.

5. Mufano wa ndugu Leo unaweza kukufundisha nini?

5 Kama tunamuogopa Yehova, tutaepuka kuwa na marafiki wenye wanafanyaka mambo ya mubaya. Ndugu Leo, mwenye anaishi mu Congo, aliona kama ile ni jambo ya lazima. Miaka ine kisha kubatizwa, alianza kuwa na marafiki wenye walikuwa nafanya mambo ya mubaya. Aliwaza kama haikukuwa mubaya kuwa na wale marafiki juu yeye hakukuwa nafanya ile mambo. Lakini kisha wakati mufupi, marafiki wake walimufanya aanze kunywa pombe kupita kiasi na kufanya uasherati. Kisha pale, alianza kufikiri sana juu ya mambo yenye wazazi wake Wakristo walimufundishaka na juu ya furaha yenye alikuwa amepoteza. Matokeo ilikuwa nini? Alianza tena kufanya mambo ya muzuri. Wazee walimusaidia na alimurudilia Yehova. Sasa, iko na furaha ya kuwa muzee na painia wa pekee.

6. Ni wanamuke gani wa mufano wenye tutazungumuzia?

6 Tuzungumuzie sasa Mezali sura ya 9, yenye inazungumuzia wanamuke wawili. c Mumoja anafananisha hekima ya kweli na mwingine anafananisha ujinga. Wakati tuko nafanya vile, tutie mu akili kama mu hii ulimwengu yenye kutawaliwa na Shetani munayala uasherati na pornografia. (Efe. 4:19) Njo maana, ni jambo ya maana kuendelea kumuogopa Mungu na kuepuka kufanya mambo ya mubaya. (Mez. 16:6) Kama tunafanya vile, ikuwe tuko wanaume ao wanamuke, mambo yenye wale wanamuke wanafananisha inaweza kutusaidia. Wote wako naalika watu wenye hawana uzoefu, ni kusema, wale wenye “hawana akili ya muzuri,” na wako nasema hivi: ‘Ukuye ku nyumba yangu na ukule.’ (Mez. 9:1, 5, 6, 13, 16, 17) Lakini, matokea iko tofauti kwa wale wenye wanakubali mualiko wa mwanamuke mujinga na kwa wale wenye wanakubali mualiko wa mwanamuke mwenye hekima.

UKATALE MUALIKO WA MWANAMUKE MUJINGA

Mualiko wa “mwanamuke mujinga” uko na matokeo ya mubaya (Ona fungu ya 7)

7. Kulingana na Mezali 9:13-18, nini njo inafikia wale wenye wanakubali mualiko wa mwanamuke mujinga? (Ona pia picha.)

7 Fikiria mualiko wa “mwanamuke mujinga.” (Soma Mezali 9:13-18.) Bila haya, anaalika wenye hawana uzoefu wakuye mu nyumba yake na wafanye karamu. Nini njo inawafikia? “Wale wenye hawana uwezo katika kifo wako pale.” Pengine unakumbuka usemi wa mufano sawa ule wenye kupatikana mu sura za kutangulia za kitabu ya Mezali. Inatuonya kuhusu mwanamuke “mwenye kupotoka” na “mwasherati.” Inasema hivi: “Nyumba yake inazama katika kifo.” (Mez. 2:11-19) Mezali 5:3-10 iko na onyo kuhusu ‘mwanamuke mwingine mwenye kupotoka’ mwenye “miguu yake inashuka kwenye kifo.”

8. Unapaswa kukamata uamuzi gani?

8 Wale wenye wanasikia mualiko wa “mwanamuke mujinga” wanapaswa kuamua ikiwa wataukubali ao hapana. Siye pia, tunapaswa kukamata uamuzi sawa ule. Kwa mufano, unaweza kufanya nini kama mutu fulani anakuchochea kufanya uasherati ao kama unaona picha za pornografia bila kutazamia?

9-10. Ni sababu gani zenye zinapaswa kutuchochea kuepuka uasherati?

9 Kuko sababu mingi za muzuri zenye zinapaswa kutuchochea kuepuka uasherati. “Mwanamuke mujinga” iko nasema hivi: “Maji yenye yaliibwa ni matamu.” Ile “maji yenye yaliibwa” njo nini? Biblia inafananisha ngono kati ya bibi na bwana na maji yenye kuburudisha. (Mez. 5:15-18) Mwanaume na mwanamuke wenye kuoana kulingana na sheria wanaruhusiwa kufanya ngono. Lakini, ile iko tofauti kabisa na “maji yenye yaliibwa.” Ile maji inaweza kumaanisha uasherati. Kwa kawaida, watu wenye wanafanyaka uasherati wanajifichikaka juu wengine wasiwaone, sawa vile tu mwizi mwenye iko naiba. Zaidi ya ile, “maji yenye yaliibwa” inaweza kuonekana kuwa butamu kama wale wenye kuikunywa wanawaza kama hakuna mutu mwenye atajua mambo yenye walifanya. Ile ni kujidanganya kabisa juu Yehova anaonaka mambo yote. Hakuna jambo ya kuhuzunisha zaidi sawa vile kupoteza kibali ya Yehova. Kwa hiyo, haiko jambo ya “butamu” ao ya kufurahisha. (1 Ko. 6:9, 10) Lakini kuko matokeo ingine ya mubaya.

10 Kufanya uasherati kunaweza kufanya mutu asikie haya, ajione kuwa wa bure, apate mimba yenye hakupanga, na aharibishe familia yake. Njo maana, ni jambo ya hekima kuepuka kuenda mu “nyumba” ya mwanamuke mujinga na kula. Zaidi tu ya kupoteza kibali ya Yehova, watu wengi wenye kufanya uasherati wanapataka magonjwa yenye inaweza kufanya wakufe mbele ya wakati. (Mez. 7:23, 26) Sura ya 9 mustari wa 18 inamalizia hivi: “Wageni wake wanapatikana katika sehemu za chini kabisa za Kaburi.” Sasa juu ya nini watu wengi wanakubali mualiko wake wenye unapeleka ku kifo?​—Mez. 9:13-18.

11. Juu ya nini ni mubaya sana kuangalia pornografia?

11 Pornografia ni mutego ingine yenye inaenea sana yenye tunapaswa kuepuka. Watu fulani wanawaza kama haiko mubaya kuiangalia, lakini ni mubaya. Inafanya mwenye kuiangalia asijiheshimie na pia wengine wasimuheshimie, na ni nguvu sana kuacha ile tabia. Kama mutu anaona picha za uasherati, inakuwaka nguvu sana kuzisahau. Zaidi ya ile, pornografia haimalizake tamaa za mubaya, lakini inazichocheaka. (Kol. 3:5; Yak. 1:14, 15) Kusema kweli, watu wengi wenye wanaangaliaka pornografia wanafikiaka kufanya uasherati.

12. Tunapaswa kufanya nini kuhusu picha zenye zinaweza kulamusha tamaa ya kufanya uasherati?

12 Mukristo anapaswa kufanya nini kama anaona picha ya pornografia bila kutazamia? Anapaswa kuacha kuiagalia palepale. Jambo yenye inaweza kutusaidia kufanya vile ni kukumbuka kama urafiki wetu pamoya na Yehova njo jambo ya maana sana. Vilevile, hata picha fulani zenye zinaweza kuonekana sawa vile hazifanane picha za pornografia, zinaweza kulamusha tamaa ya kufanya uasherati. Juu ya nini tunapaswa kuziepuka? Juu hatupendi hata kidogo kufanya uzinifu mu moyo wetu. (Mt. 5:28, 29) David, muzee wa mu Tailandi anasema hivi: “Najiulizaka hivi: ‘Hata kama hizi picha hazifanane picha za pornografia, Yehova atafurahi kama naendelea kuziangalia?’ Kujiuliza vile kunanisaidiaka nitende kwa hekima.”

13. Nini njo inatusaidiaka kutenda kwa hekima?

13 Kuogopa kufanya jambo yoyote yenye itamuhuzunisha Yehova kutatusaidia tutende kwa hekima. Kumuogopa Mungu njo “mwanzo” ao musingi “wa hekima.” (Mez. 9:10) Ile inafasiriwa muzuri ku mistari ya kwanza ya kitabu ya Mezali sura ya 9, kwenye “hekima ya kweli” inafananisha ule mwanamuke mwingine.

KUBALI MUALIKO WA MWANAMUKE MWENYE HEKIMA

14. Mu Mezali 9:1-6, muko mualiko gani?

14 Soma Mezali 9:1-6. Mu hii andiko muko mualiko wenye unatoka kwa Yehova mwenye ni Muumbaji wetu na Chanzo ya hekima yote. (Mez. 2:6; Ro. 16:27) Inazungumuzia pia nyumba kubwa yenye kuwa na nguzo saba. Ile inaonyesha kama Yehova ni mukarimu na anakaribisha wale wote wenye wanapenda kutumikisha hekima yake mu maisha yao.

15. Mungu anatuomba tufanye nini?

15 Mu mufano wa ule mwanamuke mwenye kufananisha “hekima ya kweli” mu Mezali sura ya 9, tunajifunza kama Yehova ni mukarimu na anatupatiaka mambo mingi ya muzuri. Hii andiko inasema kama ule mwanamuke alialika wageni waingie mu nyumba yake ili wakule nyama na kunywa divai ya muzuri yenye alitayarisha. (Mez. 9:1, 2, maelezo ya chini) Zaidi ya ile, mu mustari wa 4 na wa 5, ‘Ule mwanamuke [hekima ya kweli] anamuambia hivi ule mwenye hana akili ya muzuri: Ukuye, ukule mukate wangu.’ Juu ya nini tunapaswa kukubali mualiko wa mwanamuke mwenye hekima? Juu Yehova anapenda watoto wake wakuwe na hekima na wakuwe salama. Hapendi tufanye makosa yenye itatuumiza. Njo maana “anaweka kama hazina hekima yenye kutenda kwa ajili ya wanyoofu.” (Mez. 2:7) Wakati tunamuogopa Yehova mu njia yenye kufaa, tutapenda kumufurahisha, tutasikiliza mashauri yake ya hekima, na tutapenda kuitumikisha.​—Yak. 1:25.

16. Alain alikamata uamuzi gani wa hekima juu alimuogopa Mungu, na ile ilikuwa na matokeo gani?

16 Ona namna kumuogopa Mungu kulisaidia Alain akamate uamuzi wa hekima. Alain ni muzee wa kutaniko na mwalimu ku masomo fulani. Anasema hivi: “Wengi kati ya wafanyakazi wenzangu walikuwa naangalia filme za pornografia ili wajifunze namna ya kufanya ngono.” Lakini, Alain hakudanganywa. Alisema hivi: “Juu nilimuogopa Mungu, nilikatala kabisa kuangalia zile filme. Na niliambia wafanyakazi wenzangu juu ya nini nilikatala kufanya vile.” Alikuwa natumikisha mashauri ya “hekima ya kweli” ya ‘kutembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.’ (Mez. 9:6) Walimu fulani wenzake waliguswa sana na musimamo wake; na sasa wako najifunza Biblia na kukusanyika.

Kama tunakubali mualiko wa mwanamuke mwenye hekima tutapata uzima (Ona fungu ya 17-18)

17-18. Wale wenye kukubali mualiko wa mwanamuke mwenye hekima wako napata baraka gani, na wanangojea nini? (Ona pia picha.)

17 Yehova anatumia mifano ya wale wanamuke wawili ili kuonyesha mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe na furaha wakati wenye kuya. Wale wenye wanakubali mualiko wa “mwanamuke mujinga” wanapenda kujifurahisha kwa kufanya uasherati. Bila shaka, wako naishi tu kwa ajili ya leo, hawajue mambo yenye itawafikia wakati wenye kuya. Matendo yao itawafikisha mu “sehemu za chini kabisa za Kaburi.”​—Mez. 9:13, 17, 18.

18 Lakini, ile haitawafikia wale wenye wanakubali mualiko wa mwanamuke mwenye hekima. Na wako na furaha juu wako na mambo yote yenye wako nayo lazima ili waendelee kuwa karibu na Yehova. (Isa. 65:13) Yehova alisema hivi kupitia nabii Isaya: “Munisikilize kwa uangalifu, na mukule mambo ya muzuri, na mutapata furaha nyingi katika vitu vyenye kujenga mwili kabisa.” (Isa. 55:1, 2) Tuko najifunza kupenda mambo yenye Yehova anapenda na kuchukia mambo yenye anachukia. (Zb. 97:10) Na tuko nafuraha juu tunaweza kualika wengine wajifunze kupitia “hekima ya kweli.” Zaidi ya ile, tuko sawa vile watumishi wenye wako ‘naita kwa sauti kubwa kutoka nafasi za juu za muji: Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.’ Faida zenye tuko napata na zenye wale wenye kukubali mualiko watapata haziko za leo tu, ni za lote. Zitafanya ‘tuishi’ milele juu tutaendelea ‘kutembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.’​—Mez. 9:3, 4, 6.

19. Kulingana na Muhubiri 12:13, 14, tunapaswa kuazimia kufanya nini? (Ona pia kisanduku “ Kumuogopa Mungu Kunatuletea Faida.”)

19 Soma Muhubiri 12:13, 14. Kumuogopa Mungu kuendelee basi kulinda moyo wetu na kutusaidia kuwa na mwenendo safi na kumukaribia Yehova mu hii wakati ya mwisho. Kumuogopa Mungu mu njia yenye kufaa kutatuchochea tuendelee kualika watu wengi kadiri inawezekana ili watafute “hekima ya kweli” na iwaletee faida.

 

WIMBO 127 Ninapaswa Kuwa Mutu wa Namna Gani?

a Siye Wakristo tunapenda kumuogopa Mungu mu njia yenye kufaa. Woga wa vile unaweza kulinda moyo wetu na kutulinda juu tusifanye uasherati na kuangalia pornografia. Mu hii habari, tutazungumuzia Mezali sura ya 9. Mu ile andiko, tutaona tofauti kati ya mwanamuke mujinga mwenye anafananisha ujinga na mwanamuke mwenye hekima mwenye anafananisha hekima ya kweli. Mashauri yenye kuwa mu ile andiko inaweza kutusaidia sasa na wakati wenye kuya.

b Majina fulani imebadilishwa.

c Kuhusu mifano ingine yenye Biblia inazungumuzia vitu sawa vile ni watu, ona Waroma 5:14; Wagalatia 4:24.