Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Mambo ya Kufurahisha Yenye Hatukutazamia na Mambo Yenye Tulijifunza mu Utumishi wa Yehova

Mambo ya Kufurahisha Yenye Hatukutazamia na Mambo Yenye Tulijifunza mu Utumishi wa Yehova

WAKATI nilikuwa mutoto, kila wakati kama naona avion mu anga, nilikuwa napenda kusafiri mu inchi ingine. Lakini, niliona ile kuwa ndoto yenye haitawezekanaka.

Wazazi wangu walitoka Estonia mu Vita ya Pili ya Ulimwengu na kuenda Alemanye, kwenye nilizaliwa. Kisha tu miye kuzaliwa, walianza kupanga safari ya kuenda Kanada. Nyumba yetu ya kwanza ilikuwa karibu na Ottawa, mu Kanada; ilikuwa ya kidogo na mulikuwa munaishi pia makuku. Tulikuwa maskini sana, lakini hatukukuwa nakosa mayai ya kukula asubui.

Siku moya, Mashahidi wa Yehova walimusomea mama yangu Ufunuo 21:3, 4. Mambo yenye alijifunza ilimugusa sana mupaka akaanza kulia. Mama yangu na baba yangu waliendelea kujifunza Biblia, na kisha wakati mufupi, walibatizwa.

Wazazi wangu hawakujua Kiingereza muzuri, lakini walikamata kweli kwa uzito. Karibu kila siku ya Posho, hata kisha kutumika usiku wote fasi kwenye nickel ilikuwa inayeyushwa mu Sudbury, Ontario, baba yangu alikuwa naenda na miye na mudogo yangu mwanamuke, Sylvia, mu mahubiri. Na kila juma, tulikuwa najifunza Munara wa Mulinzi mu familia. Mama na baba walinichochea nimupende Mungu. Kwa hiyo, mu 1956, wakati nilikuwa na miaka kumi, niliamua kutoa maisha yangu kwa Yehova. Upendo wenye wazazi wangu walikuwa nao kwa Yehova ulinitia moyo niendelee kumutumikia.

Kisha kumaliza masomo ya segodere, sikukaza tena akili mu utumishi wa Yehova. Niliwaza kama ikiwa nakuwa painia, sitapata makuta ya kunisaidia kutimiza ndoto yangu ya kusafiri mu avion na kutembelea fasi mbalimbali mu dunia. Nilipata kazi ya kutia miziki yenye kurekodiwa mu kituo fulani ya radio. Nilipenda sana ile kazi. Lakini, nilikuwa natumika mangaribi, kwa hiyo, sikukuwa nahuzuria mikutano kwa ukawaida na nilishirikiana na wale wenye hawamupendi Mungu. Ku mwisho, zamiri yangu yenye kuzoezwa na Biblia ilinichochea kufanya mabadiliko.

Nilienda Oshawa, Ontario. Kule nilikutana na Ray Norman, dada yake mudogo Lesli, na mapainia wengine. Walinikaribisha muzuri sana. Kuona vile walikuwa na furaha, kulinisaidia nichunguze tena miradi yangu. Walinitia moyo nianze kazi ya upainia, na niliianza mu Mwezi wa 9, 1966. Nilikuwa na furaha na maisha ilionekana kuwa muzuri. Lakini, mambo yenye haitazamiwe yenye ingebadilisha maisha yangu ilikuwa karibu kutokea.

WAKATI YEHOVA ANAKUOMBA KUFANYA JAMBO FULANI, UPIME KUIFANYA

Wakati nilikuwa ningali ku masomo ya segondere, nilijaza fomu ya kutumikia ku Beteli mu Toronto, Kanada. Kisha, wakati nilikuwa painia, nilialikwa kutumika ku Beteli kwa miaka ine. Lakini, juu nilikuwa namupenda Lesli, niliwaza kama ikiwa nakubali ule mualiko, singeweza kumuona tena. Kisha kusali sana, niliamua tu kuenda kutumika ku Beteli, lakini nilihuzunika juu nilimuacha Lesli.

Kule, nilitumika fasi ya kufulia manguo na kisha nikakuwa muandishi. Ile wakati, Lesli alifikia kuwa painia wa pekee mu Gatineau, Quebec. Mara mingi nilikuwa najiuliza kama alikuwa anafanya nini na ikiwa nilikamataka uamuzi wa muzuri ao hapana. Kisha, jambo moya ya muzuri sana yenye sikutazamia ilitokea. Ray, ndugu wa Lesli, alialikwa ku Beteli. Nilianza kuishi naye mu chumba moya. Ile ilinisaidia nikuwe naongea tena na Lesli. Tulioana siku ya mwisho ya mugao wangu wa miaka ine, ni kusema, tarehe 27 Mwezi wa 2, 1971.

Tunaanza kazi ya muzunguko mu 1975

Miye na Lesli tulitumwa mu kutaniko ya Kifaransa mu Quebec. Kisha miaka fulani, bila kutazamia, nilipewa daraka ya kuwa mwangalizi wa muzunguko wakati nilikuwa na miaka 28. Niliwaza kama nilikuwa mudogo sana na kama sikukuwa na uzoefu wa kutosha ili kuwa mwangalizi wa muzunguko. Lakini, maneno ya Yeremia 1:7, 8 njo ilinitia moyo. Zaidi ya ile, Lesli alikuwa alishafanya aksida mingi na gari na hakukuwa anapata usingizi. Kwa hiyo, tuliwaza kama itakuwa nguvu sana kufanya kazi ya muzunguko. Lakini, Lesli alisema hivi: “Kama Yehova anatuomba kufanya jambo fulani, juu ya nini tusipime kuifanya?” Kwa hiyo, tulikubali kazi ya muzunguko na tuliifanya kwa miaka 17.

Juu nilikuwa mwangalizi wa muzunguko, nilikuwa na mambo mingi ya kufanya, kwa hiyo sikukuwa napata kila mara wakati wa kupitisha pamoya na Lesli. Nilipaswa kujifunza jambo ingine. Siku moya hivi, ilikuwa siku ya Kwanza asubui sana, kengele ya mulango wetu ililia. Saa nilitoka inje, sikuona mutu, niliona tu kikapu ya kubebea chakula na kitambala ya ku meza, tunda, fromage, mukate, chupa ya divai, vilauri (verres), na barua, yenye haikukuwa na jina, yenye ilikuwa tu na hii maneno: “Uende na bibi yako mu matembezi.” Ilikuwa siku ya muzuri na kulikuwa jua. Lakini, nilimuambia Lesli kama nilikuwa na hotuba za kutayarisha na singeweza kuenda. Alinielewa, lakini alihuzunika kidogo. Wakati nilitaka kuanza kutayarisha, zamiri yangu ilianza kunisumbua. Nilifikiria andiko ya Waefeso 5:25, 28. Niliona ile andiko kuwa njia yenye Yehova alitumia ili kunikumbusha kama nilipaswa kuhangaikia hisia za bibi yangu. Kisha kusali, nilimuambia Lesli hivi: “Tuende,” alifurahi sana. Tulienda fasi fulani ya muzuri, pembeni ya mutoni, na tulitandika kitambala ya ku meza. Ile njo ilikuwa siku ya muzuri sana yenye tulipitisha pamoya. Na nilifurahi juu ile haikunizuia kutayarisha hotuba zangu.

Tulitumikia kazi ya muzunguko fasi mingi na tuliifurahia, kuanzia mu Colombie-Britanique mupaka mu Newfoundland. Ndoto yangu ya kupenda kusafiri mu avion ilitimia. Nilifikiria kusoma Masomo ya Gileadi, lakini sikupenda kuwa misionere mu inchi ya kigeni. Ilionekana sawa vile wamisionere ni watu wa pekee sana. Njo maana, niliwaza kama sikustahili kuwa misionere. Zaidi ya ile, niliwaza kama pengine tungetumwa mu inchi fulani ya Afrika kwenye kulikuwa magonjwa na vita, ile iliniogopesha. Nilipenda tu kubakia mu Kanada.

BILA KUTAZAMIA, TULIPATA MUALIKO WA KUENDA ESTONIA NA MU INCHI ZA BALTIKI

Kusafiri mu inchi za Baltiki

Mu 1992 Mashahidi wa Yehova walianza tena kuhubiri mu inchi fulani zenye zilikuwaka sehemu ya Muungano wa Sovieti. Kwa hiyo, ndugu walituuliza ikiwa tutakubali kuenda Estonia na kuwa wamisionere. Tulishangaa sana, lakini tulisali. Tulijiuliza tena hivi: ‘Kama Yehova anatuomba kufanya jambo fulani, juu ya nini tusipime kuifanya?’ ‘Tulikubali ule mualiko, na nilifurahi juu hatukutumwa mu Afrika.’

Mara moya tulianza kujifunza Kiestonia. Kisha kufanya miezi fulani mu Estonia, tuliombwa kufanya kazi ya muzunguko. Tulipaswa kutembelea makutaniko 46 hivi na vikundi fulani mu inchi tatu za Baltiki na pia mu Kaliningrad, mu Urusi. Kwa hiyo, tulipaswa kujifunza Kilativia, Kilutuania, na Kirusi. Haikukuwa mwepesi kufanya vile. Lakini, marafiki wetu walifurahi kuona vile tulikuwa tunajikaza na walitusaidia. Mu 1999, mu Estonia mulifikia kuwa biro ya tawi, na nilipewa daraka ya kutumika mu Halmashauri ya Tawi pamoya na Toomas Edur, Lembit Reile, na Tommi Kauko.

Kushoto: Niko natoa hotuba ku mukusanyiko mu Lituania

Kuume: Niko natumika mu Halmashauri ya Tawi mu Estonia, yenye ilifanywa mu 1999

Tulifikia kujua Mashahidi wengi wenye walipelekwaka Siberia zamani. Hata kama walitendewaka mubaya mu gereza na kutengwa na familia yao, hawakukasirika wala kuweka kinyongo. Waliendelea kuwa na furaha na bidii mu utumishi wa Yehova. Ile ilitusaidia kuona kama siye pia tunaweza kuvumilia na kuwa na furaha hata kama tuko na magumu.

Juu tulitumika sana kwa miaka mingi na juu hatukupata wakati wa kupumuzika, Lesli alianza kusikia muchoko sana. Hatukutambua mara moya kama alikuwa nachoka juu alikuwa na magonjwa ya fibromyalgie, magonjwa yenye inaletaka muchoko. Kwa hiyo, tuliamua kurudia Kanada. Wakati tulialikwa ku Masomo ya Washiriki wa Halmashauri ya Tawi na Bibi Zao, mu Patterson, New York, Amerika, sikuwazia kama tutasoma. Lakini, kisha kusali sana, tulikubali. Yehova alibariki ule uamuzi. Mu ile kipindi tulikuwa ku masomo njo Lesli alifikia kupata matunzo ya muzuri. Ile ilifanya tuanze kutumika tena kama kawaida.

JAMBO INGINE YENYE HATUKUTAZAMIA​—KUTUMIKIA MU BARA (CONTINENT) INGINE

Mangaribi moya mu 2008 wakati tulirudia Estonia, makao makubwa iliniita na kuniuliza kama tungekubali kutumikia mu Congo. Sikujua hata nifanye nini, zaidi sana juu nilipaswa kuwajibia siku yenye kufuata. Ku mwanzo sikumuambia Lesli, juu kama ningemuambia hangelala ile usiku. Lakini miye njo sikulalaka, nilikuwa tu namuomba Yehova juu ya jambo yenye ilikuwa nafanya niogope kuenda mu Afrika.

Siku yenye ilifuata nilimuambia Lesli. Kisha tukawaza hivi: “Ni Yehova njo anatualika kuenda Afrika. Juu tujue kama tutaweza na kama tutaifurahia inaomba tupime.” Kwa hiyo, kisha kufanya miaka 16 mu Estonia, tulienda Kinshasa mu Congo. Biro ya tawi ilikuwa na bustani ya muzuri na ilikuwa fasi ya kimya. Moya kati ya vitu vyenye Lesli alitiaka kwanza mu chumba yetu ilikuwa karte yenye alikuwaka nayo wakati tulikuwa natoka Kanada. Ku ile karte kulikuwa maneno, “Ufurahi fasi kwenye uko.” Kisha kukutana na ndugu, kuongoza mafunzo ya Biblia, na kuona namna ile kazi ya umisionere ilikuwa ya muzuri, tulipenda tena zaidi kumutumikia Yehova. Ku mwisho, tulikuwa na pendeleo ya kutembelea biro za tawi 13 hivi mu inchi zingine za Afrika. Tulijifunza mambo mingi juu ya watu mbalimbali na mambo mingi ya kufurahisha. Sikuogopa tena kuwa mu Afika na tulimushukuru Yehova juu alitutuma tutumikie kule.

Mu Congo, walitupatia chakula mbambali, sawa vile vidudu vyenye sikuwaziaka kama tunaweza kula. Lakini, wakati tuliona ndugu zetu wako nakula, na siye tuliipima na tukaipenda.

Tulipeleka misaada ya kiroho na ya kimwili ku sehemu ya mashariki ya inchi ya Congo. Kule wapiganaji wa kuvizia walikuwa nashambulia vijiji na kutendea mubaya wanamuke na watoto. Ndugu wengi sana walikuwa maskini, lakini tumaini yao ya ufufuo, upendo wao kwa Yehova na ushikamanifu wao kwa tengenezo yake ilitugusa sana. Mufano wao ulituchochea kufikiri sana juu ya sababu zenye zilifanya tumutumikie Yehova na ulitusaidia tufanye imani yetu ikuwe nguvu zaidi. Ndugu fulani walipoteza nyumba zao na chakula yenye walikuwa walishapanda iliibiwa. Ile ilinikumbusha kama uhusiano wetu pamoya na Yehova njo jambo ya maana sana na kama vitu vya kimwili vinaweza kupotea haraka. Hata kama walikuwa na magumu sana, wale ndugu hawakukuwa nalalamika-lalamika. Ile ilitutia moyo tuvumilie magumu yenye tulikuwa nayo na magumu ya afya kwa uhodari.

Kushoto: Niko natoa hotuba mbele ya kikundi ya wakimbizi

Kuume: Tunapeleka misaada ya matunzo na mambo mbalimbali mu Dungu, Congo

MUGAO MUPYA MU ASIA

Kisha kulitokea jambo ingine yenye hatukatazamia. Tuliombwa kuenda ku biro ya tawi ya Hong Kong. Hatukuwaziaka hata kidogo kama tunaweza kuishi mu Asia! Lakini, kisha kuona mukono wa Yehova mu migao ingine yote yenye tulipata, tulikubali ule mualiko. Mu 2013, tulitoka mu Afrika na tuko nalia juu tuliacha marafiki wetu wenye tulipenda na mambo ya muzuri yenye tuliona mule, lakini hatukujua nini itatokea kisha.

Kulikuwa badiliko kubwa sana kuishi mu Hong Kong juu mulikuwa watu wengi sana, tena wa kutoka mu inchi mbalimbali. Haikukuwa mwepesi kujifunza Kichina. Lakini ndugu walitukaribisha muzuri, na tulifurahia sana chakula ya kule. Kazi mingi ilikuwa nafanywa ku biro ya tawi, lakini ileile wakati bei ya parcelle na majengo ilikuwa napanda haraka. Njo maana, Baraza Yenye Kuongoza ilikamata uamuzi wa hekima wa kuuzisha majengo mingi ya tawi. Wakati kidogo kisha pale mu 2015, tulitumwa mu Korea ya Kusini, kwenye tuko naendelea kutumikia sasa. Hapa pia haiko mwepesi kujifunza Kikorea. Na hata kama hatujue kuisema muzuri sana, ndugu na dada wako natutia moyo kwa kusema kama tuko nafanya maendeleo mu namna yetu ya kuongea Kikorea.

Kushoto: Maisha yetu ya mupya mu Hong Kong

Kuume: Tawi ya Korea

MAMBO YENYE TUMEJIFUNZA

Haikuwake mwepesi kupata marafiki wapya, lakini kuonyesha wengine ukarimu kunatusaidia kuwajua haraka. Tulifikia kuona kama ndugu zetu wanafanana mu mambo mingi na wako tofauti mu mambo kidogo, na kama Yehova alituumba na uwezo wa kufungua mioyo yetu na kuonyesha marafiki wengi upendo.​—2 Ko. 6:11.

Tuliona ulazima wa kuona watu sawa vile Yehova anawaona na kuona mambo yenye kuonyesha kama Yehova anatupenda na kama iko natupatia muongozo. Wakati tulivunjika moyo ao wakati tulijiuliza ikiwa ndugu na dada walitupenda ao hapana, tulisoma tena karte na barua za marafiki wetu. Tumejionea kabisa namna Yehova alijibia sala zetu kwa kutuonyesha kama anatupenda na kutupatia nguvu ya kuendelea kumutumikia.

Kadiri miaka ilipita, miye na Lesli, tulijifunza kama ni jambo ya maana kupanga wakati wa kuwa pamoya hata kama tuko na mambo mingi ya kufanya. Tulifikia pia kuelewa kama haiko mubaya kucheka wakati tunafanya makosa, zaidi sana saa yenye tulikuwa najifunza luga ya mupya. Kila usiku, tulifikiria jambo fulani yenye tulipenda na tulimushukuru Yehova juu ya ile.

Kusema kweli, niliwaza kama singewezeka kuwa misionere ao kuishi mu inchi zingine. Lakini, nilijifunza kama mambo yote inawezekana kwa musaada wa Yehova. Nakumbuka maneno ya nabii Yeremia, mwenye alisema hivi: “Umenipumbaza, Ee Yehova.” (Yer. 20:7) Bila shaka, Yehova ametupatia mambo mingi ya muzuri yenye hatukutazamia na baraka mingi zenye hatukuwazia, alitimiza hata tamaa yangu ya kusafiri mu avion. Tulisafiri mu avion fasi mingi zaidi kuliko vile nilikuwaka nawazia wakati nilikuwaka mutoto, ni kusema, kutembelea biro za tawi mu bara (continent) tano. Niko pia mwenye shukrani sana, kuona vile Lesli alikuwa tayari kunitegemeza mu ile migao yote.

Kila mara, tunakumbushanaka kama tuko nafanya mambo yote juu tunamupenda Yehova. Mambo ya muzuri yenye tuko nafurahia leo inafanya tuone namna itakuwa muzuri sana kuishi milele wakati Yehova ‘atafungua mukono wake na kutimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.’​—Zb. 145:16.