Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Kuhangaikia Wengine Kunaletaka Baraka za Wakati Murefu

Kuhangaikia Wengine Kunaletaka Baraka za Wakati Murefu

Pamoya na mama yangu na dada yangu, Pat, mu 1948

TATE yangu mwanamuke mwenye alikuwa mu kanisa ya Anglikani alisema hivi: “Watu wa mu kanisa ya Waanglikani hawafundishake kweli, na hawaitafutake.” Kisha yeye kusema vile, mama yangu alianza kutafuta dini ya kweli. Lakini, hakukuwa napenda kuongea na Mashahidi wa Yehova na alikuwa naniambia nikuwe najificha wakati wanafika ku nyumba yetu mu Toronto Kanada. Lakini, wakati mama yangu mudogo alianza kujifunza na Mashahidi wa Yehova mu 1950, mama yangu pia alijiunga naye. Walikuwa najifunzia kwa mama yangu mudogo na kisha walifikia kubatizwa.

Juu baba yangu alikuwa muchungaji mu kanisa yenye kuitwa Eglise Unifiée du Canada, njo maana kila juma alikuwa nanituma miye na dada yangu ku masomo ya Biblia ya watoto ya siku ya Yenga. Kisha, saa tano (11:00) tulikuwa naenda pamoya na baba yangu ku ibada ya kanisa. Na kisha midi tulikuwa naenda na mama ku Jumba ya Ufalme. Ilikuwa mwepesi kwetu kuona tofauti kati ya ile dini mbili.

Wakati wa Mukusanyiko wa Kimataifa wenye kichwa Mapenzi ya Kimungu mu 1958 pamoya na familia ya Hutcheson

Mama alikuwa naambia rafiki yake Bob na Marion Hutcheson mambo yenye alikuwa najifunza mu Biblia. Nao pia walifikia kuwa Mashahidi wa Yehova. Mu 1958, ndugu na dada Hutcheson pamoya na watoto wao wanaume watatu, walienda na miye ku Mukusanyiko wa Kimataifa wenye ulifanya siku munane mu Muji wa New York. Ule mukusanyiko ulikuwa na kichwa Mapenzi ya Kimungu. Kwa sasa, nafikia kutambua kama haikukuwaka mwepesi kwao kuenda na miye, na ule mukusanyiko ni moya kati ya mambo yenye siwezi kusahau mu maisha yangu.

NDUGU NA DADA WALINISAIDIA NIFANYE MAMBO MINGI ZAIDI MU UTUMISHI WA YEHOVA

Mu miaka yangu ya ujana, tulikuwa naishi mu maeneo ya mashamba, kule nilikuwa napenda sana kuhangaikia wanyama. Njo maana nilipenda sana kusoma masomo ya kuwa muganga wa wanyama. Mama yangu aliambia muzee moya wa kutaniko ile jambo. Kwa upendo, ule muzee alinikumbusha kama tuko naishi mu “siku za mwisho” na aliniambia kama kusoma masomo ya Université kwa miaka mingi kungeharibisha urafiki wangu pamoya na Yehova. (2 Ti. 3:1) Kwa hiyo, niliamua kutoenda ku Université.

Nilikuwa najiuliza mambo yenye nitafanya kisha kumaliza masomo yangu ya segondere. Hata kama nilikuwa naenda ku mukutano wa mahubiri kila mwisho wa juma, sikukuwa napenda mahubiri na sikuwaziaka kama naweza kuwa painia. Wakati uleule, baba yangu mwenye hakukuwa Shahidi na muyomba yangu walinitia moyo nijikaze sana juu siku moya nitumike mu kompanyi ya mu Toronto yenye inapatiaka watu dokima yenye kuitwa asiranse. Muyomba yangu alikuwa na cheo mu ile kompanyi, njo maana nilikubali ile kazi.

Mu Toronto, nilikuwa napitisha wakati mingi mu kazi na nilikuwa na marafiki wenye hawako Mashahidi wa Yehova; ile ilifanya nishindwe kukusanyika na kuhubiri kwa ukawaida. Ku mwanzo nilikuwa naishi na tate yangu mwanaume mwenye hakukuwa Shahidi wa Yehova, kisha yeye kufa, iliniomba kuishi fasi ingine.

Ndugu na dada Hutcheson, wenye walinipelekaka ku mukusanyiko wa 1958, walikuwa sawa vile tu wazazi wangu. Waliniambia niishi nao na walinisaidia nikomale kiroho. Mu 1960, nilibatizwa pamoya na mutoto wao mwanaume John. John alianza kazi ya upainia, ile ilinichochea nihubiri zaidi. Ndugu mu kutaniko waliona maendeleo yangu ya kiroho na kisha niliwekwa kuwa Mutumishi wa Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. a

NILIPATA BIBI MUZURI NA NILIFIKIA KUWA PAINIA

Siku ya ndoa yetu mu 1966

Mu 1966, nilioa Randi Berge, painia mwenye bidii mwenye alikuwa tayari kumutumikia Yehova fasi kwenye kulikuwa lazima kubwa. Mwangalizi wetu mwenye kusafiri alituhangaikia na akatutia moyo tusaidie kutaniko mu Orillia, Ontario. Kwa hiyo, tulienda bila kukawia.

Saa tu tulifika Orillia, nilijiunga na Randi mu kazi ya upainia wa kawaida na niliipenda sana sawa vile yeye! Kisha kuanza kujikaza sana ili kuwa painia muzuri, kutumia Biblia, na kuona namna watu wanaielewa kulinifurahisha sana. Tulifurahi juu tulisaidia bibi na bwana fulani mu Orillia kufanya mabadiliko mu maisha yao na kuwa watumishi wa Yehova.

TUNAJIFUNZA LUGA MUPYA NA TUNABADILISHA NAMNA YETU YA KUFIKIRI

Wakati tulienda Toronto, nilikutana na Arnold MacNamara, mwenye alikuwa kati ya ndugu wenye walisimamia Beteli. Alituuliza ikiwa tutapenda kuwa mapainia wa pekee. Nilijibia mara moya hivi: “Ndiyo kabisa! Naweza kuenda fasi yote lakini hapana Quebec!” Nilisema vile juu watu wa mu sehemu ya Kanada wenye kusema Kiingereza walikuwa na mawazo ya mubaya kuhusu watu wa mu jimbo ya Quebec wenye walikuwa wanasema Kifaransa. Mu ile wakati, watu walikuwa napinga serikali juu walipenda jimbo ya Quebec ijiongoze yenyewe, isiongozwe na Kanada.

Arnold alisema hivi: “Kwa sasa ni mu Quebec tu njo mwenye biro ya tawi iko natuma mapainia wa pekee.” Mara moya nilikubali kuenda. Nilikuwa nilishajua kama Randi alikuwa napenda kutumikia kule. Kisha, nilifikia kutambua kama ile ilikuwa moya kati ya maamuzi ya muzuri sana yenye tulikamata mu maisha yetu!

Kisha kusoma ku darasa ya Kifaransa, yenye ilifanya majuma tano, Miye na Randi pamoya na bibi na bwana fulani, tulienda Rimouski, ku kilometre 540 hivi mu kaskazini-mashariki mwa Montréal. Tulikuwa tungali na mambo mingi ya kujifunza, na ile ilifikia kuonekana wazi sana ku mukutano wakati nilisoma matangazo fulani. Mu ile matangazo, kuliko kusema kama ku mukusanyiko wenye kuya tutakuwa na wawakilishi wenye watatoka mu inchi ya Autriche, nilitumia kimakosa neno yenye kufanana na ile kwa kusema kama wawakilishi watakuwa ndege wakubwa.

“Nyumba ya Mweupe” mu Rimouski

Mu Rimouski, tulikuwa watu ine, kisha wadada ine wenye kuwa na bidii na wenye walikuwa hawayaolewa, pamoya na dada na ndugu Huberdeau na watoto wao wawili wanamuke walikuya kujiunga na siye. Ndugu na dada Huberdeau walilipia nyumba ya munene, na mapainia wote wenye walikuwa naishi mule walisaidia pia kulipa. Tulikuwa naita ile nyumba, Nyumba ya Mweupe juu kibambazi ya mbele ya ile nyumba ilikuwa na rangi ya mweupe na ilikuwa na nguzo za mweupe. Kwa kawaida, mule tulikuwa naishi kati ya watu 12 na 14. Juu miye na Randi tulikuwa mapainia wa pekee, tulikuwa naenda kuhubiri asubui, kisha midi, na mangaribi. Kwa hiyo, tulifurahi juu hatukukuwa nakosa mutu wa kutusindikiza mu mahubiri hata mangaribi mu kipindi ya baridi.

Tulikaribiana sana na wale mapainia waaminifu na wakakuwa sawa vile watu wa familia yetu. Wakati fulani tulikuwa naikala pembeni ya moto na tulikuwa na siku yenye tulikuwa napika chakula pamoya. Ndugu moya alikuwa mupiga-muziki, kwa hiyo mara mingi siku ya Posho usiku tulikuwa naimba na kucheza.

Watu wengi mu Rimouski walifurahia kujifunza Biblia! Mu miaka tano, tulifurahi kuona wanafunzi wengi wa Biblia wanafanya maendeleo na kufikia kubatizwa. Kutaniko iliongezeka na kuwa na wahubiri karibu 35.

Mu Quebec, tulipata mazoezi ya muzuri sana mu kazi ya kuhubiri. Tuliona namna Yehova alitusaidia mu utumishi wetu na namna alitutimizia mahitaji yetu ya kimwili. Zaidi ya ile, tulijifunza kupenda watu wenye kusema Kifaransa, tulipenda luga yao na desturi yao. Na ile ilifanya tupende pia desturi za watu wengine.—2 Ko. 6: 13.

Bila kutazamia, biro ya tawi ilituomba tuende mu muji wa Tracadie, mu mashariki, pembeni ya bahari ya New Brunswick. Ile ilileta magumu fulani juu tulikuwa tulishafanya mapatano ili kulipia nyumba fulani. Tena, nilikuwa nilishafanya mapatano na wasimamizi wa masomo ili kufundisha kwa wakati fulani. Zaidi ya ile, kulikuwa hakuyakawia tangu wanafunzi wetu wa Biblia wafikie kuwa wahubiri na tulikuwa mu katikati ya ujenzi wa Jumba ya Ufalme.

Tulisali siku ya Posho na ya Yenga yote juu ya kuhama na tulitembelea Tracadie, yenye ilikuwa tofauti kidogo na Rimouski. Tuliamua kuenda juu Yehova njo alipenda tuende kule. Tulimujaribu Yehova na tuliona namna alitutoshea vizuizi vyote. (Mal. 3:10) Kama kawaida, juu Randi anakuwaka mutu wa kiroho sana, hatafutake tu faida yake, na anakuwaka mufuraivu, ile ilifanya ikuwe mwepesi kwetu kuhama.

Robert Ross njo tu alikuwa muzee mu kutaniko yetu ya mupya. Yeye na bibi yake Linda walikuwa mapainia kule na waliamua kubakia kule kisha mutoto wao wa kwanza kuzaliwa. Hata wakati walikuwa nahangaikia mutoto wao mwanaume, walitutia moyo sana juu walikuwa wakarimu na walikuwa na bidii mu kazi ya kuhubiri.

BARAKA ZA KUMUTUMIKIA YEHOVA FASI YOYOTE KWENYE KUKO LAZIMA

Kipindi ya baridi mu muzunguko wetu wa kwanza

Kisha kufanya kazi ya upainia mu Tracadie kwa miaka mbili, bila kutazamia, tulipata tena mualiko wa kutumika mu kazi ya kusafiri. Tulitumikia mu mizunguko ya Kiingereza kwa miaka saba, kisha tulitumwa tena mu muzunguko wa Kifaransa mu Quebec. Mwangalizi wetu wa wilaya mu Quebec, Léonce Crépeault, alikuwa nanipongeza juu ya hotuba zangu. Lakini, kila mara alikuwa naniuliza hivi: “Unaweza kufanya nini juu hotuba zako zikuwe muzuri zaidi?” b Kunihangaikia mu ile njia ilinisaidia nifanye namna yangu ya kufundisha ikuwe wazi na mwepesi zaidi.

Mugao wenye sitasahawaka ni ule wenye nilitimizaka mu 1978 ku Mukusanyiko wa Kimataifa wenye kichwa “Imani yenye Ushindi” wenye ulifanywa mu Montréal. Nilitumika ku idara ya chakula. Tulitazamia kupata watu 80000, na tulipaswa kuwapatia chakula mu njia mbalimbali kuliko vile tulikuwa nafanya zamani. Mambo yote ilikuwa ya mupya: Vifaa, chakula, na namna ya kuipika. Tulikuwa na frigo 20 hivi za munene, zenye wakati fulani hazikukuwa natumika muzuri. Mbele ya siku ya kwanza ya mukusanyiko, hatukuweza hata kutayarisha kila kitu mu kiwanja ya kuchezea mupaka katikati ya usiku juu kulikuwa muchezo wenye ulikuwa ulishapangwa. Na tulikuwa nawakisha four asubui sana ili kutayarisha chakula ya asubui! Tulichoka sana, lakini kuona vile wajitoleaji wenzangu walitumika sana, walikuwa na sifa za muzuri, na wenye furaha kulinifundisha mambo mingi sana. Tangu pale tungali marafiki. Tulifurahi sana kukusanyika mu Quebec, jimbo kwenye watu waliteswa sana mu miaka ya 1940 na 1950!

Miye na Randi tuko nafanya matayarisho ya mukusanyiko mu Montréal mu 1985

Mambo yenye waangalizi wenzangu walifanya ku mikusanyiko mikubwa ya Montréal ilinifundisha mambo mingi sana. Mu mwaka moya hivi, David Splane, mwenye iko sasa natumika mu Baraza Yenye Kuongoza, alikuwa mwangalizi wa mukusanyiko fulani. Ku mukusanyiko wenye ulifuata, wakati nilipewa daraka ya kuwa mwangalizi wa mukusanyiko, David alinitegemeza sana.

Mu 2011, kisha miye na Randi kutumika kwa miaka 36 mu kazi ya kusafiri, niliombwa kuwa mwalimu ku Masomo ya Wazee wa Kutaniko. Mu miaka mbili, tulilala ku vitanda 75 tofauti, lakini ilikuwa lazima tujitolee mu ile njia. Ku mwisho wa kila juma, wazee walikuwa wenye shukrani sana juu walijionea namna Baraza Yenye Kuongoza ilihangaikia hali yao ya kiroho.

Kisha, nilikuwaka mwalimu wa Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Kulikuwa mambo mingi ya kufanya yenye ilikuwa nachokesha sana wanafunzi, sawa vile: Kuikala mu masomo kwa saa saba hivi kwa siku, kufanya dévoir kila mangaribi kwa saa tatu, na kutimiza migao ine ao tano kila juma. Miye na mwalimu mwingine tuliwafasiria kama bila musaada wa Yehova hawangeweza kufanya ile mambo yote. Sitasahawaka namna wanafunzi walishangaa kuona vile kumutegemea Yehova kuliwasaidia kutimiza mambo mingi zaidi ya ile yenye walikuwa nawazia.

KUHANGAIKIA WENGINE KUNALETAKA BARAKA ZA WAKATI MUREFU

Juu mama yangu alihangaikia wengine, ile ilisaidia wanafunzi wake wa Biblia wafanye maendeleo na ilisaidia hata baba yangu aanze kupenda kweli. Siku tatu kisha mama yangu kufa, tulishangaa kuona baba yetu anakuya kusikiliza hotuba ya watu wote ku Jumba ya Ufalme na aliendelea kukusanyika kwa miaka 26 yenye ilifuata. Hata kama baba yangu hakubatizwaka, wazee waliniambia kama yeye njo alikuwa nafika wa kwanza ku mikutano kila juma.

Mama yangu alituwekea mufano muzuri, miye na wadogo yangu wanamuke. Wote watatu na bwana zao wako namutumikia Yehova kwa uaminifu. Wawili kati ya wale wadogo yangu wako natumika ku biro za tawi, mumoja mu Portugal na mwingine mu Haiti.

Kwa sasa miye na Randi tuko mapainia wa pekee mu Hamilton, Ontario. Wakati tulikuwa mu kazi ya muzunguko, tulikuwa nafurahia kusindikiza watu ku marudio na mafunzo yao ya Biblia. Lakini sasa tuko na furaha ya kuona mafunzo yetu ya Biblia iko nafanya maendeleo ya kiroho. Na juu tuko na urafiki pamoya na ndugu na dada wa mu kutaniko yetu ya mupya, tunatiwaka moyo kuona namna Yehova iko nawategemeza mu wakati ya muzuri na ya mubaya.

Tuko nafurahi sana wakati tunakumbuka namna watu wengi sana walituhangaikia kipekee. Ile ilifanya siye pia tujikaze ‘kuhangaikia sana’ wengine na kuwatia moyo wamutumikie Yehova kwa uwezo wao wote. (2 Ko. 7: 6,7) Kwa mufano mu familia moya, bibi, mutoto mwanaume, na mutoto mwanamuke, wote walikuwa watumishi wa wakati wote. Nilimuuliza baba wa ile familia kama alishakafikiria kuwa painia siku moya. Aliniambia kama alikuwa nategemeza wale mapainia watatu, kwa hiyo nilimuuliza hivi: “Unawaza, unaweza kuwategemeza muzuri zaidi kuliko Yehova?” Nilimutia moyo ajionee furaha yenye wale mapainia walikuwa nayo. Jambo ya kufurahisha, alifikia kuwa painia kisha miezi sita.

Miye na Randi tutaendelea kuambia “kizazi chenye kitafuata” kuhusu ‘kazi za Yehova za ajabu’ na tunatumaini kama watafurahia kumutumikia Yehova sawa vile siye.—Zb. 71:17, 18.

a Mwenye leo anaitwa Mwangalizi wa Mukutano Utumishi na Maisha.

b Ona habari juu ya maisha ya Léonce Crépeault mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2020, uku. 26-30.