Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 31

“Mukuwe Imara, Bila Kutikisika”

“Mukuwe Imara, Bila Kutikisika”

“Ndugu zangu wapendwa, mukuwe imara, bila kutikisika.”​—1 KO. 15:58.

WIMBO 122 Tukuwe na Nguvu na Tusitikisike!

KIFUPI YA HABARI a

1-2. Ni mu njia gani Mukristo iko sawa vile jengo ya murefu sana? (1 Wakorinto 15:58)

 MU TOKYO, Japani, mulijengwa jengo moya ya murefu sana mu 1970. Juu mu ule muji mulikuwa natokea matetemeko mingi ya inchi, watu walikuwa najiuliza ikiwa ile jengo itabakia kabisa imara ao hapana. Juu ibakie imara, siri ilikuwa nini? Wajenzi walitumia vifaa vyenye viliifanya ikuwe nguvu sana, na waliijenga mu njia yenye ingeifanya ibakie imara hata kama kunatokea matetemeko ya inchi. Wakristo wako sawa vile ile jengo. Mu njia gani?

2 Mukristo anapaswa kujua ni wakati gani anapaswa kuwa imara na ni wakati gani anapaswa kuwa na usawaziko. Anapaswa kuwa nguvu na imara wakati inaomba kutii sheria na kanuni za Yehova. (Soma 1 Wakorinto 15:58.) Anakuwaka “tayari kutii.” Lakini anapaswa kuwa na usawaziko kama inawezekana ao kama ni lazima. (Yak. 3:17) Mukristo mwenye kuwa vile, ataepuka kuwa imara kupita kiasi ao kuachilia mambo kupita kiasi. Mu hii habari, tutazungumuzia ni wakati gani tunapaswa kuwa imara. Tutazungumuzia pia mambo tano yenye Shetani anatumiaka juu ya kuregeza azimio yetu na tutaona pia mambo yenye tunaweza kufanya ili tuendelee kuwa imara.

TUNAWEZA KUFANYA NINI JUU TUKUWE IMARA?

3. Yehova anatupatia sheria gani mu Matendo 15:28, 29?

3 Yehova njo mwenye kuwa na haki ya kutupatia sheria. Njo maana anatupatiaka sheria zenye ziko mwepesi kuelewa. (Isa. 33:22) Kwa mufano, baraza yenye kuongoza ya mu karne ya kwanza ilionyesha kama Wakristo wanapaswa kuendelea kuwa imara mu hii mambo tatu: (1) Kuepuka kuabudu sanamu na kumuabudu tu Yehova, (2) kutii sheria ya Yehova yenye inaonyesha kama damu iko takatifu, na (3) kutii amri yenye kuwa mu Biblia ya kuepuka uasherati. (Soma Matendo 15:28, 29.) Leo, Wakristo wanaweza kufanya nini juu waendelee kuwa imara mu ile mambo tatu?

4. Tutaepuka kufanya nini ili kuonyesha kama tunapenda kumuabudu Yehova tu? (Ufunuo 4:11)

4 Tunaepuka kuabudu sanamu na tunamuabudu Yehova tu. Yehova aliambia Waisraeli wamuabudu yeye tu. (Kum. 5:6-10) Na wakati Yesu alijaribiwa na Ibilisi, yeye pia alisema waziwazi kama tunapaswa kumuabudu Yehova tu. (Mt. 4:8-10) Njo maana hatutumiake sanamu za dini mu ibada yetu. Tunaepukaka pia kuabudu watu, ikuwe ni viongozi wa dini, viongozi wa politike ao wakimbiaji wenye kujulikana sana, wachezaji wa filme, ao wapiga-muziki. Tena, hatupaswe kuwaona sawa vile ni miungu. Tunamutii Yehova na kumuabudu yeye tu mwenye ‘aliumba vitu vyote.’​—Soma Ufunuo 4:11.

5. Juu ya nini tunatii sheria ya Yehova yenye inaonyesha kama uzima na damu viko takatifu?

5 Tunatii sheria ya Yehova yenye inaonyesha kama uzima na damu viko takatifu. Juu ya nini? Juu Yehova anasema kama damu inafananisha uzima, wenye ni zawadi ya muzuri yenye ametupatia. (Law. 17:14) Wakati Yehova aliruhusu kwa mara ya kwanza wanadamu wakule nyama, aliwakataza kula damu ya munyama yeyote. (Mwa. 9:4) Alirudilia tena ile amri wakati alipatia Waisraeli Sheria ya Musa. (Law. 17:10) Na aliongoza baraza yenye kuongoza ya mu karne ya kwanza iambie Wakristo wote kama wanapaswa “kuendelea kujiepusha . . . na damu.” (Mdo. 15:28, 29) Tunatii ile amri wakati tunaamua ni matunzo gani yenye tutakubali. b

6. Tunafanyaka nini ili kutii sheria ya Yehova ya kuepuka uasherati?

6 Tunatii sheria ya Yehova ya kuepuka uasherati. (Ebr. 13:4) Mutume Paulo alitumia usemi wa mufano kwa kutushauria tuue viungo vya mwili wetu, ni kusema, kufanya yote yenye tunaweza ili kuepuka tamaa yoyote ya mubaya ya mwili. Tunaepuka kuangalia ao kufanya jambo yoyote yenye inaweza kutuchochea kufanya uasherati. (Kol. 3:5; Yob. 31:1) Tunakatala palepale mawazo yoyote ao matendo yoyote yenye inaweza kuharibisha urafiki wetu pamoya na Mungu wakati tunajaribiwa.

7. Tunapaswa kuazimia kufanya nini, na juu ya nini?

7 Yehova anatuomba tukuwe “watiifu kutoka katika moyo.” (Ro. 6:17) Kila mara muongozo wake unakuwaka muzuri, na hatuwezi kubadilisha sheria zake. (Isa. 48:17, 18; 1 Ko. 6:9, 10) Tunajikazaka kumufurahisha na kuwa na mutazamo sawa ule wa mwandikaji wa zaburi mwenye alisema hivi: “Nimeazimia kutii masharti yako nyakati zote, mupaka mwisho.” (Zb. 119:112) Lakini, Shetani atajaribu kuregeza azimio yetu. Anatumiaka mambo gani?

SHETANI ANATUMIAKA MAMBO GANI ILI KUREGEZA AZIMIO YETU?

8. Namna gani Shetani anatumiaka mateso ili kuregeza azimio yetu?

8 Mateso. Ibilisi anatumiaka jeuri na mikazo ili kuregeza imani yetu. Kusudi yake ni ‘kutumeza,’ ni kusema, kuharibisha urafiki wetu pamoya na Yehova. (1 Pe. 5:8) Mu karne ya kwanza, Wakristo waliogopeshwa, walipigwa, na kuuawa juu waliazimia kuwa imara. (Mdo. 5:27, 28, 40; 7:54-60) Shetani anaendelea kutesa watu leo. Tuko najionea ile mu namna wapinzani wako natesa ndugu na dada zetu mu Urusi na mu inchi zingine na namna wako natesa ndugu na dada zetu mu njia moya ao ingine.

9. Fasiria juu ya nini ni jambo ya maana kuwa waangalifu kuhusu mikazo yenye haiko wazi.

9 Mikazo yenye haiko wazi. Zaidi ya mateso, Shetani anatumiaka “matendo ya ujanja.” (Efe. 6:11) Tuzungumuzie mufano wa ndugu Bob mwenye alikuwa mu hopitale ili afanyiwe upasuaji mukubwa. Aliambia wanganga kama hawapaswe kumutia damu hata kutokee nini. Munganga mwenye alipaswa kumufanya upasuaji alikubaliana na uamuzi wake. Lakini, kisha familia ya Bod kurudia ku nyumba, munganga mwingine alikuya kumuona usiku mbele afanyiwe upasuaji. Alimuambia Bob kama wanganga hawatamutia damu, lakini wataitayarisha tu juu pengine anaweza kujikuta mu hali yenye itaomba atiwe damu. Inawezekana ule munganga aliwaza kama, vile familia ya Bob ilikuwa ilishaenda, pengine atabadilisha mawazo yake. Lakini Bob aliendelea kuwa imara, alisema kama hataitika wamutie damu hata kutokee nini.

10. Juu ya nini mawazo ya wanadamu wenye hawatii sheria ya Yehova iko hatari? (1 Wakorinto 3:19, 20)

10 Mawazo ya wanadamu wenye hawatii sheria za Yehova. Kama tunakuwa na mawazo sawa ya watu wenye hawamutii Yehova, siye pia tunaweza kumuacha Yehova na kuacha kutii sheria zake. (Soma 1 Wakorinto 3:19, 20.) Mara mingi “hekima ya ulimwengu huu” inachocheaka watu wasimutii Mungu. Wakristo fulani wa Pergamamu na Tiatira walichochewa na watu wenye waliishi nao wenye walikuwa waasherati na waabudu sanamu. Juu wale Wakristo waliachilia uasherati uendelee, Yesu aliwapatia mashauri mazito. (Ufu. 2:14, 20) Leo, watu wanaweza kufanya tukuwe na mawazo ya mubaya. Watu wa familia na marafiki wanaweza kutuambia kama tuko wenye kushikamana kupita kiasi na mambo yenye tunaamini na wanaweza kutuambia tuvunje sheria za Yehova. Kwa mufano, wanaweza kusema kama haiko jambo ya maana kuendelea kuwa na mwenedo safi na kama kanuni zenye kuwa mu Biblia kuhusu mwenendo ni mambo ya zamani.

11. Wakati tunaendelea kuwa imara, tunapaswa kuepuka nini?

11 Wakati fulani tunaweza kuwaza kama maagizo yenye Yehova anatupatiaka haieleweke. Tunaweza hata kujaribiwa kuongeza mambo yenye ‘kupita mambo yenye yaliandikwa.’ (1 Ko. 4:6) Viongozi wa dini wa wakati wa Yesu walikuwa nafanya ile zambi. Walikuwa naongeza sheria zao ku Sheria ya Mungu, na waliifanya ikuwe nguvu sana kwa watu wa kawaida kuitii. (Mt. 23:4) Yehova anatupatiaka maagizo yenye kuwa wazi kupitia Neno yake na tengenezo yake. Hatuna lazima ya kuongeza mambo ingine ku ile maagizo. (Mez. 3:5-7) Kwa hiyo, hatupaswe kupita mambo yenye yaliandikwa mu Biblia ao kuwekea waamini wenzetu sheria kuhusu mambo yenye Biblia haizungumuzie.

12. Namna gani Shetani anatumiaka “udanganyifu wa bure”?

12 Udanganyifu. Shetani anatumiaka “udanganyifu wa bure” na “mambo ya musingi ya ulimwengu” ili kupotosha watu na kuwagawanya. (Kol. 2:8) Mu karne ya kwanza, ile ilitia ndani filozofia zenye kutegemea mawazo ya wanadamu, mafundisho ya Wayahudi yenye haikutegemea Maandiko, na fundisho ya kama Wakristo wanapaswa kufuata Sheria ya Musa. Ile yote ilidanganya watu juu ilifanya wasimukazie Yehova uangalifu, mwenye ni Chanzo ya hekima. Leo, Shetani iko natumia vyombo vya habari na site za Enternete za kupashana habari ili kueneza habari na ripoti za uongo zenye viongozi wa politike wako naeneza. Tulijionea ile mu kipindi ya ugonjwa wa korona. c Mashahidi wa Yehova wenye walifuata maagizo yenye tengenezo yetu ilitoa, hawakuhangaika kupita kiasi sawa vile wale wenye walisikiliza habari za uongo.​—Mt. 24:45.

13. Juu ya nini tunapaswa kuwa waangalifu ili tusikengeushwe?

13 Mambo ya kukengeusha. Hatupaswe kusahau “mambo ya maana zaidi.” (Flp. 1:9, 10) Mambo ya kukengeusha inaweza kutukamata wakati na nguvu mingi na inaweza kufanya tusahau mambo yenye inaweza kutusaidia zaidi. Mambo yenye tunafanyaka kila siku, sawa vile kula, kunywa, kujifurahisha, na kazi ya kimwili inaweza kutukengeusha kama tuko naiona kuwa njo mambo ya maana zaidi mu maisha yetu. (Lu. 21:34, 35) Zaidi ya ile, kila siku tunasikiaka ao kusoma habari juu ya ugomvi kati ya watu na mambo ya politike. Ile mambo haipaswe kutukengeusha. Kama tunaifuatilia, tunaweza kuanza kutegemeza upande moya ao upande ingine ya politike mu akili na mu moyo wetu. Shetani anatumiaka ile mambo yote yenye tunatoka kuzungumuzia ili kuregeza azimio yetu ya kufanya mambo ya muzuri. Tuzungumuzie sasa mambo yenye tunaweza kufanya ili kumupinga na kuendelea kuwa imara.

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI TUENDELEE KUWA IMARA?

Juu ukuwe imara, ukumbuke juu ya nini ulitoa maisha yako kwa Yehova na kubatizwa, usome Neno ya Mungu na kuitafakari, ukuwe na moyo wenye kuwa imara, na umutegemee Yehova (Ona fungu ya 14-18)

14. Ni jambo gani moya yenye inaweza kukusaidia uendelee kumutii Yehova?

14 Ukumbuke juu ya nini ulimutolea Yehova maisha yako na kubatizwa. Ulifanya vile juu ulipenda kubakia upande wake. Kumbuka mambo yenye ilikusaidia ukuwe hakika kama ulipata kweli. Ulifikia kumujua Yehova na kuanza kumuheshimia na kumupenda na kumuona kuwa baba yako wa mbinguni. Ulionyesha imani na ilikuchochea utubu. Uliacha kufanya mambo yenye Yehova anachukia na ulianza kufanya mambo yenye inamufurahisha. Ulifikia kujisikia muzuri zaidi wakati ulitambua kama Mungu alishakusamehe. (Zb. 32:1, 2) Ulianza kuenda ku mikutano ya Kikristo na ulianza kuambia watu wengine mambo ya muzuri yenye ulijifunza. Juu ulishajitoa kwa Yehova na kuwa Mukristo mwenye kubatizwa, uko natembea mu njia ya uzima na utafanya yako yote ili uendelee kutembea mu ile njia.​—Mt. 7:13, 14.

15. Juu ya nini ni jambo ya lazima kujifunza na kutafakari?

15 Ujifunze Neno ya Mungu na kuitafakari. Muti unaweza kusimama imara kama mizizi yake ilishaingia sana mu udongo. Vilevile, kama tuko na imani ya nguvu katika Yehova, tutaendelea kusimama imara. Wakati muti uko nakomala, mizizi yake inaingiaka mu udongo na inaendaka mbali zaidi. Wakati tunajifunza na kutafakari, imani yetu inakuwa nguvu na tunakuwa hakika zaidi kama njia za Mungu njo za muzuri sana. (Kol. 2:6, 7) Kufikiri juu ya maagizo, mashauri, na ulinzi wa Yehova kulisaidia watumishi wake wa zamani. Kwa mufano, Ezekieli alikaza uangalifu wake kwa malaika mwenye alikuwa napima kwa uangalifu hekalu yenye alionaka mu maono. Ile maono ilimupatia Ezekieli nguvu na inatufundisha mambo fulani juu ya namna tunaweza kutii kanuni za Yehova juu ya ibada safi. d (Eze. 40:1-4; 43:10-12) Na siye tunaweza kupata faida kama tunakamata wakati wa kujifunza na kutafakari juu ya mambo mazito yenye kuwa mu Neno ya Mungu.

16. Kuwa na moyo wenye kuwa imara kulimusaidia Bob namna gani? (Zb. 112:7)

16 Ukuwe na moyo wenye kuwa imara. Mufalme Daudi alisema kama hawezi hata kidogo kuacha kumupenda Yehova. Aliimba hivi: “Ee Mungu, moyo wangu uko imara.” (Zb. 57:7) Siye pia tunaweza kuwa na moyo wenye kuwa imara na kumutegemea kabisa Yehova. (Soma Zaburi 112:7.) Fikiria namna ile ilimusaidia Bob mwenye tulishazungumuzia. Wakati munganga moya alimuambia kama wanganga watatayarisha tu damu juu pengine anaweza kujikuta mu hali yenye itaomba atiwe damu, palepale alisema kama, ikiwa inakuwa vile, atatoka tu mara moya mu hopitale. Kisha Bob alisema hivi: “Sikukuwa na mashaka juu ya mambo yenye ningefanya na sikuogopa mambo yenye pengine ingetokea.”

Kama tuko na imani ya nguvu, tutaendelea kuwa imara hata kama tunapata majaribu ya namna gani (Ona fungu ya 17)

17. Mufano wa Bob unaweza kutufundisha nini? (Ona pia picha.)

17 Bob alikuwa imara juu alikuwaka alishaamua kubakia imara mbele hata aende ku hopitale. Kwanza, alipenda sana kumufurahisha Yehova. Pili, alijifunza kwa uangalifu mambo yenye Biblia na vichapo vyenye kutegemea Biblia vinasema kuhusu namna Mungu anaona uzima na damu kuwa takatifu. Tatu, alikuwa hakika kama kufuata muongozo wa Yehova kutamuletea faida za milele. Siye pia, tunaweza kuwa na moyo wenye kuwa imara hata kama tunapata majaribu ya namna gani.

Baraka na wanaume wake wanafuatilia jeshi ya Sisera kwa uhodari (Ona habari ya kujifunza ya 31, fungu ya 18)

18. Mufano wa Baraka unatufundisha nini kuhusu kumutegemea Yehova? (Ona picha ku jalada.)

18 Umutegemee Yehova. Ona namna Baraka alipata ushidi juu alitegemea muongozo wa Yehova. Hata kama Waisraeli hawakukuwa na ngao wala mukuki, Yehova alimuambia Baraka aende kupigana na Sisera, mwenye alikuwa mukubwa wa jeshi ya Wakanaani, na jeshi yake, wenye walikuwa na silaha mingi kwa ajili ya vita. (Amu. 5:8) Nabii mwanamuke Debora alimupatia Baraka muongozo wa kuenda mu bonde ili kupigana na Sisera na jeshi yake yenye ilikuwa na magari ya vita 900. Mu ile bonde, ingekuwa nguvu kwa Waisraeli kupigana na ile jeshi juu ile magari ya vita ilikuwa nakimbia sana. Hata kama Baraka alijua vile, alitii. Wakati maaskari walikuwa nashuka Mulima Tabori, Yehova alinyeshesha mvula kubwa sana. Magari ya Sisera ilianza kuzama mu matope na Yehova alimupatia Baraka ushindi. (Amu. 4:1-7, 10, 13-16) Vilevile, Yehova atatupatia ushindi kama tunamutegemea na kama tunategemea muongozo wenye anatupatia kupitia wale wenye kumuwakilisha.​—Kum. 31:6.

ENDELEA KUWA IMARA

19. Juu ya nini unapenda kuendelea kuwa imara?

19 Tunapaswa kujikaza ili tuendelee kuwa imara juu tunaishi mu hii dunia. (1 Ti. 6:11, 12; 2 Pe. 3:17) Kwa hiyo basi, tusiache mateso, mikazo yenye haiko wazi, mawazo ya wanadamu wenye hawatii sheria ya Mungu, udanganyifu, na mambo ya kukengeusha itutetemeshe. (Efe. 4:14) Tuendelee kuwa imara, tumuabudu Yehova tu, na tuendelee kumupenda na kumutii. Lakini, wakati tuko nafanya vile, tunapaswa kuwa na usawaziko. Mu habari yenye kufuata, tutaona namna gani Yehova na Yesu wako mifano ya muzuri sana ya usawaziko.

WIMBO 129 Tutaendelea Kuvumilia

a Kuanzia wakati wa Adamu na Eva, Shetani anaendelea kufanya watu waamini kama wanapaswa kujiamulia wao wenyewe mambo ya muzuri na ya mubaya. Anapenda na siye tukuwe na ule mutazamo kuhusu sheria za Yehova na maagizo yoyote yenye tengenezo yake iko natupatia. Hii habari, itatusaidia tujilinde na roho ya mu hii ulimwengu yenye kutawaliwa na Shetani ya kupenda kujiamulia mambo ya kufanya. Itatusaidia pia tuazimie kumutii Yehova sikuzote.

b Ili kupata habari zaidi juu ya namna Mukristo anaweza kutii sheria ya Mungu kuhusu damu, ona somo ya 39 ya kitabu Furahia Maisha Milele!

c Ona ku jw.org habari “Jilinde Dhidi ya Habari za Uwongo.”