Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Ya Kujifunza

Namna Ya Kujifunza

Ni Mambo Gani Yenye Unapaswa Kujifunza Kwanza?

Siye wote hatupatake wakati mingi ya kufanya funzo ya pekee. Kwa hiyo, tunaweza kufanya nini juu tutumie muzuri sana wakati kidogo wenye tunapataka? Kwanza, upitishe wakati wa kutosha mu mambo yenye uko nasoma. Bila shaka, kama unasoma mambo kidogo kwa uangalifu utapata faida zaidi kuliko kusoma mambo mingi mbiombio.

Pili, upange mambo yenye unapaswa kujifunza kwanza. (Efe. 5:15, 16) Fikiria hii mapendekezo:

  • Usome Biblia kila siku. (Zb. 1:2) Ni muzuri zaidi kuanza na usomaji wa Biblia wenye kupangwa kwa ajili ya mukutano wa katikati ya juma.

  • Utayarishe funzo ya Munara wa Mulinzi na mukutano wa katikati ya juma. Ukuwe tayari kutoa maelezo.—Zb. 22:22.

  • Tafazali, ujikaze pia kusoma vichapo, sawa vile magazeti ya watu wote, habari zingine zenye zinatolewaka ku jw.org, na pia kuangalia video mbalimbali.

  • Ufanye utafiti. Unaweza kufanya utafiti juu ya magumu fulani yenye uko napambana nayo, ulizo fulani yenye uko nayo, ao habari fulani yenye kuwa mu Biblia yenye unapenda kuelewa muzuri zaidi. Juu upate mawazo zaidi, uende ku sehemu “Mazoezi ya Kujifunza Habari za Biblia” ku jw.org.