Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 29

Uko Tayari Kwa Ajili ya Taabu Kubwa?

Uko Tayari Kwa Ajili ya Taabu Kubwa?

“Mukuwe tayari.”​—MT. 24:44.

WIMBO 150 Umutafute Mungu ili Akukomboe

KIFUPI YA HABARI a

1. Juu ya nini ni jambo ya hekima kujitayarisha kwa ajili ya misiba?

 KUJITAYARISHA muzuri kunaweza kuokoa uzima. Kwa mufano, kama mutu alishajitayarisha mbele musiba utokee, inaweza kuwa mwepesi kwake kuokoka na kusaidia wengine. Shirika fulani ya mu Ulaya yenye inasaidiaka watu inasemaka hivi: “Kujitayarisha muzuri kunaweza kuokoa uzima.”

2. Juu ya nini tunapaswa kujitayarisha kwa ajili ya taabu kubwa? (Matayo 24:44)

2 “Taabu kubwa” itaanza kwa kushitukia. (Mt. 24:21) Lakini, ile taabu itakuwa tofauti na misiba ingine mingi juu siye tunajua kama iko nakuya. Kumepita miaka 2000 hivi, tangu Yesu aambie wanafunzi wake wajitayarishe kwa ajili ya ile siku. (Soma Matayo 24:44.) Kama tunajitayarisha, itakuwa mwepesi kwetu kuvumilia ile kipindi ya nguvu na kusaidia pia wengine wafanye vile.​—Lu. 21:36.

3. Juu ya nini tutakuwa na lazima ya uvumilivu, huruma, na upendo wakati wa taabu kubwa?

3 Tuzungumuzie sifa tatu zenye zinaweza kutusaidia kuwa tayari kwa ajili ya taabu kubwa. Tutafanya nini kama wanatuambia tutangaze ujumbe mukali wa hukumu na wakati uleule watu wenye hawaamini wanatupinga? (Ufu. 16:21) Tutakuwa na lazima ya uvumilivu ili kumutii Yehova na kutumainia kama atatulinda. Tutafanya nini kama ndugu zetu wanapoteza vitu fulani ao vitu vyao vyote vya kimwili? (Hab. 3:17, 18) Sifa ya huruma itatuchochea tuwasaidie. Tutafanya nini kama muungano wa mataifa unatushambulia na tunalazimika kuishi pamoya na ndugu na dada zetu wengi kwa wakati fulani? (Eze. 38:10-12) Upendo mukubwa utatusaidia kuvumilia ile kipindi ya nguvu.

4. Biblia inasema nini yenye inaonyesha kama tunapaswa kuendelea kukomalisha sifa ya uvumilivu, huruma, na upendo?

4 Neno ya Mungu inatutia moyo tuendelee kukomalisha sifa ya uvumilivu, huruma, na upendo. Luka 21:19 inasema hivi: “Kupitia uvumilivu wenu mutaokoa uzima wenu.” Wakolosai 3:12 inasema hivi: “Muvae . . . huruma.” Na 1 Watesalonike 4:9, 10 inasema hivi: “Ninyi wenyewe mumefundishwa na Mungu kupendana. . . . Lakini, tunawachochea ninyi, ndugu, muendelee kufanya vile kwa ukamili zaidi.” Wanafunzi wenye tayari walikuwa walishaonyesha sifa ya uvumilivu, huruma, na upendo njo waliambiwa ile maneno. Lakini, walipaswa kuendelea kukomalisha zile sifa. Tunapaswa kufanya pia vile. Juu tuweze, tuzungumuzie namna Wakristo wa kwanza-kwanza walionyesha zile sifa. Kisha, tutaona namna tunaweza kuwaiga na namna tunaweza kuonyesha kama tuko tayari kwa ajili ya taabu kubwa.

UKOMALISHE SIFA YA UVUMILIVU

5. Nini njo ilisaidia Wakristo wa kwanza-kwanza wavumilie magumu?

5 Wakristo wa kwanza-kwanza walipaswa kuwa na uvumilivu. (Ebr. 10:36) Zaidi tu ya magumu ya kawaida yenye walikuwa napambana nayo sawa tu vile watu wengine, walipata pia magumu ingine. Wengi kati yao waliteswa, hapana tu na Viongozi wa dini ya Wayahudi na Waroma wenye walikuwa na mamlaka, lakini pia na watu wa familia zao. (Mt. 10:21) Wakati fulani, hata mu kutaniko walipaswa pia kuwa waangalifu ili wasipotoshwe na mafundisho ya uongo ya waasi-imani yenye kuleta migawanyiko. (Mdo. 20:29, 30) Hata vile, wale Wakristo walivumilia. (Ufu. 2:3) Nini njo iliwasaidia? Walifikiri sana juu ya mifano yenye kuwa mu Biblia ya watu wenye walionyesha uvumilivu, sawa vile mufano wa Yobu. (Yak. 5:10, 11) Walimuomba Yehova awapatie nguvu. (Mdo. 4:29-31) Na waliendelea kukumbuka kama Yehova angewabariki kama wanavumilia.​—Mdo. 5:41.

6. Mambo yenye Merita alifanya juu ya kuvumilia upinzani inakufundisha nini?

6 Kila mara kama tunajifunza mifano ya watu wenye walivumilia, yenye kuwa mu Neno ya Mungu na mu vichapo vyetu na kuifikiria sana, tunaweza pia kuvumilia. Ile njo ilisaidia Merita, dada wa mu Albania, avumilie upinzani mukubwa wenye ulikuwa mu familia yake. Anasema hivi: “Habari ya Yobu yenye kuwa mu Biblia ilinitia moyo sana. Alitesekaka sana. Hata kama hakujua mwenye alifanyaka apate ile magumu, alisemaka hivi: ‘Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!’ (Yob. 27:5) Niliona kama magumu ya Yobu ilikuwa ya nguvu zaidi kupita yangu. Tofauti na yeye, miye nilijua nani njo alikuwa nafanya niteseke.”

7. Hata kama hatuna magumu ya nguvu, tunapaswa kujifunza kufanya nini sasa?

7 Tunaweza pia kukomalisha sifa ya uvumilivu kwa kumuambia Yehova kwa ukawaida mambo yenye iko natuhangaisha. (Flp. 4:6; 1 Te. 5:17) Pengine kwa sasa hauna magumu ya nguvu sana. Hata vile, Je, unamuombaka Yehova akuongoze kila mara wakati unapata magumu, unahangaika, na haujue ufanye nini? Kama unamuombaka Yehova akusaidie saa unapata magumu ya kidogo-kidogo leo, itakuwa mwepesi kwako kufanya vile wakati utapata magumu ya nguvu wakati wenye kuya. Kisha, utakuwa hakika kama anajua kabisa wakati na namna ya kukusaidia.​—Zb. 27:1, 3.

UVUMILIVU

Kama tuko navumilia magumu leo, itakuwa mwepesi kwetu kuvumilia magumu ingine yenye tunaweza kupata (Ona fungu ya 8)

8. Namna gani mufano wa Mira unaonyesha kama kuvumilia magumu leo kunaweza kutusaidia kuvumilia magumu wakati wenye kuya? (Yakobo 1:2-4) (Ona pia picha.)

8 Itakuwa mwepesi sana kwetu kuvumilia taabu kubwa kama tuko navumilia magumu leo. (Ro. 5:3) Juu ya nini tunasema vile? Ndugu na dada wengi wanasemaka kama kila wakati wenye wanavumilia hali ya nguvu, ile inawasaidiaka wakuwe tayari kuvumilia magumu ingine yenye wanaweza kupata. Wakati wanavumilia magumu kwa musaada wa Yehova, ile inafanya wakuwe na imani kama anapenda kuwasaidia. Na ile imani ya nguvu itawasaidia wavumilie magumu ingine yenye wanaweza kupata. (Soma Yakobo 1:2-4.) Mira, painia wa mu Albania, alifikia kuona kama juu alivumiliaka magumu zamani, ile inamusaidia aendelee kuvumilia magumu yenye iko nayo leo. Anasema kama wakati fulani alikuwa nawaza kuwa yeye tu njo alikuwa na magumu mingi. Lakini, kisha kukumbuka namna Yehova alimusaidia mu miaka 20 yenye ilipita, anajiambia hivi: ‘Endelea kuwa muaminifu. Usiache ile miaka yote na vita yote yenye umeweza kwa musaada wa Yehova ipite bure.’ Na weye pia unaweza kufikiria namna Yehova alishakusaidia ili uvumilie. Ukuwe hakika kama kila mara anaonaka wakati unavumilia magumu fulani na kama atakubariki. (Mt. 5:10-12) Na wakati taabu kubwa itaanza, utakuwa ulishajifunza namna ya kuvumilia na utaazimia kuendelea kuvumilia.

UKOMALISHE SIFA YA HURUMA

9. Wakristo wa Antiokia ya Siria walifanya nini ili kuonyesha huruma?

9 Fikiria mambo yenye ilitokea wakati Wakristo wa mu Yudea walipigwa na njala kali. Kisha tu ndugu na dada wa mu kutaniko ya Antiokia ya Siria kusikia ile habari, bila shaka walisikilia huruma ndugu zao wa mu Yudea. Kwa hiyo, walifanya jambo fulani ili kuwasaidia. “Wakaamua, kila mumoja kulingana na uwezo wake, kutuma misaada kwa ndugu wenye kuishi Yudea.” (Mdo. 11:27-30) Hata kama wale ndugu na dada wenye walipigwa na njala walikuwa naishi mbali, Wakristo wa Antiokia waliazimia kuwasaidia.​—1 Yo. 3:17, 18.

HURUMA

Tunapata nafasi ya kuonyesha wengine huruma wakati wanapatwa na misiba ya asili (Ona fungu ya 10)

10. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunasikilia huruma waabudu wenzetu wenye wamepatwa na misiba? (Ona pia picha.)

10 Leo, siye pia tunaweza kuonyesha huruma wakati tunasikia kama waabudu wenzetu wamepatwa na misiba. Tunaweza kuonyesha kama tuko tayari kufanya vile kwa kuambia wazee kama tunapenda kusaidia mu kazi fulani, kwa kutoa michango juu ya kutegemeza kazi ya mu dunia yote, ao kwa kusali kwa ajili ya wale ndugu wenye wamepatwa na misiba. b (Mez. 17:17) Kwa mufano, mu 2020, Halmashauri za Kutoa Misaada zaidi ya 950 ziliwekwa mu dunia yote ili kusaidia wale wenye walikuwa na lazima ya musaada wakati wa ugonjwa wa korona. Tunashukuru sana ndugu na dada wenye walijitoa mu ile kazi ya kutolea ndugu misaada. Juu walisikilia ndugu zao huruma, waliwatolea vitu vya kimwili, waliwahangaikia kiroho, na mu hali fulani walitengeneza ao kujenga upya nyumba zao na fasi zao za ibada.​—Linganisha na 2 Wakorinto 8:1-4.

11. Namna gani matendo yetu ya huruma inamuleteaka Baba yetu wa mbinguni heshima?

11 Watu wanaonaka namna tunajitoleaka ili kuonyesha huruma wale wenye kupatwa na misiba. Kwa mufano, mu 2019, upepo mukali wenye kuitwa Dorian uliharibisha Jumba ya Ufalme mu Bahamas. Wakati ndugu zetu walikuwa najenga upya ile Jumba, waliomba fundi moya mujenzi mwenye hakukuwa Shahidi awaambie kama itaomba makuta ngapi juu afanye ile kazi. Aliwaambia hivi: “Nitawapatia . . . vifaa ili muvitumikishe bila kulipa, na vyombo. . . . Napenda tu kufanya vile kwa ajili ya tengenezo yenu. Kuona vile munahangaikiaka marafiki wenu kunanigusaka sana.” Watu wengi sana hawamujue Yehova. Lakini wengi kati yao wanaonaka mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanafanyiaka wengine. Ni pendeleo kubwa kujua kama matendo yetu ya huruma inaweza kuvuta watu kwa Mungu mwenye ni “tajiri katika rehema”!​—Efe. 2:4.

12. Namna gani kuonyesha huruma leo kunatutayarisha kwa ajili ya taabu kubwa? (Ufunuo 13:16, 17)

12 Juu ya nini itaomba tuonyeshe huruma wakati wa taabu kubwa? Biblia inaonyesha kama wale wenye hawataunga mukono serikali za hii dunia watapata magumu sasa na wakati wa taabu kubwa. (Soma Ufunuo 13:16, 17.) Pengine ndugu na dada zetu watakuwa na lazima ya musaada ili kupata mambo yenye wako nayo lazima juu waokoke. Wakati Kristo Yesu, Mufalme wetu, atakuya kuhukumu watu, ni muzuri atukute tayari tuko naonyesha huruma na atuambie hivi: Mukuye ‘muriti Ufalme.’​—Mt. 25:34-40.

UPENDE NDUGU NA DADA ZAKO ZAIDI

13. Sawa vile Waroma 15:7 inaonyesha, Wakristo wa kwanza-kwanza walifanya nini juu wapendane zaidi?

13 Upendo njo alama yenye ilitambulisha Wakristo wa kwanza-kwanza. Lakini ilikuwa mwepesi kwao kuonyesha ile sifa? Tuzungumuzie watu mbalimbali wenye walikuwa mu kutaniko ya Roma. Wamoja walikuwa Wayahudi wenye walifundishwa namna ya kutii Sheria ya Musa, lakini wengine walitoka mu mataifa ingine na walikuwa na desturi tofauti. Pengine Wakristo fulani walikuwa watumwa na wengine walikuwa huru, pengine wamoja walikuwa hata mabwana wa watumwa. Namna gani wale Wakristo wangepiganisha mambo yenye ilifanya wakuwe tofauti na wangefanya nini ile wapendane zaidi? Mutume Paulo aliwatia moyo ‘wakaribishane.’ (Soma Waroma 15:7.) Alipenda kusema nini? Neno yenye kutafsiriwa “mukaribishane” inamaanisha kupokea mutu muzuri ao kumuonyesha ukarimu, sawa vile kumupokea mu nyumba fulani ao mu kikundi ya marafiki. Kwa mufano, Mutume Paulo alimuambia Filemoni namna ya kumukaribisha mutumwa Onesimo, alimuambia hivi: “Umupokee muzuri.” (Flm. 17) Na Prisila na Akila walimukaribisha Apolo, mwenye hakujua mambo mingi kuhusu Wakristo sawa vile wao, na ‘walimuchukua’ na kuenda naye. (Mdo. 18:26) Kuliko kuacha tofauti yenye ilikuwa kati yao iwatenganishe, wale Wakristo walikaribishana.

UPENDO

Tunapenda ndugu na dada zetu wote watupende (Ona fungu ya 15)

14. Anna na bwana yake walifanya nini ili kuonyesha kama walipenda wengine?

14 Na siye tunaweza kuonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu kwa kuwakaribisha mu kikundi yetu ya marafiki. Mara mingi, ile itafanya wao pia watupende. (2 Ko. 6:11-13) Fikiria mufano wa Anna na bwana yake, wenye walikuwa wamisionere. Kisha kuhamia mu Afrika ya Mangaribi mu mugao wao wa mupya, ugonjwa wa korona ulianza. Juu ya ule ugonjwa, hawakukuwa nakutana na ndugu na dada zao na haikukuwa mwepesi kwao kuwajua. Sasa walifanya nini ili kuonyesha kama walipenda ndugu na dada zao? Walitumia vidéoconférence ili kuongea nao na waliwaambia kama wanapenda kuwajua muzuri zaidi. Familia za wale ndugu na dada ziliguswa sana, na mara mingi walianza kuwaita na kuwatumia ujumbe. Juu ya nini wale wamisionere walijikaza sana kujua ndugu na dada zao? Anna anasema hivi: “Siwezi kusahau upendo wenye ndugu na dada walituonyesha miye na familia yangu mu wakati ya mubaya na mu wakati ya muzuri, mifano yao imenichochea nionyeshe wengine upendo.”

15. Mufano wa Vanessa unatufundisha nini kuhusu kupenda ndugu na dada wote? (Ona pia picha.)

15 Wengi kati yetu wako mu makutaniko mwenye muko ndugu na dada wa desturi na hali tofauti ya maisha na wenye kuwa na utu mbalimbali. Tunaweza kuwapenda zaidi kwa kukazia uangalifu sifa zao za muzuri. Dada Vanessa, mwenye kutumikia mu Nouvelle-Zélande, aliona kama ni nguvu kuwa na uhusiano wa muzuri pamoya na watu fulani mu kutaniko yao. Lakini, kuliko kuepuka wale wenye walikuwa na utu wa kumukasirisha, aliamua kupitisha wakati mingi pamoya nao. Ile ilimusaidia aone mambo yenye Yehova anapendaka kwao. Anasema hivi: “Tangu bwana yangu akuwe mwangalizi wa muzunguko, tunapitishaka wakati mingi pamoya na ndugu na dada wenye kuwa na utu mbalimbali, na ile inafanyaka ikuwe mwepesi kwangu kuwakaribia. Kwa sasa napenda watu wenye kuwa na utu tofauti. Ni wazi kama Yehova pia anapendaka watu wa utu tofauti juu yeye njo alituvuta mu ile kikundi.” Wakati tunajikaza kuona wengine sawa vile Yehova anawaona, tunaonyesha kama tunawapenda.​—2 Ko. 8:24.

Wakati wa taabu kubwa, tutapata ulinzi wenye Yehova anatuahidi kama tunaendelea kuungana na waamini wenzetu (Ona fungu ya 16)

16. Juu ya nini upendo utakuwa wa maana sana wakati wa taabu kubwa? (Ona pia picha.)

16 Upendo utakuwa wa maana sana wakati wa taabu kubwa. Wakati ile taabu kubwa itaanza, wapi njo tutapata ulinzi? Fikiria mambo yenye Yehova aliomba watu wake wafanye wakati Babiloni ya zamani ilishambuliwa. Aliwaambia hivi: “Muende, watu wangu, muingie katika vyumba vyenu vya ndani, na mufunge milango nyuma yenu. Mujifiche kwa wakati mufupi mupaka kasirani kali ipite.” (Isa. 26:20) Inaonekana ile maneno inatuhusu siye pia wenye tutapambana na taabu kubwa. ‘Vyumba vya ndani’ vinaweza kumaanisha makutaniko. Wakati wa taabu kubwa, tutapata ulinzi wenye Yehova anatuahidi kama tunaendelea kuungana na waamini wenzetu. Njo maana, kwa sasa, tunapaswa kujikaza sana kuvumilia ndugu na dada zetu lakini pia kuwapenda. Ile njo inaweza kufanya tuokoke!

UJITAYARISHE KUANZIA SASA

17. Ikiwa tunajitayarisha sasa, tutaweza kufanya nini wakati wa taabu kubwa?

17 “Ile siku kubwa ya Yehova” itakuwa kipindi ya nguvu sana kwa wanadamu wote. (Sef. 1:14, 15) Watu wa Yehova watakuwa pia na magumu. Lakini, kama tunajitayarisha sasa, tutakuwa wenye kutulia na tutasaidia wengine. Tutavumilia magumu yote yenye tutakutana nayo. Wakati ndugu na dada zetu wanateseka, tutafanya yote yenye tunaweza ili kuwasaidia kwa kuwaonyesha huruma na kuwatolea musaada wenye wako nayo lazima. Na kama tunajifunza kupenda ndugu na dada zetu leo, tutaendelea kuwapenda hata wakati wenye kuya. Na ku mwisho, Yehova atatubariki kwa kutupatia uzima wa milele ku dunia kwenye misiba yote na taabu yote itakuwa ilishasahauliwa.​—Isa. 65:17.

WIMBO 144 Kaza Macho ku Zawadi!

a Hivi karibuni taabu kubwa itaanza. Sifa ya uvumilivu, huruma, na upendo njo itatusaidia kuwa tayari kwa ajili ya matukio yenye haiyatokeaka tangu kuumbwa kwa dunia. Tutaona namna Wakristo wa kwanza-kwanza walikomalisha zile sifa, namna tunaweza kufanya pia vile, na namna zitatusaidia ili kujitayarisha kwa ajili ya taabu kubwa.

b Wale wenye wanapenda kusaidia mu kazi ya kutoa misaada wanapaswa kwanza kujaza fomu Demande d’admission comme volontaire local de développement-construction (DC-50) ao Demande d’admission comme volontaire (A-19) na kungoya wakati wenye wataalikwa ili kusaidia mu ile kazi.