Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 32

Umuige Yehova kwa Kuwa na Usawaziko

Umuige Yehova kwa Kuwa na Usawaziko

“Usawaziko wenu ujulikane kwa watu wote.”​—FLP. 4:5.

WIMBO 89 Tii juu Ubarikiwe

KIFUPI YA HABARI a

Unapenda kuwa muti wa namna gani? (Ona fungu ya 1)

1. Ni mu njia gani Wakristo wanapaswa kuwa sawa vile muti? (Ona pia picha.)

 “UPEPO hauangushake muti wenye unaweza kukunjama.” Ile maneno inaonyesha kama juu muti usianguke wakati kunakuwa upepo wa nguvu, unapaswa kuwa wa kukunjama ao wa kujipatanisha na hali. Juu hali yetu ya kiroho iendelee kuwa muzuri, siye Wakristo tunapaswa pia kujipatanisha na hali wakati kunakuwa mabadiliko fulani ya nguvu mu maisha yetu. Namna gani? Tunapaswa kuwa na usawaziko kwa kujipatanisha na hali wakati kunakuwa mabadiliko fulani na kwa kuheshimia mawazo na maamuzi ya wengine.

2. Ni sifa gani zenye zitatusaidia tujipatanishe na hali, na tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Juu tuko watumishi wa Yehova, tunapenda kuwa na usawaziko. Tunapenda pia kuwa na unyenyekevu na huruma. Mu hii habari, tutazungumuzia namna zile sifa zilisaidiaka Wakristo fulani wajipatanishe na hali. Tutaona pia namna zile sifa zinaweza kutusaidia. Lakini, tuzungumuzie kwanza namna Yehova na Yesu wako mifano ya muzuri sana ya usawaziko.

YEHOVA NA YESU WAKO NA USAWAZIKO

3. Nini njo inaonyesha kama Yehova iko na usawaziko?

3 Yehova anaitwa “Mwamba” juu iko imara, ni kusema, hatikisike. (Kum. 32:4) Lakini, iko pia na usawaziko. Juu mambo mu hii dunia iko nabadilika, anaendelea kujipatanisha na hali ili kutimiza kusudi yake. Yehova alituumba kwa mufano wake. Njo maana alitupatia pia uwezo wa kujipatanisha na hali. Mu Biblia muko kanuni zenye zinaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya hekima hata tupate magumu gani. Juu Yehova yeye mwenyewe anatuwekea mufano na juu anatupatia kanuni zenye kuwa mu Biblia, ile inatusaidia kujua kama yeye ni “Mwamba,” na kama iko pia na usawaziko.

4. Zungumuzia mufano wenye unaonyesha kama Yehova iko na usawaziko. (Mambo ya Walawi 5:7, 11)

4 Njia za Yehova ni kamilifu na zenye usawaziko. Haombake wanadamu mambo yenye inapita uwezo wao. Kwa mufano, fikiria namna alionyesha Waisraeli usawaziko. Hakuomba matajiri na maskini wamutolee zabihu ileile. Mu hali fulani, aliomba kila mutu amutolee zabihu kulingana na hali yake.​—Soma Mambo ya Walawi 5:7, 11.

5. Zungumuzia mufano wenye unaonyesha kama Yehova ni munyenyekevu na mwenye huruma.

5 Unyenyekevu na huruma inafanyaka Yehova akuwe na usawaziko. Kwa mufano, Yehova alionyesha kama ni munyenyekevu wakati alikuwa karibu kuharibu watu waovu wenye waliishi mu Sodoma. Alituma malaika wamuambie Loti mwenye haki akimbilie mu maeneo ya milima. Loti aliogopa kuenda kule. Njo maana alimuomba sana Yehova aruhusu yeye na familia yake wakimbilie Soari, muji mudogo wenye Yehova alipangaka pia kuharibu. Yehova angemuambia tu Loti aende kule kwenye alikuwa namuambia aende. Lakini, alimuruhusu aende Soari, na hakuharibu tena ule muji. (Mwa. 19:18-22) Karne mingi kisha, Yehova aliwasikilia huruma wakaaji wa Ninawi. Alituma nabii Yona aambie watu waovu wa mu Ninawi kama atawaharibu na kama ataharibu pia muji wao. Lakini wakati watu wa Ninawi walitubu, Yehova aliwasikilia huruma na hakuharibu tena ule muji.​—Yon. 3:1, 10; 4:10, 11.

6. Zungumuzia mifano fulani yenye inaonyesha namna Yesu alimuiga Yehova kwa kuwa na usawaziko.

6 Yesu alimuiga Yehova kwa kuwa na usawaziko. Alitumwa hapa ku dunia ili kuhubiria “kondoo wenye kupotea wa nyumba ya Israeli.” Lakini, alionyesha kama alikuwa na usawaziko wakati alikuwa natimiza ule mugao. Siku moya, mwanamuke fulani mwenye hakukuwa Mwisraeli alimuomba aponyeshe mutoto wake mwanamuke mwenye alikuwa “anasumbuliwa sana na pepo muchafu.” Yesu alimusikilia huruma ule mwanamuke na aliponyesha mutoto wake. (Mt. 15:21-28) Fikiria mufano ingine. Ku mwanzo wa utumishi wake, Yesu alisema hivi: “Kila mutu mwenye ananikana . . . , mimi pia nitamukana.” (Mt. 10:33) Je, Yesu alimukana Petro, mwenye alimukanaka mara tatu? Hapana. Alijua kama Petro alitubu kikweli na alikuwa muaminifu. Kisha kufufuliwa, Yesu alimutokea Petro na inawezakana kabisa alimuhakikishia kama alikuwa alishamusamehe na kama alimupenda.​—Lu. 24:33, 34.

7. Kulingana na Wafilipi 4:5, tunapenda watu watuone namna gani?

7 Tumeona kama Yehova Mungu na Yesu Kristo wako na usawaziko. Halafu siye? Yehova anatazamia tukuwe na usawaziko. (Soma Wafilipi 4:5.) Tafsiri fulani inatafsiri hivi ile andiko: “Ujiendeshe mu njia yenye itafanya wengine waone kama uko mutu mwenye usawaziko.” Ujiulize hivi: ‘Watu wananionaka kuwa mutu mwenye usawaziko, mwenye kujipatanisha na hali, na mwenye kuachilia mambo kwa kupenda? Ao wananionaka kuwa mutu mugumu, mukali, ao wa kichwa nguvu? Nakazaka wengine wafanye mambo vile tu napenda ikuwe? Ao nasikilizaka wengine na kufuata mawazo yao kama ni lazima?’ Kama tunaendelea kuwa na usawaziko, tutaonyesha kama tuko namuiga Yehova na Yesu. Tuzungumuzie hizi hali mbili zenye zinaomba mutu akuwe na usawaziko: Wakati hali inabadilika na wakati mawazo na maamuzi ya wengine iko tafauti na yetu.

UKUWE NA USAWAZIKO WAKATI HALI INABADILIKA

8. Nini njo inaweza kutusaidia tukuwe na usawaziko wakati hali inabadilika? (Ona pia maelezo ya chini.)

8 Tunapaswa kuwa na usawaziko wakati hali inabadilika mu maisha yetu. Ile mabadiliko inaweza kufanya tupate magumu yenye hatuyawaziaka hata kidogo. Kwa mufano tunaweza kugonjwa sana bila kutazamia, ao mabadiliko ya kiuchumi ao ya serikali yenye haitazamiwe fasi kwenye tunaishi, inaweza kufanya maisha yetu ikuwe nguvu sana. (Muh. 9:11; 1 Ko. 7:31) Inaweza pia kuwa nguvu kwetu wakati tengenezo inabadilisha mugao wetu wa utumishi. Hata hali ibadilike namna gani, unaweza kujipatanisha nayo kwa kufanya hii mambo ine: (1) Ukubali mabadiliko, (2) ufikirie mambo ya sasa hapana ya zamani, (3) ujikaze kuona mambo ya muzuri mu maisha yako na (4) usaidie wengine. b Tuzungumuzie namna ndugu na dada zetu walipata faida kwa kufanya ile mambo.

9. Bibi na bwana fulani wenye walikuwa wamisionere walifanya nini ili kupambana na magumu yenye walipata bila kutazamia?

9 Ukubali mabadiliko. Emanuele na Francesca walitumwa mu kazi ya umisionere mu inchi ya kigeni. Wakati tu walianza kujifunza luga ya mu ile inchi na kuanza kujuana na ndugu na dada wa mu kutaniko yao ya sasa, korona ilianza na walipaswa kujitenga na wengine. Kisha mama wa Francesca alikufa kwa kushitukia. Francesca alipenda kukuwa na familia yake, lakini ugonjwa wa korona ulimuzuia kufanya safari ya kuenda kuwaona. Nini njo ilimusaidia kupambana na ile magumu yote? Kwanza, Emanuele na Francesca walimuomba Yehova awapatie hekima ili wasihangaike sana. Yehova alijibia sala zao kwa wakati wenye kufaa kupitia tengenezo yake. Kwa mufano, maneno ya ndugu moya yenye kuwa mu video yenye walionaka iliwatiaka moyo sana. Ule ndugu alisemaka hivi: “Furaha yetu inarudia wakati tunakubali haraka mambo fulani yenye inatufikia, na ile inafanya tukamate kila nafasi ili kumutumikia Yehova na kusaidia wengine.” c Pili, walijikaza kuongeza ufundi wao wa kuhubiri kupitia telefone na walianzisha funzo ya Biblia. Tatu, waliacha ndugu na dada zao wawasaidie na waliwashukuru juu ya ule upendo wenye waliwaonyesha. Dada moya mwenye fazili alikuwa anawatumia ujumbe mufupi wenye ulikuwa na andiko fulani ya Biblia. Alifanya vile kila siku kwa mwaka moya. Kama na siye tunakubali hali yetu ya mupya, tutakuwa wenye kutosheka mu mambo yenye tunaweza kufanya.

10. Dada moya alifanya nini ili kujipatanisha na badiliko kubwa mu maisha yake?

10 Ufikirie mambo ya sasa, hapana ya zamani na ujikaze kuona mambo ya muzuri mu maisha yako. Christina, dada wa mu Romania mwenye anaishi mu Japani, alivunjika moyo wakati kutaniko yao ya Kiingereza ilivunjwa. Lakini, hakuendelea kuwaza-waza juu ya ile jambo. Kuliko kufanya vile, aliamua kufanya yake yote mu kutaniko ya Kijapani mwenye alihamia. Aliomba mwanamuke fulani mwenye alikuwa mufanyakazi mwenzake aanze kumufundisha luga ya Kijapani juu hakukuwa anaijua muzuri sana. Ule mwanamuke alikubali kutumia Biblia na broshua Furahia Maisha Milele! ili kumufundisha ile luga. Ile ilimusaidia Christina ajue muzuri zaidi kusema Kijapani, lakini pia ule mwanamuke alianza kupendezwa na kweli. Kama tunaendelea kufikiri juu ya mambo ya sasa, hapana ya zamani, na kama tunajikaza kuona mambo ya muzuri mu maisha yetu, mabadiliko yenye hatukutazamia inaweza kufanya tupate baraka yenye hatukuwazia.

11. Nini njo ilisaidia bibi na bwana fulani wenye hawakukuwa tena na makuta?

11 Usaidie wengine. Wakati banke ilianguka mu inchi kwenye kazi yetu ilikatazwa, bibi na bwana fulani wenye walikuwa mule hawakukuwa tena na makuta. Walifanya nini juu ya kujipatanisha na ile hali? Kwanza, walikamata hatua ya kufanya maisha yao ikuwe mwepesi. Kisha, kuliko kukaza akili juu ya ile magumu, waliamua kukaza akili juu ya kusaidia wengine kwa kuhubiri habari njema kwa bidii. (Mdo. 20:35) Bwana alisema hivi: “Juu tulipitisha wakati mingi mu kazi ya kuhubiri, ile ilifanya tukuwe na wakati kidogo ya kufikiria magumu yetu na ilifanya tukuwe na wakati mingi zaidi ya kufanya mapenzi ya Mungu.” Wakati hali yetu inabadilika, tunapaswa kukumbuka kama ni jambo ya maana kuendelea kusaidia wengine, zaidi sana kwa kuhubiri habari njema.

12. Namna gani mufano wa mutume Paulo unaweza kutusaidia kuwa na usawaziko mu mahubiri?

12 Tunapaswa kuwa na usawaziko mu mahubiri. Tunahubiriaka watu wenye kuwa na mawazo tofauti juu ya Mungu na wenye wanatoka fasi mbalimbali ao wa desturi mbalimbali. Tunaweza kumuiga Paulo, mwenye alikuwa anajipatanisha na hali. Yesu alimuweka Paulo kuwa “mutume kwa mataifa.” (Ro. 11:13) Kwa hiyo, Paulo alihubiria Wayahudi, Wagiriki, watu wenye elimu, watu wa mu vijiji, wakubwa wa serikali, na wafalme. Juu ya kugusa mioyo ya wale watu wote, Paulo alifikia ‘kuwa mambo yote kwa watu wa namna zote.’ (1 Ko. 9:19-23) Alifikiria kwa uangalifu fasi kwenye watu wenye alikuwa nazungumuza nao walitoka na mambo yenye waliamini; na ile ilimusaidia akuwe na usawaziko ili kuzungumuza na kila mumoja wao mu njia yenye ingemuvuta katika kweli. Siye pia tunaweza kupata matokeo ya muzuri mu mahubiri kama tuko na usawaziko na kama tuko najikaza kufikiria njia ya muzuri sana ya kusaidia kila mutu mwenye tunahubiria.

UHESHIMIE MAWAZO YA WENGINE

Kama tuko na usawaziko, tutaheshimia mawazo ya wengine (Ona fungu ya 13)

13. Ni hatari gani yenye kuzungumuziwa mu 1 Wakorinto 8:9 yenye tunaweza kuepuka kama tunaheshimia mawazo ya wengine?

13 Kuwa na usawaziko kunatusaidia pia kuheshimia mawazo ya wengine. Kwa mufano, dada fulani wanapendaka kujipodoa, lakini wengine hawapendake. Wakristo fulani wanapendaka kunywa pombe kwa kiasi, lakini wengine hawakunywake hata kidogo. Wakristo wote wanapendaka kuwa na afya ya muzuri, lakini wanahangaikiaka afya yao mu njia tofauti. Ikiwa tunawaza kama siye tu njo tunakuwaka na sheria na ikiwa tunapendaka ndugu na dada waanze kufanya mambo sawa vile siye, tunaweza kuwakwaza na kuleta migawanyiko mu kutaniko. Hatupendi hata kidogo ile itokee! (Soma 1 Wakorinto 8:9; 10:23, 24) Tuzungumuzie sasa mifano mbili yenye inaonyesha namna kutumikisha kanuni zenye kuwa mu Maandiko kunaweza kutusaidia tukuwe na usawaziko na kuendeleza amani.

Kama tuko na usawaziko, tutaheshimia mawazo ya wengine (Ona fungu ya 14)

14. Ni kanuni gani zenye kuwa mu Biblia zenye tunapaswa kufikiria mbele ya kuamua manguo yenye tutavala na namna tutajipamba?

14 Kuvala na kujipamba. Yehova hatuambie manguo yenye tunapaswa kuvala, lakini anatupatia kanuni za kufuata. Tunapaswa kuvala mu njia yenye inamuletea sifa, yenye inaonyesha usawaziko, kiasi, na “akili ya muzuri.” (1 Ti. 2:9, 10; 1 Pe. 3:3) Njo maana, hatupendake kuvala mu njia yenye itafanya watu watukazie tu uangalifu. Yehova hatuwekee sheria juu ya manguo yenye tutavala ao juu ya namna tutakata ao kutengeneza nywele. Kwa mufano, wazee mu kutaniko fulani walikuwa napenda kusaidia ndugu vijana wenye walikuwa wanakatwa nywele mu namna yenye ilienea sana, ni kusema, kuacha nywele ya mufupi na yenye kuwa na mupangilio mubaya sana. Wazee walifanya nini juu ya kusaidia wale vijana bila kuwawekea sheria? Mwangalizi moya wa muzunguko alishauriaka wale wazee waambie hivi wale ndugu: “Kama uko ku jukwaa, na wasikilizaji wanakaza uangalifu zaidi juu ya namna unaonekana kuliko kukaza uangalifu juu ya mambo yenye uko nasema, ujue kama kuko shida mu namna yako ya kuvala na kujipamba.” Ile tu mafasirio ya mwepesi ilisaidia wale ndugu vijana waelewe mambo yenye wanapaswa kufanya bila wazee kuwawekea sheria. d

Kama tuko na usawaziko, tutaheshimia mawazo ya wengine (Ona fungu ya 15)

15. Ni sheria na kanuni gani zenye kuwa mu Biblia zenye zinatuongoza wakati tuko nakamata maamuzi juu ya afya yetu? (Waroma 14:5)

15 Matunzo. Kila Mukristo anapaswa kujiamulia ni matunzo gani yenye atafuata. (Gal. 6:5) Mu Biblia muko tu sheria fulani zenye kuwa wazi, sawa vile sheria ya kuepuka damu na kupashana habari na pepo wachafu, zenye zinapaswa kuongoza Mukristo wakati iko nachagua ni matunzo gani yenye atafuata. (Mdo. 15:20; Gal. 5:19, 20) Mu mambo ingine, kila Mukristo anaweza tu kujiamulia. Watu fulani wanaendaka kutunzwa tu kwa munganga, lakini wengine wanapendaka aina ingine ya matunzo. Tunaweza kuwa hakika kama aina fulani ya matunzo ni ya muzuri ao ni ya mubaya, hata vile tunapaswa kuheshimia haki ya ndugu na dada zetu ya kujiamulia matunzo yenye watafuata. Kwa hiyo, tunapaswa kukumbuka hii mambo ine: (1) Ni Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza magonjwa na kutuponyesha milele. (Isa. 33:24) (2) Kila Mukristo anapaswa ‘kusadikishwa kikamili’ kuhusu matunzo yenye anaona kuwa ya muzuri sana kwake. (Soma Waroma 14:5.) (3) Tunaepuka kuhukumu wengine ao kufanya jambo yenye inaweza kuwakwaza. (Ro. 14:13) (4) Wakristo wanaonyesha upendo na wanaelewa kama umoja wa kutaniko njo jambo ya maana zaidi kuliko mawazo yao. (Rom. 14:15, 19, 20) Kama tunachunga ile mambo mu akili, tutaendelea kuwa na urafiki wa muzuri pamoya na ndugu na dada zetu na tutaendeleza amani mu kutaniko.

Kama tuko na usawaziko, tutaheshimia mawazo ya wengine (Ona fungu ya 16)

16. Namna gani muzee anaweza kuonyesha usawaziko wakati yeye na wazee wengine wako nashugulikia jambo fulani? (Ona pia picha.)

16 Wazee wanapaswa kuwekea wengine mufano muzuri kwa kuwa na usawaziko. (1 Ti. 3:2, 3) Kwa mufano, muzee hapaswe kutazamia kama kila mara mawazo yake itakubaliwa juu tu iko na miaka mingi zaidi kupita wazee wengine. Anatambua kama roho ya Yehova inaweza kuchochea muzee yeyote aseme jambo yenye inaweza kuwasaidia wakamate uamuzi wa hekima. Na kama hakuna kanuni yoyote yenye inavunjwa, muzee mwenye kuwa na usawaziko atategemeza uamuzi wa wengi mu baraza hata kama hakukubaliana nayo.

FAIDA ZA KUWA NA USAWAZIKO

17. Tutapata faida gani kama tuko na usawaziko?

17 Kama tuko na usawaziko, tutapata faida za mingi. Tutakuwa na urafiki wa muzuri pamoya na ndugu na dada na tutaendeleza amani mu kutaniko. Tutafurahia kumuabudu Mungu kwa umoja hata kama tuko na utu na desturi tofauti. Zaidi ya yote, tutakuwa na furaha juu tunajua kama tuko namuiga Mungu wetu Yehova mwenye kuwa na usawaziko.

WIMBO 90 Tutiane Moyo

a Yehova na Yesu wako na usawaziko na wanapenda na siye pia tukuwe na ile sifa. Kama tuko na usawaziko, itakuwa mwepesi kwetu kujipatanisha na hali, sawa vile magumu ya afya ao magumu ya kupata makuta. Zaidi ya ile, tutaendeleza amani na umoja mu kutaniko.

b Ona habari “Wakati Kunakuwa Mabadiliko Katika Maisha” mu Amuka! Na. 4, 2016.

c Angalia video ku jw.org, mu sehemu Tafuta uandike Kumuuliza Maulizo Ndugu Dmitriy Mikhaylov.

d Juu upate habari zingine kuhusu namna ya kuvala na kujipamba, ona somo ya 52 mu kitabu Furahia Maisha Milele!