Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 30

Umupende Yehova Zaidi na Uendelee Kupenda Wengine

Umupende Yehova Zaidi na Uendelee Kupenda Wengine

“Kupitia upendo tuendelee kukomaa katika mambo yote.”​—EFE. 4:15.

WIMBO 2 Jina Yako Ni Yehova

KIFUPI YA HABARI a

1. Ulijua kweli gani wakati ulianza kujifunza Biblia?

 UNAKUMBUKA wakati ulianza kujifunza Biblia? Pengine ulishangaa kuona kama Mungu iko na jina. Inawezekana ulifurahi wakati ulijua kama Mungu hatesake watu mu moto wa mateso. Na pengine ulifurahi kujua kama tutaona tena wapendwa wetu wenye walishakakufa na tutaishi pamoya nao mu dunia yenye itakuwa paradiso.

2. Zaidi tu ya kujifunza kweli za Biblia, ni maendeleo gani ingine yenye ulifanya? (Waefeso 5:1, 2)

2 Kadiri ulijifunza Biblia, ni vile ulimupenda Yehova zaidi. Ule upendo ulikuchochea kutumikisha mambo yenye ulijifunza. Ulikamata maamuzi ya muzuri zaidi yenye kutegemea kanuni za Biblia. Ulijikaza kubadilisha namna yako ya kuwaza na mwenendo wako juu unapenda kumufurahisha Mungu. Sawa vile tu mutoto anaigaka baba yake mwenye upendo, ni vile pia ulikuwa naiga Baba yako wa mbinguni.​—Soma Waefeso 5:1, 2.

3. Tunaweza kujiuliza maulizo gani?

3 Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Kwa sasa niko namupenda Yehova zaidi kuliko vile nilikuwa namupenda wakati nilifikia kuwa Mukristo? Tangu nibatizwe, niko naendelea kumuiga Yehova zaidi kwa kupenda ndugu na dada zangu?’ Kama “upendo wenye ulikuwaka nao ku mwanzo” ulishapunguka mu njia fulani, usivunjike moyo. Ile ilifikia pia Wakristo wa karne ya kwanza. Lakini, Yesu hakuwakatala, na siye pia hatatukatala. (Ufu. 2:4, 7) Anajua kama tunaweza kurudisha tena upendo wenye tulikuwaka nao ku mwanzo wakati tulijifunza kweli.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Mu hii habari, tutazungumuzia namna tunaweza kumupenda Yehova zaidi na kuendelea kupenda wengine. Kisha, tutaona faida fulani zenye tutapata kama tunafanya vile.

UMUPENDE YEHOVA ZAIDI

5-6. Mutume Paulo alipata magumu gani mu utumishi wake, na ni mambo gani ilimusaidia aendelee kumutumikia Yehova?

5 Mutume Paulo alikuwa na furaha wakati alikuwa namutumikia Yehova, lakini alipata magumu mingi. Mara mingi Paulo alikuwa nafanya safari za murefu, na ile wakati haikukuwa mwepesi kusafiri. Na wakati fulani mu safari zake, alijikuta “katika hatari kutokana na mito” na “katika hatari kutoka kwa wanyanganyi.” Tena, wakati fulani maadui wake walikuwa namupiga. (2 Ko. 11:23-27) Zaidi ya ile, Wakristo wenzake hawakukuwa namushukuru juu ya mambo yenye alifanya ili kuwasaidia.​—2 Ko. 10:10; Flp. 4:15.

6 Nini njo ilimusaidia Paulo aendelee kumutumikia Yehova? Mambo mingi yenye alijifunza mu Maandiko juu ya utu wa Yehova na mambo yenye alijionea njo yenye ilimusaidia sana. Alifikia kuwa hakika kama Yehova Mungu alimupenda. (Ro. 8:38, 39; Efe. 2:4, 5) Naye alifikia kumupenda sana. Alionyesha kama anamupenda Yehova “kwa kutumikia na kuendelea kutumikia watakatifu.”​—Ebr. 6:10.

7. Ni jambo gani ya kwanza yenye tunaweza kufanya ili kumupenda Yehova zaidi?

7 Tunaweza kumupenda Yehova zaidi kwa kujifunza kwa bidii Neno yake. Wakati uko nasoma Biblia, ujikaze kuona mambo yenye kila andiko inaonyesha kuhusu Yehova. Ujiulize hivi: ‘Namna gani hii habari inaonyesha kama Yehova ananipenda? Inanipatia sababu gani za kumupenda Yehova?’

8. Namna gani sala inaweza kutusaidia tumupende Yehova zaidi?

8 Jambo ingine yenye inaweza kutusaidia tumupende Yehova zaidi ni kumufungulia moyo wetu kila mara katika sala. (Zb. 25:4, 5) Kama tunafanya vile, yeye pia atajibia sala zetu. (1 Yo. 3:21, 22) Khanh, dada wa mu Asia, anasema hivi: “Ku mwanzo upendo wangu kwa Yehova ulitegemea tu ujuzi wenye nilikuwa nao, lakini nilimupenda zaidi wakati niliona namna alikuwa najibia sala zangu. Ile ilinichochea nipende kufanya mambo yenye inamufurahishaka.” b

UENDELEE KUPENDA WENGINE

9. Nini njo inaonyesha kama Timoteo alipenda ndugu na dada zake zaidi?

9 Miaka fulani kisha Paulo kuwa Mukristo, alikutana na kijana Timoteo. Timoteo alimupenda Yehova na alipenda watu. Paulo aliambia hivi Wafilipi: “Sina mutu mwingine mwenye kuwa na muelekeo kama [wa Timoteo] mwenye atajali kabisa mahangaiko yenu.” (Flp. 2:20) Hapa, Paulo hakuzungumuzia uwezo wa Timoteo wa kufanya mambo muzuri ao wa kuwa musemaji muzuri mbele ya watu. Lakini, alizungumuzia namna Timoteo alipenda sana ndugu na dada zake. Bila shaka, ndugu na dada wenye walikuwa mu makutaniko yenye Timoteo alitumikia walimungojea sana kwa hamu.​—1 Ko. 4:17.

10. Anna na bwana yake walifanya nini ili kuonyesha kama walipenda ndugu na dada zao?

10 Na siye pia tunatafutaka njia mbalimbali za kusaidia ndugu na dada zetu. (Ebr. 13:16) Fikiria habari ya Anna, mwenye tulitaya mu habari yenye kutangulia. Kisha upepo mukali, yeye na bwana yake walitembelea familia moya ya Mashahidi na waliona kama ule upepo uliharibisha sehemu ya yulu ya nyumba ya ile familia. Ile ilifanya manguo ya ile familia ichafuke. Anna anasema hivi: “Tulikamata ile manguo, tukaifula, kuikunja na kuigoma, kisha tukabarudishia ayo. Tuliona kama ile ilikuwa tu tendo ya kidogo, lakini ilifanya tukuwe na urafiki wa nguvu sana pamoya nao tangu ile siku.” Kupenda ndugu na dada njo kulichochea Anna na bwana yake wasaidie ile familia.​—1 Yo. 3:17, 18.

11. (a) Kuonyesha upendo kunaweza kuchochea wengine wafanye nini? (b) Kulingana na Mezali 19:17, Yehova anafanyaka nini wakati tunaonyesha wengine upendo?

11 Wakati tunafanyia wengine mambo ya muzuri na kuwaonyesha kama tunawapenda, mara mingi wanaonaka vile tuko tunajikaza kumuiga Yehova, na wanaweza hata kusamini matendo yetu ya muzuri kuliko vile tunaweza kuwazia. Khanh, mwenye tulishataya, anakumbuka wale wenye walimusaidiaka. Anasema hivi: “Nashukuru sana dada zangu wote wenye walikuwa naenda na miye mu mahubiri. Walikuwa nakuya kunikamata ku nyumba, walinialika kuenda kula nao chakula fulani, na walikuwa wanahakikisha kama nilikuwa nafika muzuri ku nyumba. Kwa sasa njo natambua kama walikuwa najikaza sana ili kufanya vile. Na walifanya vile juu walinipenda.” Kusema kweli, haiko kila mutu njo atatushukuru juu ya jambo yenye tulimufanyia. Khanh anasema hivi juu ya wale wenye walimusaidiaka: “Ningependa kuwalipa juu ya mambo ya muzuri yenye walinifanyiaka, lakini sijue kwenye wote wanaishi kwa sasa. Juu Yehova anajua kwenye wote wanaishi, niko namuomba awalipe.” Khanh alisema kweli. Yehova anaonaka hata tendo ya muzuri ya kidogo sana yenye tunafanyiaka wengine. Yehova anasaminiaka ile sana na anaionaka kuwa deni yenye atalipa.​—Soma Mezali 19:17.

Wakati mutu anafanya maendeleo ya kiroho, anatafutaka njia mbalimbali za kusaidia wengine (Ona fungu ya 12)

12. Ndugu wanaweza kufanya nini ili kuonyesha kama wanapenda ndugu na dada mu kutaniko? (Ona pia picha.)

12 Kama uko ndugu, unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unapenda wengine na kama unapenda kuwasaidia? Ndugu moya kijana mwenye kuitwa Jordan alimuuliza muzee fulani mambo yenye anaweza kufanya ili kusaidia zaidi kutaniko. Ule muzee alimupongeza juu ya maendeleo yenye tayari alikuwa alishafanya na kisha alimupatia mashauri fulani juu ya namna angeweza kufanya zaidi. Kwa mufano, alimuomba ajikaze zaidi kukuwa nafika mbele ku Jumba ya Ufalme na kusalimia watu, kutoa maelezo ku mikutano, kuhubiri kikawaida pamoya na kikundi yao ya mahubiri, na kutafuta njia mbalimbali za kusaidia wengine. Wakati Jordan alifanya vile, alijifunza namna ya kufanya mambo fulani na alijifunza pia kupenda ndugu na dada zake zaidi. Tena, alijifunza kama wakati ndugu anakuwa mutumishi wa huduma, haimaanishe kama njo anaanza kusaidia wengine; lakini, anaendelea kuwasaidia.​—1 Ti. 3:8-10, 13.

13. Nini njo inaonyesha kama upendo njo ulisaidia Christian astahili tena kuwa muzee?

13 Sasa utafanya nini kama ulikuwaka mutumishi wa huduma ao muzee? Yehova hasahau kazi yenye ulifanyaka na anaendelea kukumbuka upendo wenye ulikuchochea kufanya vile. (1 Ko. 15:58) Anaona pia upendo wenye unaendelea kuonyesha. Ndugu Christian alivunjika moyo wakati madaraka yake ya kuwa muzee iliisha. Lakini, anasema hivi: “Niliamua kuendelea kufanya yote yenye naweza ili kumutumikia Yehova kwa kupenda, ikuwe niko na madaraka ao hapana.” Ku mwisho alirudilia daraka yake. Anasema tena hivi: “Kuwa tena muzee kuliniogopesha kidogo. Lakini, kwa rehema ya Yehova, alipenda nikuwe tena muzee. Kwa hiyo, niliamua kutumikia tena ile daraka juu nilimupenda na juu nilipenda ndugu na dada zangu.”

14. Maelezo ya dada fulani wa Georgia inakufundisha nini?

14 Watumishi wa Yehova wanaonyeshaka pia majirani wao upendo. (Mt. 22:37-39) Kwa mufano, dada Elena wa mu Georgia, anasema hivi: “Ku mwanzo, jambo moya tu yenye ilinichochea kuhubiri ni upendo wangu kwa Yehova. Kadiri nilimupenda Baba yangu wa mbinguni zaidi, ni vile nilipenda pia watu zaidi. Nilijaribu kuwazia magumu yenye walipata na habari yenye ingegusa mioyo yao. Kadiri niliwafikiria mu ile njia, ni vile nilipenda kuwasaidia.”​—Ro. 10:13-15.

BARAKA ZENYE TUTAPATA WAKATI TUNAONYESHA WENGINE UPENDO

Tendo moya ya upendo inaweza kuletea watu wengi baraka (Ona fungu ya 15-16)

15-16. Sawa vile picha zinaonyesha, kuonyesha wengine upendo kunaweza kuleta baraka gani?

15 Kama tunaonyesha ndugu zetu upendo, haiko wao tu njo wanapataka faida. Kisha tu ugonjwa wa korona kuanza, ndugu Paolo na bibi yake walifundisha dada wengi wenye kuzeeka namna ya kutumia vyombo vyao vya kielektroniki ili kuhubiri. Ku mwanzo, dada moya alikuwa nashindwa kutumia muzuri chombo yake ya kielektroniki, lakini ku mwisho aliweza. Aliitumia ili kualika watu wa familia yake ku Ukumbusho. Kati yao, watu makumi sita walihuzuria kupitia vidéoconférence! Bidii ya Paolo na bibi yake ilisaidia ule dada na watu wa familia yake. Kisha, ule dada aliandikia Paolo hivi: “Aksanti kwa kutufundisha siye wenye kuzeeka. Siwezi kusahau namna Yehova anatuhangaikiaka na namna ulitumikaka sana ili kutusaidia.”

16 Ile ilimukumbushaka Paolo jambo fulani ya maana. Ilimukumbushaka kama upendo ni wa maana zaidi kuliko ujuzi ao uwezo wa kizalikio. Anasema hivi: “Nilikuwaka mwangalizi wa muzunguko. Leo, nafikia kutambua kuwa hata kama pengine ndugu na dada walishasahau hotuba zangu, wangali wanakumbuka mambo yenye nilifanyaka ili kuwasaidia.”

17. Kuonyesha upendo kutaletea pia nani faida?

17 Kuonyesha wengine upendo kunatuleteaka faida mu njia zenye hatutazamie. Jonathan, mwenye anaishi mu Nouvelle-Zélande, anahakikisha ile. Siku ya Posho moya kisha midi wakati kulikuwaka kifukutu, alionaka painia fulani iko nahubiri mu barabara. Jonathan aliamua kuanza kuhubiri na ule painia kisha midi ya kila siku ya Posho yenye ilifuata. Ku mwanzo, hakutambua kama ile tendo ya muzuri ingemuletea yeye peke faida. Jonathan anasema hivi: “Ile wakati, sikukuwa napenda kuhubiri. Lakini, wakati niliona matokeo ya muzuri yenye ule ndugu alipata mu utumishi wake, nilianza kupenda kuhubiri. Ule ndugu alifikia pia kuwa rafiki yangu wa karibu, alinisaidia kiroho, alinisaidia nifurahie mahubiri, na nimukaribie Yehova zaidi.”

18. Yehova anapenda tufanye nini?

18 Yehova anapenda tumupende zaidi na tuendelee pia kupenda wengine. Sawa vile tumejifunza, tunaweza kumupenda Yehova zaidi kwa kusoma Neno yake na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma na kwa kusali kwake kwa ukawaida. Tunaweza kuonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu zaidi kwa kuwasaidia. Kadiri upendo wetu uko naongezeka, ni vile tutamukaribia zaidi Yehova na ndugu na dada zetu. Na ku mwisho, tutafurahia ule urafiki milele!

WIMBO 109 Tupendane Sana Kutoka Ndani ya Moyo

a Ikuwe tulishamutumikia Yehova kwa miaka mingi ao hapana, siye wote tunapaswa kuendelea kufanya maendeleo. Hii habari itazungumuzia jambo ya maana yenye inaweza kutusaidia kufanya vile. Ile jambo ni: Kumupenda Yehova zaidi na kuendelea kupenda wengine. Wakati uko nafikiri sana juu ya hii habari, kumbuka maendeleo yenye ulishafanya na namna unaweza kufanya maendeleo zaidi.

b Majina fulani imebadilishwa.