Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 35

WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi

Namna Wazee Wanaweza Kusaidia Wenye Wanaondolewa mu Kutaniko

Namna Wazee Wanaweza Kusaidia Wenye Wanaondolewa mu Kutaniko

“Kutakuwa furaha kubwa mbinguni kwa sababu ya mutenda-zambi mumoja mwenye anatubu, kuliko kwa watu makumi kenda na kenda (99wenye haki, wenye hawana lazima ya kutubu.”LU. 15:7.

WAZO KUBWA

Juu ya nini batu fulani banapaswa kuondolewa mu kutaniko, na namna wazee wanaisaidia bale batu batubu na bakubaliwe tena na Yehova.

1-2. (a) Yehova anaona namna gani wale wenye wanafanya zambi kimakusudi? (b) Yehova anapenda wakosaji wafanye nini?

 YEHOVA haiko Mungu mwenye anaachiliaka tu mambo. Anachukia zambi. (Zb. 5:​4-6) Anatuomba tuheshimie kanuni zake za haki zenye anatutolea mu Neno yake. Ni kweli Yehova hatazamie tukuwe wakamilifu juu anajua kama hatukamilike. (Zb. 130:​3, 4) Lakini Yehova hakubali ‘watu wenye hawamuogope, wenye wanatumia fazili zake zenye hazistahiliwe kama kisingizio cha kuwa na mwenendo mupotovu wa bila haya.’ (Yud. 4) Na hata, Biblia inazungumuzia “uharibifu wa watu wenye hawamuogope Mungu” ku vita ya Mungu ya Armagedoni.—2 Pe. 3:7; Ufu. 16:16.

2 Lakini, Yehova hapendi mutu yeyote aharibiwe. Sawa vile tuliona mu habari zingine zenye kuwa mu hii gazeti, Biblia inaonyesha wazi kama Yehova “anataka wote wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9) Wazee Wakristo wanamuiga Yehova wakati wanajikaza kusaidia wakosaji kwa uvumilivu wabadilishe matendo yao na wakuwe tena na urafiki muzuri pamoya na Yehova. Lakini, haiko wakosaji wote njo wanaitikaka musaada wa wazee. (Isa. 6:9) Hata kisha wazee kuwasaidia tena na tena, wakosaji fulani wanaendelea tu na tabia yao ya mubaya. Wazee wanapaswa kufanya nini mu hali ya vile?

“MUONDOE MUTU MUOVU”

3. (a) Biblia inasema watenda-zambi wenye wanakatala kutubu wanapaswa kufanyiwa nini? (b) Juu ya nini tunaweza kusema kama ni sawa vile mukosaji yeye peke njo anaamua kuondolewa mu kutaniko?

3 Wakati mukosaji anakatala kutubu, wazee wanalazimika kufuata muongozo wenye kuwa mu 1 Wakorinto 5:13: “Muondoe mutu muovu katikati yenu.” Ni sawa vile mukosaji yeye peke anachagua kuondolewa mu kutaniko. Anavuna byenye alipanda. (Gal. 6:7) Juu ya nini tunasema vile? Juu anakatala kutubu hata kama wazee wamejaribu kumusaidia tena na tena. (2 Fa. 17:​12-15) Matendo yake inaonyesha kama amekatala kufuata kanuni za Yehova.—Kum. 30:​19, 20.

4. Juu ya nini kunakuwaka tangazo wakati mukosaji mwenye hatubu anaondolewa mu kutaniko?

4 Wakati mukosaji mwenye hatubu anaondolewa mu kutaniko, wazee wanafanyia kutaniko tangazo kama ule mutu haiko tena Shahidi wa Yehova. a Kusudi ya ile tangazo haiko kumupatisha haya. Lakini inatolewa juu kutaniko ifuate hii mashauri ya Biblia: ‘Muache kushirikiana’ na ule mutu, na “hata musikule chakula pamoja” naye. (1 Ko. 5:​9-11) Kuko sababu ya muzuri yenye ilifanya Yehova atupatie ile muongozo. Mutume Paulo aliandika hivi: “Chachu kidogo inachachisha donge lote.” (1 Ko. 5:6) Kama mukosaji mwenye hatubu anabakia mu kutaniko, ile inaweza kufanya bengine baone kama haiko lazima kufuata kanuni za Yehova mu maisha yao.—Mez. 13:20; 1 Ko. 15:33.

5. Tunapaswa kuona namna gani mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko, na juu ya nini?

5 Sasa, tunapaswa kuona namna gani muamini mwenzetu mwenye anaondolewa mu kutaniko? Kusema kweli, hatutapitisha wakati pamoya naye. Lakini hatupaswe kuwaza kama byake binaishia pale. Tumuone kama kondoo wa Yehova mwenye amepotea. Kondoo mwenye anapotea, anaweza kurudia. Kumbuka kama ule Mukristo mwenye amepotea alijitoa kwa Yehova. Lakini kwa sasa haishi kulingana na naziri yake na ile inamutia mu hatari. (Eze. 18:31) Juu kwa Yehova kungali nafasi ya kumuonyesha rehema, kuko tumaini kama ule mutu anaweza kurudia. Sasa namna gani wazee wanaweza kusaidia wakosaji wenye wanaondolewa mu kutaniko?

NAMNA WAZEE WANASAIDIA WALE WENYE WAMEONDOLEWA MU KUTANIKO

6. Wazee watafanya mambo gani juu ya kusaidia mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko?

6 Wakati mutu anaondolewa mu kutaniko, ni kusema banamuacha yeye peke atafute namna ya kumurudilia Yehova? Hapana. Wakati halmashauri ya wazee inaambia mukosaji mwenye hatubu kama ataondolewa mu kutaniko, banamuambiaka pia mambo ya kufanya juu afikie kurudia mu kutaniko. Lakini wazee hawaishiake pale. Wanaambiaka mukosaji kama watapenda kukutana naye kisha miezi kidogo juu waone kama alishabadilika. Kama mukosaji anakubali, wakati wazee watakutana tena naye watamutia moyo atubu na kumurudilia Yehova. Kama kufikia ile wakati hayabadilika wazee watajikaza kukutana naye tena na tena wakati wenye kuya.

7. Namna gani wazee wanaiga huruma ya Yehova wakati wanashugulikia mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko? (Yeremia 3:12)

7 Kama Yehova, wazee wanajikaza kuonyesha huruma wale wenye wameondolewa mu kutaniko. Kwa mufano, Yehova hakungoya watu wake wenye walimuacha, Waisraeli wa zamani, njo wakamate hatua ya kwanza ya kumurudilia. Alikamata hatua ya kuwasaidia hata kama hakuna alama yoyote yenye ilionyesha kama walipenda kutubu. Sawa vile tuliona mu habari ya pili ya hii gazeti, Yehova alionyesha kupitia nabii Hosea namna ni mwenye huruma. Aliambia nabii Hosea aende kukamata bibi yake mwenye alikuwa angali anafanya zambi. (Hos. 3:1; Mal. 3:7) Kama Yehova, wazee Wakristo wanapenda kabisa mukosaji amurudilie Yehova, na hawafanye mambo yenye itafanya ikuwe nguvu kwake kurudia.—Soma Yeremia 3:12.

8. Namna gani mufano wa mwana mupotevu wenye Yesu alitoa unatusaidia kuelewa muzuri huruma na rehema ya Yehova? (Lu. 15:7)

8 Kumbuka mufano wa Yesu wenye tulizungumuzia mu habari ya pili ya mu hii gazeti. Wakati baba aliona kwa mbali mwana wake iko narudia “akamukimbilia, akamukumbatia kwa upole wote na kumubusu.” (Lu. 15:20) Ona kama baba hakungoya mutoto wake akuye kumulomba huruma. Lakini sawa baba mwenye upendo, alikamata hatua ya kwanza. Wazee wanajikaza pia kutendea vile wale wenye wamepotea. Wanapenda wale kondoo wenye wamepotea “warudie ku nyumba.” (Lu. 15:​22-24, 32) Wakati mutenda-zambi anarudia, mbinguni kunakuwaka furaha na ku dunia pia!—Soma Luka 15:7.

9. Yehova anapenda watenda-zambi wafanye nini?

9 Kufikia hapa tunaona kama Yehova hakubali wakosaji wenye wanakatala kutubu. Lakini anaendelea kujaribu kuwasaidia. Anapenda wamurudilie. Hosea 14:4 inaonyesha namna Yehova anajisikia juu ya wakosaji wenye wanatubu: “Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu. Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe, kwa sababu kasirani yangu imegeuka.” Kujua mawazo ya Yehova juu ya wakosaji, kunachochea wazee watafute alama yoyote yenye inaonyesha kama mutu anaanza kutubu. Na kunachochea pia wale wenye walimuacha Yehova wamurudilie bila kukawia.

10-11. Wazee watafanya nini juu ya kusaidia wale wenye waliondolewa mu kutaniko zamani?

10 Tuseme nini juu ya wale wenye waliondolewa mu kutaniko zamani, pengine kulishapita miaka mingi? Inawezekana hawako tena nafanya zambi yenye ilifanya waondolewe mu kutaniko. Mu hali fulani pengine hawakumbuke hata juu ya nini waliondolewa mu kutaniko. Hata hali ikuwe namna gani, wazee wanajikaza kuwatafuta na kuwatembelea. Wakati wazee wanawatembelea wanaweza hata kusali pamoya nao na kuwatia moyo warudie mu kutaniko. Kwa kweli kama mutu amekuwa mbali na kutaniko kwa miaka mingi, iko na lazima ya kujifunza tena juu ya Yehova na mafundisho ingine ya Biblia. Kwa hiyo, akionyesha kama anapenda kurudia mu kutaniko, wazee watakamata mipango ili Mukristo fulani aanze kujifunza naye Biblia, hata mbele arudishwe. Mu hali zote ni wazee njo wanapaswa kukamata ile mipango ya funzo ya Biblia.

11 Wazee wanaiga huruma ya Yehova kwa kujikaza kusaidia batu mingi kadiri inawezekana bajue kama mulango wa kurudia mu kutaniko uko wazi. Wakati mutenda-zambi anaonyesha kama ametubu na anaacha matendo yake ya mubaya, anaweza kurudishwa bila kukawia.—2 Ko. 2:​6-8.

12. (a) Wazeee wanapaswa kuwa waangalifu sana mu hali gani? (b) Juu ya nini hatupaswe kuwaza kama Yehova hawezi kuonyesha rehema watu wenye walifanya aina fulani ya zambi? (Ona pia maelezo ya chini.)

12 Mu hali fulani wazee wanapaswa kuwa waangalifu sana mbele ya kurudisha mutu. Kwa mufano, kama mutu alitendea mubaya mutoto kingono, ao alikuwa muasi-imani, ao tena alifanya ujanja juu ya kuvunja ndoa, wazee wanapaswa kuhakikisha kama ametubu kikweli. (Mal. 2:14; 2 Ti. 3:6) Wanapaswa kulinda kondoo wa Mungu. Lakini wanapaswa pia kukumbuka kama Yehova iko tayari kukubali mukosaji yeyote mwenye anatubu kikweli na anaacha matendo ya mubaya. Hata kama wazee wanapaswa kuwa waangalifu juu ya watu wenye walitendea wengine mambo ya mubaya sana, hawapaswe kusema kama Yehova hawezi kuonyesha rehema watu wenye walifanya aina fulani ya zambi. b1 Pe. 2:10.

KUTANIKO ITATENDA NAMNA GANI?

13. Kuko tofauti gani kati ya namna tunatendea mutu mwenye amekaripiwa na wazee na namna tunatendea mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko?

13 Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, wakati fulani wanatutangazia kama mutu fulani amekaripiwa. Mu hali ya vile, tunaendelea kupitisha wakati pamoya na ule mutu juu tunajua kama alitubu na ameacha tabia yake ya mubaya. (1 Ti. 5:20) Anaendelea kuwa Mukristo mwenzetu na iko na lazima ya kutiwa moyo na waamini wenzake. (Ebr. 10:​24, 25) Lakini, mambo iko tofauti wakati mutu anaondolewa mu kutaniko. ‘Tunaacha kushirikiana’ na ule mutu, ‘hata hatukule chakula pamoja na mutu wa namna hiyo.’—1 Ko. 5:11.

14. Namna gani Wakristo wanaweza kutumia zamiri yao yenye kuzoezwa na Biblia juu ya kujua namna ya kutendea mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko? (Ona pia picha.)

14 Je, mambo yenye tumeona inaonyesha kama hatupaswe kualika ku mikutano mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko ao kumusalimia wakati anafika ku mikutano? Hapana. Kwa kweli, hatutapitisha wakati pamoya naye. Lakini Wakristo wanaweza kutumia zamiri yao yenye kuzoezwa na Biblia ili kuamua ikiwa wanaweza kualika ku mikutano mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko, pengine mutu wa familia ao rafiki yao wa zamani. Tutafanya nini kama anafika ku mikutano? Zamani hatungesalimia mutu wa vile. Mu hii hali pia, kila Mukristo anapaswa kutumia zamiri yake yenye kuzoezwa na Biblia juu ya kuamua kama atamusalimia ao hapana. Wakristo fulani wanaweza kuamua kumusalimia na kumukaribisha wakati anafika ku mikutano. Lakini hatutafanya naye mazungumuzo ya zaidi ao kupitisha wakati pamoya naye.

Kila Mukristo anapaswa kutumia zamiri yake yenye kuongozwa na Biblia juu ya kuamua kama ataalika ku mukutano mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko ao kama atamusalimia wakati anafika ku mukutano (Ona fungu ya 14)


15. 2 Yohana 9-11 inazungumuzia watenda-zambi wa aina gani? (Ona pia kisanduku “ Yohana na Paulo Balikuwa Nazungumuzia Aina Ileile ya Zambi?”)

15 Wakristo fulani wanaweza kusema hivi: ‘Si Biblia inasema kama Mukristo mwenye anasalimia mutu wa vile anashiriki katika matendo yake maovu?’ (Soma 2 Yohana 9-11.) Wakati tunachunguza mambo yenye Yohana alikuwa anazungumuzia, tunaelewa kama ile muongozo inahusu waasi-imani na wengine wenye wanachochea batu bakuwe na matendo ya mubaya. (Ufu. 2:20) Kwa hiyo, kama mutu anaendelea kueneza mafundisho ya waasi-imani ao kuchochea bengine bafanye mambo ya mubaya. Wazee hawatapanga kumutembelea. Hata vile, kungali tumaini, ule mutu anaweza kutubu. Lakini, mbele arudie ku mustari, hatutamusalimia ao kumualika ku mikutano.

IGA HURUMA NA REHEMA YA YEHOVA

16-17. (a) Yehova anapenda watenda-zambi wafanye nini? (Ezekieli 18:32) (b) Namna gani wazee wanaweza kuonyesha kama wako natumika pamoya na Yehova wakati wako najaribu kusaidia wakosaji?

16 Tumejifunza nini mu hii gazeti yote? Yehova hapendi hata mutu moya aharibiwe! (Soma Ezekieli 18:32.) Anapenda watenda-zambi wamurudilie. (2 Ko. 5:20) Njo maana tangu zamani amesaidia tena na tena batu yake batubu na bamurudilie, ikuwe kikundi ya batu ao mutu mumoya-mumoya. Wazee wako na pendeleo ya kutumika pamoya na Yehova juu ya kusaidia wakosaji watubu.—Ro. 2:4; 1 Ko. 3:9.

17 Wazia furaha yenye inakuwaka mbinguni wakati watenda-zambi wanatubu. Baba yetu wa mbinguni Yehova anasikiaka furaha sana kila wakati kondoo wake mwenye alipotea anarudia mu kutaniko. Wakati tunafikiria huruma, rehema, na fazili zenye hazistahiliwe za Yehova, tunaendelea kumupenda zaidi.—Lu. 1:78.

WIMBO 111 Mambo Yenye Kufanya Tukuwe na Furaha

a Kuhusu bale benye habiko tena Mashahidi wa Yehova hatutasema tena kama bametengwa na kutaniko, ao kubaita batengwa. Kulingana na maneno ya Paulo yenye kuwa mu 1 Wakorinto 5:​13, tutasema bameondolewa mu kutaniko.

b Biblia inaonyesha kama zambi yenye haiwezi kusamehewa haiko aina fulani ya zambi, lakini ni zambi yenye mutu anafanya kwa moyo mugumu, yenye inaendelea kumupinga Mungu. Haiko siye njo wa kuamua ikiwa mutu amefanya zambi ya vile.—Mk. 3:29; Ebr. 10:​26, 27.