Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 39

Upole Haiko Uzaifu, Ni Nguvu

Upole Haiko Uzaifu, Ni Nguvu

“Mutumwa wa Bwana hana lazima ya kupigana, lakini anapaswa kuwa mupole.”—2 TI. 2:24.

WIMBO 120 Tukuwe Wapole Kama Kristo

KIFUPI YA HABARI a

1. Wengine wanaweza kutuuliza kuhusu nini ku kazi ao ku masomo?

 UNAJISIKIAKA namna gani wakati mwanafunzi mwenzako ao mufanyakazi mwenzako anakuuliza juu ya mambo yenye unaamini? Unakuwaka na wasiwasi? Haiko weye peke. Lakini, maulizo ya vile inaweza kukusaidia ujue mawazo yake na mambo yenye anaamini. Inaweza kukupatia nafasi ya kuzungumuza naye juu ya habari njema. Lakini wakati fulani mutu anaweza kukuuliza ulizo juu tu ya kupinga mambo yenye unaamini ao juu tu anapenda kubishana na weye. Ile haipaswe kutushangaza juu watu wengi wameambiwa habari za uongo juu ya mambo yenye tunaamini. (Mdo. 28:22) Zaidi ya ile, tunaishi mu “siku za mwisho,” wakati wenye watu wengi “hawataki makubaliano yoyote” na hata ni “wakali.”—2 Ti. 3:1, 3.

2. Juu ya nini upole ni sifa ya maana sana?

2 Unaweza kujiuliza hivi: ‘Nini njo itanisaidia nibakie mwenye kutulia wakati mutu anapinga mambo yenye kutegemea Biblia yenye ninaamini?’ Sifa ya upole. Mutu mupole hakasirikake haraka. Lakini anaweza kujizuia wakati anachokozwa ao wakati hajue namna ya kujibia. (Mez. 16:32) Kusema kweli, haikuwake mwepesi kufanya vile. Namna gani unaweza kukomalisha sifa ya upole? Namna gani unaweza kujibia kwa upole wakati mutu fulani anapinga mambo yenye unaamini? Na kama uko muzazi, namna gani unaweza kusaidia watoto wako wajifunze namna ya kutetea imani yao kwa upole. Tutazungumuzia majibu ya ile maulizo.

NAMNA YA KUKOMALISHA SIFA YA UPOLE

3. Juu ya nini tunaweza kusema kama upole haiko uzaifu lakini ni nguvu? (2 Timoteo 2:24, 25)

3 Mutu mupole haiko muzaifu, kwa sababu inaomba mutu akuwe na nguvu ya kujizuia ili abakie mwenye kutulia wakati anapambana na hali yenye inaweza kumufanya akasirike. Upole ni moja kati ya sifa za “tunda la roho.” (Gal. 5:22, 23) Neno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa upole, ilikuwa natumiwa wakati fulani ili kuzungumuzia farasi mwenye amezoezwa ili aweze kutii. Fikiria farasi mwenye hayazoezwa mwenye kuwa na nguvu mingi. Kisha kuzoezwa anakuwa “mupole.” Ni mupole lakini angali tu na nguvu. Siye wanadamu, namna gani tunaweza kuwa wapole na wakati uleule kuwa wenye nguvu? Hatuwezi kufanya vile kwa nguvu yetu wenyewe. Tunapaswa kumuomba Mungu roho yake takatifu na kumuomba atusaidie tukomalishe ile sifa. Watu wengi wameweza kufanya vile. Mashahidi wengi walitenda kwa upole wakati walipambana na upinzani. Na ile ilifanya wengine wakuwe na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova. (Soma 2 Timoteo 2:24, 25.) Unaweza kufanya nini juu ya kukomalisha sifa ya upole?

4. Mufano wa Isaka unatufundisha nini juu ya upole?

4 Mu Biblia muko habari za mingi zenye zinaonyesha juu ya nini ni jambo ya maana kuwa na sifa ya upole. Tufikirie mufano wa Isaka. Wakati alianza kuishi Gerari mu eneo ya Wafilisti, kwa sababu ya wivu majirani wake walikamata udongo na kufunika visima vyenye watumishi wa baba yake walikuwaka wamechimba. Kuliko kutetea haki yake, alihamisha jamaa yake yote fasi ingine na kuchimba visima vingine. (Mwa. 26:12-18) Lakini Wafilisti wakasema kama maji yenye ilikuwa mu ile eneo ilikuwa pia yao. Hata vile Isaka alitenda tena kwa amani. (Mwa. 26:19-25) Nini njo ilimusaidia aendelee kuwa mupole hata kama wengine waliendelea kumuonea? Bila shaka, alifuata mufano wa wazazi wake. Alijifunza mambo mingi kupitia Abrahamu, mwenye alikuwa mufanya-amani, na kupitia “roho ya utulivu na ya upole” ya Sara.—1 Pe. 3:4-6; Mwa. 21:22-34.

5. Ni mufano gani unaonyesha kama wazazi Wakristo wanaweza kusaidia watoto wao waone upole kuwa sifa ya maana?

5 Wazazi Wakristo, mukuwe hakika kama nyie pia munaweza kusaidia watoto wenu waelewe juu ya nini sifa ya upole ni ya maana sana. Fikiria mufano wa Maxence, mwenye kuwa na miaka 17. Alikutana na watu wakali ku masomo na mu mahubiri. Kwa uvumilivu, wazazi wake walimusaidia kukomalisha sifa ya upole. Wanasema hivi: “Maxence ameelewa kama wakati mutu anachokozwa, inaomba akuwe na nguvu sana aweze kujizuia, kuliko kutenda kwa kasirani ao kwa jeuri.” Jambo ya kufurahisha ni kwamba Maxence amekomalisha sifa ya upole.

6. Namna gani sala inaweza kutusaidia kuwa wapole zaidi?

6 Tunaweza kufanya nini kama tunajikuta mu hali yenye inaweza kutukasirisha? Kwa mufano, tutafanya nini kama mutu anasema mubaya juu ya jina ya Mungu wetu ao anazarau Bilbia? Tunapaswa kumuomba Yehova roho yake na hekima yake ili tujibie kwa upole. Tutafanya nini kama tunatambua kama hatukujibia muzuri? Tunaweza kusali tena juu ya ile jambo na kufikiria namna tunaweza kujibia muzuri zaidi wakati wenye kuya. Kama tunafanya vile, Yehova atatupatia roho yake takatifu ili tuweze kuzuia kasirani yetu na kutenda kwa upole.

7. Kuweka maandiko fulani katika akili kunaweza kutusaidia namna gani kuzuia maneno yetu na namna yetu ya kutenda? (Mezali 15:1, 18)

7 Maandiko fulani ya Biblia inaweza kutusaidia kujibia kwa upole wakati tuko mu hali za nguvu. Roho ya Mungu inaweza kutusaidia kukumbuka ile maandiko. (Yoh. 14:26) Kwa mufano, kanuni zenye kupatikana mu kitabu ya Mezali zinaweza kutusaidia kuwa wapole. (Soma Mezali 15:1, 18.) Ile kitabu ya Biblia inaonyesha pia faida ya kujizuia mu hali za nguvu.—Mez. 10:19; 17:27; 21:23; 25:15.

NAMNA UFAHAMU UNAWEZA KUTUSAIDIA KUWA WAPOLE

8. Juu ya nini tunapaswa kufikiria sababu yenye pengine inafanya mutu apinge mambo yenye tunaamini?

8 Ufahamu unaweza pia kutusaidia. (Mez. 19:11) Mutu mwenye kuwa na ufahamu anajizuia wakati wengine wanapinga mambo yenye anaamini. Maulizo fulani inaweza kuwa sawa vile jiwe yenye inaonekana kuwa ya kidogo lakini sehemu yake kubwa inajificha chini ya maji. Kwa mufano mutu anaweza kuuliza ulizo kwa sababu iko na nia fulani ao jambo fulani yenye iko namuhangaisha yenye hatujue. Kwa hiyo, mbele ya kujibia, ni muzuri tutambue kama inawezekana hatujue sababu yenye ilichochea ule mutu aulize ile ulizo.—Mez. 16:23.

9. Gideoni alionyesha namna gani ufahamu na upole wakati alizungumuza na wanaume wa Efraimu?

9 Fikiria namna Gideoni alijibia wanaume wa Efraimu. Walimuuliza kwa kasirani juu ya nini hakuwaita ili waende pamoya naye kupiganisha maadui wa Israeli. Lakini ni sababu gani kabisa yenye iliwafanya wakasirike sana? Waliona kama walizarauliwa? Pengine. Ikuwe ni vile ao hapana, Gideoni alihangaikia namna walikuwa najisikia na aliwajibu kwa upole. Matokeo ilikuwa nini? ‘Kasirani yao ilipoa.’—Amu. 8:1-3.

10. Ni nini itatusaidia kujibia watu wenye wanapinga mambo yenye tunaamini? (1 Petro 3:15)

10 Mufanyakazi mwenzetu ao mwanafunzi mwenzetu anaweza kuonyesha kama hakubaliane na mafundisho yetu fulani kuhusu mwenendo. Tutajikaza kutetea mambo yenye tunaamini, lakini tutafanya vile kwa kuheshimia mawazo yake. (Soma 1 Petro 3:15.) Kuliko kuwaza kama anapenda tu kupinga mambo yenye tunaamini, tuone ulizo yake kuwa nafasi ya kujua mambo yenye anaona kuwa ya maana. Hata sababu ikuwe gani yenye inafanya mutu aulize ulizo fulani, ni muzuri tumujibie kwa upole na kwa utulivu. Jibu yetu inaweza kumuchochea achunguze tena mambo yenye anaamini. Hata kama anazungumuza na siye kwa ukali ao kwa zarau, siye tunapaswa kumujibia kwa upole.—Ro. 12:17.

Tunaweza kujibia muzuri zaidi, ikiwa tunafikiri kwanza juu ya sababu zenye pengine zilifanya mutu atualike ku sikukuu ya kuzaliwa (Ona fungu ya 11-12)

11-12. (a) Tunapaswa kufikiria maulizo gani mbele ya kujibia ulizo ya nguvu? (Ona pia picha.) (b) Toa mufano wenye kuonyesha namna kuuliza ulizo kunaweza kutupatia nafasi ya kuzungumuza na mutu.

11 Kwa mufano, kama mufanyakazi mwenzako anakuuliza juu ya nini hatufanyake sikukuu za kuzaliwa, fikiria hii maulizo: Anapenda kujua ikiwa na siye tunaruhusiwa kujifurahisha? Ao anaona kama uamuzi wetu utaharibisha hali ya kirafiki yenye kuwa kati ya wafanyakazi? Tunaweza kutuliza mufanyakazi mwenzetu kwa kumuambia kama tunafurahi kuona namna anahangaikia wafanyakazi wenzake na kumuhakikishia kama na siye tunapenda kuendelea kuwa na uhusiano muzuri pamoya na wafanyakazi wenzetu. Ile inaweza kutupatia nafasi ya kuzungumuza naye kwa utulivu kuhusu mambo yenye Biblia inasema juu ya sikukuu za kuzaliwa.

12 Tunaweza kutumia ule ufundi wa kuzungumuza na watu wakati wengine wanatuuliza maulizo yenye inaletaka ubishi sana. Mwanafunzi mwenzako anaweza kusema kama Mashahidi wa Yehova wanapaswa kubadilisha mawazo yao kuhusu ngono kati ya wanaume na wanaume na wanamuke na wanamuke. Anasema vile juu haelewe mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanaamini? Ao pengine rafiki yake ao mutu fulani wa familia yake iko mu uhusiano wa vile? Anawaza kama hatupendake wale watu? Tunaweza kumuhakikishia kama tunahangaikia watu wote. Na tunajua kama kila mutu iko na uhuru wa kujikamatia maamuzi. b (1 Pe. 2:17) Ile inaweza kutupatia nafasi ya kuzungumuza naye kuhusu faida ya kufuata kanuni za mwenendo zenye kuzungumuziwa mu Biblia.

13. Namna gani tunaweza kusaidia mutu mwenye anasema kama kuamini Mungu ni kukosa akili?

13 Wakati mutu anashikilia sana mawazo yake, tusikuwe haraka kuwaza kama tunajua mambo yenye anaamini. (Tit. 3:2) Kwa mufano, kama mwanafunzi mwenzako anasema kuwa ni kukosa akili kuamini kama Mungu iko, je, unapaswa kuwaza kama anaamini kabisa mageuzi na anajua mambo mingi kuhusu mageuzi? Kusema kweli, pengine hayafikiriaka sana ile jambo. Kuliko kuanza kubishana naye juu ya mambo ya sayansi, ona namna unaweza kumutolea habari yenye ataendelea kufikiria. Pengine unaweza kumuonyesha habari zenye kuzungumuzia uumbaji zenye kuwa ku jw.org. Kisha pengine atakuwa tayari kuzungumuzia habari ao video fulani yenye alipata ku site yetu. Kwa kweli, kuzungumuza naye kwa heshima kunaweza kumuchochea achunguze tena mawazo yake.

14. Namna gani Niall alitumia muzuri site yetu ili kurekebisha mawazo ya uongo ya mwanafunzi mwenzake kuhusu Mashahidi wa Yehova?

14 Kijana fulani mwenye kuitwa Niall alitumia site yetu ili kusaidia wengine waone kama mambo fulani yenye watu wanasema juu ya Mashahidi wa Yehova haiko ya kweli. Anasema hivi. “Mwanafunzi mwenzangu alizoea kuniambia kama siamini sayansi juu ninaamini kitabu ya mambo ya kuwazia-wazia kuliko kuamini mambo ya kweli yenye imehakikishwa.” Juu ule mwanafunzi hakuachia Niall nafasi ya kufasiria mambo yenye anaamini, Niall alimupendekeza asome habari zenye kuwa ku sehemu “Sayansi na Biblia” ku jw.org. Kisha pale, Niall alitambua kama inawezekana ule mwanafunzi alisoma habari zenye kuwa ku ile sehemu na alikuwa tayari zaidi kuzungumuza kuhusu namna uzima ulianza. Na weye unaweza kupata matokeo ya vile.

MUJITAYARISHE MU FAMILIA

15. Namna gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wajibie kwa upole wakati wanafunzi wenzao wanapinga mambo yenye wanaamini?

15 Wazazi wanaweza kufundisha watoto wao namna ya kujibia kwa upole wakati wengine wanapinga mambo yenye wanaamini. (Yak. 3:13) Wazazi fulani wanafanya mazoezi pamoya na watoto wao wakati wa ibada ya familia. Wanafikiria habari ao maulizo yenye watoto wao wanaweza kuulizwa ku masomo, wanaizungumuzia, na wanafanya maonyesho juu ya namna ya kujibia. Pia wanafundisha watoto wao namna ya kuzungumuza kwa upole na mu njia yenye inaweza kuvutia.—Ona kisanduku “ Kufanya Mazoezi Kunaweza Kusaidia Familia Yenu.”

16-17. Namna gani mazoezi inaweza kusaidia vijana?

16 Kufanya mazoezi kunaweza kusaidia Wakristo watetee imani yao mu njia yenye kusadikisha, na kujihakikishia wenyewe kama wako na sababu za muzuri za kuamini mafundisho ya Biblia. Ku jw.org, mu sehemu “Vijana Wanauliza” muko karatasi za mazoezi kwa ajili ya vijana. Zimetayarishwa ili kusaidia vijana watie nguvu imani yao na watayarishe majibu mu maneno yao wenyewe. Kama munajifunza habari zenye kuwa mu ile sehemu katika familia, nyie wote munaweza kujua namna ya kutetea imani yenu kwa upole na mu njia yenye kuvutia.

17 Kijana mwenye kuitwa Matthew anaeleza namna kufanya mazoezi kulimusaidia. Mu ibada yao ya familia, Matthew na wazazi wake wanazoea kufanya utafiti juu ya habari zenye zinaweza kuzungumuziwa ku masomo. Anasema hivi: “Tunafikiriaka hali zenye zinaweza kutokea, na kwa kutumia mambo yenye tulipata wakati tulikuwa tunafanya utafiti, tunafanya mazoezi juu ya namna ya kujibia. Wakati ninaelewa juu ya nini ninaamini jambo fulani, ninakuwaka mwenye kutulia na inakuwaka mwepesi kuwa mupole wakati niko nazungumuza na wengine.”

18. Kulingana na Wakolosai 4:6 ni jambo ya maana kufanya nini?

18 Kusema kweli, watu fulani hawataamini mambo yenye tunawaambia hata kama tunafikiri nao mu njia yenye kusadikisha. Lakini kuzungumuza kwa busara na kwa upole kunaweza kusaidia. (Soma Wakolosai 4:6.) Kuelezea wengine mambo yenye tunaamini iko sawa vile kutupia mutu kabumbu. Tunaweza kuitupa kwa upole ao kwa nguvu sana. Kama tunaitupa kwa upole, itakuwa mwepesi zaidi kwa mutu mwenye tuko nacheza naye kuishika na kuendelea kucheza. Vilevile, kama tunazungumuza kwa busara na kwa upole, watu wanaweza kuwa tayari zaidi kusikiliza, na kuendelea kuzungumuza na siye. Kama mutu anapenda tu kubishana ao kuchambua mambo yenye tunaamini, hatulazimike kuendelea kuzungumuza naye. (Mez. 26:4) Lakini watu wa vile hawakuwake wengi; watu fulani, na hata watu wengi, wanakuwaka tayari kusikiliza.

19. Ni nini inapaswa kutuchochea kuwa wapole wakati tuko natetea mambo yenye tunaamini?

19 Ni wazi kama kujikaza kukomalisha sifa ya upole kuko na faida sana. Umuombe Yehova akupatie nguvu yenye uko nayo lazima ili uendelee kuwa mupole wakati uko najibia maulizo yenye inaletaka ubishi sana, ao wakati wengine wanachambua mambo yenye tunaamini. Kumbuka kama, kuwa mupole kutasaidia musifikie ku mabishano hata kama muko na mawazo tofauti. Kujibia kwa upole na kwa heshima, kunaweza kuchochea watu fulani wabadilishe mawazo yao juu yetu na juu ya mafundisho ya Biblia. ‘Sikuzote mukuwe tayari kutetea’ mambo yenye munaamini, na “mufanye vile kwa upole na heshima kubwa.” (1 Pe. 3:15) Ukomalishe basi sifa ya upole, juu haiko uzaifu lakini ni nguvu!

WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako

a Hii habari iko na mapendekezo juu ya namna ya kutetea kwa upole mambo yenye tunaamini wakati wengine wanaipinga.

b Ili kupata mapendekezo ingine, ona habari “Biblia Inasema Nini Juu ya Mwanaume Kulala na Mwanaume ao Mwanamuke Kulala na Mwanamuke?” mu Amuka! ya 2016 Na. 4.

c Unaweza kupata mapendekezo ingine ku jw.org mu habari zenye kuwa mu sehemu “Vijana Wanauliza” na mu sehemu “Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova.”