Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 39

WIMBO 125 “Wenye Furaha Ni Wale Wenye Rehema!”

Kutoa Kutakuletea Furaha

Kutoa Kutakuletea Furaha

“Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”MDO. 20:35.

WAZO KUBWA

Namna tunaweza kuendelea kuwa na furaha na kuongeza furaha yetu ya kutoa.

1-2. Juu ya nini Yehova alituumba mu namna yenye inafanya tukuwe na furaha wakati tunapatia wengine?

 YEHOVA aliumba wanadamu mu namna yenye inafanya wakuwe na furaha zaidi wakati wanatoa kuliko wakati wanapokea. (Mdo. 20:35) Ni kusema hatusikiake furaha wakati tunapokea? Hapana, siye wenyewe tumejionea kama tunajisikiaka muzuri wakati tunapewa zawadi. Lakini tunasikiaka furaha zaidi wakati siye njo tunapatia wengine zawadi. Na kama Yehova alituumba vile, ni juu ya faida yetu. Juu ya nini tunasema vile?

2 Juu Yehova alituumba vile, tunaweza kuongeza furaha yetu. Tunaweza kufanya vile kwa kutafuta nafasi zingine za kupatia watu. Hauone kama tuliumbwa mu njia ya ajabu?—Zb. 139:14.

3. Juu ya nini Yehova anaitwa “Mungu mwenye furaha”?

3 Maandiko inatuhakikishia kama kutoa kunaleta furaha. Kwa hiyo, haishangaze kuona kama Biblia inamuita Yehova kuwa “Mungu mwenye furaha.” (1 Ti. 1:11) Yeye njo wa kwanza kupatia wengine na hakuna mutu mwenye anatoaka sana kumupita. Mutume Paulo alisema kama ni kwa sababu yake njo “tuko na uzima na tunatembea na tuko.” (Mdo. 17:28) Na hata “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu” inatoka kwa Yehova.—Yak. 1:17.

4. Ni nini itatusaidia kuwa na furaha zaidi?

4 Kila mumoya wetu anaweza kupenda kuwa na furaha zaidi yenye inatokana na kutoa. Tunaweza kupata ile furaha kwa kuiga ukarimu wa Yehova. (Efe. 5:1) Mu hii habari tutaona mambo yenye tunaweza kufanya ikiwa tunawaza kama wengine hawaonyeshe shukrani juu ya mambo yenye tuko nawafanyia. Tutaona pia mambo yenye itatusaidia kuwa na furaha ao kuongeza furaha yenye tunapataka wakati tunatoa.

IGA UKARIMU WA YEHOVA

5. Yehova anatupatia vitu gani?

5 Ni mu njia gani fulani Yehova anaonyesha ukarimu? Tuzungumuzie mifano fulani. Yehova anatupatia vitu vya kimwili. Ni kweli kwamba hatukuwake sikuzote na vitu vya bei sana. Lakini Yehova anahakikisha kila siku kama tuko na vitu vyenye tuko navyo lazima. Kwa mufano, anahakikisha kama tuko na chakula, manguo, na fasi ya kuishi. (Zb. 4:8; Mt. 6:31-33; 1 Ti. 6:6-8) Yehova anatupatia vitu vya kimwili juu tu analazimika kufanya vile? Hapana. Sasa juu ya nini Yehova anatupatia vile vitu?

6. Matayo 6:25, 26 inatufundisha nini?

6 Kwa kifupi, Yehova anatupatia vitu vyenye tuko navyo lazima kwa sababu anatupenda. Ona maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 6:25, 26. (Soma.) Yesu alitumia mufano wa uumbaji. Wakati alizungumuzia ndege, alisema hivi: “Hawapande mbegu ao kuvuna ao kukusanya katika madepo.” Kisha Yesu alisema hivi: “Baba yenu wa mbinguni anawalisha.” Na kisha akauliza hivi: “Je, ninyi hamuko wa maana kuliko wao?” Yesu alipenda kufundisha nini? Yehova anaona waabudu wake kuwa wa maana zaidi kuliko wanyama. Juu Yehova anahangaikia wanyama, tuko hakika kama atatupatia vitu vyenye tuko nayo lazima. Sawa baba, Yehova anahangaikia familia yake kwa upendo.—Zb. 145:16; Mt. 6:32.

7. Ni mu njia gani moya, tunaweza kuiga ukarimu wa Yehova? (Ona pia picha.)

7 Sawa vile Yehova, na siye tunaweza kupatia watu vitu juu tunawapenda. Kwa mufano, unajua ndugu ao dada fulani mwenye iko na lazima ya chakula ao manguo? Yehova anaweza kukutumikisha juu amupatie ule mutu vitu vyenye iko navyo lazima. Watu wa Yehova wanajulikana kuwa watu wakarimu, zaidi sana wakati wa misiba. Kwa mufano mu kipindi ya Korona ndugu na dada walitolea wengine chakula, manguo, na vitu vingine vya lazima. Pia wengi walitoa michango juu ya kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote. Ile michango ilifanya iwezekane kusaidia ndugu na dada wa mu dunia yote mu ile kipindi ya nguvu. Wale ndugu na dada wakarimu walifuata shauri yenye kuwa mu Waebrania 13:16 yenye inasema: “Musisahau kutenda mema na kushiriki pamoja na wengine vile vyenye muko navyo, kwa maana Mungu anapendezwa na zabihu za namna hiyo.”

Siye wote tunaweza kuiga ukarimu wa Yehova (Ona fungu ya 7)


8. Yehova anatupatia nguvu namna gani? (Wafilipi 2:13)

8 Yehova anatupatia nguvu. Yehova iko tayari kupatia nguvu zake zenye hazina mipaka waabudu wake waaminifu. (Soma Wafilipi 2:13.) Ulishakamuomba Yehova nguvu ya kushinda jaribu ao ya kuvumilia jaribu? Ao ulishakamuomba Yehova nguvu ya kuvumilia siku ingine moya? Juu sala yako ya kuomba nguvu ilijibiwa, unakubaliana na hii maneno ya Paulo. Aliandika: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.”—Flp. 4:13.

9. Yehova anatupatia nguvu kwa ukarimu, tunaweza kumuiga namna gani? (Ona pia picha.)

9 Hata kama tuko wanadamu wenye hawakamilike, tunaweza kuiga namna ya Yehova ya kutumikisha nguvu yake. Ni kweli kwamba hatuna uwezo wa kupatia wengine nguvu, lakini tunaweza kutumikisha nguvu yetu ili kusaidia wengine. Kwa mufano unaweza kusaidia ndugu ao dada wenye kuzeeka ao wenye ni wagonjwa kuhangaikia nyumba ao kuenda kuuza vitu fulani. Kama hali yetu inaturuhusu tunaweza kujitoa juu ya kusaidia kusafisha na kutunza Jumba ya Ufalme. Kutumikisha nguvu yetu mu ile njia inaweza kuletea faida waabudu wengine wa Yehova.

Tunaweza kutumikisha nguvu yetu kwa ajili ya wengine (Ona fungu ya 9)


10. Namna gani tunaweza kutia wengine nguvu kupitia maneno yetu?

10 Usisahau kama maneno inakuwaka na nguvu. Unajua mutu mwenye anaweza kufurahi kama unamupongeza? Unajua mutu fulani mwenye iko na lazima ya kutiwa moyo? Kama ni vile onyesha ule mutu kama unamuhangaikia. Unaweza kumuita ku telefone ao kumuandikia ujumbe. Usitafutishe sana maneno ya kusema. Maneno ya mwepesi yenye kutoka mu moyo, inaweza kuwa njo yenye ndugu yako iko nayo lazima juu aendelee kuwa muaminifu na ajisikie muzuri.—Mez. 12:25; Efe. 4:29.

11. Yehova anatumia hekima yake namna gani?

11 Yehova anatupatia hekima. Mutume Yakobo aliandika hivi: “Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anapatia wote kwa ukarimu na bila kutafuta-tafuta makosa.” (Yak. 1:5; maelezo ya chini) Ile maneno inaonyesha kama Yehova haiko muchoyo. Anapatia wengine kwa ukarimu hekima yake. Ona kama wakati Yehova anapatia wengine hekima yake, anafanya vile “bila kulaumu,” ao “bila kutafuta-tafuta makosa.” Hapendi tujisikie mubaya juu tuko na lazima ya muongozo wake. Na hata, anatutia moyo tutafute muongozo wake.—Mez. 2:1-6.

12. Tuko na nafasi gani za kupatia wengine hekima yenye tuko nayo?

12 Halafu siye, tunaweza kumuiga Yehova kwa kupatia wengine hekima yenye tuko nayo? (Zb. 32:8) Watu wa Yehova wako na nafasi za mingi za kufundisha wengine mambo yenye wamejifunza. Mara mingi tunazoezaka wapya mu mahubiri. Wazee wanazoezaka kwa uvumilivu watumishi wa huduma na ndugu mu kutaniko wenye kubatizwa watimize muzuri migao yao mu kutaniko. Na ndugu na dada wenye kuwa na ufundi mu kazi ya kujenga na kutunza majengo wanasaidia kuzoeza wengine juu waweze kuhangaikia majengo ya tengenezo ya Yehova.

13. Wakati tuko nazoeza wengine, namna gani tunaweza kuiga namna ya Yehova ya kupatia wengine hekima?

13 Ni muzuri wale wenye wanazoeza wengine waige namna ya Yehova ya kupatia wengine hekima. Kumbuka kama Yehova anatoa hekima yake kwa ukarimu. Na siye tunaonyesha wengine mambo yote yenye tunajua. Hatufiche mambo fulani yenye tunajua juu ya kuogopa kama ule mwenye tuko nazoeza atakamata fasi yetu. Ao hatusemake: ‘Hakuna mwenye alinifundishaka, naye ajifunze ye peke.’ Ile mawazo ya vile haipaswe kuwa kati ya watu wa Yehova. Kwa furaha tunatoa mambo yenye tunajua lakini pia ‘tunapenda kuwapatia uzima wetu wenyewe’ wale wenye tuko nazoeza. (1 Te. 2:8) Tunatumaini kama, “nao watastahili kabisa kufundisha wengine.” (2 Ti. 2:1, 2) Kama kila mumoya wetu anapatia wengine hekima yenye iko nayo, siye wote tutaendelea kuwa na furaha zaidi.

IKIWA TUNAWAZA KAMA WENGINE HAWANA SHUKRANI

14. Mara mingi watu wengi wanatenda namna gani wakati tunawaonyesha ukarimu?

14 Wakati tunaonyesha ukarimu, zaidi sana ndugu na dada zetu, mara mingi wanatuonyesha shukrani. Wanaweza kuandika maneno fulani ya kushukuru ao kuonyesha shukrani mu njia ingine. (Kol. 3:15) Kupata ile maneno ya shukrani kunatuongezea furaha.

15. Tunapaswa kukumbuka nini wakati mutu haonyeshe shukrani?

15 Kusema kweli, watu fulani hawataonyesha shukrani. Tunaweza kutumikisha nguvu yetu, wakati yetu, ao hata vitu vyetu juu ya kusaidia mutu, lakini ule mutu haonyeshe kama anafurahia mambo yenye tulimufanyia. Kama hali ya vile inafika, namna gani tunaweza kuepuka kukasirika na kupoteza furaha yetu? Kumbuka maneno ya andiko yetu ya musingi, Matendo 20:35. Furaha yetu ya kutoa haitegemee namna watu watatenda wakati tunawapatia kitu fulani. Tunaweza kuamua kuendelea kuwa na furaha hata kama wengine hawaonyeshe shukrani. Namna gani? Tuzungumuzie njia fulani.

16. Wakati tunapatia watu ao tuko wakarimu, tunapaswa kukumbuka nini?

16 Kumbuka kama ni Yehova njo tuko naiga. Anapatia watu vitu vizuri ikuwe wataonyesha shukrani ao hapana. (Mt. 5:43-48) Yehova anaahidi kama ikiwa na siye tunapatia wengine “bila kutumaini kurudishiwa kitu chochote, zawabu [yetu] itakuwa kubwa.” (Lu. 6:35) “Kitu chochote” kinaweza kuwa kuonyeshwa shukrani. Ikuwe wengine wanaonyesha shukrani ao hapana, Yehova atatulipa juu ya mambo ya muzuri yenye tuko nafanya, juu ‘tunatoa kwa furaha.’—Mez. 19:17; 2 Ko. 9:7.

17. Ni sababu gani ya maana sana yenye inatuchochea kupatia wengine? (Luka 14:12-14)

17 Jambo ingine ya maana sana yenye tunaweza kufanya juu ya kumuiga Yehova ni kufuata mambo yenye Yesu alisema mu Luka 14:12-14. (Soma.) Haiko mubaya kuonyesha ukarimu wale wenye watatuonyesha pia ukarimu. Lakini tuseme nini basi kama tunaonyeshaka ukarimu juu tu wengine nao watuonyeshe ukarimu? Kama tunafanyaka vile tujikaze kufuata shauri ya Yesu. Tunaweza kuonyesha ukarimu mutu mwenye tunajua kama hana uwezo wa kutuonyesha ukarimu. Tukifanya vile, tutakuwa na furaha juu tuko namuiga Yehova. Ile itatusaidia pia tuendelee kuwa na furaha wakati wengine hawatuonyeshe shukrani.

18. Tunapaswa kuepuka nini na juu ya nini?

18 Tunapaswa kuepuka kushakia nia ya wengine. (1 Ko. 13:7) Kama mutu hatuonyeshe shukrani tunaweza kujiuliza: ‘Huyu mutu hana shukrani ao alisahau tu kuonyesha shukrani?’ Pengine kuko sababu zingine zenye zilifanya asionyeshe shukrani vile tuliwazia. Watu fulani ni wenye shukrani, lakini hawajue namna ya kuionyesha. Wanaweza kusikia haya kupokea musaada, zaidi sana kama zamani ni wao njo walikuwa nasaidia wengine. Hata ikuwe nini njo ilifanya wasionyeshe shukrani, upendo wa Kikristo utatusaidia tusiwawazie mubaya na tuendelee kuwa na furaha ya kutoa.—Efe. 4:2.

19-20. Juu ya nini uvumilivu ni wa maana wakati tunapatia wengine? (Ona pia picha.)

19 Ukuwe na uvumilivu. Mufalme mwenye hekima Sulemani aliandika hivi kuhusu ukarimu: “Tupa mukate wako juu ya maji, kwa maana kisha siku nyingi utaupata tena.” (Muh. 11:1) Sawa vile hii maneno inaonyesha watu fulani wanaweza kutuonyesha shukrani kisha wakati murefu ni kusema, “kisha siku nyingi.” Tuone mufano yenye inaonyesha vile.

20 Kumepita miaka mingi bibi moya wa mwangalizi wa muzunguko, aliandikia barua yenye kutia moyo dada moya mwenye alitoka tu kubatizwa, alimutia moyo aendelee kuwa muaminifu. Kisha karibu miaka munane ule dada alijibia kwa kuandika barua, alisema hivi: “Nilipenda kukuandikia juu ujue namna ulinisaidia mu hii miaka yenye imepita bila hata weye kujua. Barua yenye uliniandikia ilikuwa ya muzuri. Lakini ni andiko yenye uliniandikiaka mu ile barua njo iligusa sana moyo wangu na siwezi kuisahau.” a Kisha kuzungumuzia magumu fulani yenye alipata, ule dada alisema tena hivi: “Wakati fulani nilipenda nibiache, niache kweli, ni biaache tu byote. Lakini nilikuwa nakumbuka andiko yenye uliniandikiaka, na ilinipatia nguvu ya kuendelea kuwa muaminifu mu hii miaka munane yote. Hakuna kitu yenye ilinisaidia sana kupita barua yako na andiko yenye ulinipatia.” Wazia namna ule bibi ya mwangalizi alifurahi sana wakati alipata ile barua “kisha siku nyingi”! Mutu anaweza kutuonyesha shukrani juu ya mambo yenye tulimufanyiaka hata kama kulishapita wakati murefu.

Mutu anaweza kutuonyesha shukrani hata kisha wakati murefu (Ona fungu ya 20) b


21. Juu ya nini unaazimia kabisa kuendelea kuiga ukarimu wa Yehova?

21 Sawa vile tuliona Yehova alituumba mu njia ya ajabu. Ni kweli tunakuwaka na furaha wakati tunapewa, lakini tunakuwaka na furaha zaidi wakati tunapatia wengine. Tunajisikiaka muzuri wakati tunasaidia ndugu zetu. Na tunafurahi wakati wanatuonyesha shukrani. Lakini ikuwe wanaonyesha shukrani ao hapana, tutakuwa na furaha juu tunajua kama tulifanya jambo ya muzuri. Usisahau kama hata kama unapatia wengine nini, “Yehova anaweza kukupatia nyingi zaidi.” (2 Ny. 25:9) Hata tupatie wengine nini Yehova atatupatia vitu mingi zaidi kupita vyenye tunapatia wengine! Na hakuna furaha yenye inapita furaha ya kubarikiwa na Yehova mwenyewe. Basi tuazimie kuiga Baba yetu wa mbinguni mwenye ukarimu.

WIMBO 17 “Ninataka”

a Andiko yenye bibi ya mwangalizi alipatia ule dada ni 2 Yohana 8, yenye inasema: “Mufanye angalisho, ili musipoteze mambo yenye tumefanya kazi ili kuyatokeza, lakini ili mupate zawabu kamili.”

b MAFASIRIO YA PICHA : Hii picha inaonyesha vile mambo ilikuwa, bibi ya mwangalizi iko naandika barua yenye kutia moyo, kisha miaka anapokea barua ya shukrani.