Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 4

Juu ya Nini Tunahuzuriaka Ukumbusho?

Juu ya Nini Tunahuzuriaka Ukumbusho?

“Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”​—LU. 22:19.

WIMBO 20 Ulimutoa Mwana Wako Mupendwa

KIFUPI YA HABARI *

1-2. (a) Ni wakati gani zaidi sana tunakumbukaka mupendwa wetu mwenye alishakufa? (b) Ni jambo gani Yesu alianzisha usiku mbele akufe?

HATA kama wapendwa wetu wamekufa kumepita miaka ngapi, tunaendelea tu kuwakumbuka. Mara mingi tunawakumbukaka sana kila mwaka wakati inafika tarehe ya siku yenye walikufaka.

2 Kila mwaka, tunakuwaka kati ya mamilioni ya watu wenye kuishi mu dunia wenye wanakusanyikaka ili kukumbuka kifo ya mutu fulani mwenye tunapenda sana, Yesu Kristo. (1 Pe. 1:8) Tunakusanyikaka ili kukumbuka ule mwenye alitoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi ili kutukomboa kutoka mu zambi na kifo. (Mt. 20:28) Kwa kweli, Yesu anapenda wanafunzi wake wakumbuke kifo yake. Njo maana usiku wenye ulitangulia kifo yake alianzisha chakula cha mangaribi cha pekee sana na alitoa hii amri: “Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.” *​—Lu. 22:19.

3. Ni mambo gani tutachunguza mu hii habari?

3 Ni watu kidogo tu kati ya wale wenye wanahuzuriaka Ukumbusho wa kifo ya Yesu njo wako na tumaini ya kuenda kuishi mbinguni. Lakini hata mamilioni ya wale wenye wako na tumaini ya kuishi hapa ku dunia nao pia wanahuzuriaka. Mu hii habari, tutachunguza sababu zenye zinafanyaka wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi mbinguni na wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi hapa ku dunia wachunge kwa hamu kuhuzuria Ukumbusho kila mwaka. Tena, tutaona faida yenye tunapata kwa kuhuzuria ile Ukumbusho. Muache tuanze kwa kuchunguza kwanza sababu fulani zenye zinafanyaka watiwa-mafuta wahuzurie Ukumbusho.

JUU YA NINI WATIWA-MAFUTA WANAHUZURIAKA UKUMBUSHO?

4. Juu ya nini watiwa-mafuta njo wenye wanakulaka mukate na kunywa divai ku Ukumbusho?

4 Kila mwaka, watiwa-mafuta wanachungaka kwa hamu kuhuzuria Ukumbusho wakiwa washiriki. Juu ya nini inafaa kabisa wakule mukate na kunywa divai? Juu ya kujibia ile ulizo, fikiria mambo yenye ilitokea usiku wa mwisho wa maisha ya Yesu hapa ku dunia. Kisha kusherehekea Pasaka, Yesu alianzisha ile yenye ilifikia kuitwa Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Alipitisha mukate na divai kwa mitume wake 11 waaminifu na aliwaambia wakule ile mukate na kunywa ile divai. Yesu alizungumuza nao kuhusu maagano mbili ao mapatano, ni kusema, Agano Jipya na Agano ya Ufalme. * (Lu. 22:19, 20, 28-30) Ile maagano ilifungulia njia wale mitume wake na hesabu ingine kidogo ya wenye wangefikia kuwa wafalme na makuhani mbinguni. (Ufu. 5:10; 14:1) Ni mabaki ya watiwa-mafuta tu, * wenye kuwa mu ile maagano, njo wanakulaka mukate na kunywa divai ku Ukumbusho.

5. Watiwa-mafuta wanatambua nini kuhusu tumaini yenye wamepewa?

5 Ona sababu ingine yenye inafanya watiwa-mafuta wachunge kwa hamu sana kuhuzuria Ukumbusho. Ile Ukumbusho inawapatia nafasi ya kufikiria sana tumaini yao. Yehova aliwapatia tumaini ya pekee, ya kufurahia uzima wenye hauwezi kuharibika na wenye hauwezi kufa kule mbinguni na kutumika pamoja na Yesu Kristo mwenye ametukuzwa na pamoja na wengine wenye kufanyiza ile hesabu ya 144 000. Na zaidi ya yote, kuwa mbele ya Yehova Mungu! (1 Ko. 15:51-53; 1 Yo. 3:2) Wakristo watiwa-mafuta wanatambua kama walialikwa kufurahia ile mapendeleo yote mbinguni. Lakini ili waende mbinguni, wanapaswa kubakia waaminifu mupaka kifo yao. (2 Ti. 4:7, 8) Watiwa-mafuta wanafurahi sana wakati wanafikiria tumaini yao ya kuenda kuishi mbinguni. (Tit. 2:13) Tuseme nini juu ya “kondoo wengine”? (Yoh. 10:16) Ni sababu gani fulani zinafanyaka wahuzurie Ukumbusho?

JUU YA NINI KONDOO WENGINE WANAHUZURIAKA UKUMBUSHO?

6. Juu ya nini kondoo wengine wanahuzuriaka Ukumbusho kila mwaka?

6 Wengine wanahuzuria Ukumbusho, hapana kama washiriki, lakini kama watazamaji. Mu 1938, wale wenye walikuwa na tumaini ya kuishi hapa ku dunia walialikwa kwa mara ya kwanza kuhuzuria Ukumbusho. Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 3, 1938, ulisema hivi: “Itafaa kabisa kwa [kondoo wengine] kuwa ku mukutano kama ule na kuangalia mambo yenye iko inafanyika. . . . Inapaswa pia kuwa wakati wao wa kufurahi na ni vile iko.” Sawa vile waalikwa wenye wanafurahi kutazama ao kuangalia karamu ya ndoa, kondoo wengine wanafurahi kuwa pale, ku Ukumbusho.

7. Juu ya nini kondoo wengine wanachungaka kwa hamu kusikiliza hotuba ya Ukumbusho?

7 Kondoo wengine wanafikiria pia tumaini yao. Wanachungaka kwa hamu kusikiliza hotuba ya Ukumbusho, juu ile hotuba inazungumuzia zaidi sana mambo yenye Kristo na wale watawala wenzake 144 000 watafanya kwa ajili ya wanadamu waaminifu mu kipindi ya utawala wa miaka elfu. Chini ya uongozi wa Mufalme wao Yesu Kristo, wale watawala wenye watatawala naye mbinguni watamusaidia kugeuza hii dunia kuwa Paradiso na kuongoza wanadamu watiifu kwenye ukamilifu. Ni jambo ya kufurahisha sana kwa mamilioni ya watazamaji wenye wanahuzuria Ukumbusho wakati wanafikiria namna maunabii ya Biblia itatimia wakati wenye kuja, maunabii sawa ile yenye kuwa mu Isaya 35:5, 6; 65:21-23; na Ufunuo 21:3, 4. Wakati wanajiwazia wao wenyewe pamoja na wapendwa wao mu dunia mupya, ile inatia nguvu tumaini yao kwa ajili ya wakati wenye kuja na inawachochea kuendelea kumutumikia Yehova bila kuacha.​—Mt. 24:13; Gal. 6:9.

8. Ni sababu gani ingine yenye inafanyaka kondoo wengine wahuzurie Ukumbusho?

8 Ona sababu ingine yenye inafanya kondoo wengine wahuzurie Ukumbusho. Wanapenda watiwa-mafuta na wanapenda kuwategemeza. Neno ya Mungu ilitabiri kama watiwa-mafuta na wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi hapa ku dunia wangetumika pamoja kwa umoja. Tunajua vile namna gani? Muache tuzungumuzie mifano fulani.

9. Namna gani unabii wenye kuwa mu Zekaria 8:23 unafasiria vile kondoo wengine wanajisikia kuhusu watiwa-mafuta?

9 Soma Zekaria 8:23. Hii unabii inazungumuzia kwa njia yenye kugusa moyo sana namna kondoo wengine wanajisikia kuhusu ndugu na dada zao watiwa-mafuta. Maneno “Muyahudi” na “ninyi” inazungumuzia kikundi moja, ni kusema, mabaki ya watiwa-mafuta. (Ro. 2:28, 29) Wale “watu kumi (10) kutoka katika luga zote za mataifa” wanafananisha kondoo wengine. ‘Wanashika kwa nguvu,’ ni kusema, wanashikamana na watiwa-mafuta kwa kujiunga nao mu ibada safi. Kwa hiyo, mu usiku ya Ukumbusho, kondoo wengine wanaonyesha kama wanashikamana kabisa na watiwa-mafuta kwa kuwa pale, ku Ukumbusho.

10. Namna gani Yehova alitimiza unabii wenye kuwa mu Ezekieli 37:15-19, 24, 25?

10 Soma Ezekieli 37:15-19, 24, 25. Ili kutimiza ile unabii, Yehova alifanya watiwa-mafuta na kondoo wengine watumike pamoja kwa ukaribu. Ile unabii inazungumuzia vipande mbili vya muti. Wale wenye wako na tumaini ya kuenda kuishi mbinguni wako kama kipande ya muti “kwa ajili ya Yuda” (kabila yenye wafalme wa Israeli walikuwa wanachaguliwa ndani), na wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi hapa ku dunia wako kama kipande ya muti “kwa ajili ya Efraimu.” * Yehova angeunganisha vile vikundi mbili ili vyote vifikie kuwa “kipande kimoja cha muti.” Ile inamaanisha kama wanamutumikia Mufalme wao Yesu Kristo kwa umoja. Kila mwaka, watiwa-mafuta na kondoo wengine wanahuzuria Ukumbusho, hapana kama vikundi mbili tofauti, lakini kama “kundi moja” chini ya “muchungaji mumoja.”​—Yoh. 10:16.

11. Namna gani “kondoo” wenye kuzungumuziwa mu Matayo 25:31-36, 40 wanaonyesha kama wanategemeza kabisa ndugu za Kristo?

11 Soma Matayo 25:31-36, 40. “Kondoo” wenye kuzungumuziwa mu hii mufano wanafananisha wenye haki mu siku za mwisho wenye wako na tumaini ya kuishi hapa ku dunia, ni kusema, kondoo wengine. Wako wanategemeza kwa ushikamanifu mabaki ya watiwa-mafuta kwa kuwasaidia kutimiza daraka yao nzito sana, ni kusema, kuhubiri habari njema mu dunia yote na kufanya wanafunzi.​—Mt. 24:14; 28:19, 20.

12-13. Ni mu njia gani zingine kondoo wengine wanaonyesha kama wanategemeza ndugu za Kristo?

12 Kila mwaka mu majuma yenye inapeleka ku Ukumbusho, kondoo wengine wanaonyesha kama wanategemeza ndugu za Kristo kwa kushiriki kwa bidii mu kampanye yenye kufanyiwa mu dunia yote ya kualika watu wenye kupendezwa ku Ukumbusho. (Ona kisanduku “ Uko Unapanga Mambo Fulani kwa Ajili ya Ukumbusho?”) Wanawasaidia pia kukamata mipango mbalimbali ili Ukumbusho ufanywe mu kila kutaniko katika dunia yote, hata kama makutaniko ya mingi haina watu wenye wanakulaka mukate na kunywa divai. Kondoo wengine wanafurahi sana kutegemeza ndugu za Kristo mu zile njia. Wale kondoo wanajua kama Yesu anaona kazi yenye wako wanafanya ili kutegemeza Wakristo watiwa-mafuta kuwa sawa vile ni yeye njo wako wanafanyia ayo.​—Mt. 25:37-40.

13 Ni sababu gani zingine zenye zinafanya tuhuzurie Ukumbusho, ikuwe tuko na tumaini ya kuishi mbinguni ao hapa ku dunia?

JUU YA NINI SIYE WOTE TUNAHUZURIAKA UKUMBUSHO?

14. Namna gani Yehova na Yesu wametuonyesha upendo mukubwa zaidi?

14Tunataka kumushukuru Yehova na Yesu Kristo juu ya upendo wenye walituonyesha. Yehova ametuonyesha mu njia mbalimbali kama anatupenda. Lakini kuko njia moja yenye inapita zote. Yehova alionyesha kama anatupenda sana kwa kumutuma Mwana wake ili ateseke na kufa kwa ajili yetu. (Yoh. 3:16) Kusema kweli, Yesu naye alionyesha upendo kabisa kwa kuwa tayari kutoa uzima wake kwa ajili yetu. (Yoh. 15:13) Hakuna jambo yoyote yenye tunaweza kulipa Yehova na Yesu juu ya upendo wenye walituonyesha. Lakini tunaweza kuonyesha shukrani yetu kupitia namna tunaishi kila siku. (Kol. 3:15) Na tunahuzuriaka Ukumbusho ili kufikiri juu ya upendo wenye walituonyesha, na kuwaonyesha kama tunawapenda.

15. Juu ya nini watiwa-mafuta na kondoo wengine wanasamini sana zawadi ya bei ya ukombozi?

15Tunasamini sana zawadi ya bei ya ukombozi. (Mt. 20:28) Watiwa-mafuta wanasamini sana bei ya ukombozi, yenye inafanya tumaini yao iwezekane. Kwa sababu wako na imani katika zabihu ya Yesu, Yehova amewatangaza kuwa wenye haki na kuwafanya kuwa watoto wake. (Ro. 5:1; 8:15-17, 23) Kondoo wengine pia wako wenye shukrani kwa ajili ya bei ya ukombozi. Juu wako na imani katika damu yenye Kristo alimwanga, wako na zamiri safi mbele ya Mungu, wanaweza kumutolea utumishi mutakatifu, na kuwa na tumaini ya kuokoka ‘kutoka katika taabu kubwa.’ (Ufu. 7:13-15) Njia moja yenye watiwa-mafuta na kondoo wengine wanaonyesha shukrani yao kwa ajili ya bei ya ukombozi, ni kwa kuhuzuria Ukumbusho kila mwaka.

16. Ni sababu gani ingine yenye inafanyaka tuhuzurie Ukumbusho?

16 Sababu ingine yenye inafanyaka tuhuzurie Ukumbusho ni kwamba tunapenda kutii Yesu. Hata kama tumaini yetu ni ya kuishi mbinguni ao hapa ku dunia, tunakamata kwa uzito amri yenye Yesu alitoa usiku wakati alianzisha Ukumbusho. Ile amri ilisema hivi: “Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”​—1 Ko. 11:23, 24.

TUNAPATA FAIDA GANI KWA KUHUZURIA UKUMBUSHO?

17. Namna gani Ukumbusho unatusaidia kumukaribia zaidi Yehova?

17Tunamukaribia zaidi Yehova. (Yak. 4:8) Kama vile tumejifunza, Ukumbusho unatupatia nafasi ya kufikiri juu ya tumaini yenye Yehova ametupatia na kufiriki sana juu ya upendo wenye ametuonyesha. (Yer. 29:11; 1 Yo. 4:8-10) Wakati tunafikiria kwa uzito tumaini yetu hakika juu ya wakati wenye kuja lakini pia upendo wa Yehova, ile inafanya tumupende tena zaidi na kutia nguvu urafiki wetu pamoja naye.​—Ro. 8:38, 39.

18. Kufikiri sana juu ya mufano wa Yesu kunatuchochea kufanya nini?

18Tunachochewa kuiga mufano wa Yesu. (1 Pe. 2:21) Masiku kidogo mbele ya Ukumbusho, tunakuwaka tunakaza akili juu ya habari za Biblia zenye kuzungumzia juma ya mwisho yenye Yesu alipitisha hapa ku dunia, kifo yake, na ufufuo wake. Na kisha mangaribi ya siku ya Ukumbusho, hotuba inatukumbushaka upendo wenye Yesu alituonyesha. (Efe. 5:2; 1 Yo. 3:16) Wakati tunasoma juu ya mufano muzuri wenye Yesu alituwekea na kufikiri sana juu ya ile, tunachochewa ‘kuendelea kutembea kama vile yeye alitembea.’​—1 Yo. 2:6.

19. Namna gani tunaweza kubakia katika upendo wa Mungu?

19Tunaazimia hata zaidi kubakia katika upendo wa Mungu. (Yud. 20, 21) Tunabakia katika upendo wa Mungu kwa kuendelea kufanya yote yenye tunaweza ili kumutii, kutakasa jina yake, na kufurahisha moyo wake. (Mez. 27:11; Mt. 6:9; 1 Yo. 5:3) Kukumbuka kifo ya Yesu kunatusaidia kuazimia hata zaidi kuendelea kuishi kila siku mu njia yenye itaonyesha kama tunapenda kubakia katika upendo wa Yehova milele na milele!

20. Ni sababu gani za muzuri tuko nazo zenye zinafanya tukuwe tunahuzuria Ukumbusho?

20 Ikuwe tumaini yetu ni ya kuishi mbinguni ao hapa ku dunia, tuko na sababu za muzuri kabisa za kuhuzuria Ukumbusho. Kila mwaka tunakusanyikaka pamoja siku ya Ukumbusho ili kukumbuka kifo ya mutu moja mwenye tunapenda sana, Yesu Kristo. Zaidi ya yote, tunakumbukaka tendo kubwa ya upendo, ni kusema, upendo wenye Yehova alituonyesha kwa kututolea Mwana wake kama bei ya ukombozi. Hii mwaka, tutafanya Ukumbusho mangaribi ya Siku ya Tano, tarehe 15 Mwezi wa 4, 2022. Tunamupenda Yehova na Mwana wake, njo maana mu tarehe ya kukumbuka kifo ya Yesu, hakuna jambo ya maana sana sawa vile kuwa pale ku Ukumbusho.

WIMBO 16 Tumusifu Yehova na Mwana Wake Mutiwa-Mafuta

^ fu. 5 Ikuwe tumaini yetu ni ya kuishi mbinguni ao hapa ku dunia katika paradiso, siye wote tunachungaka kwa hamu kuhuzuria Ukumbusho kila mwaka. Hii habari itazungumuzia sababu za kimaandiko zenye zinafanyaka tuhuzurie Ukumbusho kila mwaka na faida yenye tunapataka kwa kufanya vile.

^ fu. 2 Hii maneno inatafsiriwa pia hivi: “Fanyeni hivi kwa kunikumbuka mimi.” (La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo).

^ fu. 4 Ili kupata habari zaidi juu ya Agano Jipya na Agano ya Ufalme, ona habari “Mutakuwa ‘Ufalme wa Makuhani’” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 2014, uku. 13-17.

^ fu. 4 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Maneno mabaki ya watiwa-mafuta inamaanisha Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali bado wazima hapa ku dunia.

^ fu. 10 Ili kupata maelezo zaidi juu ya vile vipande mbili vya muti vyenye kuzungumuziwa mu Ezekieli sura ya 37, ona kitabu Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!, uku. 129-135, fu. 3-17.