Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 3

Machozi ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?

Machozi ya Yesu Inaweza Kutufundisha Nini?

“Yesu akatokwa na machozi.”​—YOH. 11:35.

WIMBO 17 “Ninataka”

KIFUPI YA HABARI *

1-3. Ni magumu gani yenye inaweza kufanya watu wa Yehova walie?

ULILIA mara ya mwisho wakati gani? Wakati fulani tunaliaka juu ya furaha. Lakini mara mingi tunaliaka juu tuko na huzuni. Kwa mufano, tunaweza kulia wakati tunapoteza mupendwa wetu. Dada Lorilei wa Amerika alisema hivi: “Wakati fulani nilikuwa mwenye kuhuzunika sana juu ya kifo ya mutoto yangu mwanamuke, na ilionekana sawa vile hakuna jambo yoyote yenye ingeweza kunifariji. Sikuwazia hata kama ningeweza kuvumilia.” *

2 Tunaweza kulia juu ya sababu zingine. Hiromi, dada moja painia mwenye kuishi Japani, anasema hivi: “Wakati fulani nakuwaka mwenye kuhuzunika juu watu wenye ninahubiria hawapendezwake na ujumbe wa Biblia. Na wakati ingine na machozi iko nanitoka, naombaka Yehova anisaidie nipate mutu fulani mwenye iko anatafuta kweli.”

3 Inakufikiaka na weye pia ujisikie sawa vile wale dada? Wengi kati yetu wanajisikiaka vile. (1 Pe. 5:9) Tunapenda ‘kumutumikia Yehova kwa furaha,’ lakini wakati fulani tunaweza kulia juu mutu fulani mwenye tunapenda alikufa ao juu tunajisikia kuwa wenye kushuka moyo ao juu tuko na hali yenye inajaribu ushikamanifu wetu kwa Mungu. (Zb. 6:6; 100:2) Tunaweza kufanya nini wakati tunajisikia vile?

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Tunaweza kujifunza mambo fulani kupitia mufano wa Yesu. Wakati fulani naye pia alikutana na mambo yenye ilifanya ahuzunike na ile ilifanya ‘atokwe na machozi.’ (Yoh. 11:35; Lu. 19:41; 22:44; Ebr. 5:7) Tujikumbushe ile mambo. Wakati tunafanya vile tutaona ni somo gani tunaweza kujifunza. Tutaona pia njia fulani zenye zitatusaidia kupambana na magumu fulani yenye kutufanya tulie.

YESU ALILIA JUU ALIHANGAIKIA MARAFIKI WAKE

Tegemeza wale wenye kuwa na huzuni sawa vile Yesu alifanya (Ona fungu ya 5-9) *

5. Ni mambo gani tunajifunza kuhusu Yesu mu habari yenye kuwa mu Yohana 11:32-36?

5 Mu kipindi ya baridi, ya 32 K.K.Y., rafiki wa karibu wa Yesu, Lazaro aligonjwaka na akakufa. (Yoh. 11:3, 14) Alikuwaka na dada wawili, Maria na Marta, na Yesu alipenda sana ile familia. Wale wanamuke, walihuzunika sana juu walipoteza ndugu yao mupendwa. Kisha Lazaro kufa, Yesu alisafiri ili kuenda mu muji wa Betania kwenye Maria na Marta waliishi. Wakati Marta alisikia kama Yesu anakuya alimukimbilia mbio ili kukutana naye. Waza namna Marta alikuwa mwenye kuhuzunika wakati alisema: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” (Yoh. 11:21) Kisha wakati kidogo saa yenye Yesu aliona Maria na wengine wenye walikuwa wanalia naye “akatokwa na machozi.”​—Soma Yohana 11:32-36.

6. Juu ya nini Yesu alilia mu ile hali?

6 Juu ya nini Yesu alilia mu ile hali? Kitabu Étude perspicace des Écritures inasema hivi: “Kifo ya rafiki yake Lazaro na huzuni ya dada za Lazaro ilifanya Yesu ‘asumbuke sana na atokwe na machozi.’” * Pengine Yesu alifikiria maumivu yenye rafiki yake mupendwa Lazaro alipata wakati alikuwa mugonjwa na kuwaza namna Lazaro alijisikia wakati aliona kama anakaribia kufa. Kusema kweli, Yesu naye alitokwa na machozi wakati aliona namna Maria na Marta walikuwa na huzuni mingi juu walipoteza ndugu yao. Kama umepoteza rafiki yako wa karibu sana ao mutu wa familia yako, bila shaka na weye pia ulihuzunika sana. Ona somo tatu zenye unaweza kujifunza kupitia ile tukio.

7. Yesu alilia juu marafiki wake walikufa, ile inaweza kutufundisha nini juu ya Yehova?

7Yehova anaelewa namna unajisikia. Yesu ni “mufano kamili” wa Baba yake. (Ebr. 1:3) Wakati Yesu alilia, alionyesha namna Baba yake anajisikiaka wakati mutu anapoteza mupendwa wake. (Yoh. 14:9) Kama ulipoteza mupendwa wako ukuwe hakika kama Yehova haone tu huzuni yako lakini pia anasikia mubaya. Anapenda kukuponyesha juu uko mwenye kuvunjika moyo.​—Zb. 34:18; 147:3.

8. Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama Yesu atafufua wapendwa wetu?

8Yesu anapenda kufufua wapendwa wako. Muda kidogo mbele Yesu alie, alimuhakikishia Marta hivi: “Ndugu yako atafufuka.” Marta aliamini Yesu. (Yoh. 11:23-27) Vile Marta alikuwa muabudu muaminifu wa Yehova, bila shaka alijua ufufuo mbalimbali wenye nabii Eliya na Elisha walifanyaka zamani. (1 Fa. 17:17-24; 2 Fa. 4:32-37) Na inawezekana alisikiaka habari juu ya ufufuo mbalimbali wenye Yesu alifanyaka. (Lu. 7:11-15; 8:41, 42, 49-56) Na weye pia unaweza kuwa hakika kama utaona tena wapendwa wako. Vile Yesu alilia wakati alikuwa anafariji marafiki wake wenye walipoteza wapendwa wao, ile inatuhakikishia kama Yesu anapenda kabisa kufufua wafu!

9. Sawa vile Yesu, namna gani tunaweza kusaidia wale wenye kuwa na huzuni? Leta mufano.

9Unaweza kusaidia wale wenye kuwa na huzuni. Yesu hakulia tu pamoja na Marta na Maria lakini pia aliwasikiliza na kuwafariji. Tunaweza pia kufanya vile juu ya wale wenye kuwa na huzuni. Dan, muzee moja mwenye kuishi Australia, anasema hivi: “Kisha kupoteza bibi yangu nilikuwa na lazima ya musaada. Ndugu wengi na bibi zao, mara mingi walikuwa tayari kunisikiliza. Hawakunizuia nionyeshe huzuni yangu na hawakunihukumu wakati nilikuwa nalia. Walinisaidia pia kufanya mambo fulani, sawa vile kusafisha gari yangu, kuuza vitu fulani, na kunisaidia kupika chakula wakati nilijisikia kama siwezi kufanya ile kazi yote miye peke. Na walisali pamoja na miye mara mingi. Walionyesha kabisa kama walikuwa marafiki wa kweli, ndugu wenye ‘wamezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.’”​—Mez. 17:17.

YESU ALILIA JUU ALIHANGAIKIA MAJIRANI WAKE

10. Fasiria tukio yenye kuwa mu Luka 19:36-40.

10 Yesu alifika Yerusalemu mu Nisani 9, mwaka wa 33 K.K.Y. Wakati alikaribia ile muji, watu wengi walikusanyika na kuanza kutandika nguo zao katika barabara mbele yake ili kuonyesha kama wanamukubali kuwa Mufalme wao. Ile siku ilikuwa kabisa wakati wa furaha. (Soma Luka 19:36-40.) Pengine njo maana wanafunzi wake hawakutazamia jambo yenye ingetokea. Biblia inasema: “Wakati [Yesu] alifika karibu, akaona muji na akaulilia.” Wakati macho yake ilikuwa inayala machozi, Yesu alitabiri kama mambo ya mubaya ilikuwa karibu kupata wakaaji wa Yerusalemu.​—Lu. 19:41-44.

11. Juu ya nini Yesu alililia wakaaji wa Yerusalemu?

11 Yesu alihuzunika sana sababu alijua kama ijapokuwa watu walimupokea muzuri, kwa ujumla watu wa eneo yake tayari walionyesha kama hawapendi kusikiliza ujumbe wa Ufalme. Matokeo ni kwamba, Yerusalemu ingeharibiwa na Muyahudi yeyote mwenye angeokoka uharibifu wa ile muji angepelekwa mu uhamisho. (Lu. 21:20-24) Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba sawa vile tu Yesu alisema mbele ya wakati, watu wengi walimukatala. Mu eneo yako, kwa ujumla watu wanaonaka namna gani ujumbe wa Ufalme? Kama ni watu kidogo tu njo wanapendezwa na kweli yenye unawafundishaka, machozi ya Yesu inaweza kukufundisha nini? Ona mambo tatu yenye tunaweza kujifunza.

12. Wakati fulani Yesu alilia kwa ajili ya majirani wake, ile inatufundisha nini kumuhusu Yehova?

12Yehova anahangaikia watu. Machozi ya Yesu inatukumbusha ni kwa kiasi gani Yehova anahangaikia watu. “Hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9) Leo, tunaonyesha kama tunapenda majirani wetu kwa kujikaza kufanya yetu yote ili kugusa mioyo yao kupitia habari njema yenye tunawatangazia.​—Mt. 22:39. *

Badilisha programu yako ya mahubiri sawa vile Yesu alifanya (Ona fungu ya 13-14) *

13-14. Namna gani Yesu alionyesha kama alisikilia watu huruma, na namna gani tunaweza kuwa na ile sifa?

13Yesu alihubiri kwa bidii sana. Alionyesha kama anapenda watu kwa kuendelea kuwafundisha wakati wowote. (Lu. 19:47, 48) Ni nini njo ilimuchochea kufanya vile? Yesu aliwasikilia huruma. Wakati fulani, watu wengi walipenda kusikiliza sana maneno ya Yesu mupaka ikafikia kwamba yeye na wanafunzi wake “hawakuweza hata kula chakula.” (Mk. 3:20) Alikuwa pia tayari hata usiku wakati wenye ulifaa sana kwa musikilizaji wake fulani. (Yoh. 3:1, 2) Watu wengi wenye walisikiaka ku mwanzo-mwanzo mambo yenye alikuwa anafundisha hawakufikia kuwa wanafunzi wake. Lakini wote wenye walimusikiliza walipata habari njema. Leo, tunapenda kupatia kila mutu nafasi ya kusikiliza habari njema. (Mdo. 10:42) Juu ya kufikia ile kusudi ni jambo ya lazima kubadilisha namna yetu ya kuhubiri.

14Ukuwe tayari kufanya mabadiliko yenye inaomba kufanya. Kama hatubadilishe wakati wenye tuko tunatumia ili kuhubiri, pengine tunaweza kukosa kupata watu wenye kuwa tayari kusikiliza habari njema. Matilda, mwenye ni painia, anasema hivi: “Miye na bwana yangu tunajikazaka kutembelea watu wakati mbalimbali. Kama ni asubui, tunakuwaka tunahubiria fasi ya biashara. Lakini wakati inakuwaka midi, saa yenye watu wako wanapita mu barabara tunatumiaka prezantware. Na kisha mangaribi, tunakutaka watu wengi kwao.” Kuliko kushikilia tu programu yenye ni muzuri kwetu, tunapaswa kuwa tayari kubadilisha programu yetu ili kuhubiri saa yenye inaweza kutusaidia kupata watu wengi zaidi. Tukifanya vile, tunaweza kuwa hakika kama tutamufurahisha Baba yetu Yehova.

YESU ALILIA JUU ALIHANGAIKIA SANA JINA YA BABA YAKE

Umulilie Yehova katika sala wakati uko mu magumu sawa vile Yesu alifanya (Ona fungu ya 15-17) *

15. Ni nini ilitokea usiku wa mwisho wa maisha ya Yesu kama vile inaonyeshwa mu Luka 22:39-44?

15 Mangaribi kabisa ya Nisani 14, mwaka wa 33 K.K.Y., Yesu alienda mu bustani ya Getsemane. Kule alimumwangia Yehova moyo wake. (Soma Luka 22:39-44.) Ni ile wakati ya magumu sana njo Yesu “alitoa sala za kumulilia Mungu . . . kwa vilio vyenye nguvu na machozi.” (Ebr. 5:7) Yesu alisali kwa ajili ya nini ile usiku mbele ya kifo yake? Alimuomba Yehova amupatie nguvu ya kubakia mushikamanifu kwake na ya kuendelea kufanya mapenzi yake. Yehova alisikia kilio ya Mwana wake na alimutumia malaika ili kumutia nguvu.

16. Juu ya nini Yesu alihangaishwa sana mu akili wakati alikuwa anasali mu bustani ya Getsemane?

16 Bila shaka, Yesu alisali kwa Baba yake akiwa analia mu bustani ya Getsemane juu alikuwa anafikiria sana namna angekufa kama mutu mwenye alimutukana Mungu. Alijua pia daraka nzito yenye alikuwa nayo, ni kusema, kutetea jina ya Baba yake. Kama na weye uko mu hali ya nguvu yenye inajaribu ushikamanifu wako kwa Yehova, machozi ya Yesu inaweza kukufundisha nini? Fikiria mambo ingine tatu yenye tunaweza kujifunza.

17. Yehova alijibia sala za Yesu, ile inaweza kutufundisha nini?

17Yehova anasikilizaka sala zako za kumulilia. Yehova alisikiliza sala za Yesu. Juu ya nini? Juu, Yesu alihangaikia sana kubakia mushikamanifu kwa Baba yake na kutetea jina yake. Kama na siye tunahangaikia sana ile mambo tukuwe hakika kama atajibia sala zetu za kuomba musaada.​—Zb. 145:18, 19.

18. Ni mu njia gani Yesu ni rafiki muzuri na mwenye kutuelewa?

18Yesu anaelewa namna unajisikia. Wakati tuko na mahangaiko tunapendaka kuwa na rafiki mwenye iko anaelewa namna tunajisikia, zaidi sana ule mwenye alipataka magumu sawa yetu. Yesu ni rafiki wa vile. Anajua maana ya kuwa muzaifu na ulazima wa kupata musaada. Anaelewa uzaifu wetu na atahakikisha kama tunapata musaada wenye tuko nao lazima kwa “wakati wenye kufaa.” (Ebr. 4:15, 16) Sawa tu vile Yesu alikubali musaada kutoka kwa malaika mwenye alikuya kumutia moyo mu bustani ya Getsemane, na siye pia tunapaswa kuwa tayari kukubali musaada wenye Yehova anatutolea ikuwe kupitia kichapo fulani, video fulani, hotuba fulani, ao kupitia muzee ao rafiki fulani mukomavu mwenye anakuya kututembelea.

19. Namna gani unaweza kupata nguvu wakati uko napambana na hali yenye inajaribu ushikamanifu wako kwa Mungu? Leta mufano.

19Yehova atakupatia “amani ya Mungu.” Namna gani Yehova atatutia nguvu? Wakati tunasali tutapata “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.” (Flp. 4:6, 7) Amani yenye Yehova anatupatia inatuliza moyo wetu na mawazo yetu. Ona ile jambo kupitia mufano wa dada Luz. Anasema hivi: “Mara mingi najisikiaka kuwa peke yangu. Wakati fulani ile mawazo inanifanyaka niwaze kama Yehova hanipendake. Lakini, wakati ile mawazo inafika mara moja namuambiaka Yehova namna najisikia. Sala inanisaidiaka nijisikie muzuri zaidi.” Sawa vile mufano wake unaonyesha, tunaweza kupata amani kupitia sala.

20. Machozi ya Yesu imetufundisha mambo gani?

20 Machozi ya Yesu imetufundisha mambo mingi sana yenye kutufariji, hauone vile? Tumeona kama ni jambo ya lazima kutegemeza marafiki wetu wenye wako na huzuni na kutumainia kama Yehova na Yesu watatusaidia wakati tunapoteza wapendwa wetu katika kifo. Tunatiwa moyo kuhubiri na kufundisha kwa huruma juu Yehova Mungu na Yesu Kristo wanaonyeshaka ile sifa. Na tumeona pia kama tumepata kitulizo kutoka kwa Yehova na Mwana wake mupendwa kwa kujua kama wanaelewa namna tunajisikia, wanajua uzaifu wetu, na wanapenda kutusaidia kuvumilia. Kwa hiyo basi, muache tuendelee kutumikisha mambo yenye tumejifunza hapa mupaka siku yenye Yehova atatimiza hii ahadi yenye kusema kama “atapanguza kila chozi katika macho [yetu]”!​—Ufu. 21:4.

WIMBO 120 Tukuwe Wapole Kama Kristo

^ fu. 5 Tunasoma mu Biblia kama kuko wakati wenye Yesu aliliaka. Mu hii habari tutazungumuzia mambo tatu yenye ilifanyaka Yesu alie na tutaona somo fulani zenye tunaweza kujifunza.

^ fu. 1 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 6 Ona kitabu Étude perspicace des Écritures, Buku ya 2, uku. 34.

^ fu. 12 Neno ya kigiriki yenye inatafsiriwa “jirani” katika Matayo 22:39 inatia ndani hapana tu watu wenye unaishi nao karibu lakini pia mutu mwenye unatumika naye ao unapitisha wakati pamoja naye.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu alichochewa kumufariji Maria na Marta. Na siye tunaweza kufanya vile kwa ajili ya wale wenye wamepoteza wapendwa wao katika kifo.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu alikuwa tayari kumufundisha Nikodemo usiku. Na siye tunapaswa kuwa tayari kujifunza Biblia na watu saa yenye wanaona ni muzuri kwao.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu alisali ili kumuomba Baba yake amusaidie abakie mushikamanifu kwake. Tunapaswa pia kufanya vile wakati tuko mu majaribu.