Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 5

‘Tumia Muzuri Zaidi Wakati Wako’

‘Tumia Muzuri Zaidi Wakati Wako’

“Muendelee kuwa waangalifu sana ili namna munatembea isikuwe kama watu wenye hawana hekima lakini kama watu wenye hekima, mukitumia muzuri zaidi wakati wenu.”​—EFE. 5:15, 16.

WIMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Yangu

KIFUPI YA HABARI *

1. Namna gani tunaweza kupitisha wakati pamoja na Yehova?

TUNAPENDAKA sana kupitisha wakati pamoja na watu wenye tunahangaikia. Bibi na bwana wenye furaha wanapendaka sana kupitisha wakati pamoja. Vijana wanafurahiaka pia kupitisha wakati pamoja na marafiki wao wa karibu. Na siye wote tunapendaka kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada zetu. Lakini jambo ya maana sana, tunapendaka kupitisha wakati pamoja na Mungu wetu. Tunaweza kufanya vile kwa kusali kwake, kusoma Neno yake, na kufikiri sana juu ya kusudi yake na sifa zake za muzuri. Wakati wenye tunapitisha pamoja na Yehova ni wa maana sana!​—Zb. 139:17.

2. Ni magumu gani tunakutana nayo?

2 Hata kama tunapendaka kupitisha wakati pamoja na Yehova, mara mingi haikuwake mwepesi kufanya vile. Tuko na mambo mingi sana ya kufanya mu maisha, na ile inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kupanga wakati kwa ajili ya mambo ya kiroho. Kazi ya kimwili, madaraka ya familia, na mambo ingine ya lazima inaweza kukamata wakati wetu mingi, na ile inaweza kufanya tuone sawa vile tuko na mambo mingi sana ya kufanya na tunakosa wakati wa kusali, kujifunza, ao kufikiri sana.

3. Ni jambo gani ingine inaweza kukamata wakati wetu?

3 Kuko jambo ingine yenye inaweza kukamata wakati wetu. Kama hatuko waangalifu, tunaweza kuacha mambo yenye haiko ya mubaya ikamate wakati wenye tungetumia ili kumukaribia Yehova. Kwa mufano, fikiria mambo ya kujifurahisha. Siye wote tunapendaka kujifurahisha wakati fulani. Lakini hata mambo ya kujifurahisha yenye haiko ya mubaya inaweza kutukamata wakati mingi na kutuachia tu wakati kidogo juu ya mambo ya kiroho. Njo maana tunapaswa kutia mambo ya kujifurahisha pa nafasi yake.​—Mez. 25:27; 1 Ti. 4:8.

4. Tutazungumuzia nini sasa?

4 Mu hii habari tutaona juu ya nini tunapaswa kutanguliza mambo ya lazima zaidi mu maisha yetu. Tutaona pia namna tunaweza kutumia muzuri zaidi wakati wetu pamoja na Yehova na faida yenye tunaweza kupata kwa kutumia muzuri zaidi wakati wetu.

AMUA KWA HEKIMA; TANGULIZA MAMBO YA MAANA ZAIDI

5. Namna gani kufikiri sana juu ya shauri yenye kuwa mu Waefeso 5:15-17 kunaweza kusaidia kijana kuchagula maisha ya muzuri zaidi?

5Chagula maisha ya muzuri zaidi. Mara mingi vijana wanakuwaka wanajiuliza namna ya kutumia muzuri zaidi maisha yao. Ngambo moja, washauri wa masomo na watu wa familia wenye hawako Mashahidi wanaweza kuwashauria wasome mingi juu wapate kazi ya muzuri mu maisha. Kufanya vile, kunaweza kukamata wakati wao mingi. Ngambo ingine, wazazi na marafiki mu kutaniko, pengine wanaweza kutia moyo vijana kutumia wakati wao mu utumishi wa Yehova. Ni mambo gani inaweza kusaidia kijana mwenye anamupenda Yehova kukamata maamuzi ya muzuri zaidi? Kusoma na kufiki sana juu ya Waefeso 5:15-17 kunaweza kumusaidia. (Soma.) Kisha kusoma ile mistari, kijana anaweza kujiuliza hivi: ‘“Mapenzi ya Yehova” ni nini? Ni uamuzi gani utamupendeza? Ni uamuzi gani utanisaidia kutumia muzuri zaidi wakati wangu?’ Kijana, usisahau kama “siku hizi ni za uovu,” na kama hii dunia ya Shetani inakaribia mwisho. Ni jambo ya hekima kutumia maisha yetu ili kufanya mambo yenye itamufurahisha Yehova.

6. Maria alichagula kufanya nini, na juu ya nini uamuzi wake ulikuwa wenye hekima?

6Tanguliza mambo ya maana zaidi. Wakati fulani, kutumia muzuri zaidi wakati wetu, inatia ndani kuchagula kati ya mambo mbili yenye haiko ya mubaya. Tunaweza kuona ile wakati Yesu alitembelea Maria na Marta. Bila shaka, Marta alifurahi wakati Yesu aliwatembelea, njo maana alitayarisha chakula mingi. Lakini Maria yeye, alikuwa anaikala karibu na Yesu na alikuwa anasikiliza mafundisho yake. Hata kama Marta alikuwa na nia ya muzuri, Maria yeye alichagula “fungu la muzuri zaidi.” (Lu. 10:38-42, maelezo ya chini.) Kisha wakati fulani, pengine Maria alisahau chakula yenye dada yake alitayarishaka ile siku, lakini tunaweza kuwa hakika kama hakusahau mambo yenye alijifunza kutoka kwa Yesu. Sawa vile Maria alifurahia kupitisha wakati fulani pamoja na Yesu, na siye pia tunafurahiaka wakati wenye tunapitisha pamoja na Yehova. Namna gani tunaweza kutumia muzuri zaidi wakati wetu?

TUMIA MUZURI ZAIDI WAKATI WAKO PAMOJA NA YEHOVA

7. Juu ya nini ni jambo ya maana sana kusali, kujifunza na kufikiri sana?

7Unapaswa kuelewa kama kusali, kujifunza, na kufikiri sana ni sehemu ya ibada yetu. Wakati tunasali, tunazungumuza pamoja na Baba yetu wa mbinguni, mwenye anatupenda sana. (Zb. 5:7) Wakati tunajifunza Biblia, tutapata “ujuzi juu ya Mungu,” mwenye ni Chanzo cha hekima yote. (Mez. 2:1-5) Wakati tunafikiri sana kuhusu mambo yenye tunajifunza juu ya Yehova, ni kusema tunafikiri juu ya sifa zake za muzuri na kukumbuka mambo ya kushangaza yenye anapenda kutufanyia na kufanyia wanadamu wote kwa ujumla. Unaweza kufikiria njia ya muzuri zaidi ya kutumia wakati wako? Lakini, ni nini inaweza kutusaidia kufanya vile?

Unaweza kupata fasi ya kimya ili kufanya funzo yako ya kipekee? (Ona fungu ya 8-9)

8. Ni somo gani tunaweza kujifunza kupitia namna Yesu alipitisha wakati wake mu jangwa?

8Kama inawezekana, tafuta fasi ya kimya. Fikiria mufano wa Yesu. Mbele aanze utumishi wake hapa ku dunia, Yesu alipitisha siku 40 mu jangwa. (Lu. 4:1, 2) Mu ile fasi ya kimya, Yesu angeweza kusali kwa Yehova na kufikiri sana juu ya mapenzi yenye Baba yake alikuwa nayo juu yake. Kufanya vile bila shaka, kungemutayarisha juu ya majaribu yenye alikuwa karibu kupata. Namna gani unaweza kupata faida kupitia mufano wa Yesu? Kama uko mu familia ya watu wengi, pengine kila mara haiko mwepesi kwako kupata fasi ya kimya ku nyumba. Mu ile hali, unaweza kutafuta fasi ya muzuri inje. Njo vile Julie anafanyaka saa yenye anapenda kupitisha wakati pamoja na Yehova mu sala. Yeye na bwana yake wanaishi mu nyumba ya kidogo sana mu Ufaransa, na inakuwaka nguvu sana kwake kuwa yeye peke na bila kukengeushwa. Julie anasema hivi: “Juu ya ile hali, naendaka kujitembeza mu bustani kila siku. Kule nakuwaka miye peke na nawezaka kukaza akili fasi moja, na kuongea kabisa na Yehova.”

9. Hata kama Yesu alikuwa na mambo mingi ya kufanya, namna gani alionyesha kama alisamini uhusiano wake pamoja na Yehova?

9 Yesu alikuwa kabisa na mambo mingi ya kufanya mu maisha yake. Mu utumishi wake hapa ku dunia, watu wengi walikuwa wanamufuata fasi mbalimbali kwenye alikuwa anaenda na wote walipenda kuwa pamoja naye. Wakati fulani, “muji wote ulikuwa umekusanyika palepale kwenye mulango” ili kumuona. Hata vile, Yesu alihakikisha kama kila mara alikuwa na wakati wa kusali kwa baba yake. Mbele jua itoke, alitafuta “mahali kwenye hapakukuwa watu,” kwenye angepitisha wakati yeye peke pamoja na Baba yake.​—Mk. 1:32-35.

10-11. Kulingana na Matayo 26:40, 41, ni shauri gani yenye kufaa Yesu alipatia wanafunzi wake mu bustani ya Getsemane, lakini nini njo ilitokea?

10 Usiku wa mwisho wa maisha yake hapa ku dunia, wakati utumishi wake ulifikia ku mwisho, Yesu alitafuta tena fasi ya kimya kwenye angeweza kufikiri sana na kusali. Alipata ile fasi mu bustani ya Getsemane. (Mt. 26:36) Mu ile wakati, Yesu alipatia wanafunzi wake shauri fulani yenye kufaa juu ya sala.

11 Fikiria mambo yenye ilitokea. Wakati walifika mu ile bustani ya Getsemane, ilikuwa nyuma sana pengine ilikuwa ilishapita hata katikati ya usiku. Aliambia mitume wake ‘waendelee kukesha,’ na kisha yeye akaenda kusali. (Mt. 26:37-39) Lakini wakati alikuwa anasali, wanafunzi wake walikuwa wanasinzia. Na wakati aliwakuta wanalala, Yesu aliwaomba tena ‘waendelee kukesha na kusali bila kuacha.’ (Soma Matayo 26:40, 41.) Alielewa kama walikuwa na mahangaiko sana na walikuwa walishachoka. Yesu aliwasikilia huruma na kuelewa kama “mwili ni muzaifu.” Tena, kwa mara ingine mbili Yesu alienda kusali, na wakati alirudia alikuta wanafunzi wake wako wanalala kuliko kusali.​—Mt. 26:42-45.

Unaweza kukamata wakati ili kusali saa yenye hauko mwenye kuchoka sana? (Ona fungu ya 12)

12. Tunaweza kufanya nini, kama wakati fulani, tunajisikia kuwa wenye mahangaiko sana ao tunajisikia kuwa wenye kuchoka sana na ile inafanya tushindwe kusali?

12Chagula wakati wenye kufaa. Wakati fulani tunaweza kujisikia kuwa tuko na mahangaiko sana ao tunachoka sana na ile inafanya tushindwe kusali. Kama ile ilishakakufikia, ujue kama hauko weye peke. Ni nini unaweza kufanya? Watu fulani wenye walizoea kusali kwa Yehova ku mwisho wa siku walifikia kuona kama ni muzuri kusali mangaribi mbele kidogo wakati hawayachoka sana. Wengine wamefikia kuona kama, kwa mufano, wakati walishaikala ao kupiga magoti wakati wako wanasali kumewasaidia sana. Tuseme nini kama umejisikia kuwa na mahangaiko sana ao kuwa mwenye kuvunjika moyo sana na ile inafanya ushindwe kusali? Umuambie Yehova namna unajisikia. Unaweza kuwa hakika kama Baba yetu mwenye rehema ataelewa.​—Zb. 139:4.

Unaweza kuepuka kujibia ujumbe fulani wakati uko ku mikutano? (Ona fungu ya 13-14)

13. Namna gani vyombo vyetu vya kielektroniki vinaweza kutukengeusha saa yenye tuko tunapitisha wakati wetu pamoja na Yehova?

13Uepuke kukengeushwa wakati uko unajifunza. Sala haiko tu njo njia moja yenye tunaweza kutumia ili kuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova. Kujifunza Neno ya Mungu na kuhuzuria mikutano kunaweza pia kutusaidia kumukaribia Mungu. Kuko jambo fulani yenye unaweza kufanya juu ya kutumia muzuri wakati wenye unapitisha ili kujifunza na kuhuzuria mikutano? Ujiulize hivi: ‘Ni jambo gani inanikengeushaka wakati wa mikutano ao wakati niko napenda kujifunza?’ Je, ile inaweza kuwa juu ya kuitika appel, ao juu ya kuandika ujumbe fulani ku telefone ao ku chombo ingine ya kielektroniki? Leo, watu wengi wako na vile vyombo vya kielektroniki. Watafiti fulani wanasema kama tunapendaka kukaza akili juu ya jambo fulani, lakini kama telefone iko pembeni yetu ile inaweza kutukengeusha. Mwalimu moja wa psikolojia anasema hivi: “Utakosa kukaza akili juu ya mambo yenye uko unafanya. Akili yako itakuwa fasi ingine.” Mara mingi, mbele mikusanyiko ya eneo na ya muzunguko ianze, tunaambiwa kama tunapaswa kutia vyombo vyetu vya kielektroniki mu hali yenye haitakengeusha wengine. Je, tunaweza pia kufanya vile wakati tuko siye peke juu vyombo vyetu vya kielektroniki visitukengeushe saa yenye tuko tunapitisha wakati wetu pamoja na Yehova?

14. Kulingana na Wafilipi 4:6, 7, namna gani Yehova atakusaidia kukaza akili juu ya jambo fulani?

14Umuombe Yehova akusaidie ukaze akili juu ya jambo fulani. Kama unaona kuwa unaanza kufikiria mambo ingine wakati uko unafanya funzo yako ya kipekee ao wakati uko ku mikutano, umuombe Yehova akusaidie. Kama uko na mahangaiko ao wasiwasi fulani, pengine haitakuwa mwepesi kwako kuacha kufikiria mahangaiko yako na kukaza akili juu ya Neno ya Mungu. Lakini ni jambo ya maana sana kufanya vile. Omba amani ya Mungu yenye italinda, hapana tu moyo wako, lakini pia “nguvu [zako] za akili.”​—Soma Wafilipi 4:6, 7.

KUSALI, KUJIFUNZA, NA KUKUSANYIKA KUTAKULETEA FAIDA

15. Tutapata faida gani saa yenye tunapitisha wakati pamoja na Yehova?

15 Kama unachukua wakati wa kuzungumuza, kusikiliza, na kufikiri juu ya Yehova, utapata faidi mingi sana. Namna gani? Kwanza, utakamata maamuzi ya muzuri zaidi. Biblia inatuhakikishia kama “mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima.” (Mez. 13:20) Njo maana, saa yenye tunapitisha wakati na mwenye ni Chanzo cha hekima, ni kusema Yehova, tutakuwa na hekima zaidi. Tutaelewa muzuri zaidi namna tunaweza kumupendeza Yehova na namna tunaweza kuepuka kukamata maamuzi yenye itamuhuzunisha.

16. Namna gani kupitisha wakati pamoja na Yehova kunatusaidia kufundisha muzuri zaidi?

16 Pili, utafikia kuwa mwalimu muzuri zaidi. Wakati tuko tunajifunza Biblia pamoja na mutu fulani, kusudi yetu ya maana zaidi ni kumusaidia amukaribie Yehova. Kadiri tunazungumuza na Baba yetu wa mbinguni, ni vile upendo wetu kwake utaongezeka na ni vile tutakuwa na uwezo wa kufundisha wanafunzi wetu wa Biblia wamupende. Waza kidogo juu ya mufano wa Yesu. Alizungumuza kuhusu Yehova mu njia ya muzuri na ya upendo, yenye ilisaidia wanafunzi wake wamupende pia Yehova.​—Yoh. 17:25, 26.

17. Juu ya nini sala na funzo ya kipekee inatusaidia kutia nguvu imani yetu?

17 Tatu, imani yako itakuwa nguvu zaidi. Fikiria mambo yenye inaweza kutokea wakati unamuomba Mungu akuongoze, akufariji ao kukusaidia. Kila wakati Yehova anajibia sala zako, imani yako kwake inaongezeka. (1 Yo. 5:15) Ni jambo gani ingine inaweza kukusaidia kuongeza imani yako? Funzo ya kipekee. Usisahau kama, “imani inafuata jambo lenye lilisikiwa.” (Ro. 10:17) Kwa hiyo, juu tutie nguvu imani yetu, tuko na lazima ya kufanya mambo mingi zaidi ya kujifunza tu mambo fulani. Tuko na lazima ya kufanya nini ingine?

18. Leta mufano wenye kuonyesha juu ya nini tuko na lazima ya kufikiri sana.

18 Tuko na lazima ya kufikiri sana juu ya mambo yenye tuko tunajifunza. Fikiria mufano wa muandikaji wa Zaburi ya 77. Alikuwa na mahangaiko juu alijisikia kama yeye na Waisraeli wenzake walikosa kukubaliwa na Yehova. Ile mahangaiko ilifanya akose usingizi usiku. (Mustari wa 2-8) Alifanya nini? Alimuambia Yehova hivi: “Nitafikiri sana juu ya kazi zako zote na kufikiri sana juu ya matendo yako.” (Mustari wa 12) Kusema kweli, ule mutunga-zaburi alijua muzuri mambo fulani yenye Yehova alifanyia watu wake zamani, lakini aliendelea kuhangaika na kujiuliza hivi: “Je, Mungu amesahau kuonyesha wema wake, ao je, kasirani yake imekomesha rehema yake?” (Mustari wa 9) Ule mutunga-zaburi alifikiri sana juu ya kazi yenye Yehova alifanya na juu ya namna alionyesha huruma na rehema wakati wa zamani. (Mustari wa 11) Ile ilikuwa na matokeo gani? Mutunga-zaburi alifikia kuwa hakika kama Yehova hangeacha watu Wake. (Mustari wa 15) Mu njia ileile, imani yako itakuwa nguvu zaidi kadiri unafikiri sana juu ya mambo yenye tayari Yehova ameshafanyia watu wake na juu ya mambo yenye ameshakufanyia weye kipekee.

19. Ni mu njia gani ingine tunaweza kupata faida saa yenye tunapitisha wakati pamoja na Yehova?

19 Ine, na ya maana zaidi, upendo wako kwa Yehova utaongezeka. Upendo ni sifa ya maana sana yenye itakuchochea kumutii Yehova, kufanya yako yote ili kumupendeza, na kuvumilia jaribu yoyote. (Mt. 22:37-39; 1 Ko. 13:4, 7; 1 Yo. 5:3) Hakuna jambo yenye kuwa ya maana zaidi kuliko urafiki wetu pamoja na Yehova!​—Zb. 63:1-8.

20. Namna gani utapanga wakati wenye utapitisha pamoja na Yehova?

20 Tusisahau kama kusali, kujifunza, na kufikiri sana ni sehemu ya ibada yetu. Sawa vile Yesu, tafuta fasi ya kimya ili kupitisha wakati pamoja na Yehova. Epuka mambo yenye inaweza kufanya ukengeushwe. Umuombe Yehova akusaidie ukaze akili wakati uko unafanya mambo ya kiroho. Kama unatumia muzuri zaidi wakati wako sasa, Yehova atakupatia maisha ya milele mu dunia mupya.​—Mk. 4:24.

WIMBO 28 Rafiki ya Yehova Ni Nani?

^ fu. 5 Yehova njo Rafiki yetu muzuri zaidi. Tunasamini sana urafiki wetu pamoja naye na tunapenda kumujua muzuri zaidi. Inaomba wakati ili kujua muzuri mutu fulani, ni vile pia wakati tunapenda kukomalisha uhusiano wetu pamoja na Yehova. Leo, tuko na mambo mingi sana ya kufanya mu maisha. Namna gani tunaweza kutafuta wakati wa kumukaribia Baba yetu wa mbinguni? Na kufanya vile, kutatuletea faida gani?