Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 1

“Wale Wenye Kumutafuta Yehova Hawatakosa Kitu Kizuri”

“Wale Wenye Kumutafuta Yehova Hawatakosa Kitu Kizuri”

ANDIKO YETU YA MWAKA WA 2022: “Wale wenye kumutafuta Yehova hawatakosa kitu kizuri.”​—ZB. 34:10.

WIMBO 4 “Yehova Ni Muchungaji Wangu”

KIFUPI YA HABARI *

Daudi aliona namna ‘hakukosa kitu kizuri’ hata wakati wa magumu (Ona fungu ya 1-3) *

1. Ni hali gani ya nguvu yenye Daudi alijikuta ndani?

DAUDI alikuwa anakimbia juu ya kulinda uzima wake. Sauli, mufalme mwenye nguvu wa Israeli, alipenda kumuua. Wakati Daudi alikuwa na lazima ya chakula, alipitia mu muji wa Nobu, kwenye aliomba mikate tano. (1Sa. 21:1, 3) Kisha, yeye na wanaume wake walienda kujificha katika pango. (1Sa. 22:1) Namna gani Daudi alijikuta mu ile hali?

2. Namna gani Sauli alijitia ye peke mu hatari? (1 Samweli 23:16, 17)

2 Sauli alimuonea Daudi wivu sana juu watu wengi walimupenda sana Daudi na kumusifu juu alipata ushindi mu vita mingi. Sauli alijua pia kama kukosa kumutii Yehova njo kulifanya akataliwe kuwa mufalme wa Israeli na kama Yehova alimuchagula Daudi kuwa mufalme. (Soma 1 Samweli 23:16, 17.) Lakini, Sauli alikuwa angali mufalme wa Israeli, na alikuwa na maaskari wengi na watu wengi wenye walikuwa upande wake, njo maana Daudi alikuwa anakimbia juu ya kulinda uzima wake. Sauli aliwaza kabisa kama angeweza kumuzuia Mungu asimufanye Daudi kuwa mufalme? (Isa. 55:11) Biblia haiseme vile, lakini tunaweza kuwa hakika na jambo moja: Sauli ye peke alijitia mu hatari. Wale wenye kumupinga Mungu kila mara wanashindwaka!

3. Daudi alijisikia namna gani ijapokuwa hali yenye alikuwa ndani?

3 Daudi alikuwa mwanaume munyenyekevu. Haiko ye peke njo alichagula kuwa mufalme wa Israeli, ni Yehova njo alimuchagula. (1Sa. 16:1, 12, 13) Sauli alimuona Daudi kuwa adui yake. Lakini Daudi hakuona kama ni kosa ya Yehova wakati alijikuta mu hatari; na Daudi hakunungunika wakati alikuwa tu na chakula kidogo na hakunungunikia mule mu pango kwenye alijificha. Tofauti na ile, inawezekana ni mu ile pango njo alitunga wimbo wa muzuri sana wa kumusifu Mungu, wenye kuwa na maneno ya andiko ya musingi ya hii habari yetu, yenye inasema: “Wale wenye kumutafuta Yehova hawatakosa kitu kizuri.”​—Zb. 34:10.

4. Tutazungumuzia maulizo gani, na juu ya nini iko ya lazima?

4 Leo, wakati fulani watumishi wengi wa Yehova hawana chakula ya kutosha ao mambo ingine yenye wako nayo lazima ili kuishi. * Na ile imefikia watumishi wengi wa Yehova zaidi sana mu hii wakati wa ugonjwa wa kuambukiza. Na mambo itakuwa mubaya zaidi vile tuko tunakaribia “taabu kubwa.” (Mt. 24:21) Tukiwa na ile mu akili, tujibie basi hii maulizo ine: Ni mu njia gani Daudi ‘hakukosa kitu kizuri’? Juu ya nini tunapaswa kutosheka na mambo yenye tuko nayo? Juu ya nini tunapaswa kutumainia kama Yehova atatuhangaikia? Na namna gani tunaweza kujitayarisha tangu sasa kwa ajili ya wakati wenye kuja?

“SITAKOSA KITU”

5-6. Zaburi 23:1-6 inatusaidia namna gani kuelewa mambo yenye Daudi alipenda kumaanisha wakati alisema kama watumishi wa Mungu “hawatakosa kitu kizuri”?

5 Daudi alimaanisha nini wakati alisema kama watumishi wa Yehova “hawatakosa kitu kizuri”? Wakati Daudi aliandika Zaburi ya 23, alitumia maneno ya kufanana na ile. Njo maana ile Zaburi inaweza kutusaidia kuelewa mambo yenye ile maneno inamaanisha. (Soma Zaburi 23:1-6.) Daudi alianza ile Zaburi na maneno: “Yehova ni Muchungaji wangu. Sitakosa kitu.” Mu mistari ingine ya ile Zaburi, Daudi alitaja mambo yenye kuwa ya maana kabisa sawa vile mambo ya muzuri yenye alipata juu alimukubali Yehova kuwa Muchungaji. Yehova alimuongoza Daudi “katika njia ya haki,” na kumutegemeza kwa uaminifu mu wakati wa muzuri na wakati wa mubaya. Daudi alijua kama maisha yake katika “malisho [ya Yehova] yenye majani mengi” haingekosa magumu. Mu ile wakati, pengine angevunjika moyo, sawa vile alilinganisha kutembea “katika bonde lenye kivuli kizito,” na maadui wenye angepata. Lakini juu Yehova ni Muchungaji wake, Daudi ‘hataogopa jambo lolote lenye kuumiza.’

6 Sasa tumepata jibu ya ulizo yetu: Ni mu njia gani Daudi ‘hakukosa kitu kizuri’? Daudi alikuwa na kila kitu yenye alikuwa nayo lazima ili kubakia karibu na Yehova. Furaha yake haikutokana na vitu vya kimwili. Daudi alitosheka na vitu vyenye Yehova alimutolea. Jambo ya maana zaidi kwake ni kuona vile Yehova alimubariki na kumulinda.

7. Kulingana na Luka 21:20-24, ni hali gani ya nguvu yenye Wakristo wa karne ya kwanza wa Yudea walipambana nayo?

7 Kulingana na maneno ya Daudi tunaona namna gani ni jambo ya maana kwetu kuwa na mawazo ya muzuri juu ya vitu vya kimwili. Bila shaka, tunaweza kufurahia vitu vya kimwili vyenye tuko navyo, lakini hatupaswe kuviona kuwa vitu vya maana zaidi mu maisha yetu. Ile ilikuwa kweli ya maana yenye Wakristo wa karne ya kwanza wa Yudea walifikia kuelewa. (Soma Luka 21:20-24.) Yesu aliwaonya kama kungekuwa wakati wenye muji wa Yerusalemu ‘ungezungukwa na majeshi yenye kupiga kambi.’ Wakati ile ilitokea, walipaswa ‘kuanza kukimbilia kwenye milima.’ Kama wangekimbia wangeokoa uzima wao, hata vile wangeacha vitu mingi nyuma yao. Munara wa Mulinzi ulisema hivi kumepita miaka fulani: “Waliacha mashamba yao na nyumba zao, na hawakubeba hata vitu vyao. Walitumainia kama Yehova atawalinda na kuwasaidia, na walitia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza kuliko mambo yote yenye ingeweza kuonekana kuwa ya maana.”

8. Ni somo gani tunaweza kupata mu mambo yenye ilifikia Wakristo wa karne ya kwanza wenye walikuwa wanaishi Yudea?

8 Ni somo gani tunaweza kupata mu mambo yenye ilifikia Wakristo wa karne ya kwanza wenye walikuwa wanaishi Yudea? Munara wa Mulinzi wenye tulishataja ulisema hivi: “Wakati wenye kuja tutapata majaribu yenye itaonyesha namna tunaona vitu vya kimwili. Tunaviona kuwa vya maana sana ao ni jambo ya maana sana kwetu kupata wokovu juu tuko waaminifu kwa Mungu? Ndiyo, kukimbia kwetu kunaweza kutia ndani magumu fulani na kukosewa mambo fulani. Tunapaswa kuwa tayari kufanya mambo yote yenye inaomba kufanya, sawa vile Wakristo wa karne ya kwanza wenye walikimbia kutoka Yudea walifanya.” *

9. Ni kitia moyo gani yenye unapata mu shauri yenye Paulo alipatia Waebrania?

9 Unaweza kuwazia namna ilikuwa nguvu sana kwa wale Wakristo kuacha karibu kila kitu yenye walikuwa nayo ili kuenda kuanza maisha ya mupya? Iliomba wakuwe na imani na kumutegemea Yehova na kuwa hakika kama atawatimizia mahitaji yao ya musingi. Lakini hawakukosa musaada. Miaka tano mbele Waroma wazunguke Yerusalemu, mutume Paulo alipatia Waebrania shauri ya maana sana. Alisema hivi: “Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa. Kwa maana amesema: ‘Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.’ Ili tukuwe hodari na kusema: ‘Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunifanya nini?’” (Ebr. 13:5, 6) Hakuna shaka kama wale wenye walifuata shauri ya Paulo mbele Waroma washambulie, waliona kama ilikuwa mwepesi kwao kujipatanisha na hali, ni kusema, kuwa na maisha ya mwepesi kule kwenye walienda. Walikuwa hakika kama Yehova angewatimizia mahitaji yao ya musingi. Ile maneno ya Paulo inatupatia na siye uhakikisho uleule.

“TUTATOSHEKA NA VITU HIVYO”

10. Paulo anatuambia “siri” gani?

10 Paulo alipatia shauri ya vile Timoteo, na ile inatuhusu pia. Aliandika hivi: “Basi, kama tuko na chakula na nguo, tutatosheka na vitu hivyo.” (1Ti. 6:8) Ile inamaanisha kama hatuwezi kufurahia chakula fulani ya muzuri, kuwa na fasi fulani ya muzuri ya kuishi, ao kuuza nguo ya mupya wakati fulani? Haiko ile njo Paulo alipenda kusema. Hapa iko anasema kama tunapaswa kutosheka na vitu vyovyote vya kimwili vyenye tuko navyo. (Flp. 4:12) Ile njo ilikuwa “siri” ya Paulo. Jambo ya maana sana yenye tuko nayo ni uhusiano wetu pamoja na Mungu, hapana vitu vya kimwili vyenye tuko navyo.​—Hab. 3:17, 18.

Waisraeli ‘hawakukosa kitu’ muda wa miaka yote 40 yenye walifanya mu jangwa. Je, na siye tunaweza kutosheka na mambo yenye tuko nayo sasa? (Ona fungu ya 11) *

11. Maneno yenye Musa aliambia Waisraeli inatufundisha nini kuhusu kutosheka?

11 Kunaweza kuwa tofauti kati ya mawazo yetu na mawazo ya Yehova juu ya mambo yenye tuko nayo lazima. Fikiria mambo yenye Musa aliambia Waisraeli kisha kupitisha miaka 40 mu jangwa. Alisema: “Yehova Mungu wako amekubariki katika mambo yote yenye umefanya. Anajua muzuri kabisa safari yako katika jangwa hili kubwa. Yehova Mungu wako amekuwa pamoja na wewe miaka hii makumi ine (40), na haujakosa kitu.” (Kum. 2:7) Mu ile miaka yote 40, Yehova alipatia Waisraeli mana kama chakula. Alihakikisha kama manguo yenye walitokaka nayo kule Misri haikuharibika. (Kum. 8:3, 4) Hata kama watu fulani waliweza kuona kama ile mambo haikutosha, Musa alikumbusha Waisraeli kama walikuwa na kila kitu yenye walikuwa nayo lazima. Yehova atafurahi sana kama na siye tunajikaza kutosheka na vitu vyenye tuko navyo. Ndiyo, anapenda tukuwe wenye shukrani hata kwa mambo fulani ya kidogo yenye anatupatia na tuelewe kama ni zawadi kutoka kwake.

UKUWE HAKIKA KAMA YEHOVA ATAKUHANGAIKIA

12. Ni nini njo inaonyesha kama Daudi alimutegemea Yehova, na kama hakujitegemea yeye mwenyewe?

12 Daudi alijua kama Yehova iko mushikamanifu na anahangaikia sana wale wenye wanamupenda. Hata kama uzima wake ulikuwa mu hatari wakati alikuwa anatunga Zaburi ya 34, kupitia macho ya imani, Daudi aliona “malaika wa Yehova” iko anapiga kambi ‘kumuzunguka’ yeye. (Zb. 34:7) Pengine Daudi alikuwa analinganisha malaika wa Yehova na askari mwenye kupiga kambi fasi ya mapigano, mwenye iko macho, iko anaangalia ni wapi kwenye adui anaweza kutokea. Hata kama Daudi alikuwa askari mwenye uhodari sana na hata kama Yehova alimuahidi kama angemupatia ufalme, Daudi hakutegemea uwezo wenye alikuwa nao wa kutupa jiwe kwa kombeo ao wa kutumia upanga ili kuua adui yake. (1Sa. 16:13; 24:12) Daudi alimutegemea njo Mungu, na alikuwa hakika kama malaika wa Yehova ‘anaokoa wale wenye kumuogopa.’ Kwa kweli, hatutazamie kama Yehova anaweza kutulinda kimuujiza leo. Lakini tunajua kama kila mutu mwenye anamutegemea Yehova hatateseka milele.

Wakati wa taabu kubwa, majeshi ya Gogu wa Magogu inaweza kujaribu kutushambulia mu manyumba yetu. Lakini kujua kama Yesu na malaika wake wanajua mambo yenye kutokea na kama watatutetea, ile inatutuliza kabisa (Ona fungu ya 13)

13. Wakati Gogu wa Magogu atashambulia, juu ya nini tutaonekana sawa vile hatuna mutu wa kutulinda, lakini juu ya nini hatupaswe kuogopa? (Ona picha ku jalada.)

13 Mu siku zenye ziko zinakuya, tumaini yetu katika uwezo wa Yehova wa kutulinda itajaribiwa. Wakati Gogu wa Magogu, ni kusema muungano wa mataifa, atashambulia watu wa Mungu, uzima wetu utaonekana sawa vile uko mu hatari. Tutakuwa na lazima ya kuwa hakika kama Yehova iko na uwezo wa kutuokoa na kama atafanya vile. Ku macho ya mataifa tutaonekana sawa vile kondoo mwenye hana mutu wa kumulinda. (Eze. 38:10-12) Hatutakuwa na silaha, na hatutakuwa wenye kuzoezwa kwa ajili ya vita. Mataifa itawaza kama itakuwa mwepesi kutushinda. Hawataona mambo yenye siye tuko tunaona na macho ya imani, ni kusema, jeshi kubwa ya malaika wenye kuzunguka watu wa Mungu na wenye kuwa tayari kutupigania. Mataifa haina imani katika Mungu. Kwa hiyo, itashangala sana wakati wataona majeshi ya mbinguni inakuya kutusaidia!​—Ufu. 19:11, 14, 15.

UJITAYARISHE TANGU SASA KWA AJILI YA WAKATI WENYE KUJA

14. Ni mambo gani yenye tunaweza kufanya tangu sasa ili kujitayarisha kwa ajili ya wakati wenye kuja?

14 Tunaweza kufanya nini tangu sasa ili kujitayarisha kwa ajili ya wakati wenye kuja? Kwanza, tunapaswa kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya vitu vya kimwili, juu siku moja tutaacha ile vitu vyote. Tunapaswa pia kutosheka na kufurahia urafiki wetu pamoja na Yehova. Kadiri tunaendelea kumujua Mungu wetu, ni vile tutaendelea kuwa hakika kama atatulinda wakati Gogu wa Magogu atashambulia.

15. Ni mambo gani ilimufikiaka Daudi mu maisha yenye ilimusaidia kuelewa kama Yehova hangemuacha?

15 Fikiria pia jambo ingine yenye ilisaidia Daudi, na yenye inaweza kutusaidia kujitayarisha kwa ajili ya magumu yenye kuja. Daudi alisema hivi: “Muonje na muone kwamba Yehova ni mwema; mwenye furaha ni mutu mwenye anamukimbilia.” (Zb. 34:8) Ile maneno inaonyesha waziwazi kama Daudi alijua kuwa angemutegemea Yehova. Mara mingi Daudi alimutegemea Yehova, na hakuna siku Yehova alimuachilia. Wakati alikuwa kijana, Daudi alipambana na Mufilisti moja murefu sana, ndiyo, askari wa nguvu sana mwenye aliitwa Goliati. Siku moja alimuambia ule askari hivi: “Leo hii Yehova atakutia wewe katika mukono wangu.” (1Sa. 17:46) Wakati ingine, Daudi alikuwa anamutumikia mufalme Sauli, mwenye mara mingi alijaribu kumuua. Lakini “Yehova alikuwa pamoja” na Daudi. (1Sa. 18:12) Juu Daudi alijionea na macho yake namna Yehova alimusaidia zamani, alikuwa hakika kama Yehova atamusaidia mu magumu yenye alikuwa anapata.

16. Ni mu njia gani tunaweza ‘kuonja’ uzuri wa Yehova?

16 Kadiri tunaendelea kutafuta muongozo wa Yehova tangu sasa, ni vile tutakuwa hakika kama atatuokoa wakati wenye kuja. Inaomba imani na pia kuwa tayari kumutegemea Yehova wakati tunataka kuomba mukubwa wetu wa kazi atupatie siku fulani juu ya kuenda kuhuzuria mukusanyiko wa muzunguko ao wa eneo, ao juu ya kubadilisha kidogo programu ya kazi ili ikusaidie kuhuzuria mikutano yote na kupitisha wakati mingi mu mahubiri. Waza sasa kama ule mukubwa wa kazi anakatala ombi yako, na unapoteza kazi. Je, utakuwa na imani kama Yehova hatakuacha na kama siku zote ataendelea kukutimizia mahitaji yako ya musingi? (Ebr. 13:5) Ndugu na dada wengi wenye kuwa mu utumishi wa wakati wote, wanaweza kutufasiria mambo mingi yenye walijionea na yenye kuonyesha kama Yehova aliwasaidia wakati walikuwa na lazima yake zaidi. Yehova anakuwaka tu muaminifu.

17. Andiko ya mwaka wa 2022 ni andiko gani, na juu ya nini inafaa?

17 Wakati Yehova iko upande wetu, hatuna sababu ya kuogopa juu ya mambo yenye itatokea wakati wenye kuja. Mungu wetu hawezi kutuacha hata kidogo kama tunaendelea kumutanguliza yeye mu maisha yetu. Juu ya kutukumbusha ulazima wa kujitayarisha tangu sasa kwa ajili ya magumu yenye iko inakuja, na juu ya kuendelea kutumainia kama Yehova hatatuacha, Baraza Yenye Kuongoza ilichagula Zaburi 34:10 kama andiko yetu ya mwaka wa 2022. Ile andiko inasema hivi: “Wale wenye kumutafuta Yehova hawatakosa kitu kizuri.”

WIMBO 38 Atakupatia Nguvu

^ fu. 5 Andiko yetu ya mwaka wa 2022 inatoka mu Zaburi 34:10: “Wale wenye kumutafuta Yehova hawatakosa kitu kizuri.” Watumishi wengi waaminifu wa Yehova hawana vitu mingi vya kimwili. Juu ya nini tunaweza kusema kama ‘hawakose kitu kizuri’? Kuelewa maana ya hii andiko kunaweza kutusaidia namna gani tujitayarishe kwa ajili ya magumu yenye itakuya?

^ fu. 4 Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu,” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 9, 2014.

^ fu. 54 MAFASIRIO YA PICHA: Hata wakati alikuwa anajificha fasi fulani juu ya kumukimbia mufalme Sauli, Daudi alisamini sana mambo yenye Yehova alikuwa anafanya juu ya kumutegemeza.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Kisha Waisraeli kutoka Misri, Yehova aliwapatia mana kama chakula na alihakikisha kama manguo yao haiharibike.