Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 2

“Mugeuzwe kwa Kufanya Upya Akili Yenu”

“Mugeuzwe kwa Kufanya Upya Akili Yenu”

“Mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.”—RO. 12:2.

WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako

KIFUPI YA HABARI a

1-2. Tunapaswa kuendelea kufanya nini kisha kubatizwa? Fasiria.

 UNASAFISHAKA nyumba yako mara ngapi? Pengine mbele tu uhamie mu ile nyumba, uliisafishaka kabisa. Lakini itakuwa namna gani kama hauendelee kufanya vile? Vile tu unajua, vumbi na uchafu itayala haraka mule. Juu nyumba yako iendelee kuwa muzuri, unapaswa kuisafisha kila wakati.

2 Vilevile juu mawazo na utu wetu ikuwe muzuri, tunapaswa kuendelea kujikaza. Bila shaka, mbele ya kubatizwa tulifanyaka yetu yote juu ya kufanya mabadiliko fulani mu maisha yetu ili “tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho.” (2 Ko. 7:1) Lakini sasa tunapaswa kuendelea kufuata shauri ya mutume Paulo ya “kuendelea kufanywa upya.” (Efe. 4:23) Juu ya nini inaomba kuendelea kujikaza? Juu vumbi na uchafu wa mu hii ulimwengu vinaweza kuyala haraka ndani yetu na kutuchafua. Kwa hiyo, juu tuendelee kumufurahisha Yehova, tunapaswa kuchunguza kwa ukawaida mawazo yetu, utu wetu, na tamaa zetu.

ENDELEA “KUFANYA UPYA AKILI YAKO”

3. ‘Kufanya upya akili yako’ maana yake nini? (Waroma 12:2)

3 Tunapaswa kufanya nini ili kufanya upya akili yetu, ni kusema, kubadilisha namna yetu ya kuwaza? (Soma Waroma 12:2.) Hatupaswe kufanya tu mambo kidogo ya muzuri mu maisha yetu. Lakini, tunapaswa kuchunguza mutu mwenye tuko kwa ndani na kufanya mabadiliko fulani ili tutii kanuni za Yehova. Hatutafanya vile mara moya tu, lakini tunapaswa kuendelea.

Maamuzi yangu juu ya université na kazi yenye nachagua inaonyesha kama naona kumutumikia Yehova kuwa jambo ya maana sana mu maisha yangu? (Ona fungu ya 4-5) c

4. Tunapaswa kufanya nini ili mawazo yetu isifinyangwe na hii ulimwengu?

4 Wakati tutakuwa wakamilifu, tutamufurahisha Yehova sikuzote mu mambo yote yenye tutakuwa tunafanya. Lakini kwa sasa, inaomba tujikaze kabisa ili kumufurahisha Yehova. Mu Waroma 12:2 Paulo anasema kama tunapaswa kufanya upya akili yetu ili tujue mambo yenye Mungu anapenda tufanye. Hatupaswe kuacha hii ulimwengu itufinyange na kutuongoza, lakini tunapaswa kwanza kujichunguza siye wenyewe ili kuona namna gani tuko naacha mawazo ya Mungu iongoze miradi na maamuzi yenye tuko tunakamata.

5. Vile tunajua kama siku ya Yehova iko karibu, namna gani tunaweza kuchunguza namna yetu ya kuwaza? (Ona picha.)

5 Fikiria mufano fulani. Yehova anapenda ‘tuweke karibu katika akili kuwapo kwa siku yake.’ (2 Pe. 3:12) Ujiulize hivi: ‘Namna yangu ya kuishi inaonyesha kama ninaelewa kuwa hii ulimwengu itaharibiwa hivi karibuni? Maamuzi yangu juu ya université na kazi yenye nachagua inaonyesha kama naona kumutumikia Yehova kuwa jambo ya maana zaidi mu maisha yangu? Naamini kabisa kama Yehova atatimiza mahitaji yangu na ya familia yangu, ao nahangaikiaka kila wakati vitu vya kimwili?’ Wazia furaha yenye Yehova anakuwaka nayo wakati anaona tunajikaza kufanya mambo kupatana na mapenzi yake.—Mt. 6:25-27, 33; Flp. 4:12, 13.

6. Tunapaswa kuendelea kufanya nini?

6 Tunapaswa kuendelea kuchunguza mawazo yetu kila wakati na kufanya mabadiliko fulani kama ni lazima. Paulo aliambia Wakorinto hivi: “Muendelee kujijaribu ili kuona kama muko katika imani; muendelee kuhakikisha namna ninyi wenyewe muko.” (2 Ko. 13:5) Kuwa “katika imani” maana yake kufanya mambo mingi zaidi tu ya kuhuzuria mikutano ya Kikristo na kuhubiri. Ile inatia ndani pia mawazo yetu, muelekeo wetu, na nia ao mutazamo wetu. Tunapaswa kuendelea kufanya upya akili yetu kwa kusoma Neno ya Mungu, kujikaza kuwa na mawazo sawa vile yake mu mambo fulani na kufanya mabadiliko fulani mu maisha yetu ili kumufurahisha.—1 Ko. 2:14-16.

ENDELEA “KUVAA UTU MUPYA”

7. Kulingana na Waefeso 4:31, 32, ni jambo gani ingine yenye tunapaswa kufanya, na juu ya nini haiko mwepesi kufanya vile?

7 Soma Waefeso 4:31, 32. Zaidi ya kufanya mabadiliko fulani mu nanma yetu ya kuwaza, tunapaswa “kuvaa utu mupya.” (Efe. 4:24) Juu tuweze kufanya vile, inaomba kujikaza. Tunapaswa kujikaza sana ili kuachana na tabia fulani, sawa vile uchungu wenye uovu, hasira, na kasirani kali. Juu ya nini haiko mwepesi kufanya vile? Juu inaweza kuwa nguvu kubadilisha tabia fulani za mubaya. Kwa mufano, Biblia inasema kama watu fulani ni wenye kukasirika haraka” na wenye “kukasirika-kasirika sana.” (Mez. 29:22) Mutu mwenye alikuwa na zile tabia anapaswa kujikaza sana ili abadilike hata kama alishabatizwa. Njo vile mufano wenye kufuata unaonyesha.

8-9. Vile habari ya Stephen inaonyesha, juu ya nini ni muzuri kuendelea kuvua utu wa zamani?

8 Ilikuwa nguvu kwa ndugu mwenye kuitwa Stephen kuzuia hasira yake. Anasema hivi: “Hata kisha kubatizwa, iliomba nijikaze sana kuzuia hasira yangu. Kwa mufano, siku moya wakati tulikuwa nahubiri nyumba kwa nyumba, nilikimbizaka mwizi moya mwenye aliibaka radio mu motokari yangu. Wakati nilikuwa karibu kumukamata, aliangusha ile radio na akakimbia. Wakati niliambia wengine namna nilipata tena radio yangu, muzee fulani mu kikundi aliniuliza hivi: ‘Stephen, kama ungemukamata ule mwizi, ungefanya nini?’ Ile ullizo ilifanya nifikiri na ilinisukuma niendelee kujikaza ili kuwa mutu mwenye kufanya amani.” b

9 Tunaweza kuwaza kama tulishaachana na tabia ya mubaya, lakini, sawa vile habari ya Stephen inaonyesha, tunaweza kuonyesha ile tabia kama kunatokea jambo fulani yenye haitazamiwe. Hata mutume Paulo alisema hivi: “Wakati ninataka kufanya mambo yenye kuwa sawa, mambo ya mubaya yako pamoja na mimi.” (Ro. 7:21-23) Juu Wakristo wote hawakamilike, wako napiganisha tabia fulani za mubaya zenye zinarudiaka sawa vile tu vumbi na uchafu wenye unaweza kurudia na kuyala mu nyumba. Tunapaswa kujikaza ili tuendelee kuwa safi. Tunaweza kufanya vile namna gani?

10. Unapaswa kufanya nini ili kuachana na tabia za mubaya? (1 Yohana 5:14, 15)

10 Umuombe Yehova akusaidie kuachana na tabia yenye uko naona kama ni nguvu kuachana nayo, na ukuwe hakika kama atakusikiliza na kukusaidia. (Soma 1 Yohana 5:14, 15.) Ni kweli Yehova hatatosha ile tabia kimuujiza, lakini atakusaidia ili usiionyeshe. (1 Pe. 5:10) Kwa sasa, endelea kutenda kulingana na sala zako kwa kuepuka mambo yenye inaweza kufanya urudilie utu wako wa zamani. Kwa mufano, unaweza kuepuka kuangalia filme, programu za televizyo, ao kusoma habari zenye zinaweza kufanya ionekane sawa vile hakuna ubaya wa kuendelea kuwa na tabia za mubaya zenye uko napenda kuacha. Na usiache tamaa za mubaya zibakie mu akili yako.—Flp. 4:8; Kol. 3:2.

11. Tunapaswa kufanya nini ili kuendelea kuvala utu mupya?

11 Hata kama ulishavua utu wa zamani, ni jambo ya maana kuvala utu mupya. Unaweza kufanya vile namna gani? Wakati uko najifunza kuhusu sifa fulani za Yehova, ujiwekee muradi wa kumuiga. (Efe. 5:1, 2) Kwa mufano, wakati unasoma habari fulani ya Biblia yenye inaonyesha kama Yehova ni Mungu mwenye kusamehe, ujiulize hivi: ‘Na miye nasameheaka wengine?’ Wakati unasoma habari yenye inaonyesha kama Yehova anasikiliaka huruma wale wenye kuwa na magumu, ujiulize hivi: ‘Na miye nahangaikiaka ndugu na dada wenye kuwa na lazima ya musaada wa kimwili, na nafanyaka vile kwa matendo?’ Lakini juu ufikie kufanya vile, itaomba ukuwe muvumilivu.

12. Ni nini ilifanya Stephen aamini kama Biblia iko na nguvu ya kubadilisha maisha ya watu?

12 Stephen, mwenye tulishataya, aliona kama alikuwa anavala utu mupya hatua kwa hatua. Anasema hivi: “Tangu nibatizwe, nilishapambana na mambo mingi yenye iliomba nizuie hasira yangu. Nilianza kubakia mbali na watu wenye walikuwa nanichokoza ao kufanya mambo ingine juu hali isiharibike zaidi. Watu wengi, kutia ndani bibi yangu, walinipongeza juu nilikuwa najikaza kutulia mu hali za vile. Na miye mwenyewe nilishangaa! Najua kama sikufanya ile mabadiliko yote kwa nguvu yangu. Lakini, niko hakika kama ile yote inahakikisha kama Biblia iko na nguvu ya kubadilisha maisha ya watu.”

ENDELEA KUPIGANISHA TAMAA YA KUFANYA MAMBO YA MUBAYA

13. Ni nini itatusaidia kukomalisha tamaa ya kufanya mambo ya muzuri? (Wagalatia 5:16)

13 Soma Wagalatia 5:16. Yehova anatupatia kwa ukarimu roho yake takatifu ili itusaidie kufanya mambo ya muzuri. Wakati tunasoma Neno ya Mungu, tunaacha ile roho iongoze mawazo na matendo yetu. Tena tunapataka roho takatifu wakati tunaenda ku mikutano. Ku ile mikutano ya Kikristo, inatiaka moyo sana kupitisha wakati pamoya na ndugu na dada zetu wenye pia wako najikaza sana ili kufanya mambo ya muzuri. (Ebr. 10:24, 25; 13:7) Na wakati tunasali kwa Yehova kwa moyo wote na kumuomba atusaidie kupiganisha uzaifu fulani, atatupatia roho yake takatifu ili itusaidie. Hata kama pengine ile mambo yote haitafanya zile tamaa ziishe, itatusaidia kuzipinga wakati zinajitokeza. Sawa vile Wagalatia 5:16 inasema, wale wenye kutembea kwa roho ‘hawatatenda tamaa yoyote ya mwili.’

14. Juu ya nini ni jambo ya maana kuendelea kukomalisha tamaa ya kufanya mambo ya muzuri?

14 Wakati tunaanza kufanya mambo yenye inatusaidia tukuwe na urafiki wa muzuri pamoya na Yehova, ni jambo ya maana tuendelee kufanya vile na tuendelee kukomalisha tamaa ya kufanya mambo ya muzuri. Juu ya nini? Juu moya kati ya maadui wetu halalake. Mara mingi tunajaribiwaka kufanya mambo ya mubaya. Kujaribiwa kufanya mambo ya mubaya njo ule adui. Kisha kubatizwa, tunaweza kuanza kuvutiwa na mambo yenye tunapaswa kuepuka, sawa vile michezo ya pupa, kunywa pombe kupita kiasi, ao kuangalia pornografia. (Efe. 5:3, 4) Ndugu moya kijana anasema hivi: “Jambo moya yenye ilikuwa nguvu sana kwangu kuacha ni kuvutiwa na wanaume wenzangu. Niliwaza kama ile mambo haitaendelea, lakini naona kama ningali tu navutiwa nao.” Unaweza kufanya nini kama unaona kuwa uko na tamaa ya mubaya yenye ni nguvu kabisa kuachana nayo?

Kama unajaribiwa na tamaa ya mubaya, ujue kama siku moya hali yako itabadilika; wengine pia walipambana na mambo ya vile, lakini waliishinda (Ona fungu ya 15-16)

15. Juu ya nini kujua kama tamaa za mubaya ni za “kawaida kwa watu” kunatutia moyo? (Ona picha.)

15 Wakati unajikaza kupiganisha tamaa ya mubaya yenye ni nguvu kuacha, ukumbuke kama hauko weye peke. Biblia inasema hivi: “Hakuna jaribu lenye limewapata ninyi isipokuwa lile lenye kuwa la kawaida kwa watu.” (1 Ko. 10:13a) Tafsiri ingine ya Biblia inatafsiri hivi ile maneno: “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu.” Ile maneno iliandikiwa Wakristo wanaume na wanamuke wenye waliishi mu Korinto. Zamani wamoja kati yao walikuwa wazinifu, wanaume wenye wanakubali matendo ya kulalwa na wanaume wenzao, na walevi. (1 Ko. 6:9-11) Unawaza hawakukuwa hata na tamaa za mubaya zenye iliomba wapiganishe kisha kubatizwa? Inawezekana walikuwa nazo. Ni kweli, wote walikuwa Wakristo watiwa-mafuta, lakini walikuwa wanadamu wenye hawakamilike. Bila shaka, walikuwa na tamaa fulani za mubaya zenye walikuwa wanapiganisha wakati fulani. Kujua vile kunatutia moyo. Juu ya nini? Juu ile inaonyesha kama ikuwe uko napiganisha tamaa gani ya mubaya, kuko mutu mwingine mwenye alishakaipiganisha. Kwa hiyo, unaweza kuwa ‘imara katika imani, ukijua kwamba mateso yaleyale yanapata ushirika muzima wa ndugu zetu katika ulimwengu.’—1 Pe. 5:9.

16. Tunapaswa kuepuka kufanya nini, na juu ya nini?

16 Epuka kuwaza kama hakuna mutu mwenye anaweza kuelewa mambo yenye uko napitia. Kuwaza vile kunaweza kufanya uone kama hali yako haitabadilika na kama hautaweza kupiganisha tamaa za mubaya. Lakini Biblia inasema tena hivi: “Mungu ni muaminifu, na hatawaacha ninyi mujaribiwe kupita vile munaweza kuvumilia, lakini pamoja na jaribu hilo atafanya pia njia ya kutokea ili muweze kulivumilia.” (1 Ko. 10:13b) Kwa hiyo, hata kama tamaa ya mubaya iko nguvu kiasi gani, tunaweza kuivumilia. Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuepuka kabisa kufanya mambo ya mubaya.

17. Unaweza kufanya nini hata kama hauwezi kuepuka kabisa kuwa na tamaa za mubaya?

17 Kila mara ukumbuke hivi: Juu haukamilike, hautaweza kuepuka kabisa kuwa na tamaa za mubaya. Lakini kama zinakuya, unaweza kuzizuia haraka, sawa vile Yosefu alimukimbiaka haraka bibi wa Potifa. (Mwa. 39:12) Unapaswa kuepuka kutenda kulingana na tamaa za mubaya!

ENDELEA KUJIKAZA

18-19. Ni maulizo gani yenye tunapaswa kujiuliza wakati tuko najikaza kufanya upya akili yetu?

18 Juu ya kufanya upya akili yetu tunapaswa kuendelea kupatanisha mawazo na matendo yetu na mapenzi ya Yehova. Juu ya kufanya vile, ujichunguze kwa kujiuliza hivi kwa ukawaida: ‘Namna yangu ya kufanya mambo inaonyesha kama natumbua kuwa mwisho uko karibu sana? Niko najikaza kuvala utu mupya? Niko naruhusu roho ya Yehova iongoze maisha yangu ili nisitende kulingana na tamaa za mwili?’

19 Wakati uko najichunguza usitazamie kama utakuwa mukamilifu, lakini furahia mabadiliko yenye uko nafanya. Ikiwa unaona kama ungali na mambo fulani ya kutengeneza, usivunjike moyo. Lakini, ufuate mashauri yenye kuwa mu Wafilipi 3:16: “Kwa kadiri tumefanya maendeleo, tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo uleule.” Wakati unafanya vile, ukuwe hakika kama Yehova atabariki bidii yako ya kuendelea kufanya upya akili yako.

WIMBO 36 Tulinde Moyo Wetu

a Mutume Paulo aliambia Wakristo wenzake kama wasiache hii ulimwengu iwafinyange. Ile ni shahuri ya muzuri sana kwetu leo. Tunapaswa kufanya yetu yote ili tusifanye mambo na kuwaza sawa vile watu wa mu hii ulimwengu. Juu ya kufanya vile, tunapaswa kuendelea kubadilisha namna yetu ya kuwaza ikiwa tunatambua kama haipatane na mapenzi ya Mungu. Mu hii habari, tutaona namna tutaweza kufanya vile.

b Ona habari “Maisha Yangu Yaliendelea Kuwa Mabaya Sana” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 7, 2015.

c MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moya kijana iko nawaza ikiwa itaomba aende ku université ao kama itaomba aanze upainia.