Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 4

Yehova Anabariki Bidii Yetu ya Kuhuzuria Ukumbusho

Yehova Anabariki Bidii Yetu ya Kuhuzuria Ukumbusho

“Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”—LU. 22:19.

WIMBO 19 Chakula cha Mangaribi cha Bwana

KIFUPI YA HABARI a

1-2. Juu ya nini tunahuzuriaka Ukumbusho kila mwaka?

 KARIBU miaka 2 000 imepita tangu Yesu atoe uzima wake kwa ajili yetu, ile ilifanya tukuwe na tumaini ya kupata uzima wa milele. Usiku mbele Yesu akufe, aliambia wanafunzi wake wakumbuke ile tendo ya upendo yenye alifanya kwa kuanzisha sherehe yenye haikuomba mambo mingi, ni kusema, kutumia tu mukate na divai.—1 Ko. 11:23-26.

2 Tunatii amri ya Yesu juu tunamupenda sana. (Yoh. 14:15) Kila mwaka, majuma fulani mbele na kisha Ukumbusho, tunaonyeshaka shukrani yetu kwa ajili ya mambo yote yenye Yesu alitufanyia kwa kukamata wakati wa kuwaza sana na kusali juu ya ulazima wa kifo ya Yesu. Tunafurahiaka pia kuhubiri sana, kualika watu wengi kadiri inawezekana ili wakutane na siye kwa ajili ya ile tukio ya maana. Na kusema kweli, hatutaacha kitu yoyote ituzuie kuhuzuria Ukumbusho.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutazungumuzia mambo tatu yenye inaonyesha kama watu wa Yehova wamefanya yote yenye wanaweza ili kukumbuka kifo ya Yesu: (1) kwa kufanya Ukumbusho kulingana na maagizo ya Yesu, (2) kualika wengine ku Ukumbusho, na (3) kuhuzuria Ukumbusho hata mu hali ya nguvu.

KUFANYA UKUMBUSHO KULINGANA NA MAAGIZO YA YESU

4. Ni mafundisho gani yenye tunajifunzaka kila mwaka ku Ukumbusho na juu ya nini tunapaswa kuona ile mafundisho kuwa ya pekee? (Luka 22:19, 20)

4 Kila mwaka ku Ukumbusho tunasikilizaka hotuba yenye kutegemea Biblia yenye inajibiaka waziwazi maulizo mingi. Tunajifunzaka sababu yenye inafanya watu wakuwe na lazima ya bei ya ukombozi na namna gani kifo ya mutu moya inaweza kulipia zambi za watu wengi. Tunakumbushwaka maana ya mukate na divai na pia ni nani wenye wanastahili kula na kunywa. (Soma Luka 22:19, 20.) Tena tunawaza sana juu ya baraka zenye wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi milele ku dunia watapata. (Isa. 35:5, 6; 65:17, 21-23) Tunapaswa kuona ile mafundisho kuwa ya pekee sana. Mamiliare ya watu hawajue ile mafundisho, na hawajue kama zabihu ya Yesu Kristo ni ya maana sana. Tena hawafanyake Ukumbusho kulingana na maagizo ya Yesu. Juu ya nini?

5. Kisha tu mitume wengi wa Yesu kufa, watu walianza kufanya Ukumbusho namna gani?

5 Kisha tu mitume wengi wa Yesu kufa, Wakristo wa uwongo waliingia mu kutaniko. (Mt. 13:24-27, 37-39) Walisema “mambo yenye kupotoka ili kuvuta wanafunzi wawafuate.” (Mdo. 20:29, 30) Biblia inasema kama Yesu alitoa mwili wake “mara moja kwa wakati wote ili kubeba zambi za watu wengi.” Lakini moya kati ya “mambo yenye kupotoka” yenye Wakristo wa uongo walianza kufundisha ni kama Yesu hakufanya vile, na walifundisha pia kama zabihu yake inapaswa kurudiliwa tena na tena. (Ebr. 9:27, 28) Leo, watu wengi wanaaminiaka ile fundisho ya uwongo. Wanaendaka ku kanisa kila juma, wakati fulani kila siku juu ya kufanya sherehe ya kukumbuka zabihu ya Yesu yenye mu dini ya katoliki inaitwa “Zabihu ya Misa.” b Watu wa dini zingine hawasherekeake mara mingi kifo ya Yesu. Na wengi kati yao hawajue kama kifo ya Yesu ni ya maana. Wengine wanajiulizaka hivi: ‘Kifo ya Yesu ni ya maana sana hivi kwamba inaweza kufanya zambi zangu zisamehewe?’ juu ya nini wanajiulizaka vile? Wengine, ni juu wanaamini mambo ya uwongo yenye watu wanafundisha ya kama kifo ya Yesu haiwezi kufanya mutu asamehewe zambi. Wanafunzi wa Yesu, wamefanya nini juu ya kushugulikia ile jambo?

6. Mu 1872, wanafunzi wa Biblia walielewa nini?

6 Mu 1870, wanafunzi wa Biblia wenye waliongozwa na Charles Taze Russell walianza kujifunza maandiko kwa undani. Walipenda kujua namna gani zabihu ya Yesu ni ya maana na namna wanapaswa kukumbuka kifo yake. Mu 1872, wale wanafunzi walielewa kama Yesu alitoa bei ya ukombozi kwa ajili ya watu wote. Hawakubakia tu na mambo yenye walijifunza. Lakini, waliambia wengine ile mambo kupitia vitabu na magazeti. Kwa kuiga mufano wa Wakristo wa karne ya kwanza, walianza kufanya Ukumbusho wa kifo ya Yesu mara moya mu mwaka.

7. Mambo yenye wale wanafunzi wa kwanza wa Biblia walijifunza inatuletea faida gani?

7 Mambo yenye wale Wakristo waaminifu walijifunza kumepita miaka mingi, inatuletea faida. Mu njia gani? Yehova ametusaidia kujua kama zabihu ya Yesu ni ya maana sana, na namna watu wote watapata faida kupitia ile zabihu. (1 Yo. 2:1, 2) Tumejifunza pia kama Biblia inazungumuzia tumaini mbili kwa ajili ya wanadamu wenye kufanya mapenzi ya Mungu. Kuko wale wenye watapata uzima wenye hauwezi kufa mbinguni na mamilioni ya watu wenye watapata uzima wa milele ku dunia. Yehova anatupenda sana, na zabihu ya Yesu iko na faida sana kwetu kipekee. Kujua vile kunafanya tumukaribie zaidi Yehova. (1 Pe. 3:18; 1 Yo. 4:9) Sawa vile ndugu zetu waaminifu wa zamani walifanya, tunaalikaka watu ili wahuzurie pamoya na siye Ukumbusho kulingana na maagizo ya Yesu.

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAALIKAKA WENGINE KU UKUMBUSHO

Utafanya nini juu utumike sana mu kampanye ya kualika watu ku Ukumbusho? (Ona fungu ya 8-10) e

8. Ni mambo gani yenye watu wa Yehova wamefanya ili kualika wengine ku Ukumbusho? (Ona picha.)

8 Tangu zamani, Mashahidi wa Yehova wanaalikaka wengine ku Ukumbusho. Mu 1881, ndugu na dada mu Amerika walialikwa ili kukutana pamoya mu nyumba ya ndugu fulani mu Allegheny, Pennsylvania, kwa ajili ya ile tukio ya pekee. Kisha pale, kila kutaniko ilianza kujifanyia Ukumbusho. Mu mwezi wa 3, 1940, wahubiri waliaambiwa waalike ku Ukumbusho kila mutu wa mu eneo yao mwenye anapendezwa. Mu 1960, Beteli ilipatia makutaniko mialiko yenye kuchapishwa. Ilikuwa njo mara ya kwanza kufanya vile. Kuanzia pale, mamiliare ya mialiko inaendelea kugawanywa. Juu ya nini tunajikazaka sana kualika wengine?

9-10. Wakati tunaalika kwa bidii wengine ku Ukumbusho, ni nani watafaidika? (Yohana 3:16)

9 Sababu moya yenye inafanya tualike wengine ku Ukumbusho ni juu tunapenda wale wenye wanahuzuria na siye Ukumbusho kwa mara ya kwanza wajifunze kuhusu mambo yenye Yehova na Yesu walishatufanyia. (Soma Yohana 3:16.) Tunatumainia kama mambo yenye wataona na kusikia ku Ukumbusho itawachochea wajifunze mambo mingi zaidi na wafikie kuwa watumishi wa Yehova. Lakini, Ukumbusho unaletea pia wengine faida.

10 Tunaalika pia wale wenye hawatende tena. Tunafanya vile juu ya kuwakumbusha kama Mungu angali anawapenda. Wengi wanaitikiaka mualiko wetu, na tunakuwaka na furaha sana wakati tunawaona. Kuhuzuria Ukumbusho kunawakumbushaka furaha yenye walikuwaka wanapata wakati walikuwa wanamutumikia Yehova zamani. Fikiria mufano wa Monica. c Alianza tena kuhubiri mu kipindi ya Coronavirus. Kisha kuhuzuria Ukumbusho mu 2021, anasema hivi: “Huu Ukumbusho ni wa pekee sana kwangu. Kwa mara ya kwanza mu miaka 20, nimeweza tena kuhubiria watu na kuwaalika ku Ukumbusho. Nilijikaza sana kualika wengine juu niko mwenye shukrani kwa alili ya mambo yote yenye Yehova na Yesu walishanifanyia.” (Zb. 103:1-4) Ikuwe watu wataitika ao kukatala mualiko wetu, tunaendelea tu kuwaalika kwa bidii ku Ukumbusho juu tunajua kama Yehova iko nasamini bidii yetu.

11. Namna gani Yehova amebariki bidii yetu ya kualika wengine ku Ukumbusho? (Hagai 2:7)

11 Yehova amebariki sana bidii yetu ya kualika wengine ku Ukumbusho. Mu 2021, hata kama kulikuwa vizuizi fulani vyenye viliwekwa juu ya ugonjwa wa Coronavirus, hesabu ya wale wenye walihuzuria Ukumbusho ilikuwa 21 367 603. Ile ni karibu mara mbili na nusu hesabu ya Mashahidi wa Yehova mu dunia yote! Bila shaka, Yehova hafurahie tu kuona watu wengi wanahuzuria. Anafurahia kila mutu kipekee. (Lu. 15:7; 1 Ti. 2:3, 4) Tuko hakika kama ni kupitia kazi yetu ya kualika watu njo Yehova anatusaidiaka kupata watu wenye kuwa na mioyo ya muzuri.—Soma Hagai 2:7.

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAHUZURIAKA UKUMBUSHO HATA KAMA NI NGUVU KUFANYA VILE

Yehova anabariki bidii yetu ya kuhuzuria Ukumbusho (Ona fungu ya 12) f

12. Ni nini inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kuhuzuria Ukumbusho? (Ona picha.)

12 Yesu alitabiri kama mu siku za mwisho, kutakuwa magumu mingi, sawa vile upinzani kutoka kwa watu wa familia, mateso, vita, magonjwa ya kuambukiza, na mambo ingine. (Mt. 10:36; Mk 13:9; Lu. 21:10, 11) Wakati fulani, ile inafanyaka ikuwe nguvu kwetu kuhuzuria Ukumbusho wa kifo ya Yesu. Ndugu na dada zetu walifanya nini ili kupiganisha ile magumu, na namna gani Yehova aliwasaidia?

13. Ni nini inaonyesha kama Yehova alibariki uhodari na azimio ya Artem ya kufanya Ukumbusho hata kama alikuwa mwenye kufungwa?

13 Kufungwa. Ndugu zetu wenye wanafungwa juu ya imani yao wanafanyaka yote yenye wanaweza juu ya kukumbuka kifo ya Yesu. Fikiria mufano wa Artem. Mu kipindi ya Ukumbusho wa 2020, alifungwa mu chumba ya metre 17 za muraba (17 mètres carrés) mwenye mulikuwa munaenea wafungwa ine ao tano. Alitumia vitu vyenye alipata ili vikuwe sawa vile mukate na divai na alipanga kufanya hotuba ya Ukumbusho kwa faida yake. Lakini wafungwa wenzake walikuwa navuta na kusema sana maneno machafu. Sasa alifanya nini? Aliwaomba waache kusema maneno machafu na kuvuta kwa saa moya tu. Wale wafungwa waliitika kuacha kuvuta na kusema maneno machafu wakati wa Ukumbusho. Ile ilimushangaza sana Artem. Artem anasema hivi: “nilianza kuwaambia kuhusu Ukumbusho.” Walimuambia Artem kama hawakukuwa napenda awaambie mambo ya Ukumbusho. Lakini, kisha tu kuona vile Artem alifanya Ukumbusho, walimuuliza maulizo mingi juu ya ile.

14. Watu wa Yehova walifanya nini ili kuhuzuria Ukumbusho hata kama kulikuwa Coronavirus?

14 Coronavirus. Wakati Coronavirus ilianza, Mashahidi wa Yehova hawakuweza tena kukutana juu ya kuhuzuria Ukumbusho. Lakini ile haikuwazuia kufanya Ukumbusho sawa vile zamani. d Makutaniko yenye ilikuwa na uwezo wa kutumia enternete ilifanya ukumbusho kupitia vidéoconférence. Sasa, mamilioni ya watu wenye hawakukuwa na uwezo wa kutumia enternete walifanya nini? Mu mainchi fulani, mipango ilikamatwa juu watu wasikilize hotuba ya Ukumbusho kupitia televizyo ao radio. Zaidi ya ile, matawi mingi ilirekodi ile hotuba mu luga zaidi ya 500, ile ilisaidia hata wale wenye kuwa mu maeneo ya mbali wahuzurie Ukumbusho. Na ndugu walijikaza sana kutumia watu wa mu ile maeneo ile rekodi.

15. Mufano wa mwanafunzi fulani wa Biblia mwenye kuitwa Sue unakufundisha nini?

15 Upinzani kutoka kwa watu wa familia. Kwa watu fulani, shida kubwa yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu kwao kuhuzuria Ukumbusho ni upinzani kutoka kwa watu wa familia yao. Fikiria mufano wa mwanafunzi fulani wa Biblia mwenye kuitwa Sue. Mu 2021, siku moya mbele ya Ukumbusho, Sue aliambiaka mwalimu wake wa Biblia kama hatauzuria Ukumbusho juu alipata upinzani kutoka kwa watu wa familia yake. Mwalimu wake wa Biblia alimusomea Luka 22:44. Kisha akamufasiria kama wakati tuko na magumu tunapaswa kufuata mufano wa Yesu kwa kusali kwa Yehova na kumutegemea kabisa. Siku yenye ilifuata, Sue alitayarisha mukate na divai na akaangalia programu ya pekee ya Ibada ya Asubui ku jw.org. Na ile mangaribi, wakati alikuwa yeye peke mu chumba yake, alifuata Ukumbusho kupitia telefone. Kisha pale, Sue alimuandikia mwalimu wake wa Biblia hivi: “Jana ulinitia moyo sana. Nilifanya yangu yote juu ya kuhuzuria Ukumbusho, na Yehova alinisaidia kabisa. Namushukuru sana Yehova, na niko na furaha sana, sijue hata niseme nini!” Unawaza kama Yehova anaweza kukusaidia wakati unapambana na hali ya vile?

16. Juu ya nini tuko hakika kama Yehova atabariki bidii yetu ya kuhuzuria Ukumbusho? (Waroma 8:31, 32)

16 Yehova anafurahiaka sana wakati anaona tunajikaza ili kuhuzuria Ukumbusho wa kifo ya Yesu. Tuko hakika kama atatubariki wakati tunaonyesha shukrani yetu kwake juu ya mambo yenye alishatufanyia. (Soma Waroma 8:31, 32.) Kwa hiyo basi, tusikose kuhuzuria Ukumbusho wa hii mwaka na kufanya yetu yote ili kushiriki kwa bidii mu mambo yote ya kiroho ya mu kipindi ya Ukumbusho.

WIMBO 18 Tuko na Shukrani juu ya Bei ya Ukombozi

a Siku ya pili, tarehe 4 Mwezi wa 4, 2023, mamilioni ya watu mu dunia yote watakutana ili kukumbuka kifo ya Kristo. Kwa wengi itakuwa njo mara ya kwanza kuhuzuria. Mashahidi wa Yehova wengine wenye hawatende tena, wenye wamefanya miaka mingi bila kuhuzuria Ukumbusho, watajikaza ili kuhuzuria. Iko nguvu sana kwa wengine kuhuzuria Ukumbusho, lakini watajikaza. Hata ukuwe mu hali ya namna gani, ukuwe hakika kama Yehova atafurahi kama unajikaza ili kuhuzuria Ukumbusho.

b Wale watu wanaamini kama wakati wa sherehe ya Ukumbusho, mukate na divai vinabadilika na kuwa mwili na damu halisi ya Kristo. Wanawaza kama mwili na damu ya Yesu vinatolewa zabihu kila mara wakati mutu anafanya ile sherehe ya Ukumbusho.

c Majina fulani imebadilishwa.

d Ona pia ku jw.org habari zenye kichwa “2021 Mwadhimisho wa Ukumbusho.”

e MAFASIRIO YA PICHA: Tangu miaka ya 1960, mialiko ya Ukumbusho imekuwa muzuri zaidi, na kwa sasa tunaweza kupata ya kielektroniki na yenye kuchapishwa.

f MAFASIRIO YA PICHA: Mu hii picha, ndugu na dada wako nafanya Ukumbusho wakati wa muvurugo mu eneo yao.