Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 44

Utie Nguvu Tumaini Yako ya Kikristo

Utie Nguvu Tumaini Yako ya Kikristo

“Umutumainie Yehova.”​—ZB. 27:14.

WIMBO 144 Kaza Macho ku Zawadi!

KIFUPI YA HABARI *

1. Yehova ametupatia tumaini gani?

 YEHOVA ametupatia tumaini ya muzuri sana ya uzima wa milele. Wamoja wako na tumaini ya kuishi milele mbinguni na kuwa viumbe vya roho vyenye haviwezi kufa. (1 Ko. 15:50, 53) Wengine wengi wako na tumaini ya kuishi milele hapa ku dunia na kuwa na afya kamilifu na furaha. (Ufu. 21:3, 4) Ikuwe tuko na tumaini ya kupata uzima wa milele mbinguni ao ku dunia, tunaona tumaini yetu kuwa ya maana sana.

2. Tumaini yetu inategemea nini, na juu ya nini tunaweza kusema vile?

2 Mu Biblia, neno “tumaini” inaweza kumaanisha “kutazamia mambo ya muzuri yenye itatokea.” Tunaweza kuwa hakika kama tumaini yetu ya uzima wa milele ni ya kweli juu inatoka kwa Yehova. (Ro. 15:13) Tunajua mambo yenye ametuahidi, na tunajua kama sikuzote anatimizaka ahadi zake. (Hes. 23:19) Tuko hakika kama Yehova iko na nia na nguvu ya kutimiza kila kitu yenye anasema atafanya. Kwa hiyo, tumaini yetu haitegemee mambo ya kuwazia-wazia, ao mambo yenye tunapenda itokee, lakini inategemea mambo yenye tunajua kuwa ni ya kweli.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari? (Zaburi 27:14)

3 Baba yetu wa mbinguni anatupenda, na anapenda tumutumainie. (Soma Zaburi 27:14.) Wakati tunamutumainia kabisa Yehova, tutaweza kuvumilia magumu, na kuwa na uhodari na furaha hata kutokee nini. Tuzungumuzie namna tumaini yetu inatulinda. Kwanza, tutazungumuzia namna tumaini yetu iko sawa vile nanga na sawa vile kofia ya chuma. Kisha, tutazungumuzia namna tunaweza kutia nguvu tumaini yetu.

TUMAINI YETU IKO SAWA VILE NANGA

4. Ni mu njia gani tumaini yetu iko sawa vile nanga? (Waebrania 6:19)

4 Mu barua yake kwa Waebrania, mutume Paulo alilinganisha tumaini yetu na nanga. (Soma Waebrania 6:19.) Mara mingi Paulo alisafiri mu bahari. Kwa hiyo, alijua kama nanga inatumiwa ili kusaidia mashua isiyumbe-yumbe. Wakati fulani, upepo mukali ulitokea wakati Paulo alikuwa mu mashua. Ile wakati, Paulo aliona namna wenye kutumika mu mashua wanashusha nanga ndani ya maji juu ya kuzuia mashua isipeperushwe na kuenda kugonga miamba. (Mdo. 27:29, 39-41) Sawa vile nanga inasaidia mashua isiyumbe-yumbe, tumaini yetu inatusaidia tusiyumbe-yumbe na kumuacha Yehova wakati tunapambana na magumu yenye iko sawa vile upepo mukali. Tumaini yetu inatusaidia tukuwe watulivu wakati tunapambana na magumu juu tunajua kama mambo itakuwa muzuri zaidi. Na tusisahau kama Yesu alituambia kuwa tutateswa. (Yoh. 15:20) Kwa hiyo, kufikiri sana juu ya mambo yenye Yehova ametuahidi kunatusaidia tuendelee kumutumikia bila kuyumba-yumba.

5. Tumaini ilimusaidia namna gani Yesu wakati alikuwa karibu kufa?

5 Fikiria namna tumaini ilimusaidia Yesu aendelee kuwa muaminifu hata kama alijua kuwa atakufa kifo ya maumivu. Mu siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., mutume Petro alitaya maneno ya unabii yenye kuwa mu kitabu ya Zaburi yenye kuonyesha namna Yesu alikuwa kabisa mutulivu. Alisema hivi: “Nitakaa katika tumaini; kwa sababu hautaniacha katika Kaburi, na hautaruhusu mushikamanifu wako aone uharibifu. . . . Utanijaza furaha kubwa mbele yako.” (Mdo. 2:25-28; Zb. 16:8-11) Hata kama Yesu alijua kuwa atakufa, alitumainia kabisa kama Mungu atamufufua na kama atakuwa na furaha ya kuwa tena pamoya na Baba yake mbinguni.​—Ebr. 12:2, 3.

6. Ndugu fulani alisema nini kuhusu tumaini?

6 Tumaini yetu ya Kikristo imesaidia ndugu na dada wengi kuvumilia. Fikiria mufano wa Leonard Chinn, ndugu muaminifu mwenye alikuwa naishi Uingereza. Wakati ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, alifungwa juu alikatala kuwa askari. Kwa miezi mbili, alifungwa mu chumba yeye peke. Kisha pale, alilazimishwa kufanya kazi ya nguvu. Aliandika hivi: “Mambo yenye ilinipata ilinisaidia kuelewa namna tuko na lazima ya tumaini juu tuweze kuvumilia. Tuko na mifano ya Yesu, ya mitume, na ya manabii, na tuko na ahadi za maana zenye kuwa mu Biblia. Ile yote inafanya tumaini yetu ikuwe nguvu na inatusaidia tuvumilie.” Tumaini ilikuwa sawa vile nanga kwa Leonard, na kwetu pia inaweza kuwa nanga.

7. Namna gani magumu inatia nguvu tumaini yetu? (Waroma 5:3-5; Yakobo 1:12)

7 Wakati tunavumilia magumu, na tunaona namna Yehova anatusaidia, tunatambua kama anatukubali, na ile inafanya tumaini yetu ikuwe nguvu zaidi. (Soma Waroma 5:3-5; Yakobo 1:12.) Kwa hiyo, kwa sasa tumaini yetu inakuwa nguvu zaidi kuliko wakati tulisikia habari njema kwa mara ya kwanza. Shetani anapenda magumu yetu itulemee, lakini kwa musaada wa Yehova tunaweza kuvumilia ile magumu yote.

TUMAINI YETU IKO SAWA VILE KOFIA YA CHUMA

8. Ni mu njia gani tumaini yetu iko sawa vile kofia ya chuma? (1 Watesalonike 5:8)

8 Biblia inalinganisha pia tumaini yetu na kofia ya chuma. (Soma 1 Watesalonike 5:8.) Askari anavalaka kofia ya chuma ili kulinda kichwa yake kama maadui wanamushambulia. Mu vita yetu ya kiroho, tuko na lazima ya kulinda akili yetu na mashambulizi ya Shetani. Anatumia majaribu na mawazo yenye iko na kusudi ya kuharibisha akili yetu. Sawa vile tu kofia ya chuma inalindaka kichwa ya askari, tumaini yetu inalindaka akili yetu juu tuendelee kuwa waaminifu kwa Yehova.

9. Mambo inakuwaka namna gani kama watu hawana tumaini?

9 Tumaini yetu ya uzima wa milele itatusaidia tutende kwa hekima na kwa utambuzi. Lakini, kama tumaini yetu inakuwa zaifu na tunaaza kufikiria tu tamaa zetu, tunaweza kufikia kusahau tumaini yetu ya uzima wa milele. Kwa mufano, fikiria Wakristo fulani wenye walikuwa naishi mu Korinto ya zamani. Waliacha kuamini tumaini ya ufufuo. (1 Ko. 15:12) Paulo aliandika kama wale wenye hawakuamini ufufuo waliishi tu juu ya kutimiza tamaa zao. (1 Ko. 15:32) Leo, wengi wenye hawatumainie kabisa ahadi za Mungu wanaishi tu kwa ajili ya leo. Wanafanya yote yenye wanaweza juu waishi maisha ya raha. Lakini siye tunatumainia mambo yenye Mungu ameahidi kama atatufanyia mu wakati yenye kuya. Tumaini yetu iko sawa vile kofia ya chuma. Inalindaka akili yetu na inatusaidia tusijifikirie tu siye wenyewe juu ile inaweza kuharibisha uhusiano wetu pamoya na Yehova.​—1 Ko. 15:33, 34.

10. Tumaini inatusaidia tupiganishe mawazo gani ya uongo?

10 Tumaini yetu inaweza pia kutusaidia tusiwaze kama hatuwezi hata kidogo kumufurahisha Yehova. Kwa mufano, wamoja wanaweza kuwaza hivi: ‘Siwaze kabisa kama nitapataka uzima wa milele. Sistahili kabisa. Sitaweza kabisa kufanya mambo yenye Mungu anapenda nifanye.’ Kumbuka kama Elifazi mufariji wa uongo wa Yobu alimuambiaka maneno ya vile. Elifazi alisemaka hivi: “Je, mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nani ili akuwe safi?” Kisha, alisema hivi kuhusu Mungu: “Angalia! Hana imani katika watakatifu wake, hata mbingu haziko safi mbele ya macho yake.” (Yob. 15:14, 15) Ni uongo kabisa! Usisahau kama ni Shetani njo anapenda ukuwe na ile mawazo. Anajua kama ukiendelea kukaza akili yako juu ya ile mawazo, utapoteza tumaini yako. Kwa hiyo, achana na ile mawazo na ukaze akili yako juu ya ahadi za Yehova. Na ukuwe hakika kama anapenda uishi milele na atakusaidia ufikie ule muradi.​—1 Ti. 2:3, 4.

UTIE NGUVU TUMAINI YAKO

11. Juu ya nini tunapaswa kuwa wavumilivu wakati tuko nachunga Yehova atimize ahadi zake?

11 Kila mara haikuwake mwepesi kutia nguvu imani yetu. Wakati fulani tunaweza kufikiri kama Mungu anakawia kutimiza ahadi zake. Lakini, Yehova ni wa milele, na hahesabiake wakati sawa vile siye tunahesabiaka wakati. (2 Pe. 3:8, 9) Atatimiza ahadi zake mu njia ya muzuri zaidi, lakini anaweza kufanya vile mu wakati yenye hatutazamie. Tunaweza kufanya nini juu ya kutia nguvu tumaini yetu?​—Yak. 5:7, 8.

12. Kulingana na Waebrania 11:1, 6, kuko upatano gani kati ya tumaini na imani?

12 Tumaini yetu itakuwa nguvu kama tunabakia karibu na Yehova, mwenye atafanya mambo yenye tunatumainia itimie. Juu tukuwe na tumaini, tunapaswa kuamini kama Yehova iko na kama “anakuwa mwenye kuwapatia zawabu wale wenye wanamutafuta kwa bidii.” (Soma Waebrania 11:1, 6.) Kama tunaamini kabisa kuwa Yehova iko, tutakuwa hakika hata zaidi kama atatimiza mambo yote yenye ameahidi. Tuone mambo fulani ya kutusaidia kutia nguvu urafiki wetu pamoya na Yehova na kutia nguvu tumaini yetu.

Sala na kufikiri sana kutatia nguvu tumaini yetu (Ona fungu ya 13-15) *

13. Tunaweza kumukaribia Mungu namna gani?

13 Usali kwa Yehova, na usome Neno yake. Hata kama hatuwezi kumuona Yehova, tunaweza kumukaribia. Tunaweza kuzungumuza naye katika sala, na kuwa hakika kama atatusikiliza. (Yer. 29:11, 12) Tunaweza kumusikiliza Mungu kwa kusoma Neno yake na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma. Wakati tunasoma habari za wale wenye walibakia washikamanifu kwa Yehova zamani na namna aliwahangaikia, tumaini yetu inakuwa nguvu hata zaidi. Mu Neno ya Mungu, mambo yote yenye “yaliandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.”​—Ro. 15:4.

14. Juu ya nini ni muzuri kufikiri sana juu ya mambo yenye Yehova amefanyia wengine?

14 Ufikiri sana juu ya namna Yehova ametimiza ahadi zake. Fikiria mambo yenye Mungu alifanyia Abrahamu na Sara. Wilifikia miaka yenye hawangeweza kuzala. Lakini, Mungu aliwaahidi kama watapata mutoto. (Mwa. 18:10) Abrahamu alitenda namna gani? Biblia inasema hivi: “Alikuwa na imani kwamba angekuwa baba ya mataifa mengi.” (Ro. 4:18) Hata kama kwa maoni ya wanadamu, ile ilionekana kama haiwezekane, Abrahamu alikuwa hakika kama Yehova angetimiza ahadi yake. Ule mwanaume muaminifu hakupoteza tumaini. (Ro. 4:19-21) Habari za vile zinatufundisha kama sikuzote tunaweza kutumainia kuwa Yehova atatimiza ahadi zake, hata kama ku mawazo yetu ile inaweza kuonekana kama haiwezekane.

15. Juu ya nini tunapaswa kufikiri sana juu ya mambo yenye Mungu ametufanyia?

15 Fikiria mambo yenye Yehova amekufanyia. Fikiria faida yenye tayari umepata kwa kuona namna Yehova ametimiza ahadi zake zenye kuwa mu Biblia. Kwa mufano, Yesu aliahidi kama Baba yake atakupatia mambo yenye uko nayo lazima. (Mt. 6:32, 33) Yesu amekuahidi pia kama Yehova atakupatia roho yake takatifu wakati unaiomba. (Lu. 11:13) Yehova ametimiza zile ahadi. Unaweza pia kufikiria ahadi zingine zenye Yehova ametimiza kwa ajili yako. Kwa mufano, anaahidi kama atakusamehe, atakufariji, na atakukulisha kiroho. (Mt. 6:14; 24:45; 2 Ko. 1:3) Kama unafikiri sana kuhusu mambo yenye tayari Mungu amekufanyia, utatumainia hata zaidi mambo yenye atakufanyia wakati yenye kuya.

MUFURAHI KATIKA TUMAINI

16. Juu ya nini tumaini yetu ni zawadi ya maana sana?

16 Tumaini yetu ya uzima wa milele ni zawadi ya maana sana kutoka kwa Mungu. Tunangojea maisha ya muzuri sana, na ile ni jambo ya hakika. Tumaini yetu iko sawa vile nanga. Inatusaidia tusiyumbe-yumbe, lakini tuweze kuvumilia magumu, mateso, na hata kifo. Tumaini yetu iko sawa vile kofia ya chuma. Inalindaka akili yetu juu tuweze kuachana na mambo ya mubaya na kushikamana na mambo ya muzuri. Tumaini yenye Biblia inatupatia inatusaidia tumujue Mungu zaidi, na inatuonyesha kama Yehova anatupenda sana. Tunapata faida sana wakati tunatia nguvu tumaini yetu.

17. Juu ya nini tumaini yetu inafanya tufurahi?

17 Mu barua yenye mutume Paulo aliandikia Waroma, alitia Wakristo moyo ‘wafurahi katika tumaini.’ (Ro. 12:12) Paulo aliweza kufurahi juu alikuwa hakika kama ikiwa angeendelea kuwa mushikamanifu, angeweza kupata uzima wa milele mbinguni. Na siye pia tunaweza kufurahi katika tumaini juu tuko hakika kama Yehova atatimiza ahadi zake. Sawa vile mutunga-zaburi aliandika, “mwenye furaha ni ule . . . mwenye anamutumainia Yehova Mungu wake, . . . yeye mwenye kuwa muaminifu sikuzote.”​—Zb. 146:5, 6.

WIMBO 139 Wazia Uko mu Dunia Mupya

^ Yehova ametupatia tumaini ya muzuri ya wakati yenye kuya. Ile tumaini inatutia moyo na inatusaidia tusikaze uangalifu juu ya magumu yenye tuko nayo leo. Inatupatia nguvu ya kuendelea kubakia waaminifu kwa Yehova hata tukutane na magumu ya namna gani. Na inaweza kutusaidia tusikuwe na mawazo yenye inaweza kuharibisha akili yetu. Sawa vile tutazungumuzia mu hii habari, zile njo sababu zenye zinafanya tutie nguvu tumaini yetu ya Kikristo.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Sawa vile kofia ya chuma inalindaka kichwa ya askari na sawa vile nanga inasaidiaka mashua isiyumbe-yumbe, tumaini yetu inalindaka akili yetu na inatusaidiaka tusiyumbe-yumbe wakati ya magumu. Dada iko nasali kwa Yehova kwa moyo wake wote. Ndugu iko nafikiri sana juu ya namna Mungu alitimiza mambo yenye alimuahidi Abrahamu. Ndugu mwingine iko nafikiri sana juu ya namna Yehova amemubariki.