Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Waisraeli wa Zamani Walipigana Vita​—Juu ya Nini Siye Hapana?

Waisraeli wa Zamani Walipigana Vita​—Juu ya Nini Siye Hapana?

WAKATI ya Vita ya Pili ya Ulimwengu, mukubwa wa maaskari Wanazi aliambia hivi kwa ukali kikundi fulani ya Mashahidi wa Yehova: “Kama munakatala kupigana na Ufaransa ao Uingereza, nyiye wote munapaswa kufa!” Hata kama maaskari Wanazi walikuwa pale karibu, hakuna ndugu mwenye alikubali kuvunja sheria ya Yehova. Iliomba uhodari kabisa! Ni mufano muzuri wenye unaonyesha mawazo ya Mashahidi wa Yehova kuhusu vita: Tunakatala kupigana vita za hii dunia. Hata kama wanatuambia kuwa watatuua juu hatupigane vita, tunakatala kujiingiza mu vita za hii dunia.

Lakini, wale wote wenye kujiita kuwa Wakristo hawana ile mawazo. Wengi wanaamini kama Mukristo anaweza na anapaswa kupigania inchi yake. Wanaweza kufikiri hivi: ‘Waisraeli wa zamani walikuwa watu wa Mungu na walikuwa napigana vita, sasa juu ya nini Wakristo hawawezi kufanya vile leo?’ Unaweza kujibia namna gani ile ulizo? Unapaswa kuwafasiria kama hali ya Waisraeli wa zamani iko tofauti sana na ya watu wa Mungu leo. Ona tofauti tano.

1. WATU WA MUNGU WALIFANYIZA WOTE TAIFA MOYA

Zamani, Yehova alichagua taifa moya ikuwe taifa yake, ni kusema, Israeli. Aliita Waisraeli kuwa “mali [yake] ya pekee.” (Kut. 19:5) Mungu aliwapatia pia eneo fulani. Kwa hiyo, wakati Mungu aliamuru Waisraeli waende kupigana vita na mataifa ingine, hawakukuwa napigana ao kuua waabudu wenzao. *

Leo, waabudu wa kweli wanatoka mu “mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga.” (Ufu. 7:9) Kama waabudu wa Mungu wanaenda kupigana vita, watapigana na hata kuua waabudu wenzao.

2. YEHOVA ALIAMURU WAISRAELI WAENDE KU VITA

Zamani, Yehova aliamua ni wakati gani na juu ya nini Waisraeli walipaswa kuenda ku vita. Kwa mufano, Mungu aliamuru Waisraeli wapigane juu ya kutimiza hukumu yake juu ya Wakanaani, wenye walikuwa naabudu pepo wachafu, walikuwa waasherati sana, na walikuwa wanatoa watoto wao kuwa zabihu. Yehova aliamuru Waisraeli waharibu ile mataifa yenye ilikuwa nafanya ile mambo ya mubaya mu inchi ya ahadi, juu Waisraeli nao pia wasianze kufanya ile mambo. (Law. 18:24, 25) Kisha Waisraeli kuingia mu Inchi ya Ahadi, wakati fulani Yehova aliwaruhusu waende kupigana na maadui wao. (2 Sa. 5:17-25) Lakini, hakuna wakati Yehova aliruhusu Waisraeli wajiamulie wao wenyewe kama walipaswa kuenda ku vita. Wakati walijiamulia wao wenyewe, mara mingi matokeo ilikuwa mubaya sana.​—Hes. 14:41-45; 2 Ny. 35:20-24.

Leo, Yehova haruhusu wanadamu waende ku vita. Mataifa inapigana juu ya kuendeleza faida zao wenyewe hapana faida za Mungu. Wanaweza kuenda ku vita juu wanapenda kupata maeneo zaidi, ao juu wanapenda kuwa na makuta mingi zaidi, ao juu wanapenda kuendeleza mawazo fulani ya politike. Tuseme nini basi kuhusu wale wenye wanasema kama wanapigana katika jina ya Mungu ili kulinda dini yao ao juu ya kuua maadui wa Mungu? Yehova atalinda waabudu wake wa kweli na ataharibu maadui wake mu vita yenye iko nakuya, ni kusema, vita ya Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16) Mu ile vita, jeshi ya Mungu itafanyizwa tu na viumbe wake wa roho, hapana waabudu wake wanadamu.​—Ufu. 19:11-15.

3. WAISRAELI HAWAKUUA WALE WENYE WALIMUAMINI YEHOVA

Wenye kupigana vita leo wanahurumiaka wale wenye kuwa waaminifu sawa vile Waisraeli walihurumia Rahabu na familia yake wakati walipigana na Yeriko?

Zamani, jeshi ya Waisraeli mara mingi ilihurumia wale wenye walionyesha imani katika Mungu, na iliua tu wale wenye Yehova aliamua kama wanapaswa kufa. Fikiria hii mifano mbili. Hata kama Yehova aliamuru Yeriko iharibiwe, Waisraeli hawakumuua Rahabu na familia yake juu ya imani yake. (Yos. 2:9-16; 6:16, 17) Tena, Waisraeli hawakuua wakaaji wa muji wa Gibeoni kisha wao kuonyesha kama wanamuogopa Mungu.​—Yos. 9:3-9, 17-19.

Leo, mataifa yenye kupigana haihurumiake wale wenye wako na imani. Na wakati fulani, watu wenye hawana kosa wanauawa wakati mataifa iko napigana.

4. WAISRAELI WALIPASWA KUFUATA MAAGIZO YA MUNGU KUHUSU VITA

Zamani, Yehova alipatia maaskari Waisraeli maagizo kuhusu vita na aliwaomba waifuate. Kwa mufano, wakati fulani Mungu aliambia Waisraeli kama mbele ya kupigana na wakaaji wa muji fulani, walipaswa kuwapatia “masharti ya amani,” ni kusema, walipaswa kuwaambia mambo ya kufanya ili wasipigane nao. (Kum. 20:10) Yehova aliambia pia maaskari Waisraeli wakuwe safi, kambi yao ikuwe safi, na watii kanuni za Yehova. (Kum. 23:9-14) Maaskari wa mataifa yenye kuwazunguka mara mingi walikuwa nabaka wanamuke kisha kushinda maeneo fulani. Lakini, Yehova alikataza Waisraeli kufanya vile. Maaskari Waisraeli hawakupaswa kuoa mwanamuke mwenye walikamata mu vita mupaka wakati mwezi moya upite.​—Kum. 21:10-13.

Leo, inchi za mingi zinasikilizana ili kupigana kulingana na sheria fulani. Hata kama zile sheria ziko na kusudi ya kulinda watu, jambo ya kuhuzunisha, mara mingi hawazifuatake.

5. MUNGU ALIPIGANIA TAIFA YAKE

Mungu iko napigania taifa fulani leo sawa vile alipigania Waisraeli wakati walipigana na Yeriko?

Zamani, Yehova alipigania Waisraeli. Mara mingi alifanya miujiza juu waweze kupata ushindi mu vita. Kwa mufano, namna gani Yehova alisaidia Waisraeli wapate ushindi juu ya muji wa Yeriko? Sawa vile Yehova alisema, wakati Waisraeli ‘walifanya makelele makubwa ya vita, ukuta ulianguka chini,’ ile ilifanya ikuwe mwepesi kwao kukamata muji. (Yos. 6:20) Na namna gani walipata ushindi juu ya Waamori? “Yehova alifanya mvua ya majiwe makubwa kutoka mbinguni inyeshe juu yao . . . Kwa kweli, wenye walikufa kwa majiwe hayo walikuwa wengi kupita wenye Waisraeli waliua kwa upanga.”​—Yos. 10:6-11.

Leo, Yehova hapiganie taifa yoyote hapa ku dunia. Ufalme wake, wenye kutawaliwa na Yesu, “hauko sehemu ya ulimwengu huu.” (Yoh. 18:36) Lakini, Shetani njo iko na mamlaka juu ya serikali zote za wanadamu. Vita zote zenye kuogopesha zenye zimepiganwa mu hii dunia zinaonyesha kama Shetani ni muovu sana.​—Lu. 4:5, 6; 1 Yoh. 5:19.

WAKRISTO WA KWELI WANAJIKAZA KUFANYA AMANI NA WENGINE

Vile tumetoka kuona, hali yetu leo iko tofauti sana na ya Waisraeli wa zamani. Lakini, haiko ile tu njo inafanya tusiende ku vita. Kuko sababu zingine. Kwa mufano, Mungu alisema kama mu siku za mwisho wale wenye kufundishwa naye “hawatajifunza vita tena.” Kama hawatajifunza vita tena, halafu kupigana vita njo watafanya? (Isa. 2:2-4) Zaidi ya ile, Kristo alisema kama wanafunzi wake ‘hawako sehemu ya ulimwengu.’ Ile inamaanisha kama hawapaswe kujiingiza mu mambo ya vita ya hii dunia.​—Yohana 15:19.

Kuko mambo ingine yenye Yesu alisema kama wafuasi wake hawapaswe kufanya. Aliwaambia waepuke tabia yenye inaweza kuwafanya waweke kinyongo, wakasirike, na wapigane vita. (Mt. 5:21, 22) Tena, aliwaagiza wafuasi wake wakuwe “wenye kufanya amani” na wapende maadui wao.​—Mt. 5:9, 44.

Na siye tunaweza kufanya vile namna gani? Pengine tunaweza kusema kama hatupendake kuenda ku vita. Lakini, pengine mu moyo wetu tungali na chuki yenye inaweza kutokeza mugawanyiko mu kutaniko. Kama ni vile, tuendelee kujikaza ili kutosha ile chuki mu moyo wetu.​—Yak. 4:1, 11.

Kuliko kujiingiza mu vita za mataifa, tunajikaza kuendeleza amani na upendo kati yetu. (Yoh. 13:34, 35) Tuazimie basi kutojiingiza mu mambo ya vita wakati tuko nangojea kwa hamu siku yenye Yehova atamaliza vita milele.​—Zb. 46:9.

^ Wakati fulani, makabila ya Israeli ilipigana kati yao, lakini ile haikumufurahisha Yehova. (1 Fa. 12:24) Na wakati fulani, Yehova alikubali vita kati ya mataifa fulani juu makabila fulani ilikuwa imemuasi ao imefanya zambi nzito.​—Amu. 20:3-35; 2 Ny. 13:3-18; 25:14-22; 28:1-8..