Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 48

Chunga Akili Yako Wakati Ushikamanifu Wako Unajaribiwa

Chunga Akili Yako Wakati Ushikamanifu Wako Unajaribiwa

“Chunga akili yako katika mambo yote.”​—2 TI. 4:5.

WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi

KIFUPI YA HABARI a

1. Kuchunga akili yetu maana yake nini? (2 Timoteo 4:5)

 WAKATI fulani, inaweza kuwa nguvu kwetu kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova na kwa tengenezo yake, zaidi sana wakati kunatokea jambo fulani mu kutaniko yenye inatuhuzunisha. Tunapaswa kufanya nini mu hali ya vile? Tunapaswa kuchunga akili yetu na kuendelea kuwa macho, kusimama “imara katika imani.” (Soma 2 Timoteo 4:5.) Kuchunga akili yetu maana yake kuendelea kuwa watulivu, kuwaza muzuri, na kujikaza kuona mambo namna Yehova anaiona. Wakati tunafanya vile, hisia zetu hazitaongoza mawazo yetu.

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Mu habari yenye kutangulia, tulizungumuzia majaribu tatu yenye inaweza kutoka inje ya kutaniko. Mu hii habari, tutazungumuzia majaribu tatu yenye tunaweza kupata mu kutaniko, yenye inaweza kujaribu ushikamanifu wetu kwa Yehova. Jaribu ya kwanza: Wakati tunawaza kama Mukristo mwenzetu ametutendea mubaya. Jaribu ya pili: Wakati tunapewa nizamu. Na jaribu ya tatu: Wakati inakuwa nguvu kujipatanisha na mabadiliko ya tengenezo ya Yehova. Namna gani tunaweza kuchunga akili yetu na kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova na kwa tengenzo yake wakati tunapata ile majaribu?

WAKATI TUNAWAZA KAMA MUKRISTO MWENZETU AMETUTENDEA MUBAYA

3. Tunaweza kutenda namna gani ikiwa tunawaza kuwa Mukristo mwenzetu ametutendea mubaya?

3 Kuko siku ulishakawaza kama Mukristo mwenzako amekutendea mubaya, pengine mutu fulani mwenye kuwa na madaraka? Pengine nia ya ule ndugu haikukuwa kukuumiza. (Ro. 3:23; Yak. 3:2) Lakini inawezekana matendo yake ilikuumiza. Pengine ulikosa usingizi juu ya kuwaza kuhusu ile jambo. Pengine hata ulijiuliza hivi: ‘Kama ndugu anatenda hivi, hii kabisa ni tengenezo ya Mungu?’ Vile njo kabisa Shetani anapendaka tuwaze. (2 Ko. 2:11) Mawazo ya vile inaweza kufanya tujitenge na Yehova na tengenezo yake. Kama tunawaza kuwa ndugu ao dada fulani ametutendea mubaya, tunaweza kufanya nini juu ya kuchunga akili yetu na kuepuka kuwaza sawa vile Shetani anapenda tuwaze?

4. Namna gani Yosefu alichunga akili yake wakati alitendewa mubaya, na mufano wake unatufundisha nini? (Mwanzo 50:19-21)

4 Usiweke kinyongo. Wakati Yosefu alikuwa kijana, ndugu zake walimutendea mubaya. Walimuchukia na wamoja kati yao walipenda hata kumuua. (Mwa. 37:4, 18-22) Kisha, walimuuzisha mu utumwa. Ile ilifanya Yosefu ateseke sana kwa miaka karibu 13. Yosefu angeweza kujiuliza ikiwa Yehova anamupenda kabisa. Na angejiuliza ikiwa Yehova alikuwa amemuacha mu ile wakati yenye alikuwa na lazima yake. Yosefu hakufanya vile. Lakini, alichunga akili yake kwa kubakia mutulivu. Wakati alipata nafasi ya kulipiza kisasi juu ya mambo yenye ndugu zake walimufanyia, hakufanya vile. Lakini, aliwaonyesha upendo na kuwasamehe. (Mwa. 45:4, 5) Yosefu alitenda vile juu alijikaza kuwa na mawazo ya muzuri. Kuliko kufikiria tu magumu yake, alifikiria jambo ya maana zaidi, ni kusema, kusudi ya Yehova. (Soma Mwanzo 50:19-21.) Tunajifunza nini? Kama umetendewa mubaya, usimuwekee Yehova kinyongo, ao kuwaza kama Yehova amekuacha. Lakini, ujikaze kuona namna Yehova iko nakusaidia kuvumilia ile magumu. Zaidi ya ile, wakati wengine wanakutendea mubaya, uwaonyeshe upendo juu upendo unafunika makosa.​—1 Pe. 4:8.

5. Miqueas alifanya nini juu ya kuchunga akili yake wakati aliwaza kama ametendewa mubaya?

5 Tufikirie mufano wa Miqueas, b muzee wa kutaniko mwenye anaishi Amerika ya Kusini. Alisema kama kuko wakati yenye aliona kama ametendewa kwa ukali na ndugu fulani wenye madaraka. Alisema hivi: “Siyakuwaka na mahangaiko sawa vile ile siku. Niliogopa sana. Nilikosa usingizi, na nililia sana juu nilikosa nifanye nini.” Lakini, Miqueas alichunga akili yake na alijikaza kutulia. Alisali kwa ukawaida na kumuomba Yehova amupatie roho takatifu na nguvu ya kuvumilia. Tena, alitafuta mu vichapo vyetu habari yenye inaweza kumusaidia. Tunajifunza nini? Kama unawaza kuwa ndugu ao dada fulani amekutendea mubaya, tulia na uepuke mawazo ya mubaya. Pengine kuko jambo fulani yenye ilimufanya aseme ao atende vile. Kwa hiyo, sali kwa Yehova na umuombe akusaidie kuona mambo namna ule ndugu ao dada anaiona. Kufanya vile kunaweza kukusaidia usihukumu haraka-haraka ndugu ao dada yako na kunaweza kukusaidia umusamehe. (Mez. 19:11) Kumbuka kama Yehova anajua muzuri hali yako na atakupatia nguvu yenye uko nayo lazima juu uvumilie.​—2 Ny. 16:9; Muh. 5:8.

WAKATI TUNAPEWA NIZAMU

6. Nizamu inaonyesha kuwa Yehova anatupenda. Juu ya nini ni muzuri kuelewa vile? (Waebrania 12:5, 6, 11)

6 Tunaweza kuumia wakati tunapewa nizamu. Lakini, kama tunafikiria tu ile maumivu, tunaweza kuanza kuwaza kama hatukutendewa kwa haki, na kama haituhusu ao ilitolewa kwa ukali sana. Ile inaweza kufanya tusielewe hii jambo ya maana sana: Nizamu inaonyesha kama Yehova anatupenda. (Soma Waebrania 12:5, 6, 11.) Na kama tunaacha hisia zetu zituongoze, tunamupatia Shetani nafasi ya kutushambulia. Anapenda tukatale nizamu, na jambo ya mubaya hata zaidi, anapenda tujitenge na Yehova na kutaniko. Kama umepewa nizamu, unaweza kufanya nini juu ya kuchunga akili yako?

Petro alikubali mashauri na nizamu, na ile ilifanya Yehova amutumie zaidi (Ona fungu ya 7)

7. (a) Sawa vile picha inaonyesha, kisha Petro kukubali nizamu, Yehova alimutumia namna gani? (b) Mufano wa Petro unatufundisha nini?

7 Ukubali nizamu, na ufanye mabadiliko. Zaidi ya mara moya, Yesu alimurekebisha Petro mbele ya mitume wengine. (Mk. 8:33; Lu. 22:31-34) Inawezekana ile ilimufanya Petro asikie haya. Lakini, Petro alibakia mushikamanifu kwa Yesu. Alikubali nizamu, na aliacha makosa yake imufundishe. Njo maana, Yehova alibariki ushikamanifu wa Petro na alimupatia madaraka makubwa mu kutaniko. (Yoh. 21:15-17; Mdo. 10:24-33; 1 Pe. 1:1) Mufano wa Petro unatufundisha nini? Wakati hatufikirie tu haya yenye nizamu inaleta, lakini tunakubali kurekebishwa, na tunafanya mabadiliko, tunapata faida na wengine pia wanapata faida. Wakati tunafanya vile, tunakuwa watu wa maana sana kwa Yehova na kwa ndugu na dada zetu.

8-9. Kisha kupewa nizamu, ku mwanzo Bernardo alijisikia namna gani, lakini nini njo ilimusaidia abadilishe mawazo yake?

8 Fikiria mambo yenye ilimufikia Bernardo, ndugu mwenye kuishi Mozambique. Alipoteza daraka ya kuwa muzee. Ku mwanzo, alijisikia namna gani? Anasema hivi: “Niliweka kinyongo, juu sikufurahia nizamu yenye nilipewa.” Alijiuliza kama wengine mu kutaniko watamuona namna gani. Anasema hivi: “Iliomba miezi fulani juu nifikie tena kuwa na mawazo ya muzuri, na nimutumainie tena Yehova na tengenezo yake.” Nini njo ilimusaidia Bernardo aone mambo kwa njia yenye kufaa?

9 Bernardo alibadilisha mawazo yake. Anasema hivi: “Wakati nilikuwa muzee, nilikuwa natumia Waebrania 12:7 juu ya kusaidia wengine wakuwe na mawazo ya muzuri kuhusu nizamu ya Yehova. Sasa nikajiuliza, ‘Nani njo anapaswa kutumikisha hii andiko?’ Watumishi wote wa Yehova, na miye pia.” Kisha, Bernardo alichukua hatua zingine zenye zilimusaidia amutumainie tena Yehova na tengenezo yake. Alianza kusoma Biblia sana na kufikiri sana juu ya mambo yenye alikuwa nasoma. Hata kama alijiuliza ikiwa ndugu na dada watamuona namna gani, alihubiri pamoya nao, alikusanyika, na kutoa maelezo ku mikutano. Kama na weye umepewa nizamu, usione tu haya yenye ile nizamu inakuletea. Ukubali mashauri na ufanye mabadiliko. c (Mez. 8:33; 22:4) Kama unafanya vile, ukuwe hakika kuwa Yehova atakubariki juu unashikamana naye na tengenezo yake.

WAKATI INAKUWA NGUVU KUJIPATANISHA NA MABADILIKO MU TENGENEZO

10. Pengine ni mabadiliko gani njo ilijaribu ushikamanifu wa wanaume fulani Waisraeli?

10 Mabadiliko mu tengenezo inaweza kujaribu ushikamanifu wetu. Kama hatuko waangalifu, inaweza hata kufanya tujitenge na Yehova. Kwa mufano, fikiria namna Waisraeli fulani walijisikia wakati kulitokea mabadiliko fulani. Mbele Sheria ya Musa itolewe, vichwa vya familia ao baba njo walikuwa nafanya kazi ya ukuhani mu familia zao. Walikuwa najenga mazabahu, na kumutolea Yehova zabihu kwa ajili ya familia zao. (Mwa. 8:20, 21; 12:7; 26:25; 35:1, 6, 7; Yob. 1:5) Lakini, wakati Sheria ya Musa ilitolewa, vichwa vya familia hawakuwa tena na ile pendeleo. Yehova alichagua makuhani kutoka mu familia ya Haruni juu wakuwe natoa zabihu. Kisha pale, ikiwa baba wa familia mwenye haiko muzao wa Haruni angeanza kufanya kazi ya ukuhani, angepaswa kuuawa. d (Law. 17:3-6, 8, 9) Pengine ile badiliko ilikuwa kati ya mambo yenye ilifanya Kora, Datani, Abiramu na wakubwa wengine 250 wapinge mamlaka ya Musa na Haruni. (Hes. 16:1-3) Hatujue kama ilikuwa vile na hatuwezi kuhakikisha ile jambo. Lakini, Kora na wenzake hawakuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova. Kama kunatokea mabadiliko fulani mu tengenezo, unaweza kufanya nini?

Wakati mugao wa Wakohati ulibadilika, walikuwa tayari kufanya kazi ya kuimba, kuchunga milango, na kufanya kazi mu madepo (Ona fungu ya 11)

11. Mufano wa Wakohati unatufundisha nini?

11 Utegemeze kabisa mabadiliko mu tengenezo. Wakati Waisraeli walikuwa nasafiri mu jangwa, Wakohati walikuwa na pendeleo ya pekee sana. Wakati kambi ya Waisraeli ilikuwa nahama, Wakohati fulani walibeba Sanduku ya Agano mbele ya watu wote. (Hes. 3:29, 31; 10:33; Yosh. 3:2-4) Ilikuwa pendeleo kubwa sana! Lakini, mambo ilibadilika wakati Waisraeli waliingia mu Inchi ya Ahadi. Haikukuwa tena lazima Sanduku ihame-hame. Kwa hiyo, kufikia wakati Sulemani alikuwa mufalme, Wakohati fulani walifanya kazi ya kuimba, wengine walifanya kazi ya kuchunga milango, na wengine walifanya kazi mu madepo. (1 Ny. 6:31-33; 26:1, 24) Hakuna fasi kwenye Biblia inaonyesha kama Wakohati walinungunika ao kuomba wapewe kazi ya kuonekana sana juu zamani walikuwa na pendeleo ya pekee sana. Tunajifunza nini? Utegemeze kwa moyo wote mabadiliko yenye tengenezo ya Yehova inafanya, hata kama inakuomba ubadilishe mugao wako. Furahia mugao wowote wenye unapewa. Ukumbuke kama haiko mugao wako njo unafanya Yehova akuone kuwa wa maana. Kutii njo jambo yenye Yehova anaona kuwa ya maana sana kuliko mugao wowote.​—1 Sa. 15:22.

12. Zaina alijisikia namna gani wakati mugao wake wa kutumikia ku Beteli ulifikia mwisho?

12 Fikiria mufano wa Zaina, dada mwenye kuishi Mashariki ya Kati. Mugao wake ulibadilika na alipoteza pendeleo yenye alikuwa napenda sana. Kisha kutumikia ku Beteli kwa miaka zaidi ya 23, mugao wake ulibadilika na akakuwa painia wa pekee. Anasema hivi: “Ile badiliko ilinishitua sana. Nilijiona wa bure na niliendelea kujiuliza hivi: ‘Nilifanya kosa gani?’” Jambo ya kuhuzunisha, ndugu na dada fulani mu kutaniko walimuongezea huzuni kwa kusema hivi: “Kama ungekuwa natumika muzuri, hawangekutosha ku Beteli.” Kwa kipindi fulani, Zaina alivunjika moyo sana na alikuwa nalia kila usiku. Lakini, anasema hivi: “Nilijikaza sana juu nisikuwe hata kidogo na mashaka na tengenezo ya Yehova ao kuwaza kama Yehova hanipendi.” Nini njo ilisaidia Zaina achunge akili yake?

13. Zaina alifanya nini juu aachane na mawazo yenye haifae yenye alikuwa nayo?

13 Zaina alijikaza juu aachane na mawazo yenye haifae yenye alikuwa nayo. Alifanya nini? Alisoma mu vichapo vyetu habari zenye kuzungumuzia magumu yake. Habari “Unaweza Kukabiliana na Kivunja-Moyo!” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 2, 2001, ilimusaidia sana. Ile habari inaeleza namna inawezekana Marko, muandikaji wa Biblia, alikuwa pia na mawazo ya vile wakati mugao wake ulibadilika. Zaina anasema hivi: “Mufano wa Marko njo dawa yenye ilinisaidia niache kuvunjika moyo.” Pia, Zaina alibakia karibu na marafiki wake. Hakujitenga na wengine, na hakukuwa tu mutu wa kujisikilia huruma. Alielewa kama roho ya Yehova njo iko naongoza tengenezo yake na kama wale wenye kuongoza wanamuhangaikia sana. Lakini, alitambua pia kama tengenezo ya Yehova iko na daraka ya kukamata maamuzi yenye inaona kama itasaidia kazi ya Yehova isonge mbele.

14. Vlado alikuwa na magumu ya kujipatanisha na mabadiliko gani, na nini njo ilimusaidia?

14 Fikiria mufano wa Vlado, muzee wa kutaniko wa miaka 73 mwenye kuishi Slovenia. Wakati kutaniko yake ilichangwa na kutaniko ingine na Jumba yao ya Ufalme ikafungwa, aliona kama ilikuwa nguvu kujipatanisha na ile mabadiliko. Anasema hivi: “Sikuelewa juu ya nini Jumba ya Ufalme ya kupendeza vile ilipaswa kufungwa. Niliumia sana juu tulikuwa njo tunatoka kuirekebisha. Niko seremala, na nilisaidia kutengeneza vitu fulani vya mupya vyenye vilikuwa ndani. Tena, kuchanga makutaniko ilileta mabadiliko mingi yenye haikukuwa mwepesi kwetu siye wazee-wazee.” Nini njo ilisaidia Vlado ategemeze ile mabadiliko? Anasema hivi: “Kujipatanisha na mabadiliko ya tengenezo ya Yehova kunaletaka tu baraka. Ile mabadiliko iko natutayarisha kwa ajili ya mabadiliko makubwa zaidi ya mu siku zenye kuya.” Ni nguvu kwako kujipatanisha na mabadiliko yenye inatokea wakati makutaniko inachangwa, ao wakati mugao wako unabadilika? Ukuwe hakika kama Yehova anakuelewa. Wakati unategemeza ile mabadiliko na kushikamana na Yehova na tengenezo yake, bila shaka utabarikiwa.​—Zb. 18:25.

CHUNGA AKILI YAKO KATIKA MAMBO YOTE

15. Tunaweza kufanya nini ili kuchunga akili yetu wakati tunapata majaribu mu kutaniko?

15 Juu mwisho wa huu ulimwengu unakaribia, tunaweza kuwa hakika kama majaribu inaweza kutokea mu kutaniko. Ile majaribu inaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kuwa washikamanifu kwa Yehova. Kwa hiyo, tunapaswa kuchunga akili yetu. Kama unawaza kama Mukristo mwenzako amekutendea mubaya, usiweke kinyongo. Kama unapewa nizamu, usione tu haya yenye ile nizamu inakuletea. Kubali mashauri, na ufanye mabadiliko. Wakati tengenezo ya Yehova inafanya mabadiliko yenye inakugusa kipekee, uikubali kwa moyo wote, na ufuate muongozo wenye inakutolea.

16. Unaweza kufanya nini juu uendelee kutumainia Yehova na tengenezo yake?

16 Inawezekana kuendeleza kumutumainia Yehova na tengenezo yake wakati ushikamanifu wako unajaribiwa. Lakini, juu uweze kufanya vile, unapaswa kuchunga akili yako, ni kusema, kutulia, kuwaza muzuri, na kuona mambo namna Yehova anaiona. Uazimie kujifunza habari za watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia wenye waliweza kupambana na majaribu ya vile, na ufikiri sana kuhusu mifano yao. Umuombe Yehova akusaidie, na usijitenge hata kidogo na kutaniko. Kama unafanya vile, hata nini itokee, Shetani hataweza kukutenganisha na Yehova na tengenezo yake.​—Yak. 4:7.

WIMBO 126 Ukuwe Macho, Usimame Imara, Ukuwe na Nguvu

a Ushikamanifu wetu kwa Yehova na kwa tengenezo yake unaweza kujaribiwa, zaidi sana wakati tunapata majaribu mu kutaniko. Hii habari itazungumuzia majaribu tatu, na mambo yenye tunaweza kufanya juu tubakie washikamanifu kwa Yehova na kwa tengenezo yake.

b Majina fulani imebadilishwa.

c Juu ya kupata mapendekezo yenye inaweza kukusaidia, ona habari yenye kichwa “Umewahi Kuwa na Mapendeleo ya Utumishi? Je, Unaweza Kutumikia Tena?” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 8, 2009, uku. 30.

d Sheria ilisema kama kichwa ya familia mwenye alipenda kuchinja munyama juu apate nyama ya kula alipaswa kupeleka ule munyama ku tabenakulo ao ku hekalu. Ni wale tu wenye walikuwa naishi mbali sana na tabenakulo ao hekalu njo hawakulazimika kufanya vile.​—Kum. 12:21.