Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 45

Namna Yehova Anatusaidia Kutimiza Kazi Yetu ya Kuhubiri

Namna Yehova Anatusaidia Kutimiza Kazi Yetu ya Kuhubiri

“Hakika watajua pia kwamba nabii alikuwa kati yao.”​—EZE. 2:5.

WIMBO 67 “Hubiri Neno”

KIFUPI YA HABARI a

1. Tunaweza kutazamia nini, na tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

 TUNAWEZA kutazamia kama watu fulani watatupinga wakati tutakuwa nafanya kazi yetu ya kuhubiri. Na wanaweza kutupinga hata zaidi mu wakati yenye kuya. (Da. 11:44; 2 Ti. 3:12; Ufu. 16:21) Lakini, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatupatia musaada wenye tuko nao lazima. Juu ya nini? Juu kila mara Yehova amesaidia watumishi wake watimize kazi yenye anawapatia hata ikuwe ya nguvu namna gani. Juu ya kuelewa ile jambo, tuzungumuzie mambo fulani yenye ilimufikia nabii Ezekieli, mwenye alikuwa nahubiria wahamishwa Wayahudi katika Babiloni.

2. Yehova alisema kama watu wa mu eneo yenye Ezekieli alipaswa kuhubiria walikuwa watu wa namna gani, na ni mambo gani tutazungumuzia mu hii habari? (Ezekieli 2:3-6)

2 Mu eneo yenye Ezekieli alipaswa kuhubiria mulikuwa watu wa namna gani? Yehova alisema kama walikuwa “kichwa-nguvu,” “wenye moyo mugumu,” na ‘wenye kuasi.’ Walikuwa wenye kuumiza kama miiba na walikuwa hatari kama nge. Njo maana Yehova alimuambia Ezekieli mara mingi hivi: ‘Usiogope’! (Soma Ezekieli 2:3-6.) Ezekieli aliweza kutimiza kazi yake ya kuhubiri juu (1) Yehova njo alimutuma, (2) roho ya Mungu ilimutia nguvu, na (3) Neno ya Mungu ilimutia nguvu. Namna gani ile mambo tatu ilimusaidia Ezekieli? Na namna gani inaweza kutusaidia leo?

YEHOVA NJO ALIMUTUMA EZEKIELI

3. Yehova alimuambia Ezekieli nini yenye ilipaswa kumutia nguvu, na ni maneno gani yenye kurudiliwa mara mingi yenye ilimuhakikishia Ezekieli kama Yehova atamusaidia?

3 Yehova alimuambia Ezekieli hivi: “Ninakutuma.” (Eze. 2:3, 4) Ile ilipaswa kumutia nguvu Ezekieli. Juu ya nini? Bila shaka, Ezekieli alipaswa kukumbuka kama Yehova alitumiaka maneno ya vile wakati alifanya Musa na Isaya kuwa manabii wake. (Kut. 3:10; Isa. 6:8) Ezekieli alijua pia namna Yehova alisaidia wale manabii wawili kupambana na magumu yenye walikutana nayo mu mugao wao. Kwa hiyo, wakati Yehova alimuambia Ezekieli mara mbili: “Ninakutuma,” Ezekieli alikuwa na sababu ya muzuri ya kutumainia kama Yehova atamusaidia. Tena, hii maneno inarudiliwa mara mingi mu kitabu ya Ezekieli: “Neno la Yehova likakuja kwangu.” (Eze. 3:16) Zaidi ya ile, maneno “neno la Yehova likakuja tena kwangu,” inarudiliwa mara mingi. (Eze. 6:1) Kusema kweli, Ezekieli alikuwa hakika kama Yehova njo alimutuma. Zaidi ya ile, baba ya Ezekieli alikuwa kuhani. Inawezekana alimufundisha Ezekieli kama sikuzote Yehova alihakikishia manabii wake kama atawasaidia. Yehova aliambia Isaka, Yakobo, na Yeremia hivi: “Niko pamoja na wewe.”​—Mwa. 26:24; 28:15; Yer. 1:8.

4. Ni mawazo gani yenye kutia moyo yenye ilipaswa kumutia nguvu Ezekieli?

4 Waisraeli wengi wangetenda namna gani wakati Ezekieli angewahubiria? Yehova alisema hivi: “Nyumba ya Israeli, watakataa kukusikiliza, kwa maana hawataki kunisikiliza mimi.” (Eze. 3:7) Kwa kukatala kumusikiliza Ezekieli, watu walikuwa nakatala kumusikiliza Yehova. Ile maneno ilimuhakikishia Ezekieli kama, hata kama watu wanakatala kumusikiliza, ile haikumaanisha kuwa hakutimiza muzuri kazi yake ya kuwa nabii. Yehova alimuhakikishia pia Ezekieli kama wakati mambo yenye alikuwa natangaza itatimia, watu ‘watajua kwamba kulikuwa nabii kati yao.’ (Eze. 2:5; 33:33) Bila shaka, ile mawazo yenye kutia moyo ilimupatia Ezekieli nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili kutimiza kazi yake ya kuhubiri.

NA SIYE YEHOVA NJO ANATUTUMA

Sawa vile Ezekieli, tunaweza kukutana na watu wenye hawapendezwe na tunaweza kupingwa. Lakini, tunajua kama Yehova iko pamoya na siye (Ona fungu ya 5-6)

5. Ni maneno gani yenye kuwa mu Isaya 44:8 yenye inatupatia nguvu?

5 Na siye tunapata nguvu juu tunajua kama Yehova njo anatutuma. Anatuheshimisha kwa kutuita kuwa “mashahidi” wake. (Isa. 43:10) Ile ni pendeleo kubwa! Sawa vile Yehova alimuambia Ezekieli: ‘Usiogope,’ na siye pia anatuambia: “Musiogope.” Juu ya nini hatuna sababu ya kuogopa wapinzani wetu? Juu sawa vile Ezekieli, Yehova njo anatutuma na iko natutegemeza.​—Soma Isaya 44:8.

6. (a) Mu Isaya 43:2, Yehova anatuambia mambo gani yenye inatuhakikishia kama atatusaidia? (b) Nini njo inatufariji na kututia nguvu?

6 Yehova anatuhakikishia kama atatusaidia. Kwa mufano, mbele tu Yehova aseme: “Muko mashahidi wangu,” alisema hivi: “Wakati unapita katika maji, nitakuwa pamoja na wewe; na wakati unapita katika mito, haitakuzamisha. Wakati unatembea katika moto, hautaungua, wala mwali wa moto hautakuchoma.” (Isa. 43:2) Kadiri tunaendelea kutimiza kazi yetu ya kuhubiri, wakati fulani tunaweza kukutana na magumu yenye tunaweza kulinganisha na mito yenye kuzamisha na pia majaribu yenye kuwa nguvu yenye tunaweza kulinganisha na moto. Hata vile, kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuendelea kuhubiri. (Isa. 41:13) Sawa vile mu siku za Ezekieli, watu wengi leo wanakatala kusikiliza ujumbe wenye tunawahubiria. Tunajua kama ikiwa wanakatala kutusikiliza, ile haimaanishe kama tumeshindwa kutimiza kazi yetu ya kutoa ushahidi. Kujua kama Yehova anafurahi wakati tunaendelea kutangaza ujumbe wake kwa uaminifu inatufariji na kututia nguvu. Mutume Paulo alisema hivi: “Kila mutu atapokea zawabu yake mwenyewe kulingana na kazi yake mwenyewe.” (1 Ko. 3:8; 4:1, 2) Dada moya painia wa zamani alisema hivi: “Inanipatiaka furaha kujua kama Yehova anakuwaka nabariki bidii yetu.”

ROHO YA MUNGU ILIMUTIA NGUVU EZEKIELI

Ezekieli anaona gari ya Yehova ya mbinguni. Ile inamuhakikishia kama Yehova atamusaidia kutimiza kazi yake ya kuhubiri (Ona fungu ya 7)

7. Wakati Ezekieli alifikiri juu ya maono yenye aliona, ile ilipaswa kumusaidia akuwe hakika na jambo gani? (Ona picha ku jalada.)

7 Ezekieli aliona namna roho ya Mungu ni yenye nguvu sana. Ezekieli aliona mu maono namna roho takatifu ilikuwa natenda juu ya viumbe vya kiroho vyenye nguvu, na namna ilikuwa naendesha magurudumu makubwa ya gari ya mbinguni. (Eze. 1:20, 21) Ezekieli alitenda namna gani kisha kuona ile maono? Aliandika mambo yenye ilitokea. “Wakati niliuona, nikaanguka uso chini.” Ezekieli alishangala sana mupaka akaanguka chini. (Eze. 1:28) Kisha, wakati Ezekieli alifikiri juu ya ile maono yenye kushangaza, ile ilipaswa kumusaidia akuwe hakika kabisa kama kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu, ataweza kutimiza kazi yake ya kuhubiri.

8-9. (a) Mambo yenye Yehova alimuamuru Ezekieli afanye ilimupatia nini? (b) Yehova alifanya tena nini ili kumupatia Ezekieli nguvu juu aweze kuhubiri mu eneo yake ya nguvu?

8 Yehova alimuamuru Ezekieli hivi: “Mwana wa binadamu, simama kwa miguu yako ili nizungumuze na wewe.” Ile amri na pia roho ya Mungu ilimupatia Ezekieli nguvu yenye alikuwa nayo lazima juu aweze kusimama kutoka chini. Ezekieli aliandika hivi: “Roho ikaingia ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu.” (Eze. 2:1, 2) Kisha pale na wakati alikuwa nafanya kazi yake ya kuhubiri, Ezekieli aliongozwa na “mukono” wa Mungu, ni kusema, roho takatifu ya Mungu. (Eze. 3:22; 8:1; 33:22; 37:1; 40:1) Roho ya Mungu ilimupatia Ezekieli nguvu ya kutimiza kazi yenye alipewa, ni kusema, kuhubiria watu wenye walikuwa ‘kichwa-nguvu na wenye walikuwa na moyo mugumu’ mu eneo yake. (Eze. 3:7) Yehova alimuambia Ezekieli hivi: “Nimefanya uso wako ukuwe mugumu sawasawa na nyuso zao na paji la uso wako likuwe nguvu sawasawa na mapaji ya nyuso zao. Nimefanya paji la uso wako likuwe kama almasi, nguvu kuliko jiwe ngumu. Usiwaogope, wala kutetemeshwa na nyuso zao.” (Eze. 3:8, 9) Ni sawa vile Yehova alikuwa namuambia Ezekieli hivi: ‘Usiache ugumu wa moyo wao ukuvunje moyo. Nitakutia nguvu.’

9 Kisha pale, roho ya Mungu ilimupeleka Ezekieli mu eneo kwenye alipaswa kuhubiri. Ezekieli aliandika hivi: “Mukono wa Yehova ukatulia juu yangu kwa nguvu.” Ilimukamata Ezekieli juma moya juu aweze kujifunza kabisa na kuelewa ujumbe wenye alipaswa kutangaza. (Eze. 3:14, 15) Kisha, Yehova alimuambia aende mu bonde tambarare na wakati alifika kule, “roho ikaingia ndani [yake].” (Eze. 3:23, 24) Ezekieli alikuwa tayari kuanza kazi yake ya kuhubiri.

NA SIYE ROHO YA MUNGU INATUTIA NGUVU

Sawa vile Ezekieli, nini njo inatusaidia kutimiza kazi yetu ya kuhubiri? (Ona fungu ya 10)

10. Tuko na lazima ya nini juu tuweze kutimiza kazi yetu ya kuhubiri, na juu ya nini?

10 Tuko na lazima ya nini juu tuweze kutimiza kazi yetu ya kuhubiri? Juu ya kupata jibu ya ile ulizo, fikiria tena mambo yenye ilimufikia Ezekieli. Mbele aanze kuhubiri, roho ya Mungu ilimupatia nguvu yenye alikuwa nayo lazima. Sawa vile Ezekieli, na siye tunaweza kufanya kazi ya kuhubiri kwa musaada tu wa roho takatifu ya Mungu. Juu ya nini? Juu Shetani anatupiganisha ili tuache kazi yetu ya kuhubiri. (Ufu. 12:17) Kwa mawazo ya wanadamu, inaonekana kama haiwezekane kumushinda Shetani. Lakini, tuko namushinda kupitia kazi yetu ya kuhubiri! (Ufu. 12:9-11) Mu njia gani? Wakati tunahubiri, tunaonyesha kama hatuogopeshwe na Shetani. Kila wakati tunahubiri, tunamushinda Shetani. Kuona vile tunaweza kufanya kazi yetu ya kuhubiri ijapokuwa upinzani kunaonyesha nini? Kunaonyesha kama roho takatifu iko natutia nguvu na kama Yehova anatukubali.​—Mt. 5:10-12; 1 Pe. 4:14.

11. Roho ya Mungu itatufanyia nini, na tunaweza kufanya nini juu tuendelee kuipata?

11 Tunajifunza tena nini wakati tunafikiria namna Yehova alimupatia Ezekieli nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili kuhubiri? Tunajifunza kama roho ya Mungu itatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili kushinda magumu yoyote yenye tunaweza kukutana nayo mu kazi yetu ya kuhubiri. (2 Ko. 4:7-9) Sasa, tunaweza kufanya nini juu tuendelee kupata roho ya Mungu? Tunapaswa kuendelea kumuomba Yehova atupatie roho yake, na kuwa hakika kama atasikiliza sala zetu. Yesu alifundisha wanafunzi wake hivi: “Muendelee kuomba, . . . muendelee kutafuta, . . . muendelee kupiga hodi.” Ili kujibia sala yao, Yehova “atawapatia . . . roho yake takatifu wale wenye kumuomba.”​—Lu. 11:9, 13; Mdo. 1:14; 2:4.

NENO YA MUNGU ILIMUTIA NGUVU EZEKIELI

12. Kulingana na Ezekieli 2:9–3:3, kitabu ya kukunjwa ilitoka wapi na mulikuwa nini?

12 Ezekieli hakutiwa tu nguvu na roho ya Mungu, lakini pia alitiwa nguvu na maneno ya Mungu. Mu maono, Ezekieli aliona mukono fulani wenye ulikuwa na kitabu ya kukunjwa. (Soma Ezekieli 2:9–3:3.) Ile kitabu ya kukunjwa ilitoka wapi? Mulikuwa nini? Ilitia nguvu Ezekieli namna gani? Muache tuone. Ile kitabu ya kukunjwa ilitoka ku kiti ya Ufalme ya Mungu. Inaonekana, Yehova alitumia mumoja kati ya malaika ine wenye Ezekieli alikuwa alishaona juu ya kumupatia Ezekieli ile kitabu ya kukunjwa. (Eze. 1:8; 10:7, 20) Mu ile kitabu ya kukunjwa, mulikuwa maneno ya Mungu, ni kusema, ujumbe murefu wa hukumu wenye Ezekieli alipaswa kutangazia wahamishwa wenye kuasi. (Eze. 2:7) Ule ujumbe ulikuwa umeandikwa mbele na nyuma ya ile kitabu ya kukunjwa.

13. Yehova alimuambia Ezekieli afanye kitabu ya kukunjwa nini, na juu ya nini ile kitabu ilikuwa butamu?

13 Yehova alimuambia nabii wake akule ile kitabu ya kukunjwa na ‘aijaze katika tumbo lake.’ Ezekieli alitii na akakula ile kitabu yote ya kukunjwa. Hii sehemu ya maono inamaanisha nini? Inamaanisha kama Ezekieli alipaswa kuelewa kabisa ujumbe wenye angetangaza. Ni sawa vile ule ujumbe ulipaswa kuwa sehemu yake, ili umuchochee kuhubiri. Kisha, jambo fulani yenye kushangaza ilitokea. Ezekieli alivumbula kama ile kitabu ya kukunjwa ilikuwa butamu kama asali. (Eze. 3:3) Juu ya nini? Juu Ezekieli, aliona pendeleo ya kumuwakilisha Yehova kuwa jambo ya butamu, yenye kufurahisha. (Zb. 19:8-11) Alikuwa mwenye shukrani juu Yehova alikubali amutumikie kama nabii wake.

14. Nini njo ilimusaidia Ezekieli akuwe tayari kukubali mugao wake?

14 Kisha, Yehova alimuambia Ezekieli hivi: “Tia katika moyo wako na usikilize maneno yangu yote yenye ninakuambia.” (Eze. 3:10) Wakati alimuambia vile, Yehova alipenda Ezekieli aweke mu akili maneno yenye kuandikwa mu ile kitabu ya kukunjwa na afikiri sana juu ya ile maneno. Wakati Ezekieli alifanya vile, imani yake ilikuwa nguvu. Tena, ilimupatia ujumbe wenye angetangazia watu. (Eze. 3:11) Juu Ezekieli alielewa kabisa na kuamini ujumbe wa Mungu, alikuwa tayari kuanza kuhubiri na kuendelea mupaka wakati alimaliza mugao wake.​—Linganisha na Zaburi 19:14.

NA SIYE NENO YA MUNGU INATUTIA NGUVU

15. Juu tuendelee kufanya kazi yetu ya kuhubiri, tunapaswa ‘kutia nini katika moyo’?

15 Juu tuendelee kufanya kazi yetu ya kuhubiri, na siye pia tuko na lazima ya kuendelea kutiwa nguvu na Neno ya Mungu. Tunapaswa ‘kutia katika moyo’ mambo yote yenye Yehova anatuambia. Leo, Yehova anazungumuza na siye kupitia Neno yake, Biblia. Tunaweza kufanya nini juu Neno ya Mungu iendelee kugusa mawazo, hisia na nia yetu?

16. Tunapaswa kufanya nini na Neno ya Mungu, na tunaweza kufanya nini juu ya kujaza Neno ya Mungu mu moyo wetu?

16 Tunapataka nguvu ya kimwili wakati tunakula chakula na wakati mwili unasaga ile chakula ili iweze kufanya kazi mu mwili. Vilevile, tunakuwa nguvu kiroho wakati tunajifunza Neno ya Mungu na kufikiri sana juu yake. Ile njo jambo yenye tunajifunza kuhusu kitabu ya kukunjwa. Yehova anapenda “tujaze tumbo [yetu] neno yake,” ni kusema, kuelewa muzuri Neno yake. Tunaweza kufanya vile kupitia sala, kusoma, na kutafakari. Kwanza, tunasali juu ya kutayarisha moyo wetu ili kupokea mawazo ya Mungu. Kisha, tunasoma andiko ya Biblia. Kisha pale, tunatua kidogo ili kutafakari, ao kuwaza sana, juu ya mambo yenye tumesoma. Kufanya vile kutatusaidia namna gani? Kutatusaidia kujaza Neno ya Mungu mu moyo wetu.

17. Juu ya nini ni jambo ya maana kutafakari kuhusu mambo yenye tunasoma mu Biblia?

17 Juu ya nini ni jambo ya maana kusoma Biblia na kutafakari kuhusu mambo yenye tunasoma? Juu wakati tunafanya vile, tunapata nguvu yenye tuko nayo lazima ili kutangaza ujumbe wa Ufalme sasa na ili kutangaza ujumbe muzito wa hukumu wenye tunaweza kutangaza karibuni. Pia, wakati tunafikiri sana juu ya sifa zenye kuvutia za Yehova, tutakuwa na uhusiano wa karibu sana pamoya naye. Na ile itafanya tufurahie jambo fulani ya butamu sana ao yenye kupendeza, ni kusema, amani ya moyo na kutosheka.​—Zb. 119:103.

TUENDELEE KUHUBIRI

18. Watu mu eneo yetu watafikia kuelewa nini, na ni wakati gani wataelewa vile?

18 Ezekieli alikuwa nabii, siye hatuko manabii. Lakini, tunaazimia kuendelea kutangaza ujumbe wa Yehova, wenye kuandikwa mu Neno yake, mupaka wakati Yehova atasema tuachie pale. Wakati saa ya hukumu itafika, watu mu eneo yetu hawatakuwa na sababu ya kusema kama hatukuwaambiaka ao kama Mungu hawahangaikie. (Eze. 3:19; 18:23) Lakini, watafikia kuelewa kama ujumbe wenye tulikuwa nahubiri ulitoka kabisa kwa Mungu.

19. Nini njo itatupatia nguvu ya kutimiza kazi yetu ya kuhubiri?

19 Nini njo itatupatia nguvu ya kutimiza kazi yetu ya kuhubiri? Ni ileile mambo tatu yenye ilimupatia nguvu Ezekieli. Tunaendelea kuhubiri juu tunajua kama Yehova njo anatutuma, roho takatifu ya Mungu inatutia nguvu, na Neno ya Mungu inatutia nguvu. Kwa musaada wa Yehova, tunatiwa nguvu kuendelea kutimiza utumishi wetu na kuvumilia “mupaka mwisho.”​—Mt. 24:13.

WIMBO 65 Fanya Maendeleo!

a Mu hii habari, tutazungumuzia mambo tatu yenye ilimusaidia nabii Ezekieli atimize kazi yake ya kuhubiri. Tutaona namna Yehova alimusaidia nabii wake, na ile itatusaidia tukuwe hakika kama atatusaidia kutimiza kazi yetu ya kuhubiri.