Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 46

Namna Yehova Anatusaidia Kuvumilia Magumu Yetu kwa Furaha

Namna Yehova Anatusaidia Kuvumilia Magumu Yetu kwa Furaha

“Yehova anawangojea kwa uvumilivu ili awaonyeshe wema, na atasimama ili kuwaonyesha rehema.”​—ISA. 30:18.

WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea

KIFUPI YA HABARI a

1-2. (a) Tutazungumuzia maulizo gani? (b) Nini njo inaonyesha kama Yehova iko tayari kabisa kutusaidia?

 YEHOVA anaweza kutusaidia kupambana na magumu mu maisha yetu na kuendelea kumutumikia kwa furaha. Anatusaidiaka mu njia gani? Na tunaweza kufanya nini juu tufaidike kabisa na musaada wa Yehova? Hii habari itajibia ile maulizo. Lakini, mbele ya kujibia ile maulizo, tujibie kwanza hii ulizo: Yehova iko tayari kabisa kutusaidia?

2 Mu barua yenye mutume Paulo aliandikia Waebrania, alitumia neno yenye inaweza kutusaidia kupata jibu. Paulo aliandika hivi: “Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunifanya nini?” (Ebr. 13:6) Kitabu moya inasema kama mu hii andiko neno “musaidizi” inaleta wazo ya mutu mwenye kukimbia ili kusaidia mutu fulani mwenye iko anaita watu juu wakuye kumusaidia. Uwazie Yehova iko anakimbia ili kuenda kusaidia mutu mwenye iko mu magumu. Bila shaka, ile mafasirio inaonyesha kama Yehova iko tayari kabisa kutusaidia. Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuvumilia magumu yetu kwa furaha.

3. Ni mambo gani tatu yenye Yehova anafanyaka juu ya kutusaidia tuvumilie magumu yetu kwa furaha?

3 Ni mambo gani yenye Yehova anafanyaka juu ya kutusaidia tuvumilie magumu yetu kwa furaha? Juu ya kujibia ile ulizo, muache tusome sehemu fulani ya kitabu ya Isaya. Juu ya nini? Juu maunabii mingi yenye Yehova aliongoza Isaya kuandika inahusu watumishi wa Yehova leo. Tena, mara mingi wakati Isaya anazungumuza juu ya Yehova, anatumia maneno ya mwepesi yenye tunaweza kuelewa. Isaya sura ya 30 iko na mifano fulani. Mu ile sura, Isaya anatumia maneno ya mufano ili kuonyesha namna Yehova anasaidiaka watu wake. Aliandika kama Yehova anatusaidiaka (1) kwa kusikiliza kwa uangalifu na kujibia sala zetu, (2) kwa kutuongoza, na (3) kwa kutubariki sasa na wakati yenye kuya. Tuchunguze basi kwa ukaribu mambo tatu yenye Yehova anafanyaka ili kutusaidia.

YEHOVA ANATUSIKILIZA

4. (a) Namna gani Yehova aliita Wayahudi wa wakati ya Isaya, na aliruhusu jambo gani itokee? (b) Ni tumaini gani yenye Yehova alipatia wale waaminifu? (Isaya 30:18, 19)

4 Ku mwanzo wa Isaya sura ya 30, Yehova anaita Wayahudi kuwa “wana wenye wako kichwa-nguvu,” wenye ‘wanaongeza zambi juu ya zambi.’ Anaendelea kwa kusema hivi: “Wao ni watu waasi, . . . wenye hawataki kusikia sheria ya Yehova.” (Isa. 30:1, 9) Juu watu walikatala kusikiliza, Isaya alitabiri kama Yehova angewaacha wateseke. (Isa. 30:5, 17; Yer. 25:8-11) Na ni vile mambo ilikuwa. Wababiloni walipeleka Waisraeli katika uhamisho Babiloni. Lakini, kulikuwa waaminifu fulani kati ya Wayahudi, na Isaya alikuwa na ujumbe fulani wa tumaini kwa ajili yao. Aliwaambia kama siku moya Yehova atawarudisha mu inchi yao. (Soma Isaya 30:18, 19.) Na ni vile mambo ilikuwa kabisa. Yehova aliwakomboa mu uhamisho kule Babiloni. Lakini, miaka mingi ilipita mbele Yehova awakomboe. Maneno “Yehova anawangojea kwa uvumilivu ili awaonyeshe wema” ilionyesha kama wakati fulani ingepita mbele wale waaminifu wakombolewe. Kwa hiyo, Waisraeli walipitisha miaka 70 mu uhamisho Babiloni mbele wamoja kati yao waruhusiwe kurudia Yerusalemu. (Isa. 10:21; Yer. 29:10) Wakati tu walifika mu inchi yao, machozi ya huzuni yenye waliangusha mu uhamisho iligeuka na kuwa machozi ya furaha.

5. Isaya 30:19 inatuhakikishia nini?

5 Leo tunaweza kutiwa moyo kupitia hii maneno: “Atakuonyesha wema wakati utalia kwa sauti kubwa ili kuomba musaada.” (Isa. 30:19) Mu ile andiko, Isaya anatuhakikishia kama Yehova atasikiliza kwa uangalifu wakati tunamulilia, na atajibia haraka sala zetu. Isaya anaongezea hivi: “Atakujibu wakati tu atasikia kilio chako.” Ile maneno yenye kutia moyo inatukumbusha kama Baba yetu iko tayari kabisa kusaidia wale wenye wanamulilia. Kujua vile kunatusaidia kuvumilia kwa furaha.

6. Maneno ya Isaya inaonyesha namna gani kama Yehova anasikilizaka sala ya kila mutumishi wake?

6 Ile andiko inatufundisha jambo gani ingine kuhusu sala? Inatufundisha kama Yehova anasikilizaka kwa uangalifu sala ya kila mutumishi wake. Juu ya nini tunasema vile? Mu sehemu ya kwanza ya Isaya sura ya 30, Yehova anazungumuza na watu wake kwa ujumla. Lakini, mu mustari wa 19, Yehova anazungumuza na mutu mumoja-mumoja. Isaya anaandika hivi: “Hautalia tena”; “hakika atakuonyesha wema”; “atakujibu.” Juu Yehova ni Baba mwenye upendo, haambiake mutumishi wake mwenye amevunjika moyo hivi: “Unapaswa kuwa roho nguvu sawa ndugu ao dada fulani.” Lakini, anahangaikia kila mumoja wetu kipekee, na anasikilizaka kwa uangalifu sala zake.​—Zb. 116:1; Isa. 57:15.

Isaya alimaanisha nini wakati alisema: “Musiache [Yehova] apumuzike”? (Ona fungu ya 7)

7. Isaya na Yesu walisema nini yenye kuonyesha kama ni jambo ya maana kusali tena na tena?

7 Wakati tunamuambia Yehova mambo yenye kutuhangaisha, jambo yenye anaweza kufanya kwanza ni kutupatia nguvu ya kuvumilia ile hali. Na kama magumu yetu haimalizike haraka sawa vile tuliwazia, tunaweza kumuomba Yehova tena na tena atupatie nguvu ya kuivumilia. Anatuomba tufanye vile. Hii maneno ya Isaya njo inatusaidia kujua vile: “Musiache [Yehova] apumuzike.” (Isa. 62:7) Ile inamaanisha nini? Tunapaswa kusali kwa Yehova tena na tena, ikuwe sawa vile hatumuache Yehova apumuzike. Maneno ya Isaya inatukumbusha mufano wenye Yesu alitoa kuhusu sala mu Luka 11:8-10, 13. Mu ile andiko, Yesu anatutia moyo ‘tuendelee kuomba kwa uhodari’ na ‘tuendelee kuomba’ Mungu atupatie roho takatifu. Tunaweza pia kumuomba Yehova atuongoze juu tukamate maamuzi ya muzuri.

YEHOVA ANATUONGOZA

8. Namna gani maneno ya Isaya 30:20, 21 ilitimia zamani?

8 Soma Isaya 30:20, 21. Wakati jeshi ya Babiloni ilizunguka Yerusalemu kwa mwaka moya na nusu, watu waliteseka sana mupaka ile mateso ikakuwa sawa vile mukate na maji yao ya kila siku. Lakini, kulingana na mistari ya 20 na 21, Yehova aliahidi Wayahudi kama, ikiwa wanatubu na kubadilisha tabia yao, angewaokoa. Isaya alimuita Yehova kuwa “Mufundishaji wao Mukubwa,” na aliahidi watu kama Yehova angewafundisha namna ya kumuabudu mu njia yenye anakubali. Ile maneno ilitimia wakati Wayahudi waliwekwa huru kutoka mu uhamisho. Yehova alionyesha kama alikuwa Mufundishaji wao Mukubwa, na aliwasaidia waweze kurudisha ibada safi. Leo, tuko wenye kubarikiwa sana juu Yehova njo Mufudishaji wetu Mukubwa.

9. Ni njia gani ya kwanza yenye Yehova anatumia juu ya kutuongoza leo?

9 Wakati anaendelea na maneno yake ya mufano, Isaya anaonyesha kama tuko sawa vile wanafunzi wenye kufundishwa na Yehova mu njia mbili. Kwanza, Isaya anasema hivi: “Utamuona Mufundishaji wako Mukubwa kwa macho yako mwenyewe.” Mu ile maneno ya mufano, Isaya anaonyesha kama Mufundishaji ni mwenye kusimama mbele ya wanafunzi wake. Tuko na pendeleo sana ya kufundishwa na Yehova leo. Yehova anatufundisha namna gani? Anafanya vile kupitia tengenezo yake. Tuko wenye shukrani sana juu ya muongozo wenye kuwa wazi wenye tengenezo ya Yehova inatupatia! Mafundisho yenye tunapata ku mikutano yetu ya kutaniko, na ku mikusanyiko, na hata kupitia vichapo vyetu, programu za JW Télédiffusion, na kupitia njia zingine za mingi inatusaidia kuvumilia magumu kwa furaha.

10. Ni mu njia gani tunasikia “neno nyuma [yetu]”?

10 Isaya anaonyesha njia ya pili yenye Yehova anatumia juu ya kutuongoza, wakati anasema hivi: “Masikio yako yatasikia neno nyuma yako.” Hapa nabii Isaya anaonyesha kama Yehova ni Mufundishaji muangalifu, mwenye anatembea nyuma ya wanafunzi wake na kuwaonyesha njia yenye wanapaswa kufuata. Leo, tunasikia sauti ya Mungu nyuma yetu. Mu njia gani? Maneno yenye kuongozwa na roho ya Mungu iliandikwa mu Biblia zamani sana, wakati ya zamani sana yenye kuwa nyuma yetu. Kwa hiyo, wakati tunasoma Biblia, ni sawa vile tuko tunasikia sauti ya Mungu yenye kutoka nyuma yetu.​—Isa. 51:4.

11. Juu tuendelee kumutumikia Yehova kwa furaha, ni mambo gani tunapaswa kufanya, na juu ya nini?

11 Tunapaswa kufanya nini juu muongozo wenye Yehova anatutolea kupitia tengenezo yake na Neno yake utuletee faida? Ona mambo mbili yenye Isaya anaonyesha. Kwanza, “hii ndiyo njia.” Pili, “mutembee ndani yake.” (Isa. 30:21) Haitoshe tu kujua “njia.” Tunapaswa pia “kutembea ndani yake.” Kupitia Neno ya Yehova, na mafasirio yenye tengenezo yake inatupatia, tunajifunza mambo yenye Yehova anapenda tufanye. Tunajifunza pia namna ya kutumikisha mambo yenye tunajifunza. Juu tuendelee kumutumikia Yehova kwa furaha, tunapaswa kufanya ile mambo mbili. Ni kwa kufanya vile tu njo tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatubariki.

YEHOVA ANATUBARIKI

12. Kulingana na Isaya 30:23-26, Yehova alibariki watu wake namna gani?

12 Soma Isaya 30:23-26. Ule unabii ulitimia namna gani kwa Wayahudi wenye walitoka katika uhamisho Babiloni na kurudia mu inchi yao, Israeli? Walipata baraka mingi, za kimwili na za kiroho. Yehova alibariki watu wake kwa kuwapatia chakula ya kimwili. Lakini, jambo ya maana zaidi, aliwabariki kwa kuwapatia chakula mingi ya kiroho kadiri ibada safi ilirudishwa pole kwa pole. Baraka za kiroho zenye watu wa Mungu walifurahia mu ile wakati zilipita sana jambo yoyote yenye walikuwa wamepata mbele. Mustari wa 26 unaonyesha kama Yehova aliwaangazia, ni kusema, aliwasaidia kuelewa Neno yake. (Isa. 60:2) Baraka za Yehova zilisaidia watumishi wake waendelee kumutumikia kwa furaha na nguvu “kwa sababu ya hali ya muzuri ya moyo.”​—Isa. 65:14.

13. Unabii juu ya kurudishwa kwa ibada safi umetimia namna gani leo?

13 Unabii juu ya kurudishwa kwa ibada safi unatuhusu pia leo? Ndiyo! Namna gani? Tangu 1919 K.K.Y., mamilioni ya watu hawako tena watumwa wa Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo. Wameingia fasi ya muzuri sana kuliko Inchi ya Ahadi ya Waisraeli. Wameingia mu paradiso ya kiroho. (Isa. 51:3; 66:8) Ile paradiso ya kiroho njo nini?

14. Paradiso ya kiroho njo nini, na ni wanani njo wanaishi ndani yake leo? (Ona Mafasirio ya Maneno Fulani.)

14 Tangu 1919 K.K.Y., watiwa-mafuta wamefurahia kuishi mu paradiso ya kiroho. b Kadiri wakati imepita, wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi ku dunia, ni kusema, “kondoo wengine,” wameingia pia mu hii inchi ya kiroho na wamefurahia baraka mingi za Yehova.​—Yoh. 10:16; Isa. 25:6; 65:13.

15. Paradiso ya kiroho iko wapi?

15 Inchi ya kiroho, ao paradiso ya kiroho, iko wapi leo? Waabudu wa Yehova wanapatikana fasi yote mu dunia. Kwa hiyo, paradiso ya kiroho yenye wanaishi ndani iko pia mu dunia yote. Njo maana leo, hata tukuwe wapi, tuko mu paradiso ya kiroho wakati tunategemeza kwa bidii ibada ya kweli.

Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini juu ya kusaidia paradiso ya kiroho ipendeze zaidi? (Ona fungu ya 16-17)

16. Tunapaswa kufanya nini juu tuendelee kuona uzuri wa paradiso ya kiroho?

16 Juu tubakie mu paradiso ya kiroho, tunapaswa kuendelea kuona kutaniko ya Kikristo ya mu dunia yote kuwa ya maana sana. Tunaweza kufanya vile namna gani? Tunapaswa kukaza akili juu ya uzuri hapana uzaifu wa wale wenye kuwa ndani ya paradiso ya kiroho. (Yoh. 17:20, 21) Juu ya nini ile ni jambo ya maana sana? Tukamate mufano. Tunajua kama mu pori ya kupendeza munakuwaka miti mbalimbali. Vilevile, mu makutaniko yetu leo kuko watu mbalimbali wenye wanalinganishwa na miti. (Isa. 44:4; 61:3) Tunapaswa kuendelea kukaza akili juu ya uzuri wa ile “pori,” ni kusema, kutaniko, hapana juu ya uzaifu wa “miti,” ni kusema, ndugu na dada. Hatupaswe kuacha uzaifu wetu ao uzaifu wa wengine mu kutaniko utufanye tusione uzuri wa kutaniko ya Kikristo yenye umoja ya mu dunia yote.

17. Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini juu kutaniko iendelee kuwa na umoja?

17 Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini juu kutaniko iendelee kuwa na umoja? Kila mumoja wetu anapaswa kuwa mwenye kufanya amani. (Mt. 5:9; Ro. 12:18) Kila mara wakati tunakamata hatua ya kuendeleza amani pamoya na wengine mu kutaniko, tunafanya paradiso ya kiroho ipendeze zaidi. Tusisahau kama Yehova amevuta kila mukaaji wa paradiso ya kiroho mu ibada safi. (Yoh. 6:44) Wazia namna Yehova anapaswa kufurahi sana wakati anaona vile tunajikaza ili kuendeleza amani na umoja kati ya wale wenye anaona kuwa wa maana sana, ni kusema, watumishi wake!​—Isa. 26:3; Hag. 2:7.

18. Ni muzuri tukuwe nafikiri sana juu ya mambo gani, na juu ya nini?

18 Tunaweza kufanya nini juu tufaidike kabisa na baraka zenye Mungu anapatia watumishi wake? Ni muzuri tukuwe nafikiri sana juu ya mambo yenye tunajifunza mu Neno ya Mungu na vichapo vyetu vyenye vinategemea Biblia. Kufanya vile kutatusaidia kukomalisha sifa za Kikristo zenye zitatuchochea kuonyesha “upendo wa kindugu” na “upendo wenye upole kwa mutu na mwenzake” mu kutaniko. (Ro. 12:10) Wakati tunafikiri sana juu ya baraka zenye tunapata sasa, urafiki wetu na Yehova unakuwa nguvu zaidi. Na kufikiri sana juu ya baraka zenye Yehova ametuwekea kunatusaidia tuone tumaini yetu ya kumutumikia Yehova milele kuwa jambo ya kweli kabisa. Ile yote inatusaidia tumutumikie Yehova kwa furaha sasa.

TUENDELEE KUVUMILIA

19. (a) Kulingana na Isaya 30:18, tuko hakika na jambo gani? (b) Nini njo itatusaidia tuendelee kumutumikia Yehova kwa furaha?

19 Yehova “atasimama” ili kutupigania wakati ataharibu huu ulimwengu muovu. (Isa. 30:18) Tuko hakika kama Yehova, “Mungu wa haki,” hataacha ulimwengu wa Shetani uendelee kwa siku mingi kuliko vile haki inaomba. (Isa. 25:9) Tunaendelea kungojea kwa uvumilivu ile siku ya wokovu pamoya na Yehova. Mbele ile wakati ifike, tunaazimia kuendelea kusamini pendeleo ya sala, kujifunza na kutumikisha Neno ya Mungu, na kufikiri sana juu ya baraka zetu. Wakati tunafanya vile, Yehova atatusaidia tuendelee kumutumikia kwa furaha.

WIMBO 142 Tusiache Tumaini Yetu

a Hii habari itazungumuzia mambo tatu yenye Yehova anafanyaka ili kusaidia waabudu wake kuvumilia magumu ya maisha kwa furaha. Tutajifunza ile mambo tatu kwa kuchunguza Isaya sura ya 30. Wakati tutazungumuzia ile sura, tutaona juu ya nini ni jambo ya maana kusali kwa Yehova, kujifunza Neno yake, na kufikiri sana juu ya baraka zenye tuko nazo sasa, na zenye tutapata wakati yenye kuya.

b MAFASIRIO YA MANENO FULANI: “Paradiso ya kiroho” ni fasi ya usalama kwenye tunamuabudu Yehova kwa umoja. Mu paradiso ya kiroho, tuko na chakula mingi ya kiroho yenye haina ndani uongo wa dini, na tuko na kazi ya muzuri sana ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Tuko na uhusiano wa karibu sana pamoya na Yehova, na tunaishi kwa amani pamoya na ndugu na dada zetu, wenye kutupenda na wenye kutusaidia kuvumilia magumu ya maisha kwa furaha. Tunaingia mu paradiso ya kiroho wakati tunaanza kumuabudu Yehova mu njia yenye anapenda na wakati tunafanya yetu yote ili kumuiga.