Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

“Nilipenda Kumutumikia Yehova”

“Nilipenda Kumutumikia Yehova”

TULILAGANA na kikundi kidogo ya watu wenye tulikuwa tumetembelea karibu na kijiji ya Granbori, yenye inapatikana mu maeneo ya mapori ya Suriname. Kisha tuliingia mu mutumbwi wa mbao na tukatembea juu ya muto Tapanahoni. Kisha wakati fulani, wakati tulikuwa napita juu ya maporomoko ya maji, chombo yenye ilikuwa naendesha mashua iligonga mwamba. Mara moya, sehemu ya mbele ya mutumbwi ikaangukia mu muto na siye tukaangukia mu maji. Moyo wangu ukashituka. Hata kama kwa miaka mingi nilikuwa nasafiri kwa mutumbwi wakati nilikuwa mwangalizi wa muzunguko, sikukuwa najua namna ya kuogelea!

Mbele niwaambie mambo yenye ilitokea kisha, acha niwaambie namna nilianza utumishi wa wakati yote.

Nilizaliwa mu kisiwa ya muzuri ya Karibea ya Curaçao mu 1942. Baba yangu alikuwa wa Suriname, lakini alihamiaka mu ile kisiwa juu ya kazi. Miaka fulani mbele nizaliwe, alikuwa kati ya Mashahidi wa Yehova wa kwanza kubatizwa katika Curaçao. a Alikuwa najifunza Biblia na siye kila juma, hata kama hatukukuwa napenda kujifunza. Wakati nilikuwa na miaka 14, baba yangu alihamishia familia yetu Suriname juu ya kuchunga mama yake mwenye alikuwa amezeeka.

MARAFIKI WAZURI WALINISAIDIA

Mu Suriname, nilianza kufanya urafiki na vijana mu kutaniko, wenye walikuwa namutumikia Yehova kwa bidii. Walikuwa na miaka mingi kunipita na walikuwa mapainia wa kawaida. Wakati walikuwa naeleza mambo yenye walikutana nayo mu mahubiri, nilikuwa naona namna walikuwa na furaha sana. Kisha mikutano, miye na marafiki wangu tulikuwa pia nazungumuzia habari za Biblia. Wakati fulani, tulikuwa nafanya vile na tulishaikala inje, na tuko naangalia nyota. Wale marafiki walinisaidia kutambua mambo yenye nilipenda kufanya mu maisha yangu: Nilipenda kumutumikia Yehova. Njo maana, nilibatizwa wakati nilikuwa na miaka 16. Kisha, wakati nilikuwa na miaka 18, nilianza kazi ya upainia wa kawaida.

MAMBO YA MAANA YENYE NILIJIFUNZA

Wakati nilikuwa painia mu Paramaribo

Wakati nilikuwa painia, nilijifunza mambo mingi ya maana na imenisaidia mu utumishi wangu wote. Kwa mufano, jambo ya kwanza yenye nilijifunza ni kama ni muzuri kuzoeza wengine. Wakati nilianza kazi ya upainia, misionere moya mwenye kuitwa Willem van Seijl alinisaidia sana. b Alinifundisha mambo mingi kuhusu namna ya kushugulikia migao mu kutaniko. Ile wakati, sikujua kama nilikuwa na lazima sana ya mazoezi. Mwaka wenye kufuata, niliwekwa kuwa painia wa pekee na kisha pale nilianza kutegemeza vikundi vidogo-vidogo vya ndugu na dada wenye walikuwa naishi mu maeneo ya mapori ya Suriname, mbali na makutaniko ingine. Niko mwenye shukrani sana juu ya mazoezi yenye ndugu walinipatiaka! Tangu ile wakati, nimejikaza kufuata mufano wao kwa kukamata wakati ya kuzoeza wengine.

Jambo ya pili yenye nilijifunza ni kama ni muzuri kuishi maisha ya mwepesi na kujua kujipanga. Ku mwanzo wa kila mwezi, miye na painia wa pekee mwenzangu tulikuwa nachunguza kama tutakuwa na lazima ya vitu gani mu majuma yenye kufuata. Kisha, mumoja kati yetu alikuwa nafanya safari ya murefu ili kuenda mu muji mukubwa na kuuza vitu vyenye tulikuwa navyo lazima. Tulipaswa kutumia muzuri makuta zenye tulikuwa napewa kila mwezi, na tulipaswa kubembeleza vile vitu juu vitufikishe ku mwisho wa mwezi. Kama vile vitu vinaisha wakati tulikuwa mu maeneo ya mapori, ilikuwa nguvu kupata mutu mwenye anaweza kutusaidia. Ninaamini kama juu nilijifunza kuishi maisha ya mwepesi wakati nilikuwa mutoto na pia kujua kujipanga muzuri kulinisaidia nikaze akili yangu juu ya kazi ya Yehova maisha yangu yote.

Jambo ya tatu yenye nilijifunza ni kama ni muzuri kufundisha watu mu luga yao ya kizalikio. Wakati nilikomala, nilikuwa nazungumuza Kijerumani, Kiingereza, Papiamento, na Sranantongo (inaitwa pia Sranan). Sranantongo ni luga yenye watu wengi wanazungumuza katika Suriname. Lakini mu maeneo ya mapori, niliona kama watu walisikiliza muzuri zaidi habari njema wakati tuliwahubiria mu luga yao ya kizalikio. Ilikuwa nguvu kwangu kuzungumuza luga fulani, sawa vile Saramaccan, yenye inatumia sauti za kupanda na sauti za kushuka. Lakini, bidii yenye nilifanya haikukuwa ya bure. Kwa miaka mingi, nimeweza kufundisha watu wengi kweli juu niliweza kuzungumuza luga yao ya kizalikio.

Nilikutana na mambo yenye ilinifanya nisikie haya. Kwa mufano, siku moya nilipenda kuuliza mwanafunzi fulani mwenye alikuwa nazungumuza luga ya Saramaccan kama alikuwa najisikia namna gani, juu alikuwa nasikia tumbo inaluma. Kuliko kumuuliza namna alikuwa najisikia, nilimuuliza kama alikuwa na mimba! Hakufurahia ulizo yangu. Hata kama nilifanya makosa ya vile, sikuzote nilijikaza kuzungumuza luga ya kizalikio ya watu ya mu maeneo kwenye nilitumwa.

KUKUBALI MADARAKA ZAIDI

Mu 1970, niliwekwa kuwa mwangalizi wa muzunguko. Ile wakati, nilikuwa naonyesha ndugu na dada wengi wa mu vikundi vya kidogo-kidogo, wenye walikuwa naishi mu maeneo ya mapori, filme yenye kichwa “Kutembelea Makao Makubwa ya Mashahidi wa Yehova.” Juu ya kutembelea wale ndugu na dada, miye na ndugu fulani tulitumia mutumbwi murefu wa mbao ili kusafiri juu ya mito. Tulikuwa nabeba générateur, tanki ya kubeba mafuta ya motere, tala za petroli, na projecteur. Wakati tulifika, tulikuwa nabeba vile vitu vyote na kuvipeleka fasi kwenye tutaonyeshea watu ile filme. Lakini, jambo yenye siyasahawaka ni kuona namna watu mu ile maeneo ya mbali walikuwa napenda ile filme. Nilifurahia sana kusaidia wengine wajifunze juu ya Yehova na juu ya sehemu ya ku dunia ya tengenezo yake. Baraka zenye nilipata zilipita sana mambo yote yenye nilijikaza kufanya mu utumishi wa Yehova.

KUINGIA MU KAMBA YA NYUZI TATU

Ethel na miye tulioana Mwezi wa 9, 1971

Hata ikiwa niliona kama kubakia bila kuoa kulifanya ikuwe mwepesi kwangu kutimiza utumishi wangu, nilijisikia kama iliomba nioe bibi mwenye tutaendelesha naye utumishi wa wakati yote. Kwa hiyo, nilianza kusali juu nipate bibi mwenye angeweza kutumika kwa furaha mu mugao wangu wa nguvu, wa kutumikia mu maeneo ya mapori. Kisha mwaka moya hivi, nilianza kumuchumbia Ethel, painia wa pekee mwenye alikuwa na roho ya kujitoa. Tangu utoto, Ethel alipenda sana mutume Paulo na alipenda kujitoa mu utumishi sawa vile mutume Paulo. Tulioana mu Mwezi wa 9, 1971, na tulianza kutumika mu muzunguko.

Wakati Ethel alikuwa nakomala, familia yake haikukuwaka na vitu mingi vya kimwili. Kwa hiyo, hakukuwa na magumu ya kuzoea kazi ya kusafiri mu maeneo ya mapori. Kwa mufano, wakati tulijitayarisha ili kutembelea makutaniko ya mbali mu maeneo ya mapori, hatukubeba vitu mingi. Tulinawa na kufula nguo mu mito. Tena, tulizoea kukula chakula yoyote yenye walitutayarishia, sawa vile iguanas, piranhas, ao kitu yoyote yenye waliwinda mu pori ao kuvua mu mito. Wakati hatukukuwa na sahani, tulikulia ku majani ya migomba. Wakati hatukukuwa na kanya na vijiko, tulikula na mikono. Ethel na miye tunawaza kama kujitoa pamoya mu kazi ya Yehova kumetusaidia tukuwe kamba ya nyuzi tatu. (Muh. 4:12) Hakuna kitu yenye inaweza kulinganishwa na ile mambo yote yenye tulikutana nayo!

Ni wakati nilikuwa natoka kutembelea kikundi fulani ya mbali mu maeneo ya mapori njo tulikutana na mambo yenye nilieleza ku mwanzo. Wakati mutumbwi wetu uliingia mu maporomoko, ulizama kidogo lakini ulipanda juu haraka. Jambo ya kufurahisha, tulikuwa navala koti za kusaidia mutu asizame na hatukutoka inje ya mutumbwi. Lakini, mutumbwi wetu uliyala maji. Tulitosha vitu vyote vyenye vilikuwa mu vyungu vya kupikia chakula na kuvimwanga mu muto, na kisha tukatumia vile vyungu juu ya kutosha maji mu mutumbwi.

Juu hatukubakia na chakula yoyote, tulianza kuvua samaki wakati tulikuwa naendelea na safari yetu. Lakini, hatukupata samaki yoyote. Kwa hiyo, tulisali kwa Yehova na kumuomba atupatie chakula ya ile siku. Kisha tu kusali, ndugu moya alitupa ndoano mu maji na kukamata samaki mukubwa mwenye siye wote watano tulikula ile usiku na kushiba.

BWANA, BABA, NA MWANGALIZI WA MUZUNGUKO

Kisha miaka tano mu kazi ya muzunguko pamoya, Ethel na miye tulipata baraka yenye hatukutazamia: Kuwa wazazi. Nilifurahi kusikia ile habari, hata kama sikujua namna ingebadilisha maisha yetu. Ethel na miye tulipenda sana kubakia mu utumishi wa wakati yote kama ingewezekana. Mu 1976, mutoto wetu mwanaume, Ethniël, alizaliwa. Mutoto wetu wa pili mwanaume, Giovanni, alizaliwa kisha miaka mbili na nusu.

Kuhuzuria ubatizo mu Muto Tapanahoni karibu na Godo Holo mu Suriname ya Mashariki mu 1983

Juu ya mahitaji mu Suriname ile wakati, biro ya tawi ilifanya mipango juu niendelee kuwa mwangalizi wa muzunguko wakati tulikuwa nakomalisha watoto wetu. Wakati watoto wetu walikuwa wangali wadogo, niliombwa kutembelea mizunguko yenye ilikuwa na makutaniko kidogo. Ile ilikuwa nanisaidia nitumike majuma mbili kila mwezi mu kazi ya muzunguko na kufanya upainia mu sehemu yenye kubakia ya mwezi mu kutaniko kwenye nilitumwa. Ethel na watoto wetu walikuwa nanisindikiza wakati nilitembelea makutaniko ya karibu na kwenye tulikuwa naishi. Lakini, nilisafiri miye peke wakati nilienda kutembelea makutaniko na kusimamia mikusanyiko mu maeneo ya mapori.

Mara mingi, mu kazi ya muzunguko, nilisafiri na mutumbwi juu ya kutembelea makutaniko ya mbali

Nilipaswa kupanga mambo muzuri juu niweze kutimiza madaraka yangu yote. Nilihakikisha kama tunafanya funzo ya familia kila juma. Wakati nilitembelea makutaniko ya mu maeneo ya mapori, Ethel alikuwa naongoza funzo ya familia pamoya na watoto wetu wanaume ku nyumba. Lakini mara mingi, tulifanya mambo pamoya kadiri iliwezekana. Pia, Ethel na miye, tulijifurahisha kwa ukawaida pamoya na watoto wetu wanaume. Wakati fulani, tulicheza michezo ao kuenda kutembelea nafasi zenye kupendeza za karibu na kwetu. Mara mingi, nilikuwa nalala nyuma, juu ya kutayarisha migao. Na Ethel, sawa vile mwanamuke mwenye uwezo, mwenye kuzungumuziwa mu Mezali 31:15, alikuwa nalamuka asubui sana juu tuweze kusoma andiko ya siku na kula chakula ya asubui pamoya mbele watoto wetu wanaume waende ku masomo. Niko mwenye shukrani sana kuwa na bibi mwenye roho ya kujitoa, mwenye sikuzote amenisaidia kutimiza madaraka yote yenye Yehova amenipatia!

Juu tuko wazazi, tunajikaza sana kusaidia watoto wetu wanaume wamupende Yehova na wapende kazi ya kuhubiri. Tulipenda watoto wetu wanaume wachague utumishi wa wakati yote, hapana juu tu siye njo tunapenda wafanye vile, lakini ikuwe uamuzi wao. Sikuzote tulikuwa nawaambia namna utumishi wa wakati yote unaweza kuwasaidia wakuwe na furaha. Bila kusahau magumu, tuliwaonyesha namna Yehova alisaidia na kubariki familia yetu. Tena, tulihakikisha kama watoto wetu wanaume wanafanya urafiki na Mashahidi wenzao, wenye wanatia Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yao.

Yehova alitupatia mambo yote yenye tulikuwa nayo lazima wakati tulikuwa nakomalisha watoto wetu. Sikuzote nilijikaza kufanya yote yenye ninaweza juu ya kutegemeza familia yangu. Mambo yenye nilijionea wakati nilikuwa painia wa pekee mwenye hana bibi mu maeneo ya mapori ilinifundisha kama ni muzuri kuweka makuta yenye itatusaidia kuuza vitu vyenye tutakuwa navyo lazima. Lakini, hata kama tulifanya yote yenye tuliweza, wakati fulani hatukukuwa na kila kitu yenye tulikuwa nayo lazima. Ile wakati, ninaamini kama Yehova alitusaidia. Kwa mufano, ku mwisho wa miaka ya 1980 na ku mwanzo-mwanzo wa miaka ya 1990, kulitokea vita mu Suriname. Ile wakati, ilikuwa nguvu sana kupata hata mahitaji ya musingi. Lakini, Yehova alitusaidia.​—Mt. 6:32.

KUFIKIRIA MAISHA YANGU

Kutoka kushoto mupaka kuume: Miye na bibi yangu, Ethel

Mutoto wetu wa kwanza, Ethniël, na bibi yake, Natalie

Mutoto wetu Giovanni na bibi yake, Christal

Sikuzote, Yehova ametusaidia mu maisha yetu yote, na ametusaidia tukuwe wenye furaha kabisa na wenye kutosheka. Watoto wetu ni baraka kubwa kwetu, na kuwasaidia wamupende Yehova ni pendeleo. Tuko na furaha sana kuona kama wao pia wamechagua kumutumikia Yehova mu utumishi wa wakati yote. Ethniël na Giovanni wamesoma masomo ya kiteokrasi, na kwa sasa wanatumikia ku biro ya tawi ya Suriname pamoya na bibi zao.

Ethel na miye tumezeeka sasa, lakini tunaendelea kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova. Kwa sasa, tuko mapainia wa pekee. Tuko na mambo mingi ya kufanya. Mupaka sasa, siyapataka wakati ya kujifunza kuogelea! Lakini, sihuzunikie jambo fulani. Wakati nafikiria maisha yangu, naweza kabisa kusema kama uamuzi wenye nilikamataka na niko kijana, wa kumutumikia Yehova mu utumishi wa wakati yote, njo uamuzi muzuri zaidi kuliko maamuzi yote yenye nilishakakamata.

b Habari juu ya maisha ya Willem van Seijl, yenye kichwa “Mambo Halisi Yamezidi Mataraja Yangu,” ilitolewa mu Amuka! ya tarehe 8, Mwezi wa 10, 1999.