Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Mordekai aliishi kabisa?

MUYAHUDI mwenye kuitwa Mordekai alitimiza daraka ya maana sana mu mambo yenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Esta. Alikuwa muhamishwa mwenye alikuwa natumika kwenye makao ya mufalme wa Waajemi. Ilikuwa ku mwanzo wa karne ya tano M.K.Y., “katika siku za [Mufalme] Ahasuero.” (Mara mingi ule mufalme anajulikana kwa jina ya Artashasta wa Kwanza.) Mordekai alizuia mupango wa kumuua mufalme. Juu ya kumushukuru, mufalme alifanya mipango ili Mordekai apewe heshima mbele ya watu wote. Kisha kifo ya Hamani, adui wa Mordekai na wa Wayahudi wengine, mufalme alimupandisha Mordekai cheo na kumufanya kuwa waziri mukubwa. Juu alikuwa na mamlaka, Mordekai aliweza kutoa amri yenye ilisaidia Wayahudi wenye walikuwa mu utawala wa Waajemi wasiuawe.​—Est. 1:1; 2:5, 21-23; 8:1, 2; 9:16.

Ku mwanzo-mwanzo wa karne ya 20, wanahistoria fulani walisema kama kitabu ya Esta inazungumuzia mambo ya kuwazia-wazia na kama Mordekai hakuishi. Lakini, mu 1941, watu wenye kuvumbula vitu vya zamani walipata vitu vyenye vinaunga mukono mambo yenye Biblia inasema kuhusu Mordekai. Walipata nini?

Walipata bamba yenye maandishi ya Waajemi yenye ilikuwa na jina ya mwanaume mwenye kuitwa Marduka (mu Kiswahili Mordekai). Alikuwa mufanyakazi wa serikali. Pengine kazi yake ilikuwa kufanya hesabu ya mali ya mufalme katika Shushani. Wakati ile bamba ilivumbuliwa, Arthur Ungnad, mutu mwenye elimu ya historia ya Mashariki, alisema kama “zaidi ya Biblia na ile bamba tu, hakuna kitu ingine yenye ilizungumuzia Mordekai” ile wakati.

Tangu Ungnad aseme vile, watu wenye elimu wametafsiri maandishi yenye kupatikana ku maelfu ya mabamba ingine ya Waajemi. Kati ya ile mabamba, kuko mabamba ya Persépolis yenye ilivumbuliwa mu mabomoko ya Nyumba ya Hazina karibu na kuta za muji. Ile mabamba iliandikwa wakati wa utawala wa Mufalme Artashasta wa Kwanza. Iliandikwa mu luga ya Waelamu, na iko na majina mingi yenye inapatikana mu kitabu ya Esta. a

Namna jina Mordekai (Marduka) inaandikwa ku mabamba yenye maandishi ya Waajemi

Mabamba mbalimbali ya Persépolis inataya jina Marduka, mwenye alikuwa mwandishi kwenye makao ya mufalme katika Shushani wakati ya utawala wa Artashasta wa Kwanza. Bamba moya inasema kama Marduka alikuwa mutafsiri. Ile ina- patana na mambo yenye Biblia inasema juu ya Mordekai. Alikuwa ofisa kwenye makao ya mufalme Ahasuero (Artashasta wa Kwanza) na alikuwa nazungumuza karibu luga mbili. Mara mingi Mor- dekai aliikala ku mulango mukubwa wa makao ya mufalme katika Shushani. (Est. 2:19, 21; 3:3) Mu- lango mukubwa wa makao ya mufalme ulikuwa jengo kubwa kwenye maofisa wa nyumba ya mufalme walikuwa natumikia.

Kuko mambo mingi yenye kufanana kati ya Marduka mwenye ile mabamba inazungumuzia na Mordekai mwenye Biblia inazungumuzia. Waliishi wakati ileile, fasi ileile, walitumikia cheo ileile, na walitumikia fasi ileile. Wakati tunatia ile mambo yote pamoya, tunaona kama mambo yenye wale wenye kuvumbula vitu vya zamani walivumbula inapatana na Mordekai mwenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Esta.

a Mu 1992, Profesere Edwin alitangaza majina kumi yenye alitosha mu Maandishi ya Persépolis yenye inapatikana pia mu kitabu ya Esta.