Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 47

Usiache Jambo Yoyote Ikutenganishe na Yehova

Usiache Jambo Yoyote Ikutenganishe na Yehova

“Ninakutegemea wewe, Ee Yehova.”​—ZB. 31:14.

WIMBO 122 Tukuwe na Nguvu na Tusitikisike!

KIFUPI YA HABARI a

1. Nini njo inaonyesha kama Yehova anapenda tumukaribie?

 YEHOVA anatuomba tumukaribie. (Yak. 4:8) Anapenda kuwa Mungu wetu, Baba yetu na Rafiki yetu. Anajibiaka sala zetu, na anatusaidiaka mu wakati ya magumu. Na anatumiaka tengenezo yake ili kutufundisha na kutulinda. Lakini, tunapaswa kufanya nini juu ya kumukaribia Yehova?

2. Juu ya kumukaribia Yehova, tunapaswa kufanya nini?

2 Juu ya kumukaribia Yehova, tunapaswa kusali kwake, kusoma Neno yake, na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma. Wakati tunafanya vile, tunamupenda zaidi, na tunakuwa wenye shukrani kwake. Tunakuwa na hamu ya kumupatia sifa yenye anastahili kabisa. (Ufu. 4:11) Kadiri tunamujua Yehova, ni vile tunamutumainia na kutumainia tengenezo yenye ametupatia ili kutusaidia.

3. Shetani anafanya nini ili kujaribu kututenganisha na Yehova, lakini nini njo itatusaidia tusimuache Mungu wetu na tengenezo yake? (Zaburi 31:13, 14)

3 Lakini, Shetani anajaribu kututenganisha na Yehova, zaidi sana wakati tunapambana na majaribu. Anatumia mayele gani? Pole kwa pole anajaribu kutufanya tuache kumutumainia Yehova na tengenezo yake. Lakini, tunaweza kumupinga. Kama imani yetu iko nguvu na kama tunamutumainia kabisa Yehova, hatutamuacha na hatutaacha tengenezo yake.​—Soma Zaburi 31:13, 14.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Mu hii habari, tutazungumuzia majaribu tatu yenye inaweza kutoka inje ya kutaniko. Ile majaribu inaweza kufanya tuache kumutumainia Yehova na tengenezo yake. Namna gani ile majaribu tatu inaweza kututenganisha na Yehova? Na tunaweza kufanya mambo gani juu Shetani asitutenganishe na Yehova?

WAKATI TUNAPAMBANA NA MAGUMU

5. Namna gani magumu inaweza kufanya tuache kumutumainia Yehova na tengenezo yake?

5 Wakati fulani, tunapambana na magumu, sawa vile kupingwa na familia ao kupoteza kazi. Namna gani magumu sawa ile inaweza kufanya tuache kutumainia tengenezo ya Yehova na kututenganisha na Yehova? Wakati tunavumilia magumu kwa wakati murefu, tunaweza kupoteza tumaini na kuvunjika moyo. Shetani anatumiaka ile nafasi juu ya kutufanya tuwaze kama Yehova hatupendi. Shetani anapenda tuwaze kama Yehova ao tengenezo yake njo inafanya tuteseke. Jambo ya kufanana na ile ilifikia Waisraeli fulani Misri. Ku mwanzo, waliamini kama Yehova aliweka Musa na Haruni ili kuwakomboa katika utumwa. (Kut. 4:29-31) Kisha Farao kufanya maisha yao ikuwe nguvu, walimulaumu Musa na Haruni juu ya magumu yao, kwa kuwaambia hivi: “Mumefanya Farao na watumishi wake watuzarau na mumeweka upanga katika mikono yao ili watuue.” (Kut. 5:19-21) Walilaumu watumishi washikamanifu wa Yehova. Jambo ya kuhuzunisha kabisa! Kama umevumilia magumu kwa wakati murefu, unaweza kufanya nini juu uendelee kabisa kutumainia Yehova na tengenezo yake?

6. Sawa vile nabii Habakuki, tunaweza kufanya nini juu ya kupambana na magumu? (Habakuki 3:17-19)

6 Umuambie Yehova mambo yote yenye kuwa mu moyo wako, na umuombe akusaidie. Nabii Habakuki alipambana na magumu mingi. Inawezekana wakati fulani aliwaza kama Yehova hamuhangaikie. Kwa hiyo, alimuelezea Yehova namna alikuwa anajisikia. Alisema hivi: “Ee Yehova, nililie musaada mupaka wakati gani, lakini wewe hausikie? . . . Sababu gani unaachilia ukandamizaji?” (Hab. 1:2, 3) Yehova alijibia sala ya kutoka ku moyo ya mutumishi wake mushikamanifu. (Hab. 2:2, 3) Kisha kufikiri sana juu ya namna Yehova aliokoa watu wake, Habakuki alikuwa tena na furaha. Alifikia kuwa hakika kama Yehova alimuhangaikia na kama atamusaidia kuvumilia magumu yoyote. (Soma Habakuki 3:17-19.) Tunajifunza nini? Wakati unapambana na magumu, usali kwa Yehova na umuambie namna unajisikia. Kisha, umuombe Yehova akusaidie. Kama unafanya vile, unaweza kuwa hakika kama Yehova atakupatia nguvu yenye uko nayo lazima ili kuvumilia. Na wakati utaona namna anakusaidia, imani yako itakuwa nguvu zaidi.

7. Mutu wa familia ya Shirley alijaribu kumufanya akuwe na mawazo gani, na nini njo ilimusaidia asiache kumutumainia Yehova?

7 Uheshimie progamu yako ya kiroho. Fikiria namna kufanya vile kulimusaidia Shirley, dada wa Papouasie-Nouvelle-Guinée, wakati alipambana na magumu. b Familia ya Shirley ilikuwa maskini, na wakati fulani ilikuwa nguvu kwao kupata chakula. Mutu fulani wa familia yake alijaribu kumufanya akuwe na mashaka juu ya Yehova. Alimuambia hivi: “Munasemaka kama roho takatifu ya Mungu inawasaidiaka, sasa mbona sione vile inawasaidiaka? Familia yenu ingali tu maskini. Muko napoteza tu wakati mu kuhubiri.” Shirley anasema hivi: “Nilijiuliza: ‘Kweli Mungu anatuhangaikiaka?’ Kwa hiyo, mara moya nilisali kwa Yehova na kumuambia kila kitu yenye ilikuwa mu akili yangu. Sikuacha kusoma Biblia na vichapo vyetu, na niliendelea kuhubiri na kukusanyika.” Kisha wakati kidogo, Shirley alianza kutambua kama Yehova alikuwa nahangaikia familia yake. Familia yake haikulala na njala, na walikuwa na furaha. Shirley anasema hivi: “Nilitambua kama Yehova alikuwa najibia sala zangu.” (1 Ti. 6:6-8) Kama unaendelea kuheshimia programu yako ya kiroho, na weye pia hautaacha magumu ao mashaka ikutenganishe na Yehova.

WAKATI NDUGU WENYE KUWA NA MADARAKA WANATENDEWA MUBAYA

8. Ni mambo gani inaweza kupata ndugu wenye kuwa na madaraka mu tengenezo ya Yehova?

8 Maadui wetu wanatumia vyombo vya habari na site za Enternete za kupashana habari juu ya kueneza habari za uongo kuhusu ndugu wenye kuwa na madaraka mu tengenezo ya Yehova. (Zb. 31:13) Ndugu fulani wamefungwa na kushitakiwa kuwa watu wabaya sana. Wakristo wa kwanza-kwanza walipambana na hali ya vile wakati mutume Paulo alishitakiwa mambo ya uongo na kufungwa. Walitenda namna gani?

9. Wakristo fulani walitenda namna gani wakati Paulo alifungwa?

9 Wakristo fulani wa kwanza-kwanza waliacha kumutegemeza mutume Paulo wakati alifungwa katika Roma. (2 Ti. 1:8, 15) Juu ya nini? Ni juu walimusikilia Paulo haya sababu watu walimuona kuwa mutu mubaya sana? (2 Ti. 2:8, 9) Ao waliogopa kama wao pia watateswa? Ikuwe sababu ilikuwa nini, wazia namna Paulo alijisikia. Alikuwa amevumilia magumu mingi na hata alihatarisha maisha yake kwa ajili yao. (Mdo. 20:18-21; 2 Ko. 1:8) Tusikuwe hata kidogo sawa wale wenye walimuacha Paulo mu wakati yenye alikuwa na lazima yao! Tunapaswa kukumbuka nini wakati ndugu wenye kuwa na madaraka wanateswa?

10. Tunapaswa kukumbuka nini wakati ndugu wenye kuwa na madaraka wanateswa?

10 Ukumbuke juu ya nini tunateswa na nani njo anafanya tuteswe. 2 Timoteo 3:12 inasema hivi: “Wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.” Kwa hiyo, hatupaswe kushangala wakati Shetani anashambulia ndugu wenye kuwa na madaraka. Kusudi yake ni kutuogopesha na kufanya wale ndugu waache kuwa washikamanifu kwa Yehova.​—1 Pe. 5:8.

Hata kama Paulo alikuwa mu kifungo, Onesiforo hakuogopa kumutegemeza. Sawa vile hii picha inaonyesha, leo ndugu na dada zetu wanategemeza waamini wenzao wenye wamefungwa (Ona fungu ya 11-12)

11. Mufano wa Onesiforo unatufundisha nini? (2 Timoteo 1:16-18)

11 Uendelee kutegemeza ndugu zako na ushikamane nao. (Soma 2 Timoteo 1:16-18.) Mukristo wa karne ya kwanza mwenye kuitwa Onesiforo alitenda tofauti wakati Paulo alifungwa. “Hakusikia haya juu ya minyororo [ya Paulo] ya gereza.” Lakini, Onesiforo alimutafuta Paulo, na wakati alimupata, alifanya mambo fulani juu ya kumusaidia. Kwa kufanya vile, Onesiforo alitia maisha yake mu hatari. Tunajifunza nini? Hatupaswe kuacha woga wa mwanadamu utuogopeshe ao kutuzuia tusitegemeze ndugu zetu wenye wako wanateswa. Lakini, tunapaswa kuwatetea na kuwasaidia. (Mez. 17:17) Wako na lazima ya upendo na musaada wetu.

12. Mufano wa ndugu na dada zetu wa Urusi unatufundisha nini?

12 Fikiria namna ndugu na dada zetu wa Urusi wamefikia kusaidia waamini wenzao wenye wamefungwa. Wakati ndugu na dada fulani wanasambishwa ku tribinali, ndugu na dada wengi wanakuya kuwategemeza. Tunajifunza nini? Hatupaswe kuogopa wakati ndugu wenye kuwa na madaraka wanasemewa uongo, wanafungwa, ao kuteswa. Tunapaswa kusali kwa ajili yao, kuhangaikia watu wa familia zao, na kuona ni mu njia gani ingine tunaweza kuwasaidia.​—Mdo. 12:5; 2 Ko. 1:10, 11.

WAKATI WATU WANATUCHEKA

13. Namna gani kuchekwa kunaweza kufanya tuache kumutumainia Yehova na tengenezo yake?

13 Watu wa familia, wafanyakazi wenzetu, ao wanafunzi wenzetu wenye hawako Mashahidi wanaweza kutucheka juu tunahubiri ao juu tunaishi kulingana na kanuni za juu za Yehova. (1 Pe. 4:4) Wanaweza kusema hivi: “Nafurahiaka vile unakuwaka, lakini ile dini yako inakuwaka na sheria-sheria mingi, na iko tu na mambo ya zamani.” Watu fulani wanaweza kuchambua namna tunatendea watengwa, kwa kusema hivi: “Munaweza kusema kabisa kama munapendaka watu?” Maneno ya vile inaweza kupanda mbegu za mashaka mu akili yetu. Tunaweza kuanza kuwaza kama ‘sheria ya Yehova inapitisha mipaka na kama tengenezo yake inatufungafunga.’ Kama unajikuta mu hali ya vile, unaweza kufanya nini juu ubakie karibu na Yehova na tengenezo yake?

JYobu alikatala kuamini mawazo ya uongo yenye wale wenye walijifanya kuwa marafiki wake walisema ili kumucheka. Lakini, aliazimia kuendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu kwa Yehova (Ona fungu ya 14)

14. Unapaswa kutenda namna gani wakati watu wanakucheka juu unaishi kulingana na kanuni za Yehova? (Zaburi 119:50-52)

14 Uazimie kuishi kulingana na kanuni za Yehova. Yobu alikuwa mwanaume mwenye aliishi kulingana na kanuni za Yehova hata kama watu walimucheka kwa kufanya vile. Mumoja kati ya wanaume wenye walijifanya kuwa marafiki wa Yobu alijaribu hata kumusadikisha Yobu kama, ikuwe anaishi kulingana na kanuni za Mungu ao hapana, Mungu hahangaikie ile. (Yob. 4:17, 18; 22:3) Lakini, Yobu alikatala kuamini ile mambo ya uongo. Alijua kama kanuni za Yehova za mema na mabaya ziko sawa, na aliazimia kushikamana nazo. Hakuruhusu wengine wamufanye aache kuwa muaminifu-mushikamanifu kwa Yehova. (Yob. 27:5, 6) Tunajifunza nini? Usiache kuchekwa ifanye uanze kuwa na mashaka na kanuni za Yehova. Fikiria mambo yenye ilikupata mu maisha. Bila shaka, mara mingi umejionea mu maisha yako namna kanuni za Yehova ziko sawa na namna zinakuletea faida. Uazimie kubakia mu tengenezo ya Yehova yenye inategemeza zile kanuni. Kama unafanya vile, hata watu wakucheke namna gani, ile haitakutenganisha na Yehova.​—Soma Zaburi 119:50-52.

15. Juu ya nini watu wa familia ya Brizit walimucheka?

15 Fikiria mambo yenye ilimupata Brizit, dada mwenye kuishi India. Watu wa familia yake walimucheka juu ya imani yake. Wakati kidogo kisha yeye kubatizwa mu 1997, bwana yake, mwenye haiko Shahidi, alipoteza kazi yake. Kwa hiyo, aliamua kama yeye, Brizit, na watoto wao wanamuke wanapaswa kuenda kuishi kwa wazazi wake, mu muji mwingine. Lakini, Brizit angepata magumu mingi zaidi. Juu bwana yake hakukuwa na kazi, Brizit alipaswa kutumika wakati mingi juu ya kutegemeza familia yake. Zaidi ya ile, kutaniko ya karibu ilikuwa ku kilometre 350 hivi. Jambo ya kuhuzunisha, familia ya bwana yake ilimupinga juu ya imani yake. Hali ilikuwa mubaya sana, mupaka familia ya Brizit ikalazimika kuhama tena. Kisha bila kutazamia, bwana yake alikufa. Kisha, mutoto wake mumoja mwanamuke akakufa na kansere. Alikuwa tu na miaka 12. Na sawa vile ile magumu yote haikutosha, hata watu wa familia ya Brizit walisema kama yeye njo alituma ile magumu yote imupate. Walisema kama ikiwa hangekuwa Shahidi wa Yehova, ile magumu yote haingemupata. Lakini, aliendelea kumutumainia Yehova na kubakia karibu na tengenezo yake.

16. Brizit alibarikiwa namna gani juu alishikamana na Yehova na tengenezo yake?

16 Juu Brizit aliishi mbali na kutaniko, mwangalizi wa muzunguko alimutia moyo ahubiri mu eneo kwenye aliishi na aongoze mikutano kwake. Ku mwanzo, aliona kama ile ni nguvu sana. Lakini, alitii mambo yenye mwangalizi alimuambia. Alihubiria wengine habari njema, alifanya mikutano kwake, na alipanga wakati juu ya kufanya ibada ya familia pamoya na watoto wake wanamuke. Ile ilikuwa na matokeo gani? Brizit alianza kuongoza mafunzo mingi ya Biblia, na wengi kati ya wanafunzi wake walibatizwa. Mu 2005, alianza kazi ya upainia wa kawaida. Alibarikiwa juu alimutumainia Yehova na juu ya ushikamanifu wake kwa tengenezo ya Yehova. Watoto wake wanamuke wanamutumikia Yehova kwa uaminifu, na mu ile eneo, muko kwa sasa makutaniko mbili! Brizit iko hakika kama Yehova alimupatia nguvu ya kupambana na magumu yake na kuvumilia wakati watu wa familia yake walimucheka.

UBAKIE MUSHIKAMANIFU KWA YEHOVA NA TENGENEZO YAKE

17. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

17 Shetani anapenda tuamini kama Yehova atatuacha mu wakati ya magumu na kama kutegemeza tengenezo ya Yehova kunafanyaka tu maisha yetu ikuwe nguvu zaidi. Shetani anapenda tuogope wakati ndugu wenye kuwa na madaraka wanasemewa uongo, wanateswa, ao kufungwa. Na anachochea watu watucheke juu tuache kutumainia kanuni za Yehova na tengenezo yake. Lakini, tunajua muzuri kabisa njia zake za mubaya na hatuache atudanganye. (2 Ko. 2:11) Tuazimie basi kupinga uongo wa Shetani, na tubakie washikamanifu kwa Yehova na tengenezo yake. Tusisahau kama Yehova hatatuacha hata kidogo. (Zb. 28:7) Kwa hiyo, usiache jambo yoyote ikutenganishe na Yehova!​—Ro. 8:35-39.

18. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

18 Mu hii habari, tumezungumuzia majaribu yenye inaweza kutoka inje ya kutaniko. Lakini kuko pia majaribu yenye inaweza kutoka ndani ya kutaniko na kufanya tusimutumainie Yehova na tengenezo yake. Tunaweza kufanya nini juu ya kupambana na ile majaribu? Tutazungumuzia ile mu habari yenye kufuata.

WIMBO 118 ‘Unipatie Imani Zaidi’

a Juu ya kuvumilia kwa uaminifu mu hizi siku za mwisho, tunapaswa kuendelea kutumainia Yehova na tengenezo yake. Shetani anatumia majaribu juu ya kufanya tusimutumainie Yehova na tengenezo yake. Mu hii habari, tutazungumuzia majaribu tatu yenye Shetani anatumia na mambo yenye tunaweza kufanya juu tuendelee kuwa waaminifu kwa Yehova na tengenezo yake.

b Majina fulani imebadilishwa.