Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 51

Inawezekana Kuwa na Amani Hata Wakati ya Magumu

Inawezekana Kuwa na Amani Hata Wakati ya Magumu

“Mioyo yenu isivurugike wala kuregea kwa woga.”​—YOH. 14:27.

WIMBO 112 Yehova Ni Mungu wa Amani

KIFUPI YA HABARI a

1. “Amani ya Mungu” njo nini, na kuwa na ile amani kuko na faida gani? (Wafilipi 4:6, 7)

 KUKO aina fulani ya amani yenye watu wa mu hii dunia hawajue. Ni “amani ya Mungu,” ni kusema, utulivu wenye mutu anakuwaka nao juu iko na urafiki muzuri pamoya na Baba yetu wa mbinguni. Kuwa na amani ya Mungu kunafanya tujisikie salama. (Soma Wafilipi 4:6, 7.) Kunafanya pia tukuwe na urafiki wa karibu na wale wenye wanamupenda Mungu. Na tena, kunafanya tufurahie urafiki muzuri pamoya na “Mungu wa amani.” (1 Te. 5:23) Kama tunamujua Baba yetu, tunamutumania, na kumutii, amani ya Mungu inaweza kufanya tutulie wakati ya magumu.

2. Juu ya nini tuko hakika kama inawezekana kuwa na amani ya Mungu?

2 Inawezekana kabisa kuwa na amani ya Mungu wakati tuko napambana na magumu sawa vile magonjwa yenye kuenea sana, misiba, muvurugo mu eneo yetu, ao wakati tunateswa juu ya imani yetu? Ile mambo yote inaweza kutuogopesha. Lakini, Yesu alishauria hivi wanafunzi wake: “Mioyo yenu isivurugike wala kuregea kwa woga.” (Yoh. 14:27) Inatia moyo kuona kama ndugu na dada wamefuata shauri ya Yesu. Kwa musaada wa Yehova, wameendelea kuwa na amani hata wakati wanapambana na magumu ya nguvu.

MAMBO YA KUFANYA JUU TUKUWE NA AMANI WAKATI KUNATOKEA MAGONJWA FULANI

3. Namna gani ugonjwa wa kuambukiza unaweza kuvuruga amani yetu?

3 Ugonjwa wa kuambukiza unaweza kubadilisha karibu kila kitu mu maisha yetu. Kwa mufano, fikiria matokeo ya ugonjwa wa Coronavirus. Uchunguzi fulani ulionyesha kama ule ugonjwa ulifanya watu wengi wakuwe nakosa usingizi, wakuwe na mahangaiko, washuke moyo, wakunywe pombe kupita kiasi, watumie dawa za kulewesha, bibi na bwana waanze kupigana, na wengine watafute kujiua. Kama kunatokea magonjwa fasi kwenye unaishi, unaweza kufanya nini juu usihangaike sana lakini ukuwe na amani ya Mungu?

4. Juu ya nini kujua mambo yenye Yesu alisema kuhusu siku za mwisho kunafanya tukuwe na amani?

4 Yesu alisema kama mu siku za mwisho kutakuwa magonjwa ya kuambukiza, ao magonjwa yenye kuenea sana, “mahali pamoja kisha pengine.” (Lu. 21:11) Juu ya nini kujua vile kunafanya tukuwe na amani? Juu hatushangale wakati kunatokea magonjwa fulani. Tunaona kama ile mambo yote iko natokea sawa tu vile Yesu alisema. Kwa hiyo, tunapaswa kufuata hii shauri yenye Yesu alipatiaka wale wenye kuishi mu siku za mwisho: “Mufanye angalisho kwamba musiogope.”​—Mt. 24:6.

Kusikiliza usomaji wa Biblia wenye kurekodiwa kunaweza kukusaidia ukuwe na amani ya akili wakati kunatokea magonjwa fulani (Ona fungu ya 5)

5. (a) Kulingana na Wafilipi 4:8, 9, tunapaswa kumuomba Yehova nini wakati kunatokea magonjwa fulani? (b) Kuko faida gani kusikiliza usomaji wa Biblia wenye kurekodiwa?

5 Kama magonjwa fulani inatokea, ni mwepesi kuhangaika na hata kuogopa. Ile njo ilimufikia dada mwenye kuitwa Desi. b Wakati mujomba wake, mutoto mukubwa wa mukubwa yake na baba yake, na munganga wake walikufa na Coronavirus, aliogopa kama naye angepata ile virus na kisha angeambukiza mama yake mwenye alikuwa alishazeeka. Aliogopa pia kama angepoteza kazi yake. Kwa hiyo, alijiuliza kama atapata namna gani makuta ya chakula na ya kulipia nyumba. Ile mambo ilianza kumuhangaisha sana mupaka akaanza kukosa usingizi. Lakini, Desi alipata tena amani. Alifanya nini juu akuwe na amani? Alimuambia Yehova waziwazi kama amusaidie atulie na akuwe na mawazo yenye kufaa. (Soma Wafilipi 4:8, 9.) Alimusikiliza Yehova “anasema” naye kwa kusikiliza usomaji wa Biblia wenye kurekodiwa. Anasema hivi: “Sauti zenye kutulia za wasomaji zilinisaidia nitulie na zilinikumbusha kama Yehova ananihangaikia.”​—Zb. 94:19.

6. Funzo ya pekee na mikutano iko na faida gani?

6 Ni kweli magonjwa inaweza kuvuruga mambo fulani yenye ulizoea kufanya. Lakini, usiache ile ikuzuie kufanya funzo ya pekee ao kuhuzuria mikutano. Habari juu ya maisha ya watu zenye kupatikana mu vichapo vyetu na mu video zitakukumbusha kama ndugu na dada zako wako naendelea kuwa waaminifu kwa Yehova hata kama wako napambana na magumu ya vile. (1 Pe. 5:9) Mikutano itakusaidia ufikirie mambo yenye kutia moyo yenye kuwa mu Biblia. Itakupatia pia nafasi ya kutia wengine moyo na kutiwa moyo. (Ro. 1:11, 12) Wakati unafikiria namna Yehova alisaidia watumishi wake wakati walikuwa wagonjwa, wakati waliogopa, ao kujisikia kuwa peke yao, imani yako itakuwa nguvu, na utakuwa hakika kama na weye atakusaidia.

7. Habari ya mutume Yohana inatufundisha nini?

7 Ujikaze kuzungumuza na ndugu na dada zako. Magonjwa ya kuambukiza inaweza kufanya tusikaribiane sana hata wakati tuko pamoya na ndugu na dada zetu. Mu hali ya vile, unaweza kujisikia sawa vile mutume Yohana alijisikia. Alipenda kumuona rafiki yake Gayo uso kwa uso. (3 Yo. 13, 14) Lakini, Yohana alitambua kama haigewezekana kumuona Gayo kwa wakati fulani. Kwa hiyo, Yohana alifanya jambo yenye aliweza. Alimuandikia Gayo barua. Kama haiwezekane kuonana na ndugu na dada zako uso kwa uso, upime kuwaita ku telefone, uwaite kwa njia ya vidéoconférence, ao uwaandikie ujumbe. Kama unaendelea kuzungumuza na ndugu na dada zako, utajisikia salama zaidi, na utakuwa na amani. Uzungumuze na wazee wa kutaniko yako wakati uko na mahangaiko, na usikilize maneno yao ya kutia moyo.​—Isa. 32:1, 2.

MAMBO YA KUFANYA JUU TUKUWE NA AMANI WAKATI KUNATOKEA MUSIBA

8. Namna gani musiba unaweza kuvuruga amani yako?

8 Kisha mvua kubwa, tetemeko ya inchi, ao moto kutokea mu eneo yenu, unaweza kubakia na mahangaiko kwa wakati murefu. Kama ulifiwa na wapendwa wako, ao vitu vyako viliharibiwa, unaweza kuwa na huzuni, kukosa tumaini, ao hata kukasirika. Ile haimaanishe kama unapenda sana vitu vya kimwili ao unakosa imani. Ile ni magumu yenye ilikufikia, na wengine wanaweza kutazamia utende vile. (Yob. 1:11) Ijapokuwa ile magumu yote, unaweza kuwa na amani. Namna gani?

9. Yesu alisemaka nini juu ya kututayarisha kuhusiana na misiba?

9 Kumbuka mambo yenye Yesu alisemaka. Watu fulani wanawazaka kama hawatafikiwaka na misiba, lakini siye tunajua kama misiba itaongezeka mu siku zetu. Na misiba fulani kati ya ile inaweza kutufikia. Yesu aliambia wanafunzi wake kama “matetemeko makubwa ya inchi” na misiba ingine itatokea mbele mwisho ufike. (Lu. 21:11) Alisema tena kama kutakuwa “kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria.” Njo mambo yenye tuko naona leo. Kwa mufano, tuko naona matendo ya mubaya, jeuri, na mashambulizi ya wateroriste. (Mt. 24:12) Yesu hakusemaka kama ile magumu itafikia tu wale wenye Yehova ameacha. Kusema kweli, watumishi wengi waaminifu wa Yehova wamefikiwa na misiba mbalimbali. (Isa. 57:1; 2 Ko. 11:25) Yehova hatulinde kimuujiza na misiba yote, lakini atatupatia mambo yote yenye tuko nayo lazima juu tuendelee kutulia na kuwa na amani.

10. Juu ya nini kujitayarisha mbele musiba utokee kunaonyesha kama tunamutumainia Yehova? (Mezali 22:3)

10 Kama tulijitayarisha mbele ya wakati, inaweza kuwa mwepesi kuendelea kutulia wakati kunatokea hali yenye inaomba kutenda kwa haraka. Lakini, kama tunajitayarisha, ni kusema, hatumutumainie Yehova? Hapana. Kwa kweli, kujitayarisha mbele musiba utokee kunaonyesha kama tunaamini kuwa Yehova iko na uwezo wa kutusaidia. Juu ya nini tunasema vile? Juu Neno ya Mungu inatushauria tukuwe najitayarisha kwa ajili ya misiba yenye inaweza kutokea. (Soma Mezali 22:3.) Na kupitia habari zenye kuwa mu magazeti, na kupitia mikutano na matangazo, tengenezo ya Yehova imetutia moyo tena na tena tujitayarishe kwa ajili ya hali yenye inaomba kutenda haraka. c Tunamutumainia Yehova? Kama ni vile, tutafuata ile shauri sasa, ni kusema, mbele musiba utokee.

Kujitayarisha mbele ya wakati kunaweza kukusaidia uokoke wakati kunatokea musiba fulani (Ona fungu ya 11) d

11. Mufano wa Margaret unatufundisha nini?

11 Fikiria mambo yenye ilimufikia dada mwenye kuitwa Margaret. Wakubwa wa serikali walimuomba atoke haraka mu nyumba yake juu kulitokea moto mu eneo yake. Juu watu wengi sana walikuwa wanakimbia, kulikuwa magari mingi sana mu barabara na ilikuwa nguvu sana kupata fasi ya kupita. Kulikuwa moshi sana. Kwa hiyo, Margaret hakuweza kutoka mu gari yake kwa wakati fulani. Lakini, aliokoka juu alijitayarishaka. Mu sakoshe yake mulikuwa karte yenye alikuwa naangalia juu apate barabara ya kufuata ili kutoka mu ile eneo. Na hata mbele moto utokee, alipitaka mu ile barabara juu ajue njia yenye inaomba kufuata kama kunatokea hali yenye inaomba kutenda haraka. Matayarisho yenye Margaret alifanya ilimusaidia aokoke.

12. Juu ya nini ni muzuri kufuata maagizo yenye tunapewa?

12 Juu ya kutulinda, wenye mamlaka wanaweza kutuwekea saa yenye hatupaswe kutoka ku nyumba, wanaweza kutuomba tutoke haraka mu nyumba yetu, ao kutupatia maagizo ingine. Watu fulani hawatii mara moya maagizo yenye wanapewa, ao wanachelewesha mambo juu hawapendi mara moya kutoka ku nyumba na kuacha vitu vyao. Wakristo wanapaswa kutenda namna gani? Biblia inatuambia hivi: “Kwa ajili ya Bwana, mujitiishe kwa kila kitu chenye kilifanywa na mwanadamu, ikuwe ni kwa mufalme akiwa mukubwa, ao kwa magavana wakiwa wametumwa naye.” (1 Pe. 2:13, 14) Pia tengenezo ya Yehova inatupatia maagizo ya kutusaidia tukuwe salama. Tumekumbushwa mara na mara kama tunapaswa kupatia wazee namba yetu ya sasa ya telefone juu waweze kutuita kama kunatokea hali yenye inaomba kutenda haraka. Ulishafanya vile? Tengenezo inaweza pia kutuambia fasi ya kukimbilia, inaweza kutuambia tutoke haraka mu eneo fulani, na inaweza kutuambia namna ya kupata misaada ao namna ya kusaidia wengine na wakati gani tunaweza kufanya vile. Kama hatutii, tunaweza kutia uzima wetu na uzima wa wazee mu hatari. Usisahau kama wale wanaume waaminifu wako pale juu ya kutulinda. (Ebr. 13:17) Margaret alisema hivi: “Ninaamini kabisa kama kufuata maagizo ya wazee na ya tengenezo kuliokoa uzima wangu.”

13. Nini njo imesaidia Wakristo wengi wenye wameacha nyumba zao wakuwe na furaha na amani?

13 Ndugu na dada wengi wenye walilazimika kutoka ku nyumba zao juu ya musiba, vita, ao muvurugo mu eneo yao, wamefanya yao yote ili kujipatanisha na hali yao ya mupya na kuendelea na mambo ya kiroho bila kukawia. Sawa vile Wakristo wa kwanza-kwanza wenye walitawanyika kwa sababu waliteswa juu ya imani yao, wanaendelea ‘kutangaza habari njema ya lile neno.’ (Mdo. 8:4) Kuhubiri kunawasaidia wakaze akili juu ya Ufalme kuliko kukaza akili juu ya magumu yao. Ile imefanya waendelee kuwa na furaha na amani.

MAMBO YA KUFANYA JUU TUKUWE NA AMANI WAKATI TUNATESWA JUU YA IMANI YETU

14. Namna gani mateso inaweza kuvuruga amani yetu?

14 Wakati tunateswa juu ya imani yetu, tunaweza kupoteza mambo mingi yenye inatusaidiaka tukuwe na amani. Tunafurahiaka kukutana pamoya bila vizuizi, kuhubiri kwa uhuru, na kufanya mambo yetu bila kuogopa kama tunaweza kufungwa. Kama hatuna uhuru wa kufanya vile, tunaweza kuhangaika na tunaweza kujiuliza kama ni nini itatokea kisha. Ni kawaida kujisikia vile. Lakini, tunapaswa kuwa waangalifu. Yesu alionyesha kama mateso inaweza kufanya wanafunzi wake wakwazike. (Yoh. 16:1, 2) Kwa hiyo, tunaweza kufanya nini juu tuendelee kuwa na amani wakati tunateswa juu ya imani yetu?

15. Juu ya nini hatupaswe kuogopa mateso? (Yoh. 15:20; 16:33)

15 Neno ya Mungu inatuambia hivi: “Wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.” (2 Ti. 3:12) Kisha kazi yetu kukatazwa mu inchi yake, ilikuwa nguvu kwa ndugu mwenye kuitwa Andrei kuamini kama watumishi wote wa Yehova wangeteswa. Aliwaza hivi: ‘Mu inchi yetu muko Mashahidi wengi sana. Wenye mamlaka wanaweza kabisa kutufunga siye wote?’ Ile mawazo haikumufanya Andrei akuwe na amani, lakini aliendelea tu kuhangaika. Ndugu wengine waliacha ile mambo mu mikono ya Yehova, na hawakuwaza kama wao hawawezi kufungwa. Walijua kama wanaweza kufungwa, lakini hawakuhangaika sana sawa vile Andrei. Kwa hiyo, aliamua kuwa na mawazo sawa ile ya Mashahidi wenzake na alimutumainia Yehova. Kisha tu kufanya vile, akakuwa na amani. Na sasa iko na furaha ijapokuwa magumu mingi. Ile inaweza pia kutufikia. Yesu alituambia kama tutateswa, lakini pia alituhakikishia kama tunaweza kuendelea kuwa waaminifu.​—Soma Yohana 15:20; 16:33.

16. Ni wanani njo wanaweza kututolea maagizo wakati kazi yetu inakatazwa ao kutiliwa vizuizi?

16 Wakati kazi yetu inakatazwa ao kutiliwa vizuizi, ndugu wa biro ya tawi na wazee wanaweza kututolea maagizo. Kusudi ya ile maagizo ni kutulinda, kutuonyesha namna tunaweza kuendelea kupata chakula ya kiroho, na kutusaidia tuendelee kuhubiri kadiri inawezekana. Ufanye yako yote ili kutii maagizo yenye unapewa, hata kama hauelewe kabisa juu ya nini ilitolewa. (Yak. 3:17) Tena, usiambie hata kidogo wale wenye hawastahili kujua habari kuhusu ndugu na dada zetu ao kuhusu mambo ya kutaniko.​—Muh. 3:7.

Ni mambo gani itakusaidia ukuwe na amani hata mu wakati ya magumu? (Ona fungu ya 17) e

17. Sawa vile mitume mu karne ya kwanza, tumeazimia kufanya nini?

17 Sababu moya kubwa yenye inafanya Shetani apiganishe watu wa Mungu ni juu “wako na kazi ya kutoa ushahidi juu ya Yesu.” (Ufu. 12:17) Usiache Shetani na dunia yake ikuogopeshe. Kuhubiri na kufundisha ijapokuwa upinzani kunatuletea furaha na amani. Mu karne ya kwanza wakati Wayahudi wenye mamlaka waliamuru mitume waaminifu waache kuhubiri, mitume walichagua kumutii Mungu. Waliendelea kuhubiri, na ile kazi iliwaletea furaha. (Mdo. 5:27-29, 41, 42) Kwa kweli, wakati kazi yetu inatiliwa vizuizi, tunapaswa kuwa waangalifu wakati tunahubiri. (Mt. 10:16) Lakini, kama tunafanya yetu yote, tutakuwa na amani juu tunamufurahisha Yehova na juu tunaambia wengine ujumbe wenye kuokoa uzima.

“MUNGU WA AMANI ATAKUWA PAMOJA NA NINYI”

18. Ni nani tu njo anaweza kutupatia amani ya kweli?

18 Ukuwe hakika kama hata wakati ya magumu ya nguvu sana, tunaweza kuwa na amani. Mu ile wakati, tunapaswa kukumbuka kama amani yenye tuko nayo lazima ni amani ya Mungu, ni kusema, amani yenye Yehova tu njo anaweza kutupatia. Umutegemee wakati kunatokea magonjwa fulani, wakati ya musiba, ao wakati unateswa juu ya imani yako. Ushikamane kabisa na tengenezo ya Yehova. Fikiria baraka zenye zinakuchunga. Kama unafanya vile, ‘Mungu wa amani atakuwa pamoja na weye.’ (Flp. 4:9) Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna tunaweza kusaidia Wakristo wenzetu wenye wanapambana na magumu wakuwe na amani ya Mungu.

WIMBO 38 Atakupatia Nguvu

a Yehova anaahidi kupatia amani wale wenye wanamupenda. Amani yenye Mungu anatupatia njo nini, na tunaweza kufanya nini juu tuipate? Kuwa na “amani ya Mungu” kutatusaidia namna gani wakati magonjwa inatokea mu eneo yetu, wakati tunapambana na misiba, ao wakati tunateswa juu ya imani yetu? Hii habari itajibia ile maulizo.

b Majina fulani imebadilishwa.

d MAFASIRIO YA PICHA: Dada mwenye alijitayarisha mbele ya wakati, iko natoka haraka ku nyumba yake.

e MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mwenye anaishi fasi kwenye kazi yetu imetiliwa vizuizi anaendelea kuwa muangalifu wakati iko nahubiri.