Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakati Daudi aliandika kama atasifu jina ya Mungu “milele,” mu Zaburi 61:8, alimaanisha kama hangekufa?

Hapana. Mambo yenye Daudi aliandika ilikuwa ya kweli.

Fikiria mambo yenye Daudi aliandika mu ile andiko na mu maandiko ingine yenye kufanana na ile: “Nitaimbia jina lako sifa milele, wakati nitakuwa ninatimiza naziri zangu siku kwa siku.” “Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote, na nitatukuza jina lako milele.” “Nitasifu jina lako milele na milele.”​—Zb. 61:8; 86:12; 145:1, 2.

Wakati Daudi aliandika ile maneno, hakuwaza kama hatakufaka. Daudi alijua kama Yehova alisema kuwa wanadamu wangekufa juu ya zambi. Tena, Daudi alikubali kama alikuwa mutenda-zambi. (Mwa. 3:3, 17-19; Zb. 51:4, 5) Alijua pia kama hata wanaume wenye kukubaliwa na Mungu, sawa vile Abrahamu, Isaka, na Yakobo, walikufaka. Na alijua kama hata yeye maisha yake itafikia mwisho. (Zb. 37:25; 39:4) Lakini, maneno yake yenye kuwa mu Zaburi 61:8 inaonyesha kama alikuwa na tamaa na azimio ya kumusifu Mungu milele, ni kusema, wakati yote yenye angekuwa muzima.​—2 Sa. 7:12.

Wakati fulani Daudi aliandika kuhusu mambo yenye ilimufikia mu maisha, sawa vile maneno ya utangulizi ya Zaburi 18, 51, na 52 inaonyesha. Mu Zaburi ya 23, Daudi alionyesha kama Yehova ni muchungaji mwenye kutoa muongozo, kitulizo, na ulinzi. Daudi naye alikuwa muchungaji wa vile. Na alipenda kumutumikia Mungu ‘sikuzote za maisha yake.’​—Zb. 23:6.

Ukumbuke pia kama ni Yehova njo alimuongoza Daudi aandike ile maneno. Mambo yenye aliandika ilikuwa pia na maunabii kuhusu mambo yenye ingetokea kisha. Kwa mufano, mu Zaburi ya 110, Daudi aliandika kuhusu wakati yenye Bwana wake ‘angekaa kwenye mukono wa kuume [wa Mungu]’ mbinguni na kupokea mamlaka makubwa. Mamlaka ya kufanya nini? Ya kutiisha maadui wa Mungu na ‘kuleta hukumu juu ya mataifa’ ku dunia. Na Daudi alikuwa babu wa Yesu, mwenye alikuwa Masiya, na ule Masiya angetawala na iko mbinguni, na angekuwa “kuhani milele.” (Zb. 110:1-6) Yesu alionyesha kama unabii wenye kuwa mu Zaburi ya 110 ulimuhusu na kama ungetimia mu wakati yenye kuya.​—Mt. 22:41-45.

Daudi aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika kuhusu wakati yake na kuhusu wakati yenye kuya yenye angefufuliwa na kufurahia kumusifu Yehova milele. Ile inatusaidia kuelewa kama Zaburi ya 37:10, 11, 29 inahusu wakati yenye Daudi aliiandika na pia wakati yenye kuya. Ile maandiko ilitimia zamani mu inchi ya Israeli na itatimia wakati Mungu atatimiza ahadi zake.​—Ona fungu ya 8 mu habari “Utakuwa Pamoja na Mimi Katika Paradiso” mu hii gazeti.

Zaburi 61:8 na maandiko yenye kufanana na ile inaonyesha kama Daudi alipenda kumusifu Yehova mu Israeli ya zamani mupaka kifo yake. Na inaonyesha pia mambo yenye Daudi atafanya wakati Yehova atamufufua.