Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 50

“Utakuwa Pamoja na Mimi Katika Paradiso”

“Utakuwa Pamoja na Mimi Katika Paradiso”

“Kwa kweli ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.”​—LU. 23:43.

WIMBO 145 Mungu Anatoa Ahadi ya Paradiso

KIFUPI YA HABARI a

1. Mbele Yesu akufe, alimuambia nini mutenda-mabaya mwenye alikuwa pembeni yake? (Luka 23:39-43)

 YESU na watenda-mabaya wawili wenye walikuwa pembeni yake waliteseka sana wakati walikaribia kufa. (Lu. 23:32, 33) Wale watenda-mabaya wote walikuwa nasema mambo ya mubaya juu ya Yesu. Ile inaonyesha waziwazi kama hawakukuwa wanafunzi wake. (Mt. 27:44; Mk. 15:32) Lakini, mumoja alibadilisha mawazo yake. Alisema hivi: “Yesu, unikumbuke wakati utaingia katika Ufalme wako.” Yesu alimuambia hivi: “Kwa kweli ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.” (Soma Luka 23:39-43.) Hakuna kitu yenye inaonyesha kama ule mutenda-mabaya alikubali habari ya “Ufalme wa mbinguni,” wenye Yesu alihubiri wakati alikuwa ku dunia. Na hata Yesu hakusema kama ule mutenda-mabaya ataingia mu Ufalme. (Mt. 4:17) Yesu alikuwa nazungumuzia Paradiso yenye itakuwa ku dunia wakati yenye kuya. Juu ya nini tunasema vile?

Maneno yenye ule mutenda-mabaya alisema inaonyesha nini? (Ona fungu ya 2-3)

2. Nini njo inaonyesha kama ule mutenda-mabaya mwenye alitubu alikuwa Muyahudi?

2 Inawezekana ule mutenda-mabaya mwenye alitubu alikuwa Muyahudi. Aliambia mwenzake hivi: “Je, wewe haumuogope Mungu hata kidogo, kwa kuwa sasa umepata hukumu ileile?” (Lu. 23:40) Wayahudi walikuwa naabudu Mungu moya, lakini watu wa mataifa walikuwa naabudu miungu mingi. (Kut. 20:2, 3; 1 Ko. 8:5, 6) Kama wale watenda-mabaya hawangekuwa Wayahudi, pengine ule mutenda-mabaya angeuliza hivi: “Hauogope miungu yetu?” Zaidi ya ile, Yesu alitumwa kwa “kondoo wenye kupotea wa nyumba ya Israeli,” hapana kwa watu wa mataifa. (Mt. 15:24) Mungu aliambiaka Waisraeli kama atafufua wafu. Inawezekana ule mutenda-mabaya mwenye alitubu alijua vile. Na sawa vile maneno yake inaonyesha, alijua kama Yehova atamufufua Yesu ili akuwe Mufalme wa Ufalme wake. Inaonekana kama ule mutenda-mabaya aliamini kuwa Mungu atamufufua yeye pia.

3. Inawezekana ule mutenda-mabaya mwenye alitubu alifikiria nini wakati Yesu alitaya Paradiso? Fasiria. (Mwanzo 2:15)

3 Inaonekana ule mutenda-mabaya alikuwa Muyahudi. Kwa hiyo, alipaswa kujua habari ya Adamu na Eva na ya Paradiso yenye Yehova aliumba ili waishi ndani yake. Njo maana, inawezekana ule mutenda-mabaya aliamini kama Paradiso yenye Yesu alizungumuzia ingekuwa bustani ya muzuri hapa ku dunia.​—Soma Mwanzo 2:15.

4. Maneno yenye Yesu aliambia ule mutenda-mabaya inapaswa kutuchochea tufikirie nini?

4 Maneno yenye Yesu aliambia ule mutenda-mabaya inapaswa kutuchochea tufikirie namna maisha itakuwa mu Paradiso. Utawala wenye amani wa Mufalme Sulemani unaweza kutufundisha jambo fulani kuhusu Paradiso. Biblia inasema kama Yesu anamupita Sulemani. Kwa hiyo, tuko hakika kama Yesu na watawala wenzake watafanya maisha ikuwe muzuri ku dunia. (Mt. 12:42) Njo maana, inaomba “kondoo wengine” wajue mambo yenye wanapaswa kufanya juu wastahili kuishi milele mu Paradiso.​—Yoh. 10:16.

MAISHA ITAKUWA NAMNA GANI MU PARADISO?

5. Unawaza maisha itakuwa namna gani mu Paradiso?

5 Unawaza maisha itakuwa namna gani mu Paradiso? Pengine unawaza kama dunia itakuwa bustani ya muzuri sana sawa vile bustani ya Edeni. (Mwa. 2:7-9) Pengine unakumbuka unabii wa Mika wenye kuonyesha kama watu wa Mungu wataikala “kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya muti wake wa tini.” (Mik. 4:3, 4) Unaweza pia kukumbuka maandiko fulani ya Biblia yenye kuonyesha kama chakula itakuwa mingi. (Zb. 72:16; Isa. 65:21, 22) Kwa hiyo, unaweza kujiwazia na uko mu bustani ya muzuri, na uko naikala ku meza yenye inayala chakula ya muzuri. Unaweza pia kuwazia harufu ya muzuri ya mimea na maua. Na pengine unawazia namna weye, watu wa familia yako, marafiki, na wale wenye watafufuliwa muko nafurahia kupitisha wakati pamoya. Ile haiko ndoto. Bila shaka, ile mambo yote itatimia ku dunia. Lakini, tutakuwa pia na kazi ya muzuri ya kufanya mu Paradiso.

Tutakuwa na kazi ya maana sana ya kufundisha wale wenye watafufuliwa (Ona fungu ya 6)

6. Tutakuwa na mambo gani ya kufanya mu Paradiso? (Ona picha.)

6 Yehova alituumba na uwezo wa kufurahia kazi. (Muh. 2:24) Tutakuwa na mambo mingi ya kufanya wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu. Wale wenye wataokoka taabu kubwa, pamoya na mamilioni ya wale wenye watafufuliwa, watakuwa na lazima ya nguo, chakula, na fasi ya kuikala. Itaomba kutumika sana juu wapate ile mambo yote yenye watakuwa nayo lazima. Sawa vile tu Adamu na Eva waliombwa kutunza bustani yao, tutakuwa na pendeleo ya kufanya dunia yote ikuwe Paradiso! Wazia pia vile tutafurahi wakati tutakuwa nafundisha mamilioni ya watu, wenye watafufuliwa wenye hawamujue Yehova muzuri na kusudi yake. Na tutafurahi pia kufundisha mambo mingi waaminifu wenye walikufaka zamani mbele Yesu akuye ku dunia!

7. Tuko hakika na jambo gani, na juu ya nini?

7 Tuko hakika kama tutaishi kwa amani mu Paradiso. Tutakuwa na mambo yote yenye tutakuwa nayo lazima, na mambo yote itakuwa yenye kupangwa muzuri. Juu ya nini? Juu tayari Yehova ametuonyesha namna maisha itakuwa mu utawala wa Mwana wake. Habari ya utawala wa Mufalme Sulemani inatusaidia kujua namna maisha itakuwa mu Paradiso.

UTAWALA WA MUFALME SULEMANI UNAONYESHA NAMNA MAISHA ITAKUWA MU PARADISO

8. Nini njo inaonyesha kama maneno ya Zaburi 37:10, 11, 29 ilitimia zamani? (Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu hii gazeti.)

8 Roho ya Mungu ilimuongoza Mufalme Daudi aandike kuhusu namna maisha itakuwa wakati Mufalme mwenye hekima na muaminifu atatawala. (Soma Zaburi 37:10, 11, 29.) Mara mingi tunasomeaka wengine maneno ya Zaburi 37:11 wakati tuko nazungumuzia Paradiso yenye kuya. Hatukosee wakati tuko tunafanya vile, juu Yesu alirudiliaka ile maneno mu mahubiri yake ya ku mulima. Na kwa kufanya vile, alionyesha kama ile maneno itatimia pia mu wakati yenye kuya. (Mt. 5:5) Lakini, maneno yenye Daudi alisema ilionyesha pia namna maisha ingekuwa mu utawala wa Mufalme Sulemani. Wakati Sulemani alitawala Israeli, watu wa Mungu waliishi kwa amani kabisa na walikuwa na maisha ya muzuri mu inchi “yenye kutiririka maziwa na asali.” Mungu alisema hivi: “Kama munaendelea kufuata sheria zangu . . . , nitatia amani katika inchi, na mutalala pasipo mutu wa kuwaogopesha.” (Law. 20:24; 26:3, 6) Ile maneno ilitimia wakati ya utawala wa Sulemani. (1 Ny. 22:9; 29:26-28) Na Yehova aliahidi kama waovu “hawatakuwa tena.” (Zb. 37:10) Kwa hiyo, maneno ya Zaburi 37:10, 11, 29 ilitimia zamani, na itatimia pia wakati yenye kuya.

9. Kisha kujionea vile mambo ilikuwa mu utawala wa Sulemani, malkia wa Sheba alisema nini?

9 Malkia wa Sheba alipata habari kama Waisraeli walikuwa naishi kwa amani na walikuwa na maisha ya muzuri wakati Sulemani alikuwa mufalme. Kwa hiyo, alifanya safari ya murefu ili kuenda Yerusalemu ajionee. (1 Fa. 10:1) Kisha kujionea vile mambo ilikuwa mu utawala wa Sulemani, malkia wa Sheba alisema hivi: “Sikukuwa nimeambiwa hata nusu yake. . . . Wenye furaha ni watu wako, na wenye furaha ni watumishi wako wenye wanasimama mbele yako kila wakati, wakisikiliza hekima yako!” (1 Fa. 10:6-8) Lakini, mambo yenye Mufalme Sulemani alifanyia watu wakati alitawala ilikuwa tu mufano wa mambo yenye Yehova atafanyia wanadamu wakati Mwana wake, Yesu, atatawala.

10. Ni mambo gani inaonyesha kama Yesu anamupita Sulemani?

10 Yesu anamupita Sulemani mu kila njia. Sulemani hakukuwa mukamilifu na alifanya makosa mazito yenye ililetea watu wa Mungu magumu. Lakini, Yesu ni kiongozi mukamilifu mwenye hakoseake. (Lu. 1:32; Ebr. 4:14, 15) Yesu aliendelea kuwa muaminifu kwa Mungu hata kama Shetani alimuletea majaribu ya nguvu. Kristo ameonyesha kama hatafanyaka zambi ao kufanya jambo yoyote yenye inaweza kuletea magumu wale wenye atatawala. Atakuwa Mufalme muzuri sana.

11. Ni wanani njo watatawala na Yesu?

11 Juu ya kuhangaikia wanadamu na kutimiza kusudi yenye Yehova alikuwa nayo wakati aliumba dunia, Yesu atatawala na watawala wenzake 144 000. (Ufu. 14:1-3) Walivumilia majaribu na mateso mingi wakati walikuwa ku dunia, kwa hiyo watatuelewa. Lakini, watakuwa na kazi gani kabisa?

WATIWA-MAFUTA WATAKUWA NA KAZI GANI?

12. Wale 144 000 watakuwa na kazi gani?

12 Yesu na watawala wenzake watakuwa na kazi kubwa zaidi kuliko ile ya Sulemani. Sulemani alipaswa kuhangaikia mamilioni ya watu mu inchi moya tu. Lakini, Yesu na watawala wenzake watahangaikia mamiliare ya watu mu dunia yote. Yehova amepatia wale 144 000 pendeleo kubwa sana!

13. Wale wenye watatawala na Yesu watakuwa na kazi gani ya pekee?

13 Sawa vile Yesu, wale 144 000 watakuwa wafalme na makuhani. (Ufu. 5:10) Wakati Waisraeli waliongozwa na Sheria ya Musa, kazi ya kwanza ya makuhani ilikuwa kusaidia watu waendelee kuwa na afya ya muzuri kimwili na kiroho. Sheria ilikuwa “kivuli cha mambo ya muzuri yenye yatakuja.” Kwa hiyo, tunaweza kusema kama wale wenye watatawala na Yesu watakuwa na kazi ya pekee ya kusaidia watu wa Mungu wakuwe na hali ya muzuri ya kimwili na ya kiroho. (Ebr. 10:1) Hatujue namna wale wafalme na makuhani watakuwa nazungumuza na wale wenye watakuwa hapa ku dunia. Hata ikuwe Yehova atakamata mipango gani, tuko hakika kama mu Paradiso yenye kuya, wale wenye wataishi ku dunia watapewa muongozo wenye watakuwa nao lazima.​—Ufu. 21:3, 4.

“KONDOO WENGINE” WANAPASWA KUFANYA NINI ILI WASTAHILI KUISHI MU PARADISO?

14. “Kondoo wengine” na “kundi ndogo” wako natumika namna gani?

14 Yesu aliita wale wenye watatawala naye “kundi ndogo.” (Lu. 12:32) Alizungumuzia pia kikundi ya pili, yenye aliita “kondoo wengine.” Vile vikundi viwili vinafanyiza kundi moya yenye umoja. (Yoh. 10:16) Tayari wale wenye kufanyiza vile vikundi viwili wako natumika kwa umoja leo, na wataendelea kufanya vile kadiri dunia itakuwa Paradiso. Bila shaka, ile wakati “kundi ndogo” itakuwa mbinguni na “kondoo wengine” watakuwa na nafasi ya kufurahia maisha milele ku dunia. Lakini, kuko mambo yenye “kondoo wengine” wanapaswa kufanya sasa juu wastahili kuishi mu Paradiso.

Kuanzia leo, tunaweza kujitayarisha ili kuishi mu Paradiso yenye kuya (Ona fungu ya 15) b

15. (a) “Kondoo wengine” wanafanya nini ili kutegemeza ndugu za Kristo? (b) Unaweza kufanya nini ili kuiga mufano wa ule ndugu mwenye kuwa mu pharmacie? (Ona picha.)

15 Ule mutenda-mabaya mwenye alitubu alikufa mbele akuwe na nafasi ya kuonyesha kabisa shukrani yake juu ya mambo yenye Yesu alimufanyia. Lakini leo, siye “kondoo wengine” tuko na nafasi za mingi za kuonyesha shukrani yetu juu ya mambo yenye Yesu alitufanyia. Kwa mufano, tunaonyesha kuwa tunamupenda Yesu mu namna yenye tunatendea ndugu zake watiwa-mafuta. Yesu alionyesha kama juu ya kuhukumu kondoo, atakuwa naangalia namna walitendea ndugu zake. (Mt. 25:31-40) Tunaweza kutegemeza ndugu za Kristo kwa kuwasaidia kufanya kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi kwa bidii. (Mt. 28:18-20) Juu tuweze kufanya vile, tunapaswa kutumia muzuri vichapo vyenye vinatusaidia kujifunza na watu Biblia, sawa vile kitabu Furahia Maisha Milele! Kama hauyaanza kujifunza Biblia na mutu fulani, ujiwekee muradi wa kuanza kujifunza Biblia na watu wengi, kadiri unaweza.

16. Ni mambo gani yenye tunapaswa kufanya juu ya kujitayarisha ili kuishi mu Paradiso?

16 Tusichunge tu mupaka Paradiso ifike njo tukuwe watu wenye Yehova anapenda waishi mule. Tangu sasa tunapaswa kujikaza ili kuwa wanyoofu mu maneno na matendo yetu na kuwa na kiasi mu maisha yetu. Na tunapaswa kuwa waaminifu kwa Yehova, kwa bibi ao bwana yetu, na kwa Wakristo wenzetu. Kama tuko najikaza sasa kufuata sheria za Yehova mu hii dunia yenye kuharibika, itakuwa mwepesi kwetu kuzifuata wakati tutaishi mu Paradiso. Ni muzuri pia tujifunze ufundi fulani na kukomalisha sifa fulani juu ya kuonyesha kama tuko najitayarisha ili kuishi mu Paradiso. Ona habari “Uko Najitayarisha ili ‘Kuriti Dunia’?” yenye kuwa mu hii gazeti.

17. Tunapaswa kuendelea kujilaumu juu ya zambi nzito zenye tulifanyaka zamani? Fasiria.

17 Tena, hatupaswe kuendelea kujilaumu juu ya zambi nzito zenye tulifanyaka zamani. Kwa kweli, hatupaswe hata kidogo kuona bei ya ukombozi kuwa kisingizio ya “kutenda zambi kimakusudi.” (Ebr. 10:26-31) Kama tumetubu kabisa zambi nzito yenye tulifanya, tumeomba Yehova atusamehe, tumetafuta musaada wa wazee, na kubadilisha mwenendo wetu, tukuwe hakika kama Yehova ametusamehe kabisa. (Isa. 55:7; Mdo. 3:19) Kumbuka hii maneno yenye Yesu aliambia Wafarisayo: “Sikukuja kuita wenye haki, lakini nilikuja kuita watenda-zambi.” (Mt. 9:13) Bei ya ukombozi iko na nguvu kabisa ya kufunika zambi zetu zote.

UNAWEZA KUISHI MILELE MU PARADISO

18. Utapenda kuzungumuzia nini na ule mutenda-mabaya mwenye alikufiaka pembeni ya Yesu?

18 Wazia uko mu Paradiso na uko naongea na ule mutenda-mabaya mwenye alisemaka na Yesu. Kwa kweli, nyiye wote wawili mutapenda kuzungumuzia namna muko wenye shukrani juu ya bei ya ukombozi ya Yesu. Pengine utamuuliza akufasirie zaidi mambo yenye ilifanyika saa kidogo mbele Yesu akufe, na namna alijisikia wakati Yesu alijibia ombi yake. Na pengine naye atakuuliza umufasirie namna maisha ilikuwa mu siku za mwisho za dunia ya Shetani. Itakuwa pendeleo kabisa kujifunza Neno ya Mungu na watu wa vile!​—Efe. 4:22-24.

Mu Utawala wa Miaka Elfu, ndugu anafurahia kufanya kazi fulani ya ufundi yenye alichungaka kwa hamu kufanya (Ona fungu ya 19)

19. Juu ya nini maisha mu Paradiso haitachokesha? (Ona picha ku jalada.)

19 Maisha mu Paradiso haitachokesha hata kidogo. Kila siku tutakuwa na watu wazuri wa kukutana nao na tutakuwa na kazi ya muzuri ya kufanya. Na jambo ya maana zaidi, kila siku tutakuwa na nafasi ya kumujua Baba yetu wa mbinguni muzuri zaidi na kufurahia mambo yenye ametupatia. Kutakuwa mambo mingi ya kujifunza juu ya Yehova na juu ya uumbaji wake. Kadiri tutaishi siku mingi, ni vile tutamupenda Mungu zaidi. Tuko wenye shukrani sana kwa Yehova na Yesu kwa kutupatia ahadi ya kama inawezekana kuishi milele mu Paradiso!

WIMBO 22 Ufalme Unatawala​—Tunasali Ukuye!

a Unafikiriaka mara mingi namna maisha itakuwa mu Paradiso? Inatia moyo kufanya vile. Kama tunaendelea kufikiri juu ya mambo yenye Yehova atatufanyia, ile itatusaidia tukuwe na hamu sana ya kufundisha wengine kuhusu dunia mupya. Hii habari itatusaidia kuamini kabisa kama ahadi ya Paradiso yenye Yesu alitoa itatimia.

b MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mwenye iko na tumaini ya kufundisha watu wenye watafufuliwa iko nafundisha wengine tangu sasa.