Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 8

Shauri Yako ‘Inafurahishaka Moyo’?

Shauri Yako ‘Inafurahishaka Moyo’?

“Mafuta na uvumba vinafurahisha moyo; ni vile pia urafiki mutamu wenye unatokana na shauri la unyoofu.”​—MEZ. 27:9.

WIMBO 102 ‘Musaidie Wale Wenye Kuwa Wazaifu’

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Ndugu moya alijifunza nini kuhusu kutoa shauri?

MIAKA mingi yenye imepita, wazee wawili walitembelea dada mumoja mwenye alikuwa amekosa mikutano kwa wakati fulani. Muzee mwenye aliongoza ile mazungumuzo alimuonyesha ule dada maandiko fulani kuhusu kuhuzuria mikutano. Aliwaza kama ile mazungumuzo ilimutia moyo ule dada. Na wakati yeye na ule muzee mwingine walitaka kurudia, ule dada alisema hivi: “Ndugu hamujue hata kitu kuhusu magumu yangu.” Wale ndugu walimushauria ule dada bila hata kumuuliza juu ya magumu yake na hali yake. Ile ilifanya asione kama ile shauri ni ya maana.

2 Muzee mwenye aliongoza mazungumuzo alisema kama: “Ku mwanzo, niliwaza kama ule dada alikuwa anatukosea heshima. Lakini, nilifikia kutambua kama nilikuwa tu namuonyesha maandiko yenye kufaa kuliko kumuuliza maulizo yenye kufaa sawa vile: ‘Ni mambo gani haiendeke mu maisha yako?’ ‘Namna gani naweza kusaidia?’” Ule muzee alijifunza jambo ya maana sana mu ile mufano. Leo ule muzee, ni mwenye huruma na ni muchungaji muzuri.

3. Ni nani anaweza kutoa shauri mu kutaniko?

 3 Wakiwa wachungaji, wazee wako na daraka ya kutoa shauri kama ni lazima kufanya vile. Hata vile, kuko wakati wenye wengine mu kutaniko wanaweza kutoa shauri. Kwa mufano, ndugu ao dada fulani anaweza kupatia rafiki fulani shauri yenye inategemea Biblia. (Zb. 141:5; Mez. 25:12) Ao dada mwenye kuzeeka anaweza ‘kushauria wanamuke vijana’ mu hali sawa zile zenye zinatajwa mu Tito 2:3-5. Na kusema kweli, mara mingi wazazi wanakuwaka na lazima ya kushauria na kurekebisha watoto wao. Hata kama hii habari inazungumuzia zaidi sana wazee, siye wote tunaweza kupata faida kwa kujikumbusha njia zenye zinaweza kutusaidia kutoa shauri ya muzuri na yenye ‘itafurahisha moyo.’​—Mez. 27:9.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Mu hii habari, tutazungumuzia maulizo ine kuhusu namna ya kutoa shauri: (1) Kuko sababu gani zenye kufaa za kutoa shauri? (2) Inafaa kabisa kutoa shauri? (3) Nani njo anapaswa kutoa shauri? (4) Namna gani unaweza kutoa shauri yenye kufaa?

KUKO SABABU GANI ZENYE KUFAA ZA KUTOA SHAURI?

5. Nini njo itasaidia muzee atoe shauri ya muzuri? (1 Wakorinto 13:4, 7)

5 Wazee wanapenda ndugu na dada zao. Wakati fulani, wanaonyeshaka ule upendo kwa kushauria mutu fulani mwenye wanaona iko mu njia ya kuangukia katika kosa. (Gal. 6:1) Mbele ya kuzungumuza na mutu, ni muzuri muzee afikirie mambo fulani yenye Paulo alisema kuhusu upendo. “Upendo ni wenye uvumilivu na wenye fazili. . . . Unafunika mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote, unavumilia mambo yote.” (Soma 1 Wakorinto 13:4, 7.) Kufikiri sana juu ya ile mistari ya Biblia, kutamusaidia ule muzee achunguze sababu yenye inafanya atoe shauri na amushaurie ndugu yake mu njia ya upendo. Kama mwenye anapewa shauri anaona kuwa muzee anamuhangaikia, ile inaweza kumusaidia kukubali ile shauri.​—Ro. 12:10.

6. Paulo alituachia mufano gani muzuri?

6 Akiwa muzee, mutume Paulo alituachia mufano muzuri. Kwa mufano, wakati ndugu wa Tesalonike walikuwa na lazima ya shauri, Paulo hakusita kuwashauria. Lakini, mu barua zake, Paulo aliwapongeza kwanza juu ya kazi yenye walifanya kwa uaminifu, juu ya upendo wao, na juu ya uvumilivu wao. Tena, alifikiri juu ya hali zao, na aliwaambia kama anajua vile maisha yao haikukuwa mwepesi na kama walikuwa wanavumilia upinzani. (1 Te. 1:3; 2 Te. 1:4) Na hata aliwaambia kama walikuwa mufano muzuri kwa Wakristo wengine. (1 Te. 1:8, 9) Walipaswa kufurahi sana wakati Paulo aliwapongeza! Hakuna shaka kama Paulo alipenda sana ndugu zake. Njo maana alitoa shauri yenye kufaa kabisa mu barua zake kwa Watesalonike.​—1 Te. 4:1, 3-5, 11; 2 Te. 3:11, 12.

7. Nini njo inaweza kufanya mutu fulani akatale shauri?

7 Nini njo inaweza kutokea kama hatukutoa shauri mu njia yenye kufaa? Muzee fulani mwenye uzoefu anasema hivi: “Watu fulani wanakatalaka shauri, hapana juu shauri ni ya mubaya, lakini juu haikutolewa mu njia ya upendo.” Ile inatufundisha nini? Ni mwepesi kukubali shauri wakati inatolewa kwa upendo, hapana kwa hasira.

INAFAA KABISA KUTOA SHAURI?

8. Ni maulizo gani muzee anaweza kujiuliza kama iko anafikiria ikiwa atatolea mutu fulani shauri ao hapana?

8 Wazee hawapaswe kuwa haraka kutoa shauri. Mbele ya kutoa shauri, muzee anapaswa kujiuliza hivi: ‘Inafaa kabisa niseme jambo fulani? Niko hakika kama mambo yenye ule mutu iko anafanya ni ya mubaya? Kuko sheria fulani ya Biblia yenye imevunjwa? Ao mawazo yake tu njo iko tofauti na yangu?’ Kwa hekima, wazee wanaepuka kuwa “haraka kusema.” (Mez. 29:20) Ikiwa muzee haiko hakika kama inaomba ashaurie mutu fulani, anaweza kuuliza muzee mwingine juu ya kuzungumuzia ile jambo ili kuona kama kuko sababu ya kimaandiko yenye inaweza kumuchochea atoe shauri.​—2 Ti. 3:16, 17.

9. Paulo anatufundisha nini kuhusu namna ya kutoa shauri juu ya kuvala na kujipamba? (1 Timoteo 2:9, 10)

9 Fikiria mufano fulani. Waza muzee fulani anahangaishwa na namna muhubiri fulani anavalaka na kujipamba. Muzee anaweza kujiuliza hivi: ‘Kuko sababu fulani ya kimaandiko yenye itafanya niseme jambo fulani?’ Juu ya kuepuka kutoa mawazo yake, ule muzee anaweza pengine kuuliza muzee mwingine ao muhubiri mukomavu mawazo yake na pengine pamoya wanaweza kurudilia shauri ya Paulo kuhusu kuvala na kujipamba. (Soma 1 Timoteo 2:9, 10.) Paulo alionyesha kanuni fulani zenye zinaweza kusaidia Mukristo avale na ajipambe kwa njia yenye kufaa na kwa kiasi. Lakini Paulo hakufanya liste ya mambo yenye tunapaswa kuvala na yenye hatupaswe. Paulo alijua kama Wakristo wanaweza kuchagula kuvala vile wanapenda lakini bila kuvuka mipaka yenye maandiko inaweka. Njo maana ikiwa wazee wako wanafikiria kama inaomba kutoa shauri ao hapana, wanapaswa kuchunguza ili kuona kama namna ya kuvala na ya kujipamba ya ule mutu inaonyesha kama ni mwenye kiasi na akili ya muzuri.

10. Hatupaswe kusahau nini kuhusu maamuzi yenye wengine wanakamata?

10 Tusisahau kama Wakristo wawili wanaweza kukamata maamuzi yenye kuwa tofauti. Lakini ile haionyeshe kama uamuzi wa huyu Mukristo wa kwanza ni wa muzuri lakini wa ule mwingine ni wa mubaya. Njo maana hatupaswe kukaza ndugu zetu kufanya mambo yenye tunawaza kama njo ya muzuri.​—Ro. 14:10.

NANI NJO ANAPASWA KUTOA SHAURI?

11-12. Kama inafaa kutoa shauri, ni maulizo gani muzee anapaswa kujiuliza, na juu ya nini?

11 Kama inafaa kabisa kutoa shauri, ulizo ingine ni hii: Nani njo anapaswa kuitoa? Mbele ya kushauria dada mwenye alishaolewa ao mutoto fulani, muzee atazungumuza na kichwa ya familia, mwenye pengine anaweza kupendelea kuhangaikia ile hali yeye mwenyewe. * Ao kichwa ya familia anaweza kupenda kuwa pale wakati muzee atatoa ile shauri. Na sawa vile ilionyeshwa mu  fungu ya 3, wakati fulani kama inafaa, dada fulani mwenye kukomala anaweza kushauria dada kijana.

12 Kuko jambo ingine yenye muzee anapaswa kufikiria. Anaweza kujiuliza hivi: ‘Je, inafaa kabisa miye njo nitoe shauri, ao inaweza kuwa muzuri zaidi kama mwingine njo anaitoa?’ Kwa mufano, inaweza kuwa mwepesi kwa mutu mwenye anajionaka kuwa wa bure kusikiliza shauri ya muzee mwenye alikuwaka pia anajisikia vile. Muzee mwenye alikuwa anajisikia vile anaweza kuonyesha huruma zaidi, na inawezekana mambo yenye atasema ule muhubiri atakuwa tayari kuikubali. Hata vile, wazee wote wako na daraka ya kutia moyo na kuchochea ndugu na dada zao wafanye mabadiliko yenye Maandiko inaomba. Kwa hiyo, jambo ya maana zaidi ni kutoa shauri, hata kama muzee mwenye anaitoa hayakutanaka na ile hali.

NAMNA GANI UNAWEZA KUTOA SHAURI YENYE KUFAA?

Juu ya nini wazee Wakristo wanapaswa kuwa “haraka kusikiliza”? (Ona fungu ya 13-14)

13-14. Juu ya nini ni jambo ya maana kwa muzee kusikiliza?

13Ukuwe tayari kusikiliza. Wakati muzee iko anajitayarisha juu ya kutoa shauri fulani, anapaswa kujiuliza hivi: ‘Nini njo najua kuhusu hali ya ndugu yangu? Ni mambo gani yenye iko inamufikia mu maisha? Kuko magumu fulani iko inamufikia yenye sijue? Kwa sasa iko na lazima zaidi ya nini?’

14 Kanuni yenye kuwa mu Yakobo 1:19 inafaa kabisa kwa wale wenye kutoa shauri. Yakobo aliandika hivi: “Kila mutu anapaswa kuwa mwepesi wa kusikiliza, hapana mwepesi wa kusema, hapana mwepesi wa kukasirika.” Muzee anaweza kuwaza kama anajua habari zote, lakini anazijua kabisa? Mezali 18:13 inatukumbusha kama: “Wakati mutu anajibu mbele ya kusikia ukweli wa mambo, huo ni upumbavu na haya.” Ni muzuri zaidi kupata habari zote moja kwa moja kwa mutu mwenye anahusika. Ile inatia ndani kusikiliza mbele ya kusema. Kumbuka somo yenye ule muzee mwenye tulitaja ku mwanzo ya hii habari alijifunza. Alitambua kama, kuliko kuanza mazungumuzo kwa kusema mambo yenye alitayarisha, alipaswa kwanza kuuliza ule dada maulizo sawa vile, “Ni nini iko inakufikia mu maisha?” “Namna gani naweza kukusaidia?” Kama wazee wanakamata wakati wa kutafuta habari zote, ile itafanya wasaidie na watie moyo ndugu na dada zao.

15. Namna gani wazee wanaweza kutumikisha kanuni yenye kuwa mu Mezali 27:23?

15Ujue muzuri kundi. Sawa vile tulishazungumuzia kule mwanzo, kutoa shauri yenye kufaa haiko tu kusoma maandiko fulani ao kutoa pendekezo ao mapendekezo fulani. Ndugu na dada zetu wako na lazima ya kuona kama tunawahangaikia, kama tunawaelewa, na kama tunapenda kuwasaidia. (Soma Mezali 27:23.) Wazee wanapaswa kufanya yao yote juu wakuwe na uhusiano wa karibu sana pamoya na ndugu na dada zao.

Nini njo itafanya ikuwe mwepesi zaidi kwa wazee kutoa shauri (Ona fungu ya 16)

16. Nini njo itasaidia wazee kutoa shauri yenye kufaa?

16 Wazee hawapendi ndugu zao wawaze kama wakati tu wenye wanazungumuza pamoya nao ni wakati tu ndugu ao dada fulani alifanya jambo fulani ya mubaya. Kuliko kufanya vile, wazee wanaonyesha kama wanahangaikia ndugu na dada zao wakati wanapambana na magumu fulani kwa kuzungumuza pamoya nao kila mara. Muzee fulani mwenye uzoefu anasema hivi: “Kama unafanya vile, utatia nguvu uhusiano wako pamoya nao.” Na kisha wakati itakuwa lazima kutoa shauri, itakuwa mwepesi sana kwako kufanya vile, na itakuwa mwepesi sana kwa mwenye anashauriwa kukubali shauri.

Juu ya nini muzee anapaswa kuwa muvumilivu na mwenye fazili wakati iko anatoa shauri? (Ona fungu ya 17)

17. Muzee iko na lazima ya kuwa muvumilivu na mwenye fazili zaidi sana wakati gani?

17Ukuwe muvumilivu na mwenye fazili. Uvumilivu na fazili ni ya maana sana, zaidi sana wakati ku mwanzo, mutu fulani hapendi kutumikisha mambo yenye Biblia inasema. Muzee anapaswa kuepuka kuwa na muelekeo wa kukasirika wakati shauri yake inakataliwa ao haitumikishwe. Ilitabiriwa hivi kuhusu Yesu: “Hataponda utete wenye ulivunjika, na hatazimisha utambi wenye kutoa moshi.” (Mt. 12:20) Kwa hiyo, mu sala zake za kipekee, muzee anaweza kumuomba Yehova amusaidie ule mwenye iko na lazima ya shauri aelewe sababu ya ile shauri na aitumikishe. Ndugu mwenye alishauriwa anaweza kuwa na lazima ya wakati ili kufikiria mambo yenye walimuambia. Kama muzee ni muvumilivu na mwenye fazili, ule mwenye wanatolea shauri hatahangaishwa na namna shauri ilitolewa lakini atakazia uangalifu mambo yenye ilisemwa. Kusema kweli, kila wakati shauri inapaswa kutegeme Neno ya Mungu.

18. (a) Kuhusu kutoa shauri, ni jambo gani hatupaswe kusahau? (b) Kulingana na picha ya juu ku ukurasa wa 18 na kisanduku ya ukurusa wa 19, wazazi wako wanazungumuzia nini?

18Ujifunze kupitia makosa yako. Juu hatuko wakamilifu, hatutaweza kutumikisha kwa ukamilifu mashauri yote yenye tumepata mu hii habari. (Yak. 3:2) Tutafanya makosa, lakini wakati tunafanya vile, tunapaswa kujifunza kupitia makosa yetu. Kama ndugu na dada zetu wanaona kuwa tunawapenda, itakuwa mwepesi kwao kutusamehe wakati tunawakosea kupitia maneno na matendo yetu.​—Ona pia kisanduku “ Vikumbusho Fulani kwa Wazazi.”

TUMEJIFUNZA NINI?

19. Namna gani tunaweza kufurahisha moyo wa ndugu na dada zetu?

19 Sawa vile tumetoka kuona, haiko mwepesi kutoa shauri yenye kufaa. Hatukamilike na wale wenye tunashauria hawakamilike pia. Usisahau kanuni zenye tumezungumuzia mu hii habari. Uhakikishe kabisa kama uko na sababu ya kutoa shauri fulani. Tena, uhakikishe kama inafaa kabisa kutoa shauri na kama ni weye njo inaomba kutoa ile shauri. Mbele ya kutoa shauri, uliza maulizo fulani na usikilize kwa uangalifu ili ujue mambo yenye mutu iko anapambana nayo. Jaribu kuona mambo vile yeye anaiona. Ukuwe mwenye fazili, na utie nguvu uhusiano wako pamoya na ndugu na dada zako. Usisahau kusudi: Tunapenda shauri yetu ikuwe yenye kufaa lakini pia ‘ifurahishe moyo.’​—Mez. 27:9.

WIMBO 103 Yehova Ametupatia Wachungaji

^ fu. 5 Kila mara haikuwake mwepesi kutoa shauri. Wakati tunaona kama ni lazima kutoa shauri, namna gani tunaweza kusema mu njia yenye itasaidia na kutia moyo wengine? Hii habari itasaidia zaidi sana wazee watoe shauri yenye itafanya wengine waikubali na kuitumikisha.

^ fu. 11 Ona habari “Ukichwa mu Kutaniko” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2021.