Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 7

“Usikilize Maneno ya Wenye Hekima”

“Usikilize Maneno ya Wenye Hekima”

“Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye hekima.”​—MEZ. 22:17.

WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi

KIFUPI YA HABARI *

1. Watu fulani wanaweza kutushauria juu ya nini, na juu ya nini siye wote tunakuwaka na lazima ya shauri?

KILA mara, siye wote tunakuwaka na lazima ya kushauriwa. Wakati fulani, tunaweza kulomba shauri kwa mutu mwenye tunaheshimiaka. Wakati ingine, ndugu mwenye kutuhangaikia anaweza kutuambia kama tuko karibu kuangukia mu “hatua fulani ya mubaya” yenye inaweza kufanya tuhuzunike kisha. (Gal. 6:1) Ku mwisho, mutu fulani anaweza kutupatia shauri juu ya kuturekebisha kisha kufanya kosa nzito. Ikuwe ni juu ya nini tunashauriwa, tunapaswa kusikiliza. Ni muzuri kufanya vile na ile inaweza kuokoa uzima wetu!​—Mez. 6:23.

2. Kulingana na Mezali 12:15 juu ya nini tunapaswa kusikiliza shauri?

2 Andiko yetu ya musingi ya hii habari inatutia moyo ‘kusikiliza maneno ya wenye hekima.’ (Mez. 22:17) Hakuna mutu mwenye anajuaka mambo yote, kunakuwaka tu mutu mwenye kutushinda ao mwenye kuwa na uzoefu mingi kuliko siye. (Soma Mezali 12:15 na maelezo ya chini.) Njo maana kusikiliza shauri ni alama ya unyenyekevu. Ile inaonyesha kama tunajua mipaka yetu na kama tuko na lazima ya musaada juu tufikie miradi yetu. Yehova alimuongoza Sulemani, Mufalme mwenye hekima aandike hivi: “Mambo yanatimizwa kupitia washauri wengi.” ​—Mez. 15:22.

Ni shauri gani yenye unaona nguvu kukubali kati ya hizi shauri mbili? (Ona fungu ya 3-4)

3. Ni mu njia gani mbalimbali tunaweza kushauriwa?

3 Tunaweza kutolewa shauri ya moja kwa moja na yenye haiko ya moja kwa moja. Shauri yenye haiko ya moja kwa moja njo nini? Tunaweza kusoma jambo fulani yenye kuwa mu Biblia ao mu moya kati ya vichapo vyetu yenye itafanya tufikiri kuhusu mambo yenye tuko tunafanya na kisha mambo yenye tuko tunasoma itatuchochea kubadilisha mawazo na matendo yetu. (Ebr. 4:12) Ile njo tunaweza kuita shauri yenye haiko ya moja kwa moja. Shauri ya moja kwa moja njo nini? Muzee ao ndugu fulani mwenye kuwa na uzoefu anaweza kutuambia kuhusu jambo fulani yenye anaona kwetu yenye tunapaswa kufanyia mabadiliko. Ile njo tutaita shauri ya moja kwa moja. Kama mutu fulani mwenye anatupenda sana anatupatia shauri yenye inategeme Biblia, tunapaswa kuonyesha shukrani yetu kwa kusikiliza mambo yenye anatuambia na kujikaza kutumikisha ile shauri.

4. Kulingana na Muhubiri 7:9, tunapaswa kuepuka kufanya nini wakati wanatushauria?

4 Kusema kweli, inaweza kuwa nguvu kwetu kukubali shauri ya moja kwa moja. Tunaweza hata kukwazika. Juu ya nini? Hata kama tunajua kama hatukamilike, inaweza kuwa nguvu kwetu kukubali shauri wakati mutu fulani anatuambia kuhusu kosa fulani yenye tulifanya. (Soma Muhubiri 7:9.) Pengine tunaweza kutoa visababu. Pengine tunaweza kujiuliza nini njo ilimuchochea akuye kutushauria ao tunaweza kukasirika juu ya namna alitutolea shauri. Na pengine tunaweza hata kutafuta makosa kwa ule mwenye alitushauria na kusema hivi: ‘Alijiona mbele ya kuya kunishauria? Naye anafanyaka makosa!’ Na kama hatupende shauri yenye wanatutolea pengine tunaweza tu kuipuuza ao kuomba mutu mwingine atupatie shauri juu tunatumainia kama yeye njo atatuambia mambo yenye tunapenda kusikia.

5. Mu hii habari tutazungumuzia mambo gani?

5 Mu hii habari tutazungumuzia mifano ya Biblia ya wale wenye walikatala shauri na ya wale wenye waliikubali. Tutazungumuzia pia mambo yenye inaweza kutusaidia kukubali shauri na kupata faida kupitia ile shauri.

WALIKATALA SHAURI

6. Tunaweza kujifunza mambo gani mu njia yenye Mufalme Rehoboamu alitenda wakati alishauriwa?

6 Fikiria mufano wa Rehoboamu. Wakati alikuwa mufalme wa Israeli, watu wake walikuja kwake ili kumuomba jambo fulani. Walimuomba apunguze uzito wa muzigo kuliko baba yake Sulemani. Rehoboamu alikamata uamuzi wa muzuri wa kuenda kuuliza wazee waisraeli ili kujua namna angejibia wale watu. Wale wanaume wazee walimushauria mufalme kama, ikiwa anakubali ombi ya wale watu wangemutumikia sikuzote. (1 Fa. 12:3-7) Inaonekana kama, Rehoboamu hakufurahia ile shauri, njo maana alienda kuomba shauri kwa vijana wanaume wenye walikomala pamoya naye. Inaonekana wale vijana walikuwa na miaka 40 hivi, kwa hiyo, walipaswa kuwa na uzoe fulani mu maisha. (2 Ny. 12:13) Lakini mu ile wakati, walimupatia Rehoboamu shauri ya mubaya. Walimushauria awaongezea wale watu mizigo. (1 Fa. 12:8-11) Akiwa mbele ya ile mawazo mbili, Rehoboamu angemuambia Yehova katika sala na kumuuliza ni shauri gani alipaswa kufuata. Lakini, alifuata shauri yenye aliona kuwa ya muzuri na akafanya mambo yenye wale vijana walisema. Ile ilikuwa na matokeo ya mubaya kwa Rehoboamu na kwa watu wa Israeli. Mu hali yetu, pengine shauri yenye wanatutolea sikuzote haitakuwa njo yenye tungependa kusikia. Lakini, kama inategemea Neno ya Mungu tunapaswa kuikubali.

7. Mufano wa Mufalme Uzia unatufundisha nini?

7Mufalme Uzia alikatala shauri. Aliingia mu hekalu ya Yehova kwenye makuhani tu njo waliruhusiwa kuingia, na alijaribu kutoa uvumba. makuhani wa Yehova walimuambia hivi: “Haiko kazi yako, Uzia, kumuchomea Yehova uvumba! Ni makuhani tu ndio wanapaswa kuchoma uvumba.” Uzia alitenda namna gani? Kama angekubali kwa unyenyekevu ile shauri na kutoka mara moya mu hakalu, pengine Yehova angemusamehe. Lakini, “Uzia . . . akakasirika sana.” Juu ya nini alikatala ile shauri? Inaonekana, aliwaza kama juu alikuwa mufalme angeweza kufanya mambo yote yenye anapenda. Lakini Yehova hakuona mambo mu ile njia. Juu alifanya jambo fulani yenye hakuruhusiwa kufanya, Uzia alipigwa ukoma na “alibakia mwenye ukoma mupaka siku ya kifo chake.” (2 Ny. 26:16-21) Mufano wa Uzia unatufundisha kama ikuwe tuko watu wa hali gani, kama tunakatala shauri yenye inategemea Biblia tutakosa kukubaliwa na Yehova.

WALIKUBALI SHAURI

8. Yobu alitenda namna gani wakati alishauriwa?

8 Tofauti na mifano yenye kuonya yenye tumetoka tu kuzungumuzia, Biblia inatutuolea mifano ya muzuri ya wale wenye walibarikiwa juu walikubali shauri. Fikiria Yobu. Hata kama alikuwa anamuogopa Mungu, hakukuwa mukamilifu. Wakati alikuwa na mahangaiko sana, alisema mawazo fulani ya mubaya. Ile ilifanya Elihu na Yehova wamutolee shauri ya moja kwa moja. Yobu alitenda namna gani ? Kwa unyenyekevu alikubali shauri. Alisema hivi: “Nilisema, lakini bila kuelewa . . . Ninaondoa mambo yenye nilisema, na ninatubu katika mavumbi na majivu.” Yehova alimubariki Yobu juu alitenda kwa unyenyekevu.​—Yob. 42:3-6, 12-17.

9. Musa alitenda namna gani wakati alishauriwa, na juu ya nini iko mufano muzuri?

9Musa ni mufano muzuri juu alikubali kurekebishwa kisha kufanya kosa nzito. Siku moya, alikasirika na hakumutukuza Yehova. Ile ilifanya Musa apoteze pendeleo ya kuingia mu Inchi ya Ahadi. (Hes. 20:1-13) Wakati Musa alimuomba Yehova afikirie tena uamuzi wake, Yehova alimuambia hivi: “Usiniambie tena juu ya jambo hili.” (Kum. 3:23-27) Musa hakukasirika. Lakini, alikubali uamuzi wa Yehova na Yehova aliendelea kumutumikisha ili kuongoza Israeli. (Kum. 4:1) Yobu na Musa walikubali shauri na wako mifano muzuri kwetu. Yobu alibadilisha mawazo yake, hakutoa visababu. Musa alionyesha kama alikubali shauri ya Yehova kwa kuendelea kuwa muaminifu hata wakati alipoteza pendeleo yenye ilikuwa ya maana sana kwake.

10. (a) Mezali 4:10-13 inaonyesha nini kuhusu faida zenye tunapata wakati tunakubali shauri? (b) Ni mutazamo gani muzuri watu fulani wameonyesha wakati wanashauriwa?

10 Tunapata faida wakati tunaiga mufano yenye wanaume waaminifu walituachia sawa vile Yobu na Musa. (Soma Mezali 4:10-13.) Ndugu na dada zetu wengi waliwaiga na kukubali shauri. Fikiria mambo yenye ndugu Emmanuel, mwenye anaishi Congo anasema hivi kuhusu onyo yenye alipewa: “Mu kutaniko yangu ndugu na dada wakomavu waliona kama nilikuwa karibu kuaribisha urafiki wangu pamoya na Yehova, na walijikaza kunisaidia. Nilitumikisha mashauri yao na ilinisaidia kuepuka magumu mingi.” * Painia moya wa Kanada, Megan anasema: “Wakati fulani mambo yenye watu walikuwa nanishauria haikukuwa nanifurahisha lakini shauri yenye walinipatia njo yenye nilikuwa nayo lazima.” Na ndugu Marko mwenye kuishi Kroatia anasema hivi: “Nilipoteza pendeleo yenye nilikuwa nayo, lakini saa yenye nafikiria kuhusu ile wakati nafikia kutambua kama shauri yenye nilipewa imenisaidia kutia tena nguvu uhusiano wangu pamoya na Yehova.”

11. Ndugu Karl Klein alisema nini kuhusu kukubali shauri?

11 Mufano ingine ya mutu fulani mwenye alipata faida kwa kukubali shauri ni wa ndugu Karl Klein, mwenye alikuwa mushiriki wa Baraza Yenye Kuongoza. Mu maisha yake Ndugu Klein anaeleza wakati wenye Joseph F. Rutherford, mwenye alikuwa naye urafiki wa karibu sana alimupatia karipio kali. Ndugu Klein anasema kama ku mwanzo hakufurahia ile shauri. Anasema hivi: “Wakati Ndugu Rutherford aliniona tena, aliniambia mu njia ya kirafiki, ‘Jambo Karl!’ Lakini juu nilikuwa ningali na uchungu, nilimujibia tu kwa sauti ya chini. Akaniambia, ‘Karl, fanya angalisho! Ibilisi anapenda kukunasa!’ Nikiwa mwenye kukasirika nikamujibu, ‘Oh, Ndugu Rutherford hakuna kitu.’ Lakini alijua kama nilimukasirikia njo maana alirudilia tena onyo yake na kusema hivi, ‘Sawa. Lakini fanya angalisho. Ibilisi anapenda kukunasa.’ Alisema kweli kabisa! Wakati tunawekea ndugu kinyongo zaidi sana juu alisema mambo fulani yenye alipaswa kusema . . . , tunapatia Ibilisi nafasi ya kutunasa.” * (Efe. 4:25-27) Ndugu Klein alikubali shauri ya Ndugu Rutherford na urafiki wao uliendelea kuwa muzuri.

NI MAMBO GANI ITATUSAIDIA KUKUBALI SHAURI?

12. Unyenyekevu unaweza kutusaidia namna gani kukubali shauri? (Zaburi 141:5)

12 Ni mambo gani inaweza kutusaidia kukubali shauri? Ni muzuri kuwa wanyenyekevu na kukumbuka kama hatukamilike na wakati fulani tunaweza kutenda mubaya. Sawa vile tumesha zungumuzia, Yobu alikuwa na mawazo ya mubaya lakini alibadilisha mawazo yake na Yehova alimubariki. Juu ya nini? Juu Yobu alikuwa munyenyekevu. Alionyesha unyenyekevu wake kwa kukubali shauri yenye Elihu alimupatia, hata kama Elihu alikuwa mudogo sana kuliko yeye. (Yob. 32:6, 7) Unyenyekevu utatusaidia pia kutumikisha shauri hata kama tunaona kuwa hatustahili kuipewa ao mwenye anatutolea ile shauri ni mudogo sana kuliko siye. Muzee moya wa Kanada anasema hivi: “Vile hatuwezi kujiona sawa vile wengine wanatuonaka namna gani tunaweza kufanya maendeleo kama hakuna mutu wa kutushauria?” Siye wote tuko na lazima ya kukomalisha tunda ya roho na kufikia kuwa muhubiri na mwalimu muzuri zaidi wa habari njema​—Soma Zaburi 141:5.

13. Tunapaswa kuona namna gani shauri yenye wanatutolea?

13Uone shauri kuwa njia ya Mungu ya kutuonyesha upendo. Yehova anatutakia mambo ya muzuri zaidi. (Mez. 4:20-22) Wakati anatushauria kupitia Neno yake, kichapo fulani yenye inategemea Biblia, ao kupitia muamini fulani mukomavu, ni njia ya kutuonyesha upendo. Waebrania 12:9, 10 inasema: “Yeye anafanya vile kwa faida yetu.”

14. Wakati mutu fulani anatushauria, tunapaswa kukazia akili nini?

14Ukazie akili shauri, hapana namna ilitolewa. Wakati fulani tunaweza kuwaza kama, hawakututolea shauri mu njia ya muzuri zaidi. Kusema kweli, kila mutu mwenye anatoa shauri anapaswa kujikaza kufanya ile shauri ikuwe mwepesi kadiri inawezekana juu ikubaliwe. * (Gal. 6:1) Lakini kama ni siye njo wanatushauria tunapaswa kufikiria mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia ile shauri hata kama tunawaza kuwa mutu mwenye alitutolea ile shauri angepaswa kufanya vile mu njia ya muzuri zaidi. Pengine tunaweza kujiuliza hivi: ‘Hata kama sikupenda namna shauri ilitolewa kuko jambo fulani naweza kujifunza kupitia mambo yenye ilisemwa? Je, naweza kutia pembeni makosa ya mutu mwenye alinitolea shauria na kujifunza mambo fulani kupitia shauri yake?’ Ni jambo ya hekima kwetu kutafuta njia fulani ya kupata faida kupitia shauri yoyote yenye wanatutolea.​—Mez. 15:31.

UOMBE SHAURI NA UTAPATA FAIDA

15. Juu ya nini tunapaswa kuomba shauri?

15 Biblia inatutia moyo kuomba shauri. Mezali 13:10 inasema hivi: “Hekima ni ya wale wenye kutafuta shauri.” Ile maneno ni ya kweli kabisa! Wale wenye wanalombaka shauri kuliko kuchunga mutu fulani awashaurie, mara mingi watakamata maamuzi ya muzuri zaidi kuliko wale wenye hawalombake shauri. Kwa hiyo, ujikaze kuomba shauri.

Juu ya nini dada kijana anaombaka dada mukomavu shauri? (Ona fungu ya 16)

16. Ni mu hali gani tunaweza kuomba shauri?

16 Ni wakati gani tunaweza kuomba waamini wenzetu shauri? Fikiria hizi hali. (1) Dada fulani anaomba muhubiri fulani mwenye uzoefu amusindikize ku funzo yake ya Biblia na kisha anamuomba shauri juu ya namna anaweza kuwa mwalimu muzuri zaidi. (2) Dada fulani mwenye hajaolewa anapenda kuuza nguo fulani, kwa hiyo anaomba dada fulani mukomavu amusaidie kuchagula. (3) Ndugu fulani iko na pendeleo ya kutoa hotuba yake ya kwanza ya watu wote. Anaomba musemaji fulani mwenye uzoefu asikilize kwa uangalifu hotuba yake na kisha amupatie shauri fulani juu ya namna anaweza kufanya muzuri zaidi. Hata ndugu mwenye alishakatoa hotuba mingi kwa miaka mingi anaweza kulomba shauri kwa wasemaji wenye uzoefu na kisha anatumikisha shauri yenye anapata.

17. Namna gani tunaweza kupata faida kupitia shauri yenye wanatutolea?

17 Mu majuma ao miezi yenye iko inakuya, siye wote tutapata ikuwe shauri ya moja kwa moja ao shauri yenye haiko ya moja kwa moja. Wakati ile inatokea tukumbuke somo fulani zenye tumetoka kujifunza. Uendelee kuwa munyenyekevu. Ukazie uangalifu shauri hapana namna inatolewa. Na utumikishe shauri yenye wanakutolea. Hakuna mwenye alizaliwaka na hekima. Lakini wakati ‘tunasikiliza shauri na kukubali nizamu,’ Neno ya Mungu inaahidi kama ‘tutakuwa na hekima.’​—Mez. 19:20.

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

^ fu. 5 Watu wa Yehova wanaona kama ni jambo ya maana kusikiliza mashauri ya Biblia na kuitumikisha. Lakini kila mara haikuwake mwepesi kukubali shauri na kuitumikisha. Juu ya nini inakuwaka nguvu kufanya vile? Na nini njo inaweza kutusaidia kupata faida kupitia shauri yenye wanatutolea?

^ fu. 10 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 11 Ona Munara wa Mulinzi wa Tarehe 1 Mwezi wa 5, 1985, uku. 20-27 (ya Kifaransa).

^ fu. 14 Mu habari yenye kufuata tutazungumuzia namna wale wenye wanatoa shauri wanaweza kufanya vile kwa busara.