Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 16

Ukuwe na Furaha Wakati Unafanya Yako Yote kwa Ajili ya Yehova

Ukuwe na Furaha Wakati Unafanya Yako Yote kwa Ajili ya Yehova

“Kila mutu achunguze matendo yake mwenyewe.”​—GAL. 6:4.

WIMBO 37 Nitakutumikia kwa Nafsi Yangu Yote

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni nini inafanyaka tukuwe na furaha sana?

 YEHOVA anapenda tukuwe na furaha juu furaha ni sehemu ya tunda ya roho yake takatifu. (Gal. 5:22) Juu kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea, tunakuwaka na furaha sana wakati tunatumika kwa bidii mu utumishi wa Kikristo na wakati tunasaidia ndugu zetu mu njia mbalimbali.​—Mdo. 20:35.

2-3. (a) Sawa vile Wagalatia 6:4 inaonyesha, ni mambo gani mbili itatusaidia kuendelea kumutumikia Yehova kwa furaha? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Mu andiko ya Wagalatia 6:4, mutume Paulo anazungumuzia mambo mbili yenye itatusaidia tuendelee kuwa na furaha. (Soma.) Jambo ya kwanza, muradi wetu unapaswa kuwa kufanya yetu yote kwa ajili ya Yehova. Tunapaswa kuwa na furaha kama tuko nafanya yetu yote kwa ajili yake. (Mt. 22:36-38) Jambo ya pili, tunapaswa kuepuka kujilinganisha na wengine. Kama afya yetu, ufundi, ao uwezo fulani wa kizalikio wenye tuko nao vinatuwezesha kufanya mambo fulani, tunapaswa kumushukuru Yehova. Kusema kweli, kila kitu yenye tuko nayo inatoka kwake. Kwa upande mwingine, kama wengine wako napata matokeo ya muzuri zaidi mu kazi ya kuhubiri kuliko siye, tunapaswa kufurahi juu wako natumia uwezo wenye wako nao ili kumusifu Yehova, haiko juu ya kutafuta faida zao wenyewe. Kwa hiyo kuliko kushindana nao, tunapaswa kujifunza kutoka kwao.

3 Mu hii habari, tutazungumuzia namna tunaweza kupambana na hali ya kuvunjika moyo kama hatuna tena uwezo wa kufanya mambo mingi mu utumishi wetu. Tutaona pia namna tunaweza kutumia muzuri zaidi zawadi yenye tunaweza kuwa nayo, na tutaona mambo yenye tunaweza kujifunza kutoka kwa wengine.

WAKATI HALI YAKO INAKUWEKEA MIPAKA FULANI

Wakati tunafanya yetu yote mu maisha yetu tunamufurahisha Yehova (Ona fungu ya 4-6) *

4. Ni hali gani yenye inaweza kufanya mutu avunjike moyo? Leta mufano.

4 Uzee na magonjwa vinaweza kufanya ikuwe nguvu kwa watumishi fulani wa Yehova kufanya mambo yenye wangependa kufanya mu kazi ya Yehova. Na njo mambo ilimufikia Carol. Wakati fulani alitumikiaka fasi kwenye kulikuwaka lazima kubwa. Ile wakati, alikuwaka naongoza mafunzo ya Biblia 35 na alisaidiaka wengi wafikie kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Carol alipataka matokeo ya muzuri mu mahubiri! Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba aligonjwa sana, kwa hiyo iliomba akuwe anabakia wakati mingi ku nyumba yake. Carol anasema hivi, “Najua kama juu niko mugonjwa, sitaweza kufanya mambo yenye wengine wanaweza kufanya, lakini najisikiaka kama siko muaminifu sawa vile wao, siwezi kufanya kila kitu yenye napenda kufanya. Na ile inanivunjaka moyo.” Carol anapenda kufanya yake yote kwa ajili ya Yehova. Kwa kweli, anastahili pongezi sana! Tuko hakika kama Mungu wetu mwenye huruma iko nafurahia ile yenye iko anafanya.

5. (a) Tunapaswa kukumbuka nini kama hali yetu inatuwekea mipaka fulani yenye inatuvunja moyo? (b) Vile picha zinaonyesha, namna gani ndugu anaendelea kufanya yake yote mu utumishi wa Yehova?

5 Kama wakati fulani unavunjika moyo juu hali yako inakuwekea mipaka fulani, ujiulize hivi, ‘Yehova anapenda nifanye nini?’ Anapenda ufanye yote yenye unaweza kulingana na hali yako. Wazia hii hali: Dada mumoja mwenye iko na miaka 80 anavunjika moyo juu hawezi kufanya tena mambo mingi zaidi mu utumishi wake sawa vile alikuwaka nafanya wakati alikuwaka na miaka 40. Anawaza kama, hata kama iko nafanya yake yote ile haimufuraishe Yehova. Lakini ile ni kweli? Waza kidogo. Kama ule dada alifanya yake yote wakati alikuwa na miaka 40 na angali anafanya yake yote wakati iko na miaka 80, ile haionyeshe kama iko anaendelea kufanya yake yote? Kama tunanza kuwaza kama utumishi wetu haumufurahishe Yehova, ni muzuri tukumbuke kama Yehova njo anaamuaka ni nini mutu atafanya juu amufurahishe. Kama unafanya yako yote, bila shaka Yehova atakuambia: “Umefanya muzuri!”​—Linganisha na Matayo 25:20-23.

6. Mufano wa Maria unaweza kutufundisha nini?

6 Tutakuwa na furaha kama tunakaza akili yetu juu ya mambo yenye tunaweza kufanya kuliko kukaza akili juu ya mambo yenye hatuwezi kufanya. Fikiria mufano wa dada mwenye kuitwa Maria, mwenye kuwa na ugonjwa wenye unamuzuia kufanya mambo mingi mu kazi ya mahubiri. Ku mwanzo, alivunjika moyo na kujisikia kuwa hafae. Lakini alifikiria dada moya mu kutaniko mwenye alikuwa anabakia tu ku kitanda juu alikuwa mugonjwa, na akaamua kumusaidia. Maria anasema hivi: “Nilifanya mipango ya kuanza kuhubiri naye kupitia telefone na barua. Kila wakati tulihubiri pamoya, nilikuwa narudia ku nyumba mwenye furaha na mwenye kutosheka juu nilikuwa nimemusaidia dada yangu.” Siye pia tunaweza kuongeza furaha yetu kama tunakaza akili juu ya mambo yenye tunaweza kufanya kuliko kukaza akili juu ya mambo yenye hatuwezi kufanya. Lakini tunaweza kufanya nini kama tuko na uwezo wa kufanya mambo mingi zaidi ao kama tayari kuko mambo fulani yenye tuko nafanya muzuri mu utumishi wetu kwa Yehova?

KAMA UKO NA ZAWADI, “UITUMIE”!

7. Ni mashauri gani yenye mutume Petro alipatia Wakristo?

7 Mu barua yake ya kwanza, mutume Petro alitia moyo ndugu zake watumie zawadi ao vipawa vyenye wako navyo ili kujenga waamini wenzao. Petro aliandika hivi: “Kwa kadiri kila mumoja amepokea zawadi, muitumie ili kutumikiana kama wasimamizi-nyumba wazuri wa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu.” (1 Pe. 4:10) Hatupaswe kujizuia kutumia zawadi zetu kwa ukamili juu ya kuogopa kama wengine wanaweza kutusikilia wivu ao kuvunjika moyo. Juu kama tunajizuia, hatutafanya yetu yote kwa ajili ya Yehova.

8. Kulingana na 1 Wakorinto 4:6, 7, juu ya nini tunapaswa kuepuka kujivuna juu ya zawadi zenye tuko nazo?

8 Tunapaswa kutumia zawadi zetu kwa ukamili, lakini tunapaswa kuwa waangalifu tusijivune juu ya zile zawadi. (Soma 1 Wakorinto 4:6,7.) Kwa mufano, unaweza kuwa fundi mu kuanzisha mafunzo ya Biblia. Haupaswe kujizuia kutumia ile zawadi! Lakini hata kama uko na ile zawadi haupaswe kujivuna. Wazia hivi karibuni ulikuwa mu mahubiri na unaanzisha funzo ya Biblia. Unapenda kabisa kuambia kikundi yenu ya mahubiri ile jambo. Lakini wakati muko pamoya, unaona dada moya iko anawafasiria namna alifurahia kuachia mutu gazeti. Yeye aliachia mutu gazeti; weye ulianzisha funzo ya Biblia. Utafanya nini? Unajua muzuri kama ile jambo yenye ulifanya itatia moyo kikundi yenu ya mahubiri, lakini unaweza kuamua kuizungumuzia siku ingine, juu ule mwenye alitoa gazeti asione kama hakupata matokeo ya muzuri sawa weye. Ni muzuri kufanya vile. Lakini unapaswa kuendelea tu kuanzisha mafunzo ya Biblia. Uko na zawadi, uitumie!

9. Tunapaswa kutumia zawadi zetu ili kufanya nini?

9 Tukumbuke kama uwezo wote wa kizalikio wenye tuko nao ni zawadi kutoka kwa Mungu. Tunapaswa kutumia zile zawadi juu ya kujenga kutaniko, hapana juu ya kujionyesha. (Flp. 2:3) Wakati tunatumia nguvu na uwezo wenye tuko nao juu ya kufanya mapenzi ya Mungu, tutakuwa na furaha hapana juu tunapita wengine ao tunajionyesha kama tuko wazuri zaidi kuliko wao, lakini juu tunatumia zawadi zenye tuko nazo ili kumusifu Yehova.

10. Juu ya nini haiko muzuri kujilinganisha na wengine?

10 Kama hatuko waangalifu, tunaweza kulinganisha mambo yenye tuko na uwezo wa kufanya na yenye wengine hawana uwezo wa kufanya. Kwa mufano, ndugu moya anaweza kuwa na uwezo wa kutoa muzuri hotuba za watu wote. Ule ni uwezo wake. Lakini mu moyo wake, anaweza kuanza kuzarau ndugu mwingine mwenye hana ule uwezo. Lakini inawezekana ule ndugu mwingine ni mukarimu sana, anazoezaka watoto wake muzuri, ao iko na bidii sana mu mahubiri. Tuko na furaha kabisa ya kuwa na ndugu na dada wengi wenye wako natumia vipawa ao zawadi zao ili kumutumikia Yehova na kusaidia wengine!

UJIFUNZE KUPITIA MIFANO YA WENGINE

11. Juu ya nini tunapaswa kufuata mufano wa Yesu?

11 Hata kama hatupaswe kujilinganisha na wengine, mifano yao ya uaminifu inaweza kutufundisha mambo fulani. Tufikirie mufano wa Yesu. Hata kama hatukamilike, sifa za Yesu na mambo ya muzuri yenye alifanya inaweza kutufundisha mambo mingi. (1 Pe. 2:21) Kama tunafanya yetu yote ili kufuata mufano wake kwa ukaribu kulingana na uwezo wetu, tutakuwa watumishi wa Yehova wazuri zaidi na wenye kuwa na matokeo ya muzuri zaidi mu utumishi.

12-13. Mufano wa Mufalme Daudi unaweza kutufundisha nini?

12 Mu Neno ya Mungu, muko mifano mingi ya wanaume na wanamuke waaminifu wenye tunaweza kuiga hata kama hawakukuwa wakamilifu. (Ebr. 6:12) Fikiria Mufalme Daudi, mwenye Yehova aliita “mutu mwenye kufurahisha moyo wangu” ao, sawa vile tafsiri ingine ya Biblia inasema, “mtu mwenye kunipendeza.” (Mdo. 13:22) Lakini, Daudi hakukuwa mukamilifu. Kwa kweli, alifanyaka makosa fulani mazito. Hata vile, ni mufano muzuri kwetu. Juu ya nini? Juu wakati alirekebishwa, hakujitetea. Lakini, aliitika shauri nzito yenye alipewa na alihuzunika sana juu ya mambo yenye alifanyaka. Matokeo ilikuwa nini? Yehova alimusamehe.​—Zb. 51:3, 4, 10-12.

13 Tunaweza kumuiga Daudi kwa kujiuliza hivi: ‘Natendaka namna gani wakati nashauriwa? Nakuwaka haraka kukubali makosa yangu, ao najiteteaka? Nakuwaka haraka kulaumu wengine? Najikazaka sana juu nisirudilie makosa yangu?’ Unaweza kujiuliza maulizo ya vile wakati uko nasoma habari kuhusu wanaume na wanamuke waaminifu wenye kutajwa mu Biblia. Walipambana na magumu sawa ile yako? Ni sifa gani za muzuri zenye walionyesha? Mu kila hali ujiulize hivi: ‘Namna gani ninaweza kuwa sawa ule mutumishi muaminifu wa Yehova?’

14. Kufikiria hali ya waamini wenzetu kunaweza kutuletea faida gani?

14 Kufikiria hali ya waamini wenzetu, ikuwe ni vijana ao wazee kunaweza pia kutuletea faida. Kwa mufano, mu kutaniko yenu muko mutu fulani mwenye iko navumillia kwa uaminifu jaribu fulani, pengine mukazo kutoka kwa wenzake, upinzani mu familia, ao magonjwa? Ule mutu iko na sifa fulani za muzuri zenye ungependa kuiga? Kufikiria mufano wake, kunaweza kukusaidia ujue ni mu njia gani ya muzuri unaweza kuvumilia magumu yenye uko nayo. Tuko wenye shukrani na furaha ya kuwa na ndugu na dada wa vile, wenye kutuachia mufano muzuri wa imani!​—Ebr. 13:7; Yak. 1:2, 3.

UKUWE NA FURAHA WAKATI UNAMUTUMIKIA YEHOVA

15. Ni shauri gani yenye mutume Paulo alitoa yenye inaweza kutusaidia tuendelee kuwa na furaha wakati tuko namutumikia Yehova?

15 Juu mu kutaniko mukuwe amani na umoja, kila mutu anapaswa kujikaza kufanya yake yote. Fikiria Wakristo wa wakati wa mitume. Walikuwa na zawadi na migao mbalimbali. (1 Ko. 12:4, 7-11) Lakini ile haikufanya kukuwe migawanyiko na roho ya mashindano. Lakini, Paulo alitia moyo kila mutu afanye yenye anaweza “ili kujenga mwili wa Kristo.” Aliandikia hivi Waefeso: “Wakati kila kiungo kinafanya kazi muzuri, hilo linafanya mwili ukomae wakati unajijenga wenyewe katika upendo.” (Efe. 4:1-3, 11, 12, 16) Wale wenye walifanya vile, walifanya kukuwe amani na umoja, mambo yenye tuko najionea leo mu makutaniko yetu.

16. Unapaswa kuazimia kufanya nini? (Waebrania 6:10)

16 Azimia kuepuka kujilinganisha na wengine. Kuliko kufanya vile, acha mufano wa Yesu ukufundishe na ujikaze kuiga sifa zake. Faidika na mifano ya imani ya watu wenye kutajwa mu Biblia na ya watu wa siku zetu. Vile unaendelea kufanya yako yote, ukuwe hakika kama Yehova “hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yako.” (Soma Waebrania 6:10.) Endelea kuwa na furaha wakati uko namutumikia Yehova, na ujue kama iko na furaha wakati anakuona unafanya yako yote.

WIMBO 65 Fanya Maendeleo!

^ fu. 5 Siye wote tunaweza kujifunza kupitia mifano ya wengine. Lakini kuko hatari yenye tunapaswa kuepuka, kujilinganisha na wengine. Hii habari itatuonyesha namna tunaweza kuendelea kuwa na furaha na namna ya kuepuka kuwa na kiburi ao kuvunjika moyo wakati tunalinganisha mambo yenye tunaweza kufanya na yenye wengine wako nafanya.

^ fu. 49 MAFASIRIO YA PICHA Ndugu moya alitumikaka ku Beteli wakati alikuwaka kijana. Kisha alioa na akafanya upainia pamoya na bibi yake. Wakati walipata watoto, aliwazoeza mu kazi ya kuhubiri. Sasa alishazeeka, na anaendelea kufanya yake yote kwa kuhubiri kupitia barua.