Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 21

Kitabu ya Ufunuo—Iko na Maana Gani Juu ya Wakati Wako Wenye Kuya?

Kitabu ya Ufunuo—Iko na Maana Gani Juu ya Wakati Wako Wenye Kuya?

“Amina! Kuja, Bwana Yesu.”​—UFU. 22:20.

WIMBO 142 Tusiache Tumaini Yetu

KIFUPI YA HABARI *

1. Wanadamu wote wanapaswa kukamata uamuzi gani wa maana?

 LEO watu wanapaswa kukamata uamuzi wa maana. Inaomba waamue kama watamuunga mukono Yehova na kumukubali kuwa mwenye haki ya kutawala ulimwengu, ao kama watamuunga mukono adui yake mwenye hana huruma, Shetani Ibilisi. Haiwezekane kuunga mukono pande zote mbili. Lakini hata watu waamue nini, mambo yenye wanaamua itakuwa na matokeo juu ya wakati wao wenye kuya. (Mt. 25:31-33, 46) Wakati wa “taabu kubwa,” watatiwa alama ya kuokolewa ao ya kuharibiwa.​—Ufu. 7:14; 14:9-11; Eze. 9:4, 6.

2. (a) Waebrania 10:35-39 inatutia moyo tufanye nini? (b) Kitabu ya Ufunuo inaweza kutusaidia namna gani?

2 Soma Waebrania 10:35-39. Kama umeamua kuunga mukono utawala wa Yehova, umekamata uamuzi wenye hekima. Sasa unapenda sana kusaidia wengine wakamate uamuzi muzuri. Unaweza kutumia habari yenye iko mu kitabu ya Ufunuo juu ya kuwasaidia. Ile kitabu ya maana sana inatusaidia kujua mambo yenye itapata wale wenye kumupinga Yehova. Lakini inatusaidia pia kujua baraka zenye wale wenye kwa ushikamanifu wanaunga mukono utawala wake watapata. Ni muzuri tufikirie zile kweli za maana sana. Kufanya vile kutatusaidia tuazimie hata zaidi kuendelea kumutumikia Yehova. Zaidi ya ile, tunaweza kutumia mambo yenye tumejifunza juu ya kusaidia wengine waamue kumutumikia Yehova na waendelee kufanya vile.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutajibia hii maulizo: Wale wenye wanaunga mukono utawala wa Mungu watapata nini? Ni nini itapata wale wenye wanaamua kuunga mukono ule munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa, mwenye anazungumuziwa mu kitabu ya Ufunuo?

WALE WENYE KUUNGA MUKONO UTAWALA WA MUNGU WATAPATA NINI?

4. Mutume Yohana aliona kikundi gani inasimama pamoya na Yesu mbinguni?

4 Mutume Yohana aliona vikundi mbili vya watu wenye kuunga mukono utawala wa Mungu na aliona wanapata uzima wa milele. Kikundi ya kwanza iko na watu 144 000. (Ufu. 7:4) Wanatoka ku dunia na kuenda mbinguni juu ya kujiunga na Yesu na kufanyiza serikali ao Ufalme wenye utatawala dunia. (Ufu. 5:9, 10; 14:3, 4) Mu maono, Yohana anaona wanasimama pamoya na Yesu ku Mulima Sayuni mbinguni.​—Ufu. 14:1.

5. Ni nini itawafikia wenye kubakia kati ya wale 144 000?

5 Tangu wakati wa mitume, maelfu ya watu wamechaguliwa juu wakuwe sehemu ya wale 144 000. (Lu. 12:32; Ro. 8:17) Lakini Yohana anaambiwa kama, ni hesabu kidogo tu ya wenye watabakia kati yao njo watakuwa wangali wazima wakati wa siku za mwisho. Wale “wenye kubakia” watapata “muhuri” wa mwisho juu ya kuonyesha kama Yehova anawakubali. (Ufu. 7:2, 3; 12:17) Na ile itafanyika mbele taabu kubwa ianze. Kisha wakati fulani mu kipindi ya taabu kubwa, wale wenye kubakia wataenda mbinguni juu wajiunge na wengine wa mu kikundi ya wale 144 000, wenye walikufa na wako waaminifu. Kule, watatawala pamoya na Yesu mu Ufalme wa Mungu.​—Mt. 24:31; Ufu. 5:9, 10.

6-7. (a) Yohana anaona kundi gani ingine, na tunajua nini juu ya ile kundi? (b) Juu ya nini wale wenye kubakia kati ya wale wenye wataenda mbinguni na wale wa “kundi kubwa” wanapaswa kupendezwa na mambo yenye kuzungumuziwa mu sura ya 7 ya kitabu ya Ufunuo?

6 Kisha kuona kundi ya wale wenye wataenda mbinguni, Yohana anaona “kundi kubwa.” Tofauti na wale 144 000, hii kundi haiwezi kuhesabiwa. (Ufu. 7:9, 10) Tunajua nini juu yao? Yohana anaambiwa hivi: “Hawa ndio wale wenye wanatoka katika ile taabu kubwa, na wamefua kanzu zao na kuzifanya mweupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” (Ufu. 7:14) Kisha kuokoka taabu kubwa, wenye kufanyiza hii “kundi kubwa” wataishi hapa ku dunia na watabarikiwa sana.​—Zb. 37:9-11, 27-29; Mez. 2:21, 22; Ufu. 7:16, 17.

7 Ikuwe tumechaguliwa kuenda mbinguni ao tutabakia hapa ku dunia, tunapaswa kujiuliza hii ulizo ya maana: Ninajiona mu picha ya mufano yenye kuzungumuziwa mu Ufunuo sura ya 7? Kusema kweli, tunapaswa kuhakikisha kama tutajionea utimizo wa ile maneno. Utimizo wa ile maneno utafurahisha sana kundi yote mbili ya watu wa Mungu! Tutafurahi kuona kama tuliamuaka kuunga mukono utawala wa Yehova. Kitabu ya Ufunuo inatuambia mambo gani ingine juu ya taabu kubwa?​—Mt. 24:21.

NI NINI ITAPATA WALE WENYE KUMUPINGA MUNGU?

8. Taabu kubwa itaanza na tukio gani, na watu wengi watatenda namna gani?

8 Vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, matengenezo ya politike ya hii dunia itageukia Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo. (Ufu. 17:16, 17) Ile tukio njo itaanzisha taabu kubwa. Sasa, ile itafanya watu wote waamue kumutumikia Yehova? Hapana. Tofauti na ile, Ufunuo sura ya 6 inaonyesha kama mu ile wakati, watu wenye hawamutumikie Yehova watatafuta ulinzi ku matengenezo ya politike na ya biashara ya huu ulimwengu, yenye Biblia inafananisha na milima. Juu wale watu hawataunga mukono Ufalme wa Mungu, Yehova atawaona kuwa wenye kumupinga.​—Lu. 11:23; Ufu. 6:15-17.

9. Wakati wa taabu kubwa namna gani watumishi wa Yehova wataonyesha kama wako tofauti na watu wengine, na ile itakuwa na matokeo gani?

9 Kusema kweli, wakati wa taabu kubwa watumishi waaminifu wa Yehova watakuwa tofauti na watu wengine. Wao tu njo wataendelea kuwa kundi ya watu wenye kumutumikia Yehova hapa ku dunia na wenye wanakatala kuunga mukono “munyama wa pori.” (Ufu. 13:14-17) Juu wataendelea kubakia waaminifu kwa Yehova, wale wenye kumupinga Yehova watawakasirikia sana. Ile itafanya muungano wa mataifa ushambulie watu wa Mungu mu dunia yote. Ile shambulizi kali njo yenye Biblia inaita shambulizi ya Gogu wa Magogu.​—Eze. 38:14-16.

10. Kulingana na Ufunuo 19:19-21, Yehova atatenda namna gani wakati watu wake watashambuliwa?

10 Yehova atatenda namna gani wakati wa ile shambulizi? Anatuambia hivi: “Kasirani yangu kali itawaka.” (Eze. 38:18, 21-23) Ufunuo sura ya 19 inazungumuzia mambo yenye itatokea kisha pale. Yehova atamutuma Mwana wake juu apiganie watu wake na apate ushindi juu ya maadui wake. “Majeshi katika mbingu,” ni kusema malaika waaminifu pamoya na wale 144 000, watajiunga na Yesu juu ya kupigania watu wa Mungu. (Ufu. 17:14; 19:11-15) Mambo itakuwa namna gani ku mwisho wa ile vita? Matengenezo na wanadamu wote wenye kumupinga Yehova wataharibiwa!​—Soma Ufunuo 19:19-21.

KISHA ILE VITA, KUTAKUWA NDOA

11. Kitabu ya Ufunuo inazungumuzia tukio gani yenye kufurahisha?

11 Pima kuwaza namna watumishi waaminifu wa Yehova watajisikia kisha kuokoka wakati maadui wa Mungu wataharibiwa. Itakuwa furaha kubwa sana! Ni kweli kutakuwa makelele ya furaha mbinguni wakati Babiloni Mukubwa ataharibiwa, lakini kuko jambo ingine yenye italeta furaha zaidi. (Ufu. 19:1-3) Ni “ndoa ya Mwana-Kondoo.” Ile njo tukio yenye kufurahisha sana yenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Ufunuo.​—Ufu. 19:6-9.

12. Vile Ufunuo 21:1, 2 inaonyesha, ndoa ya Mwana-kondoo itafanyika wakati gani?

12 Ile ndoa itafanyika wakati gani? Tunajua kama wale 144 000 wote watakuwa mbinguni wakati kidogo tu mbele vita ya Armagedoni ianze. Lakini, ile haiko njo wakati wenye ndoa ya Mwana-kondoo itafanyika. (Soma Ufunuo 21:1, 2.) Ndoa ya Mwana-kondoo itafanyika kisha vita ya Armagedoni na kisha maadui wote wa Mungu kuharibiwa.​—Zb. 45:3, 4, 13-17.

13. Ni nini itafanyika ku ndoa ya Mwana-kondoo?

13 Ni nini itafanyika ku ndoa ya Mwana-kondoo? Vile tu ndoa inaunganishaka mwanaume na mwanamuke, ni vile pia ile ndoa ya mufano itaunganisha Mufalme, Yesu Kristo na “bibi-arusi” wake, ni kusema, wale 144 000. Ile tukio yenye kufurahisha sana njo itaanzisha serikali ya mupya yenye itatawala dunia kwa miaka 1 000.​—Ufu. 20:6.

MUJI WENYE UTUKUFU NA WAKATI WAKO WENYE KUYA

Ufunuo sura ya 21 inaonyesha kama muji wa mufano wa Yerusalemu Mupya ‘unashuka kutoka mbinguni kwa Mungu.’ Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moya, ule muji utaletea wanadamu watiifu baraka mingi sana (Ona fungu ya 14-16)

14-15. Ufunuo sura ya 21 inafananisha wale 144 000 na nini? (Ona picha ku jalada ya hii gazeti.)

14 Kisha, Ufunuo sura ya 21 inafananisha wale 144 000 na muji muzuri sana wenye unaitwa “Yerusalemu Mupya.” (Ufu. 21:2, 9) Ule muji unajengwa juu ya majiwe 12 ya musingi, na juu ya ile majiwe kunaandikwa “majina kumi na mbili ya mitume kumi na mbili wa Mwana-Kondoo.” Bila shaka Yohana anapendezwa sana na mambo yenye anaona. Juu ya nini? Juu anaona jina yake inaandikwa ku jiwe moya kati ya ile majiwe kumi na mbili. Ile ni pendeleo kubwa sana!​—Ufu. 21:10-14; Efe. 2:20.

15 Ule muji wa mufano uko tofauti na miji ingine yote. Uko na barabara kubwa za zahabu, milango mikubwa 12 ya lulu, na pia kuta na misingi yenye inapambwa na majiwe ya bei sana. Zaidi ya ile, urefu na upana wake na urefu wake kuenda juu viko sawa. (Ufu. 21:15-21) Lakini, inaonekana sawa vile kunakosa jambo fulani! Ona namna Yohana anaendelea kusema: “Sikuona hekalu ndani yake, kwa maana Yehova Mungu Mweza-Yote ndiye hekalu lake, na pia Mwana-Kondoo. Na ule muji hauna lazima ya jua wala mwezi ili kuuangazia, kwa maana utukufu wa Mungu uliuangazia, na taa yake ilikuwa ule Mwana-Kondoo.” (Ufu. 21:22, 23) Wale wenye wanafanyiza Yerusalemu Mupya watakuwa kabisa pamoya na Yehova. (Ebr. 7:27; Ufu. 22:3, 4) Njo maana Yehova na Yesu njo hekalu ya ule muji.

Ni nani watafaidika na mambo ya muzuri yenye inafananishwa na “muto” na “miti”? (Ona fungu ya 16-17)

16. Wanadamu watapata faida gani wakati wa utawala wa Miaka Elfu wa Ufalme wa Mungu?

16 Watiwa-mafuta wanafurahia sana kuwaza juu ya ule muji. Lakini wale wenye wako na tumaini ya kuishi hapa ku dunia nao pia wanapaswa kupendezwa na ule muji. Juu ya nini? Juu wakati wa utawala wa Miaka Elfu wa Ufalme wa Mungu, Yerusalemu Mupya italetea wanadamu baraka za mingi. Yohana anaona zile baraka ziko nashuka sawa “muto wa maji ya uzima” na kwenye pande zote mbili za ule muto kuko “miti ya uzima” yenye inatosha majani “ya kuponyesha mataifa.” (Ufu. 22:1, 2) Wanadamu wote wenye wataishi ile wakati watakuwa na pendeleo ya kufurahia ile mambo ya muzuri. Polepole, wanadamu wote wenye kumutii Mungu watafanywa kuwa wakamilifu. Hakutakuwa tena magonjwa, wala maumivu, wala machozi ya huzuni.​—Ufu. 21:3-5.

17. Vile Ufunuo 20:11-13 inaonyesha, ni nani watafaidika na Utawala wa Miaka Elfu Moya?

17 Ni nani watafaidika na ile mambo ya muzuri? Kwanza, ni kundi kubwa ya watu wenye wataokoka Armagedoni, pamoya na watoto wenye pengine watazaliwa mu dunia mupya. Lakini Ufunuo sura ya 20 inatuambia kama wafu watafufuliwa. (Soma Ufunuo 20:11-13.) Waaminifu “wenye haki” wenye walikufa zamani, pamoya na “wenye hawako wenye haki,” wenye hawakupata nafasi ya kujifunza kumuhusu Yehova, wataishi tena hapa ku dunia. (Mdo. 24:15; Yoh. 5:28, 29) Ni kusema kila mutu atafufuliwa na kuishi ku dunia mu Utawala wa Miaka Elfu Moya? Hapana. Watu waovu wenye walikatala kumutumikia Yehova mbele ya kufa hawatafufuliwa. Walikuwa na nafasi ya kumutumikia Yehova lakini walishindwa kuonyesha kama wanastahili kuishi milele mu Paradiso ku dunia.​—Mt. 25:46; 2 Te. 1:9; Ufu. 17:8; 20:15.

JARIBU YA MWISHO

18. Wanadamu watakuwa na hali gani ku mwisho wa miaka 1 000?

18 Ku mwisho wa miaka 1 000, wote wenye wataishi ku dunia watafanywa tena kuwa wakamilifu. Hakuna mutu mwenye atateseka juu ya zambi yenye tuliriti kutoka kwa Adamu. (Ro. 5:12) Laana ya zambi ya Adamu itaondolewa kabisa. Ni mu ile maana njo wale wenye watakuwa ku dunia ‘watakuwa wazima,’ ni kusema, watakuwa wakamilifu ku mwisho wa ile miaka 1 000.​—Ufu. 20:5.

19. Juu ya nini itaomba kukuwe jaribu ya mwisho?

19 Tunajua kama Yesu alibakia muaminifu-mushikamanifu hata kama Shetani alifanya yake yote juu ya kumujaribu. Lakini wanadamu wote wakamilifu watakuwa tayari kubakia waaminifu-washikamanifu ikiwa Shetani anapewa nafasi ya kuwajaribu? Kila mutu atapewa nafasi ya kujibia ile ulizo yeye mwenyewe wakati Shetani atafunguliwa ku mwisho wa ile miaka 1 000. (Ufu. 20:7) Wale wenye watabakia waaminifu wakati wa ile jaribu ya mwisho watapata uzima wa milele na watakuwa sasa na uhuru wa kweli. (Ro. 8:21) Wale wenye watamuasi Yehova wataharibiwa milele pamoya na Shetani na mashetani wake.​—Ufu. 20:8-10.

20. Unajisikia namna gani kisha kuzungumuzia maunabii ya muzuri yenye kuwa mu kitabu ya Ufunuo?

20 Unajisikia namna gani kisha kuzungumuzia mawazo fulani yenye kuwa mu kitabu ya Ufunuo? Bila shaka ile imefanya ukuwe na hamu ya kujionea namna ile maunabii itatimia, na unapenda kualika wengine wajiunge na ibada safi ya Mungu wetu. (Ufu. 22:17) Kisha kuzungumuzia hii mambo ya muzuri yenye itafanyika mu siku zenye ziko nakuya, bila shaka tunapenda kurudilia maneno ya mutume Yohana, mwenye alisema: “Amina! Kuja, Bwana Yesu.”​—Ufu. 22:20.

WIMBO 27 Kufunuliwa kwa Wana wa Mungu

[Maelezo ya chini]

^ Tumezungumuzia habari mbili zenye zinahusu kitabu ya Ufunuo, na hii njo habari ya tatu na ya mwisho. Vile tutaona mu hii habari, wale wenye wanabakia waaminifu kwa Yehova watapata furaha mu siku zenye ziko nakuya. Lakini wale wenye kumupinga Mungu na utawala wake, wataishia pabaya.