Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 20

Kitabu ya Ufunuo—Iko na Maana Gani kwa Maadui wa Mungu?

Kitabu ya Ufunuo—Iko na Maana Gani kwa Maadui wa Mungu?

“Yakawakusanya pamoja mahali kwenye kunaitwa katika Kiebrania Armagedoni.”​—UFU. 16:16.

WIMBO 150 Umutafute Mungu ili Akukomboe

KIFUPI YA HABARI *

1. Kitabu ya Ufunuo inatusaidia kuelewa nini juu ya watu wa Mungu?

 KITABU ya Ufunuo inaonyesha kama Ufalme wa Mungu umeanza kutawala mbinguni na kama Shetani ametupwa kutoka mbinguni. (Ufu. 12:1-9) Juu Shetani amefukuzwa mbinguni, kule kumekuwa amani, lakini ile imetuletea magumu. Juu ya nini? Juu Shetani iko na kasirani kali na iko nashambulia watumishi waaminifu wa Yehova hapa ku dunia.​—Ufu. 12:12, 15, 17.

2. Ni nini itatusaidia tuendelee kubakia waaminifu kwa Yehova?

2 Ni nini inaweza kutusaidia tuendelee kubakia waaminifu hata kama Shetani iko natushambulia? (Ufu. 13:10) Jambo moya ni kujua mambo yenye itafanyika mu siku zenye ziko nakuya. Kwa mufano, mu kitabu ya Ufunuo, mutume Yohana anazungumuzia baraka fulani zenye tutapata hivi karibuni. Kati ya zile baraka, kuko kuharibiwa kwa maadui wa Mungu. Tuzungumuzie sasa namna kitabu ya Ufunuo inatusaidia tutambue maadui wa Mungu na mambo yenye itawapata.

MAADUI WA MUNGU WANAZUNGUMUZIWA “KWA NJIA YA ALAMA”

3. Kitabu ya Ufunuo inatumia alama gani fulani?

3 Mu mustari tu wa kwanza, kitabu ya Ufunuo inatuambia kama habari yenye tunataka kusoma mu ile kitabu inazungumuziwa “kwa njia ya alama,” ni kusema, kwa njia ya mufano. (Ufu. 1:1) Mu ile habari, maadui wa Mungu wanafananishwa na wanyama fulani wa pori. Kwa mufano, Yohana anaona “munyama wa pori akipanda kutoka katika bahari.” Ule munyama iko na “pembe kumi (10) na vichwa saba.” (Ufu. 13:1) Kisha ule munyama, Yohana anaona “munyama mwingine wa pori akipanda kutoka katika dunia.” Ule munyama iko nasema sawa nyoka mukubwa na anafanya “moto ushuke kutoka mbinguni.” (Ufu. 13:11-13) Kisha, Yohana anaona munyama mwingine tofauti, “munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa,” mwenye iko anaongozwa na kahaba mwenye anaikala juu yake. Wale wanyama wa pori watatu wanafananisha maadui wenye kumupinga Yehova Mungu na Ufalme wake kwa muda murefu. Njo maana ni jambo ya maana tuwatambue.​—Ufu. 17:1, 3.

WANYAMA INE WAKUBWA

‘Wanatoka katika bahari.’ (Da. 7:1-8, 15-17) Wanafananisha serikali za ulimwengu zenye zilikuwa na matokeo makubwa juu ya watu wa Mungu kuanzia wakati wa Danieli (Ona fungu ya 4, 7)

4-5. Namna gani Danieli 7:15-17 inatusaidia kuelewa maana ya alama zenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Ufunuo?

4 Mbele tujue wale maadui ni nani, tunapaswa kwanza kuelewa maana ya ile maneno ya mufano. Juu tuielewe, tuache Biblia ifasirie. Maneno mingi ya mufano yenye inatumiwa mu kitabu ya Ufunuo tayari inafasiriwa mu vitabu vingine vya Biblia. Kwa mufano, nabii Danieli alilotaka ndoto, na mu ile ndoto aliona “wanyama ine (4) wakubwa sana walitoka katika bahari.” (Da. 7:1-3) Danieli anatusaidia kujua jambo yenye wale wanyama wakubwa wanafananisha. Wale wanyama wakubwa, wanafananisha “wafalme” ine, ao serikali ine. (Soma Danieli 7:15-17.) Ile mafasirio yenye kuwa wazi, inatusaidia kuelewa kama inawezekana wanyama wenye wanazungumuziwa mu Ufunuo nao pia wanafananisha serikali mbalimbali.

5 Tuchunguze sasa alama mbalimbali zenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Ufunuo. Wakati tunafanya vile, tutaona namna Biblia inatusaidia tujue maana ya zile alama. Tutaanza kwa kuzungumuzia wale wanyama wa pori. Kwanza tutaona wanafananisha nani. Kisha tutaona mambo yenye itawapata. Na ku mwisho, tutaona kama ile matukio iko na maana gani kwetu.

MAADUI WA MUNGU WANATAMBULISHWA

MUNYAMA WA PORI MWENYE KUWA NA VICHWA SABA

Anapanda “kutoka katika bahari” na iko na vichwa saba, pembe kumi, na mataji kumi. (Ufu. 13:1-4) Anafananisha serikali zote za ulimwengu zenye zimetawala wanadamu mu historia yote. Vichwa saba vinafananisha serikali saba za ulimwengu zenye zimekuwa na matokeo makubwa juu ya watu wa Mungu (Ona fungu ya 6-8)

6. Munyama wa pori mwenye vichwa saba mwenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 13:1-4 ni nani?

6 Munyama wa pori mwenye vichwa saba anafananisha nini? (Soma Ufunuo 13:1-4.) Sehemu kubwa ya ule munyama inafanana chui. Lakini miguu yake iko sawa ya dubu, kinywa yake iko sawa ya simba, na iko na pembe kumi. Zile sehemu zote zinafanana na wale wanyama ine wenye kuzungumuziwa mu Danieli sura ya 7. Lakini mu kitabu ya Ufunuo, munyama mumoja njo iko na zile sehemu zote. Ile inaonyesha kama huyu munyama wa pori hafananishe tu serikali moya ao utawala moya wa ulimwengu. Anazungumuziwa kuwa anatawala “juu ya kila kabila na watu na luga na taifa.” Njo maana utawala wake unapaswa kuwa mukubwa kuliko utawala wa serikali moya. (Ufu. 13:7) Kwa hiyo, bila shaka ule munyama wa pori anafananisha serikali zote za ulimwengu zenye zimetawala wanadamu mu historia yote. *​—Muh. 8:9.

7. Kila kichwa ya ule munyama wa pori mwenye vichwa saba inafananisha nini?

7 Kila kichwa ya ule munyama wa pori mwenye vichwa saba inafananisha nini? Ufunuo sura ya 17 inatusaidia kupata jibu. Ile sura inafasiria sanamu ya ule munyama mwenye kuzungumuziwa mu Ufunuo sura ya 13. Ufunuo 17:10 inasema hivi: “Kuko wafalme saba (7): Watano (5) wameanguka, mumoja iko, na ule mwingine bado hajafika; lakini wakati atafika, anapaswa kukaa wakati kidogo.” Kati ya serikali zote za ulimwengu zenye Shetani ametumia, serikali saba zimekuwa sawa “vichwa” juu zimekuwa na mamlaka zaidi. Zile serikali, ni serikali kubwa za ulimwengu zenye zimekuwa na matokeo makubwa juu ya watu wa Mungu. Mu siku za mutume Yohana, tayari serikali tano zilikuwa zilishatokea, ni kusema Misri, Ashuru, Babiloni, Umedi na Uajemi, na Ugiriki. Serikali ya sita, ni kusema, Roma, ilikuwa ingali natawala wakati Yohana aliona maono yenye kuwa mu kitabu ya Ufunuo. Kichwa ya saba, ao serikali kubwa ya ulimwengu ya saba na ya mwisho, ingekuwa nini?

8. Kichwa ya saba ya ule munyama wa pori inafananisha nini?

8 Unabii wenye uko mu kitabu ya Danieli unatusaidia tutambue kichwa ya saba, na njo ya mwisho, ya ule munyama wa pori. Ni serikali gani ya ulimwengu iko natawala mu hizi siku za mwisho, ni kusema, katika “siku ya Bwana”? (Ufu. 1:10) Ni muungano wa serikali mbili zenye kutumika kwa umoja, wenye unafanyizwa na Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika. Njo maana tunaweza kusema kama ile serikali njo kichwa ya saba ya ule munyama mwenye anatajwa mu Ufunuo 13:1-4.

MUNYAMA WA PORI MWENYE KUWA NA PEMBE MBILI KAMA MWANA-KONDOO

Anapanda “kutoka katika dunia” na anasema “kama ule nyoka mukubwa.” Anafanya “moto ushuke kutoka mbinguni” na anafanya alama kama “ule nabii wa uongo.” (Ufu. 13:11-15; 16:13; 19:20) Serikali kubwa ya Uingereza na Amerika inafananishwa na munyama mwenye kuwa na pembe mbili na anaitwa nabii wa uongo juu iko nadanganya wakaaji wa dunia, na iko nawaambia “watengeneze sanamu” ya “ule munyama wa pori” mwenye iko na vichwa saba na pembe kumi (Ona fungu ya 9)

9. Munyama wa pori mwenye “pembe mbili kama mwana-kondoo” anafananisha nini?

9 Ufunuo sura ya 13 inasema tena kama ile kichwa ya saba, ni kusema, Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika, inafananishwa pia na munyama wa pori mwenye ‘pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini [mwenye] alianza kusema kama ule nyoka mukubwa.’ Ule munyama “anafanya alama kubwa, anafanya hata moto ushuke kutoka mbinguni mupaka duniani mbele ya macho ya wanadamu.” (Ufu. 13:11-15) Ufunuo sura ya 16 na 19 inamuita “nabii wa uongo.” (Ufu. 16:13; 19:20) Danieli anazungumuzia jambo yenye kufanana na ile. Anaonyesha kama Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ‘ingeleta uharibifu mukubwa.’ (Da. 8:19, 23, 24, maelezo ya chini) Na ni vile mambo ilifanyika wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Bombe mbili za atomu zenye wanasayansi wa Uingereza na Amerika walitengeneza, zilisaidia sana juu ya kumaliza ile vita mu Pasifiki. Kwa kutengeneza zile bombe, Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika ilifanya “moto ushuke kutoka mbinguni mupaka duniani.”

MUNYAMA WA PORI MWENYE KUWA NA RANGI NYEKUNDU YENYE KUNGAA

Anaongozwa na kahaba, ni kusema, Babiloni Mukubwa. Ule munyama anazungumuziwa kuwa mufalme wa munane. (Ufu. 17:3-6, 8, 11) Ku mwanzo ule kahaba alikuwa anaongoza ule munyama wa pori, lakini kisha ule munyama wa pori anamuharibu ule kahaba. Ule kahaba anafananisha dini zote za uongo. Leo, ule munyama anafananisha Umoja wa Mataifa, wenye uko nasaidia kuendeleza mufumo wa mambo ya politike (Ona fungu ya 10, 14-17)

10. “Sanamu ya ule munyama wa pori” inafananisha nini? (Ufunuo 13:14, 15; 17:3, 8, 11)

10 Kisha, Yohana anaona munyama mwingine wa pori. Huyu munyama iko tu karibu sawa na ule munyama wa pori mwenye vichwa saba. Tofauti tu ni kwamba iko na rangi nyekundu yenye kungaa. Anaitwa “sanamu ya ule munyama wa pori” na anazungumuziwa kuwa “mufalme wa munane.” * (Soma Ufunuo 13:14, 15; 17:3, 8, 11.) Huyu “mufalme” anazungumuziwa kuwa alitokea, kisha akapotea, na kisha tena akatokea. Ile maelezo inafaa kabisa kuhusiana na Umoja wa Mataifa, wenye uko nasaidia kuendeleza mufumo wa mambo ya politike! Ku mwanzo, uliitwa Ushirika wa Mataifa, kisha ukapotea wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, kisha ukatokea tena na ukakuwa Umoja wa Mataifa.

11. Wale wanyama wa pori wako nachochea watu kufanya nini, na juu ya nini hatupaswe kuwaogopa?

11 Wale wanyama wa pori, ni kusema serikali mbalimbali za ulimwengu, wanatumia propaganda juu ya kuchochea watu wamupinge Yehova na watu wake. Kwa njia ya mufano, wanakusanya pamoya “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” kwenye vita ya Armagedoni, yenye ni “siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu. 16:13, 14, 16) Lakini hatutakuwa na lazima ya kuogopa. Mungu wetu mukubwa, Yehova, atatenda bila kuchelewa juu ya kuokoa wale wote wenye wanaunga mukono utawala wake.​—Eze. 38:21-23.

12. Ni nini itawapata wale wanyama wote?

12 Ni nini itawapata wale wanyama wote? Ufunuo 19:20 inatupatia jibu: “Ule munyama wa pori akakamatwa, na pamoja naye ule nabii wa uongo mwenye alifanya mbele yake alama zenye alitumia ili kupotosha wale wenye walipokea alama ya ule munyama wa pori na wale wenye kuabudu sanamu yake. Wakiwa wangali wazima, wote wawili walitupwa ndani ya ziwa la moto lenye linawaka kwa kiberiti.” Kwa hiyo, wakati zile serikali zenye kumupinga Mungu zitakuwa zingali natawala, Mungu ataziharibu lote.

13. Serikali za wanadamu ziko nakaza Wakristo wafanye nini?

13 Ile iko na maana gani kwetu? Siye Wakristo tunapaswa kuwa washikamanifu kwa Mungu na Ufalme wake. (Yoh. 18:36) Juu ya kufanya vile tunapaswa kuepuka kuunga mukono upande wowote mu mambo ya politike ya huu ulimwengu. Lakini kufanya vile inaweza kuwa nguvu sana, juu serikali za ulimwengu zinapenda tuziunge mukono kabisa kwa maneno na matendo. Wale wenye wanaziunga mukono, wanapata alama ya ule munyama wa pori. (Ufu. 13:16, 17) Lakini, Yehova hawezi kumukubali mutu yeyote mwenye anapata ile alama. Na ule mutu hatapata uzima wa milele. (Ufu. 14:9, 10; 20:4) Kwa hiyo, ni jambo ya maana sana kwetu kuendelea kuepuka kuunga mukono upande fulani mu mambo ya politike, hata serikali zitukaze namna gani kufanya vile!

ULE KAHABA MUKUBWA ANAISHIA PABAYA

14. Kulingana na Ufunuo 17:3-5, mutume Yohana anaona jambo gani ingine yenye kushangaza?

14 Mutume Yohana anazungumuzia jambo ingine yenye aliona. Na wakati aliona ile jambo, ‘alishangaa sana.’ Ni jambo gani ile? Mwanamuke alikuwa naongoza wale wanyama wakali. (Ufu. 17:1, 2, 6) Ule mwanamuke anafananishwa na “kahaba mukubwa” na anaitwa “Babiloni Mukubwa.” Anafanya “uasherati” na “wafalme wa dunia.”​—Soma Ufunuo 17:3-5.

15-16. “Babiloni mukubwa ni nani,” na namna gani tunajua vile?

15 “Babiloni Mukubwa” ni nani? Huyu mwanamuke hawezi kufananisha matengenezo ya politike, juu Biblia inasema kama iko nafanya uasherati na viongozi wa politike wa hii dunia. (Ufu. 18:9) Kusema kweli, kwa njia ya mufano anaikala juu yao, ni kusema, iko nafanya yake yote juu awaongoze. Tena, hawezi kufananisha matengenezo ya kibiashara yenye pupa ya huu ulimwengu wa Shetani. Ile matengenezo inazungumuziwa fasi ingine mu kitabu ya Ufunuo, na inaitwa “wafanyabiashara wa dunia.”​—Ufu. 18:11, 15, 16.

16 Wakati fulani Biblia inatumia neno “kahaba” juu ya kuzungumuzia wale wenye wanasema kama wanamutumikia Mungu, lakini wako naabudu sanamu ao kwa njia fulani wanakuwa marafiki wa ulimwengu. (1 Nya. 5:25; Yak. 4:4) Tofauti na ile, Biblia inaita wale wenye wanamutumikia Mungu kwa uaminifu kuwa wenye “mwenendo safi” ao “bikira.” (2 Ko. 11:2; Ufu. 14:4) Mu muji wa zamani wa Babiloni watu walikuwa nafanya ibada ya uongo sana kuliko fasi ingine yoyote. Njo maana tunaweza kusema kama Babiloni Mukubwa anafananisha aina zote za ibada ya uongo, ni kusema anafananisha dini zote za uongo.​—Ufu. 17:5, 18; soma ku jw.org habari yenye kichwa “Babiloni Mukubwa ni Nani?

17. Ni nini itamupata Babiloni Mukubwa?

17 Ni nini itamupata Babiloni Mukubwa? Ufunuo 17:16, 17 inajibia ile ulizo kwa kusema hivi: “Zile pembe kumi (10) zenye uliona, na ule munyama wa pori, hawa watamuchukia ule kahaba na kumuacha bila kitu na uchi, na watakula nyama yake na kumuteketeza kabisa kwa moto. Kwa maana Mungu alitia jambo hilo ndani ya mioyo yao ili kutimiza wazo lake.” Ndiyo, Yehova atachochea mataifa itumie ule munyama wa pori mwenye rangi nyekundu yenye kungaa, ni kusema Umoja wa Mataifa, juu ageukie dini zote za uongo na kuziharibu kabisa.​—Ufu. 18:21-24.

18. Tunapaswa kufanya nini juu ya kuonyesha kama hatuunge mukono Babiloni Mukubwa?

18 Ile iko na maana gani kwetu? Tunapaswa kuendelea kushikamana na “namna ya ibada yenye kuwa safi na yenye haina uchafu kwa maoni ya Mungu wetu.” (Yak. 1:27) Tunapaswa kuepuka kabisa mafundisho ya uongo na sherehe za kipagani za Babiloni Mukubwa. Na hatupendi kuwa sawa watu wa dini za uongo wenye hawafuate kanuni za juu za mwenendo na wenye wako wanajiingiza mu mambo ya uchawi. Zaidi ya ile, ni jambo ya maana tuendelee kusaidia watu ‘watoke kwake’ juu Mungu asiwaone kuwa wenye makosa kwa sababu ya zambi zake.​—Ufu. 18:4.

ADUI MUKUBWA WA MUNGU ANAHUKUMIWA

NYOKA MUKUBWA WA RANGI YA MOTO

Shetani anapatia ule munyama wa pori mamlaka. (Ufu. 12:3, 9, 13; 13:4; 20:2, 10) Shetani, adui mukubwa wa Yehova, atatupwa mu abiso kwa muda wa miaka 1 000. Kisha pale, Shetani atatupwa mu “ziwa la moto na kiberiti” (Ona fungu ya 19-20)

19. “Nyoka mukubwa wa rangi ya moto” ni nani?

19 Kitabu ya Ufunuo inazungumuzia pia “nyoka mukubwa wa rangi ya moto.” (Ufu. 12:3) Ule nyoka mukubwa anapigana na Yesu na malaika zake. (Ufu. 12:7-9) Anashambulia watu wa Mungu na anapatia nguvu wale wanyama wa pori, ni kusema, serikali za wanadamu. (Ufu. 12:17; 13:4) Ule nyoka mukubwa ni nani? Ni “ule nyoka wa zamani, mwenye kuitwa Ibilisi na Shetani.” (Ufu. 12:9; 20:2) Yeye njo iko nyuma ya maadui wengine wote wa Yehova.

20. Ni nini itamupata ule nyoka mukubwa?

20 Ni nini itamupata ule nyoka mukubwa? Ufunuo 20:1-3 inasema kama malaika atamutupa Shetani mu abiso, yenye iko sawa vile gereza mwenye hatakuwa na uwezo wa kufanya jambo yoyote. Wakati Shetani atakuwa mu abiso, ‘hatapotosha mataifa tena mupaka wakati ile miaka elfu moja (1 000) itaisha.’ Ku mwisho, Shetani na mashetani wake wataharibiwa lote. Kwa njia ya mufano, ni sawa vile watatupwa mu “ziwa la moto na kiberiti.” (Ufu. 20:10) Waza kidogo namna dunia itakuwa wakati Shetani na mashetani wake hawatakuwa tena. Maisha itakuwa muzuri sana!

21. Juu ya nini tunapaswa kufurahia mambo yenye tumetoka kuzungumuzia, yenye kuwa mu kitabu ya Ufunuo?

21 Kuelewa maana ya alama zenye kitabu ya Ufunuo inazungumuzia ni jambo yenye kutia moyo sana! Zaidi ya kutambua maadui wa Yehova, tumeona mambo yenye itawapata. Ndiyo, “mwenye furaha ni ule mwenye anasoma kwa sauti na wale wenye wanasikia maneno ya unabii huu”! (Ufu. 1:3) Lakini kisha tu maadui wa Mungu kuharibiwa, wanadamu waaminifu watapata baraka gani? Ile njo tutazungumuzia mu habari yenye kufuata.

WIMBO 23 Yehova Anaanza Kutawala

^ Kitabu ya Ufunuo inatumia alama juu ya kutusaidia tutambue maadui wa Mungu. Kitabu ya Danieli inatusaidia tuelewe maana ya zile alama. Mu hii habari tutalinganisha unabii fulani wenye uko mu kitabu ya Danieli na unabii wenye kufanana nao, wenye uko mu kitabu ya Ufunuo. Kufanya vile kutatusaidia tutambue maadui wa Mungu. Kisha, tutazungumuzia mambo yenye itawapata.

^ Jambo ingine yenye inaonyesha kama ule munyama wa pori mwenye vichwa saba anafananisha serikali zote ni kwamba iko na “pembe kumi.” Mara mingi, namba kumi inatumiwa mu Biblia juu ya kuzungumuzia jambo yenye kuwa kamili, ni kusema yenye kuenea.

^ Tofauti na ule munyama wa kwanza, ile sanamu haina “mataji” kwenye mapembe yake. (Ufu. 13:1) Juu ya nini? Ni juu ile sanamu inatokana na wale wafalme wengine saba, na ni wao njo wanaipatia mamlaka.​—Soma ku jw.org habari yenye kichwa “Mnyama-Mwitu Mwenye Rangi Nyekundu wa Ufunuo Sura ya 17 Ni Nini?