Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 22

Mashauri ya Hekima Yenye Inaweza Kutusaidia mu Maisha

Mashauri ya Hekima Yenye Inaweza Kutusaidia mu Maisha

“Yehova mwenyewe anatoa hekima.”​—MEZ. 2:6.

WIMBO 89 Tii juu Ubarikiwe

KIFUPI YA HABARI *

1. Juu ya nini tuko na lazima ya hekima yenye inatoka kwa Mungu? (Mezali 4:7)

 KUKO siku iliombaka ukamate uamuzi wa maana sana? Bila shaka, uliombaka Yehova akupatie hekima. Na kusema kweli, njo vile tu ulipaswa kufanya. (Yak. 1:5) Mufalme Sulemani aliandika hivi: “Hekima ndilo jambo la maana zaidi.” (Soma Mezali 4:7.) Kusema kweli, Sulemani hakukuwa anazungumuzia hekima ya wanadamu. Alikuwa anazungumuzia hekima yenye inatoka kwa Yehova Mungu. (Mez. 2:6) Lakini hekima yenye inatoka kwa Mungu inaweza kutusaidia mu magumu yenye tunapata leo? Ndiyo kabisa, na njo vile tutaona mu hii habari.

2. Ni jambo gani moya yenye inaweza kutusaidia tukuwe na hekima ya kweli?

2 Jambo moya yenye inaweza kutusaidia tukuwe na hekima ya kweli ni kujifunza na kutumikisha mambo yenye wanaume wawili, wenye walikuwa na hekima sana, walifundisha. Kwanza, tutazungumuzia Sulemani. Biblia inasema kama ‘Mungu alimupatia Sulemani hekima na utambuzi kwa wingi sana.’ (1 Fa. 4:29) Kisha, tutazungumuzia Yesu, mwenye alikuwa na hekima kupita mwanadamu yeyote. (Mt. 12:42) Biblia ilisema hivi juu ya Yesu: “Roho ya Yehova itakaa juu yake, roho ya hekima na ya uelewaji.”​—Isa. 11:2.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Juu Mungu alipatia Sulemani na Yesu hekima, walifikia kutoa mashauri juu ya mambo ya maana, yenye inatuhusu siye wote leo. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo tatu kati ya ile mambo. Tutaona juu ya nini ni jambo ya maana kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya makuta, juu ya kazi ya kimwili, na juu yetu wenyewe.

MAWAZO YENYE KUFAA JUU YA MAKUTA

4. Hali ya maisha ya Sulemani ilikuwa sawa na ya Yesu? Fasiria.

4 Sulemani alikuwaka tajiri sana na aliishi mu nyumba ya muzuri sana. (1 Fa. 10:7, 14, 15) Yesu yeye hakukuwaka na vitu mingi vya kimwili na hakukuwaka hata na nyumba. (Mt. 8:20) Lakini, wote wawili walikuwa na mawazo yenye kufaa juu ya vitu vya kimwili, juu hekima yenye wote wawili walikuwa nayo ilitoka kwa Yehova Mungu.

5. Sulemani alikuwa na mawazo gani yenye kufaa juu ya makuta?

5 Sulemani alijua kama makuta ni “ulinzi.” (Muh. 7:12) Kama tuko na makuta, tunaweza kupata mambo yenye tuko nayo lazima kabisa juu ya kuishi na mambo ingine yenye tunapendaka tu. Lakini, hata kama Sulemani alikuwa tajiri sana, alitambua kama kuko mambo ya maana sana kuliko makuta. Kwa mufano, aliandika hivi: “Inafaa kuchagua jina la muzuri [ao, “sifa ya muzuri,” maelezo ya chini] kuliko kuchagua mali nyingi.” (Mez. 22:1) Sulemani alijionea pia kama watu wenye wanapenda makuta, mara mingi hawatoshekake nayo. (Muh. 5:10, 12) Na alisema kama hatupaswe kuwaza kama makuta njo jambo ya maana sana mu maisha, juu hata tukuwe na makuta ngapi, inaweza tu kupotea mu wakati kidogo.​—Mez. 23:4, 5.

Namna tunaonaka vitu vya kimwili inafanya tusitie kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza? (Ona fungu ya 6-7) *

6. Yesu alikuwa na mawazo gani yenye kufaa juu ya vitu vya kimwili? (Matayo 6:31-33)

6 Yesu alikuwa na mawazo yenye kufaa juu ya vitu vya kimwili. Alifurahia kula na kunywa. (Lu. 19:2, 6, 7) Siku moya, alifanya divai ya muzuri sana. Ile njo ilikuwa muujiza wake wa kwanza. (Yoh. 2:10, 11) Tena, siku yenye alikufaka alikuwaka amevala nguo ya bei sana. (Yoh. 19:23, 24) Lakini Yesu hakuachaka vitu vya kimwili vikamate nafasi ya kwanza mu maisha yake. Aliambia wanafunzi wake hivi: “Hakuna mutu mwenye anaweza kutumikia mabwana wawili . . . Hamuwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.” (Mt. 6:24) Yesu alifundisha kama ikiwa tunatafuta kwanza Ufalme, Yehova atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima.​—Soma Matayo 6:31-33.

7. Ndugu moya alipataka faida gani juu alikuwa na mawazo yenye kufaa juu ya makuta?

7 Ndugu na dada wengi wamepata faida kwa kutumikisha mashauri ya Mungu yenye hekima kuhusu makuta. Fikiria mufano wa ndugu moya mwenye hayaoa, mwenye kuitwa Daniel. Anasema hivi: “Wakati nilikuwa kijana, niliamua kama nitatia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza mu maisha yangu.” Juu Daniel alifanya maisha yake ikuwe mwepesi, ile ilimusaidia atumie wakati na ufundi wake juu ya kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova. Anasema tena hivi: “Naweza kusema kwa moyo mweupe kama, sihuzunike hata kidogo juu ya uamuzi wenye nilikamataka. Kusema kweli, kama ningesemaka makuta njo ikuwe jambo ya maana mu maisha yangu, pengine ningepataka makuta mingi. Lakini ile makuta haingenipatia marafiki wazuri wenye niko nao leo. Tena haingenipatia furaha yenye niko napata juu niko natia kazi ya Ufalme pa nafasi ya kwanza. Kusema kweli, Yehova amenipatia baraka mingi sana zenye singepataka hata nikuwe na makuta ngapi.” Ni wazi kama, tunapata faida mingi wakati tunakaza akili yetu juu ya mambo ya kiroho kuliko kukaza akili yetu juu ya makuta.

MAWAZO YENYE KUFAA JUU YA KAZI YA KIMWILI

8. Tunajua namna gani kama Sulemani alikuwa na mawazo yenye kufaa juu ya kazi? (Muhubiri 5:18, 19)

8 Sulemani alisema kama furaha yenye tunapata wakati tunatumika kwa bidii ni “zawadi ya Mungu.” (Soma Muhubiri 5:18, 19.) Aliandika hivi: “Kila namna ya kazi ya nguvu iko na faida.” (Mez. 14:23) Sulemani alijua muzuri mambo yenye alikuwa nasema, juu alikuwa mufanyakazi mwenye bidii. Alijenga manyumba, alipanda mashamba ya mizabibu, na alitengeneza bustani za mingi na viziwa vya maji. Alijenga pia miji. (1 Fa. 9:19; Muh. 2:4-6) Ile ilikuwa kazi kubwa, na bila shaka ilimusaidia akuwe na furaha kwa kiasi fulani. Lakini, Sulemani alijua kama juu akuwe na furaha ya kweli alipaswa kufanya mambo ingine. Njo maana, alijitoa pia mu kazi ya Yehova. Kwa mufano, aliongoza kazi ya kujenga hekalu yenye utukufu kwa ajili ya ibada ya Yehova. Ile ilikuwa kazi kubwa yenye ilikamata miaka saba! (1 Fa. 6:38; 9:1) Kisha kufanya kazi mbalimbali za kimwili na za kiroho, Sulemani alitambua kama kazi ya kiroho ni ya maana zaidi kuliko kazi ya kimwili. Aliandika hivi: “Huu ndio mwisho wa jambo, mambo yote yamekwisha kusikiwa: Ogopa Mungu wa kweli na ushike amri zake.”​—Muh. 12:13.

9. Ni nini inaonyesha kama Yesu alikuwa na mawazo yenye kufaa juu ya kazi ya kimwili?

9 Yesu alikuwa anatumika kwa bidii. Wakati alikuwa kijana, alikuwa seremala. (Mk. 6:3) Bila shaka, wazazi wake walifurahia kuona namna aliwasaidia wakati walikuwa wanajikaza kutimiza mahitaji ya familia yao yenye ilikuwa na watoto wengi. Juu Yesu alikuwa mukamilifu, bila shaka watu wengi walipenda awafanyie kazi! Na inawezekana kabisa kama Yesu alifurahia kazi yake. Lakini, hata wakati alikuwa anafanya kazi ya kimwili, Yesu alikuwa anapanga wakati wa kufanya mambo ya kiroho. (Yoh. 7:15) Kisha, wakati alianza utumishi wa wakati wote, aliambia hivi watu wenye walikuwa wanamusikiliza: “Musifanye kazi kwa ajili ya chakula chenye kinaharibikaka, lakini mufanye kazi kwa ajili ya chakula chenye kinadumu kwa ajili ya uzima wa milele.” (Yoh. 6:27) Na mu Mahubiri yake Kwenye Mulima, Yesu alisema hivi: “Mujiwekee hazina mbinguni.”​—Mt. 6:20.

Namna gani tunaweza kuendelea kuwa na usawaziko kati ya kazi yetu ya kimwili na mambo ya kiroho? (Ona fungu ya 10-11) *

10. Wakristo fulani wanaweza kuwa na magumu gani mu kazi yao ya kimwili?

10 Hekima yenye kutoka kwa Mungu, inatusaidia tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya kazi ya kimwili. Biblia inatushauria tufanye “kazi kwa bidii . . . , kazi ya muzuri.” (Efe. 4:28) Mara mingi, wakubwa wa kazi wanaonaka kama hatuibake na tunatumikaka kwa bidii, na wanatuambiaka kama wanafurahia namna tunatumika. Kama hatuko waangalifu, ile inaweza kufanya tuanze kutumika kisha saa za kazi juu tunawaza kama ile inaweza kusaidia mukubwa wetu wa kazi aendelee kuwa na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova. Kisha, tunaweza kuanza kukosa kukamata kwa uzito madaraka yetu ya familia na mambo ya kiroho. Kama ni vile, tunapaswa kufanya mabadiliko, ni kusema, tunapaswa kuwa na usawaziko.

11. Ndugu moya alijifunzaka nini juu ya kuwa na mawazo yenye kufaa kuhusu kazi?

11 Ndugu moya kijana, mwenye kuitwa William, alijionea kama ni jambo ya maana kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya kazi ya kimwili. Zamani alikuwa natumikia ndugu moya muzee wa kutaniko. William anasema hivi juu yake: “[Ule ndugu] ni mufano muzuri juu anakuwaka na usawaziko mu kazi yake. Anatumikaka kwa bidii. Na juu anatumikaka muzuri, anasikilizanaka na watu wenye anafanyia kazi. Lakini wakati saa ya kufunga kazi inaenea, anaachaka mambo ya kazi, na kisha anapitisha wakati pamoya na watu wa familia yake na anafanya mambo ya kiroho. Kusema kweli, ule ndugu iko kati ya watu wenye furaha sana wenye ninajua!” *

MAWAZO YENYE KUFAA JUU YETU WENYEWE

12. Namna gani Sulemani alionyesha kama alikuwa na mawazo yenye kufaa juu yake mwenyewe, na namna gani alifikia kubadilika?

12 Wakati alikuwa mutumishi muaminifu wa Yehova, Sulemani alikuwa na mawazo yenye kufaa juu yake mwenyewe. Wakati alikuwa kijana, alikuwa mwenye kiasi na alitambua mipaka yake. Njo maana, alimuomba Yehova amuongoze. (1 Fa. 3:7-9) Ku mwanzo wa utawala wake, Sulemani alitambua pia kama kuwa na kiburi kunaweza kuwa na matokeo ya mubaya. Aliandika hivi: “Kiburi kinatangulia kuanguka, na roho yenye majivuno inatangulia kujikwaa.” (Mez. 16:18) Lakini, inahuzunisha kuona kama kisha, Sulemani alishindwa kutumikisha shauri yenye yeye mwenyewe aliandika. Wakati fulani kisha yeye kuwa mufalme, alifikia kuwa na kiburi na akaanza kukosa kutii sheria za Mungu. Kwa mufano, sheria moya ilisema kama mufalme Mwebrania hakupaswa “kujichukulia bibi wengi, ili moyo wake usipotoke.” (Kum. 17:17) Lakini Sulemani alikosa kutii ile sheria, alioa wanamuke 700 na akakuwa na masuria 300, na wengi kati yao walikuwa wapagani! (1 Fa. 11:1-3) Pengine Sulemani aliwaza kama ile haingekuwa na matokeo ya mubaya. Ikuwe aliwaza vile ao hapana, tunajua kama ku mwisho Sulemani alipata matokeo ya mubaya juu alifikia kuwa na kiburi na akamuacha Yehova.​—1 Fa. 11:9-13.

13. Tunajifunza nini wakati tunafikiri sana juu ya unyenyekevu wa Yesu?

13 Yesu aliendelea kuwa na mawazo yenye kufaa juu yake mwenyewe. Mbele akuye ku dunia, Yesu alifanya mambo mingi ya muzuri mu kazi ya Yehova. Kupitia Yesu “vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani.” (Kol. 1:16) Wakati alibatizwa, bila shaka Yesu alikumbuka mambo yenye alikuwa ametimiza wakati alikuwa na Baba yake. (Mt. 3:16; Yoh. 17:5) Lakini ile haikufanya Yesu akuwe na kiburi. Na hakujiona kuwa wa maana kuliko wengine. Aliambia wanafunzi wake kama, hakukuya ku dunia “ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine na atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.” (Mt. 20:28) Tena juu alikuwa na kiasi, Yesu alitambua kama hangejiamulia hata jambo moya yeye mwenyewe. (Yoh. 5:19) Kwa kweli, Yesu alikuwa munyenyekevu kabisa na alituachia siye wote mufano muzuri sana.

14. Namna gani maneno yenye Yesu aliambia wanafunzi wake inaweza kutusaidia tukuwe na mawazo yenye kufaa juu yetu wenyewe?

14 Yesu alishauria wanafunzi wake wakuwe na mawazo yenye kufaa juu yao wenyewe. Siku moya, aliwaambia hivi: “Nywele zote za vichwa vyenu zimehesabiwa.” (Mt. 10:30) Ile maneno inatutia moyo kabisa, zaidi sana kama tunawazaka kuwa hatuko wa maana. Ile maneno inaonyesha kama Baba yetu wa mbinguni anatuhangaikia sana na anatuona kuwa wa maana. Hatupaswe hata kidogo kuwaza kama hatuko wa maana kwa Yehova na kama hatustahili kumutumikia ao kuingia mu dunia mupya.

Kujiona kuwa wa maana sana kunaweza kutukosesha mambo gani ya muzuri? (Ona fungu ya 15) *

15. (a) Munara wa Mulinzi moya ilitupatia shauri gani kuhusu kuwa na mawazo yenye kufaa juu yetu wenyewe? (b) Vile picha yenye iko ku ukurasa wa 24 inaonyesha, ni mambo gani ya muzuri tunaweza kukosa kama tunajiona kuwa wa maana sana?

15 Kumepita miaka 15 hivi, Munara wa Mulinzi moya ilitoaka hii shauri kuhusu kuwa na mawazo yenye kufaa juu yetu wenyewe: “Hatupaswe kujiona kuwa wa maana sana na kufikia kuanza kuwa na kiburi. Lakini pia, hatupaswe kujiona kuwa wa bure na kufikia hata kuvunjika moyo. Tofauti na ile, tunapaswa kujikaza kuwa na mawazo yenye kufaa juu yetu wenyewe. Ni kusema tunapaswa kukumbuka kama tuko na uwezo mbalimbali na tuko pia na uzaifu. Mwanamuke moya Mukristo alisemaka hivi juu ya ile: ‘Siko mutu mubaya sana kuliko wengine wala siko mutu muzuri sana kuliko wengine. Niko na sifa za muzuri na niko na uzaifu pia, na njo vile tu kila mutu anakuwaka.’” * Ile habari inatusaidia tuelewe juu ya nini ni jambo ya maana tukuwe na mawazo yenye kufaa juu yetu wenyewe.

16. Juu ya nini Yehova anatupatia muongozo wenye hekima?

16 Yehova anatupatia muongozo wenye hekima mu Neno yake. Anafanya vile juu anatupenda na anapenda tukuwe na furaha. (Isa. 48:17, 18) Uamuzi muzuri zaidi wenye tunaweza kukamata mu maisha yetu ni kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza. Ile njo jambo yenye inaweza kutuletea furaha ya kweli mu maisha. Kama tunafanya vile, tutaepuka magumu mingi yenye inafikiaka watu wenye wanapenda sana makuta na kazi ya kimwili, na wenye wanajipenda wenyewe sana. Siye wote tuazimie basi kuwa na hekima na kufurahisha moyo wa Yehova!​—Mez. 23:15.

WIMBO 94 Aksanti Yehova kwa Kutupatia Neno Yako

^ Sulemani na Yesu walikuwa na hekima sana. Yehova Mungu njo aliwapatia ile hekima. Mu hii habari, tutaona namna mashauri yenye kuongozwa na roho, yenye Sulemani na Yesu walitoa, inaweza kutusaidia. Ile mashauri inahusu kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya makuta, juu ya kazi ya kimwili, na juu yetu wenyewe. Tutaona pia namna Wakristo wenzetu wamepata faida juu walitumikisha mashauri ya Biblia mu ile mambo tatu.

^ Ona habari yenye kichwa “Namna ya Kufurahia Kazi Ngumu” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 2, 2015.

^ Ona habari “Biblia Inaweza Kukusaidia Upate Shangwe” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 8, 2005.

^ MAFASIRIO YA PICHA: John na Tom ni ndugu vijana wenye wako mu kutaniko moya. John anapitisha wakati mingi juu ya kuhangaikia motokari yake. Tom anatumia motokari yake juu ya kupeleka wengine mu mahubiri na ku mikutano.

^ MAFASIRIO YA PICHA: John iko natumika kisha saa za kazi. Hapendi kumuhuzunisha mukubwa wake wa kazi. Njo maana, kila mara wakati mukubwa wake wa kazi anamuomba atumike kisha saa za kazi anaitikaka tu. Mangaribi ileile, Tom mwenye ni mutumishi wa huduma, anasindikiza muzee mu ziara ya uchungaji. Tom aliambiaka mukubwa wake wa kazi kama mara mingi atakuwa napitisha wakati wa mangaribi mu kazi ya Yehova.

^ MAFASIRIO YA PICHA: John anajiona kuwa wa maana sana. Tom, aliamua kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza. Ile inamusaidia apate marafiki wengi wakati iko nasaidia mu kazi ya kurekebisha Jumba ya Mukusanyiko.