Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Nilimuacha Yehova Aongoze Njia Yangu

Nilimuacha Yehova Aongoze Njia Yangu

WAKATI nilikuwa kijana, nilijichagulia njia yangu. Nilichagua kazi fulani yenye nilipenda sana. Lakini, Yehova alinichagulia njia ingine. Ni sawa vile aliniambia hivi: “Nitakupatia ufahamu na kukufundisha katika njia yenye unapaswa kufuata.” (Zb. 32:8) Juu nilimuacha Yehova aongoze njia yangu, nimeweza kutumia maisha yangu mu kazi yake na nilipata baraka nyingi, kutia ndani miaka 52 ya utumishi mu Afrika.

KUTOKA BLACK COUNTRY MUPAKA INCHI YENYE KUCHANGAMUKA YA AFRIKA

Nilizaliwa mu 1935 mu Darlaston, sehemu ya Black Country yenye ni eneo ya Angleterre. Iliitwa Black Country juu ya moshi wenye uliyala mu anga juu ya izine zenye kupatikana kule. Wakati nilikuwa na miaka ine hivi, wazazi wangu walianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Na wakati nilikuwa na miaka kati ya 14 na 15, nilivumbula kweli na nikabatizwa mu 1952 na miaka 16.

Ni mu ileile wakati njo nilianza kujifunza mambo ya biashara mu izine fulani kubwa yenye ilikuwa natengeneza vyombo vya kufanya navyo kazi za mikono na pia sehemu za magari. Nilianza kupata mazoezi juu nikuwe sekretere mu kompanyi fulani, na nilipenda sana ile kazi.

Iliniomba kukamata uamuzi wa maana sana wakati mwangalizi mwenye kusafiri aliniomba nianze kuongoza funzo ya kitabu mu kutaniko yetu ya Willenhall. Nilikosa nifanye nini. Ile wakati, nilikuwa nakusanyikia mu makutaniko mbili. Wakati tulikuwa na mukutano siku moya kati ya Siku ya Kwanza mupaka Siku ya Tano, nilikuwa nakusanyikia mu kutaniko ya karibu na fasi kwenye nilikuwa natumikia mu Bromsgrove, kilometre 32 hivi na ku nyumba. Na ku mwisho wa juma, wakati nilikuwa naenda kuona wazazi wangu, nilikuwa nakusanyikia mu kutaniko ya Willenhall.

Juu nilipenda kutegemeza tengenezo ya Yehova, nilikubali ombi ya ule mwangalizi wa muzunguko, hata kama ile ingeomba niache kazi yenye nilikuwa napenda sana. Hakuna siku nilishakajuta uamuzi wenye nilikamataka wa kuacha Yehova aongoze njia yangu juu ulinisaidia nikuwe na maisha ya muzuri sana.

Wakati nilikusanyikia mu kutaniko ya Bromsgrove, nilikutana na Anne, dada mwenye kuvutia, na mwenye kupenda sana mambo ya kiroho. Tulioana mu 1957, na tulitumikia migao mbalimbali mu tengenezo ya Yehova, sawa vile kuwa mapainia wa kawaida, mapainia wa pekee, kazi ya muzunguko na kazi ya Beteli. Anne amefanya nikuwe na furaha mu maisha yangu yote.

Mu 1966, tulifurahi sana kuhuzuria darasa ya 42 ya Masomo ya Gileadi. Tulitumwa Malawi, yenye kujulikana kuwa inchi yenye kuchangamuka mu Afrika juu watu ni wenye fazili na wakaribishaji. Lakini, hatukutazamia kama tungebakia kule siku mingi.

KUTUMIKIA MALAWI WAKATI YA MUVURUGO

Gari ya aina ya Kaiser Jeep yenye tulitumia mu kazi ya muzunguko mu Malawi

Tulifika Malawi tarehe 1, Mwezi wa 2, 1967. Mu mwezi wa kwanza, tulipitisha wakati yetu mingi mu kujifunza luga, na kisha tulianza kazi ya wilaya. Tulikuwa natembea mu gari ya aina ya Kaiser Jeep yenye watu fulani waliwaza kama inaweza kutembea fasi yote, hata kupita mu mito. Lakini, ile haikukuwa kweli. Tulikuwa naweza tu kutembea mu muto wenye haukukuwa na maji mingi. Wakati fulani, tuliishi mu nyumba za kidogo zenye kujengwa na udongo. Na wakati tulikuwa mu kipindi ya mvua, iliomba tutie hema juu ya nyumba ili maji isiingie. Ni vile njo tulianza kazi yetu ya umisionere, lakini tuliipenda!

Mu Mwezi wa 4, nilitambua kama karibuni, tungekuwa na matatizo na serikali. Nilisikia ku radio hotuba ya raisi wa Malawi, Hastings Banda. Alitangaza kama Mashahidi wa Yehova hawakukuwa nalipa kodi na kama walikuwa najiingiza mu mambo ya politike. Kusema kweli, ile mashitaka yote ilikuwa ya uongo. Siye wote tulijua kama jambo yenye ilikuwa natuletea matatizo na serikali ni juu hatukuunga mukono upande wowote, zaidi sana tulikatala kuuza karte za chama fulani ya politike.

Mu Mwezi wa 9, tulisoma mu gazeti fulani kama raisi alishitaki ndugu kama walikuwa wanaleta muvurugo fasi yote. Ku mukutano fulani wenye alifanya na wakubwa wengine wa serikali, alitangaza kama karibuni serikali yake itakataza kazi ya Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo, kazi yetu ilikatazwa tarehe 20 Mwezi wa 10, 1967. Wakati kidogo kisha pale, wakubwa wa polisi na wenye kusimamia mambo ya wale wenye kuhamia mu inchi walifika ku biro ya tawi juu ya kuifunga na kufukuza wamisionere mu ile inchi.

Wakati tulikamatwa na kufukuzwa mu inchi ya Malawi mu 1967 na wamisionere wenzetu Jack na Linda Johansson

Kisha kufanya siku tatu mu gereza, tulipelekwa mu inchi yenye kutawaliwa na Uingereza, ni kusema, Maurice. Lakini, wenye mamlaka mu nchi ya Maurice hawakukubali tukuwe wamisionere mu inchi yao. Kwa hiyo, tulitumwa Rhodésie yenye (sasa ni Zimbabwe). Wakati tulifika kule, tulikutana na mukubwa fulani mwenye kusimamia mambo ya wale wenye kuhamia mu inchi. Alituambia hivi: “Hawatawaruhusu kuingia Maurice, na kama muko hapa ni juu inchi zingine haziwapendi.” Anne alianza kulia. Ilionekana kama kila mutu hatupendi! Ile wakati, nilipenda tu kutoka pale na kurudia kwetu Uingereza. Ku mwisho, wenye kusimamia mambo ya wale wenye kuhamia mu inchi walituruhusu tubakie ile usiku ku biro ya tawi, lakini walituambia kama tulipaswa kufika ku biro yao siku yenye kufuata. Tulikuwa tumechoka sana, lakini tuliendelea kuacha mambo yote mu mikono ya Yehova. Bila kutazamia, siku yenye kufuata, wakati ya muchana, tuliruhusiwa kubakia sawa vile wageni mu Zimbabwe. Siwezi kusahau hata kidogo namna nilijisikia ile siku. Nilikuwa hakika kama Yehova alikuwa naongoza njia yetu.

MUGAO MUPYA: KUTUMIKIA MALAWI NA TUKO ZIMBABWE

Miye na Anne ku Beteli ya Zimbabwe, mu 1968

Ku biro ya tawi ya Zimbabwe, nilikuwa natumikia mu Idara ya Utumishi, na tulikuwa tunashugulikia makutaniko ya Malawi na Mozambique. Ndugu wa Malawi walikuwa nateswa sana. Nilikuwa pia na mugao wa kutafsiri ripoti zenye zilitumwa na waangalizi wa muzunguko wa Malawi. Siku moya mangaribi, nilikawia mu biro juu nimalize ripoti fulani, na wakati nilisoma vile ndugu zangu wako nateswa sana, nililia sana. * Lakini, uaminifu wao, imani yao, na uvumilivu wao, vilinitia moyo.​—2 Ko. 6:4, 5.

Tulifanya yetu yote juu ya kutolea chakula ya kiroho ndugu wenye walibakia Malawi, na pia wale wenye walikimbilia Mozambique juu ya kuepuka mateso. Watafsriri wa Chichewa, luga yenye kuzungumuziwa sana Malawi, walihamishwa na kupelekwa ku shamba kubwa ya ndugu fulani wa Zimbabwe. Aliwajengea nyumba na biro. Kule, waliendelea na kazi yao ya maana sana ya kutafsiri vichapo vyenye vinategemea Biblia.

Tulifanya mipango juu kila mwaka waangalizi wa muzunguko wa Malawi wahuzurie mukusanyiko wa wilaya katika Chichewa mu Zimbabwe. Wakati walifika Zimbabwe, walipewa plans za hotuba. Wakati walikuwa narudia Malawi, walikuwa naelezea ndugu na dada mambo yenye ilizungumuziwa ku mukusanyiko. Mwaka moya, wakati walitembelea tena Zimbabwe, tulipanga Masomo ya Huduma ya Ufalme juu ya kutia moyo wale waangalizi wa muzunguko wenye uhodari.

Niko natoa hotuba mu luga ya Chichewa ku mukusanyiko wenye ulifanywa mu Chichewa na Shona katika Zimbabwe

Mu Mwezi wa 2, 1975, nilienda kutembelea Mashahidi wa Malawi wenye walikuwa wamekimbilia mu kambi za Mozambique. Wale ndugu walikuwa nafuata maagizo ya sasa ya tengenezo ya Yehova, kutia ndani mupango wa mupya wa kuwa na baraza ya wazee. Wazee wapya walikuwa wamefanya mipango mingi ya kiroho. Kwa mufano, walipanga hotuba za watu wote zitolewe, ndugu wakuwe nazungumuzia andiko ya siku na kujifunza Munara wa Mulinzi, na hata walikuwa nafanya mikusanyiko. Walikuwa napanga kambi sawa vile tu mukusanyiko, kulikuwa idara za usafi, za kugawanya chakula, na za kufanya ulinzi. Kwa musaada wa Yehova, wale ndugu waaminifu walifanya mambo mingi, na kisha kuwatembelea, nilitiwa moyo sana.

Ku mwisho wa miaka ya 1970, biro ya tawi ya Zambia ilianza kusimamia kazi yetu mu inchi ya Malawi. Lakini, niliendelea kukumbuka ndugu wa Malawi na kusali kwa ajili yao, na ni vile wengine pia walifanya. Mara mingi, nikiwa mushiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Zimbabwe, nilikutana na wakilishi wa makao makubwa, na pia ndugu wenye kusimamia kazi yetu mu inchi ya Malawi, Afrika ya Kusini, na Zambia. Kila mara, tulikuwa najiuliza hivi: “Tunaweza kufanya nini ingine juu ya kusaidia ndugu zetu wa Malawi?”

Kadiri wakati ilipita, mateso ilipunguka. Ndugu wenye walikuwa wamekimbia walianza kurudia Malawi, na wale wenye walibakiaka hawakuteswa tena sana sawa vile zamani. Inchi za karibu-karibu zilianza kuruhusu Mashahidi wa Yehova kuhubiri na kukusanyika na kuwaondolea vizuizi. Mozambique ilifanya pia vile mu 1991. Lakini tulijiuliza hivi: ‘Ni wakati gani njo Mashahidi wa Yehova wa Malawi watakuwa huru?’

TUNARUDIA MALAWI

Mambo ilifikia kubadilika mu inchi ya Malawi, na mu 1993 serikali iliondoa vizuizi juu ya kazi ya Mashahidi wa Yehova. Kisha pale, nilikuwa naongea na misionere fulani mwenye aliniuliza hivi: “Utarudia Malawi?” Ile wakati nilikuwa na miaka 59. Kwa hiyo, nilimuambia hivi: “Hapana, nilishazeeka!” Lakini, ileile siku Baraza Yenye Kuongoza ilitutumia ujumbe ili kutuomba turudie Malawi.

Tulikuwa napenda sana mugao wetu katika Zimbabwe. Kwa hiyo, ilikuwa nguvu sana kuamua kurudia. Tulikuwa tumetia mizizi mu Zimbabwe, na tulikuwa na marafiki wengi sana. Lakini Baraza Yenye Kuongoza ilituambia kama tunaweza kubakia Zimbabwe kama tunapenda. Kwa hiyo, tungeweza kujichagulia njia yetu na kubakia Zimbabwe. Lakini, nilikumbuka namna Abrahamu na Sara waliachaka nyumba yao ya muzuri mu miaka yao ya uzee juu ya kumutii Yehova.​—Mwa. 12:1-5.

Tuliamua kufuata muongozo wa tengenezo ya Yehova na tukarudia Malawi tarehe 1, Mwezi wa 2, 1995. Kulikuwa kumepita miaka 28 kisha wakati yenye tulifikaka Malawi kwa mara ya kwanza. Halmashauri ya Tawi iliundwa, ilifanyizwa na miye na ndugu wengine wawili, na bila kukawia, tulianza tena kupanga mambo.

YEHOVA AMEFANYA KAZI ISONGE MBELE

Tumebarikiwa kuona namna Yehova amefanya kazi isonge mbele haraka! Hesabu ya wahubiri iliongezeka haraka. Mu 1993, tulikuwa na wahubiri 30 000 lakini mu 1998, hesabu ya wahubiri ilifikia 42 000. * Baraza Yenye Kuongoza ilikubali biro ya mupya ya tawi ijengwe juu ya kusimamia kazi kubwa yenye ilikuwa nafanywa. Tuliuza kiwanja ya hektare 12 mu muji wa Lilongwe, na nilipewa kazi ya kutumika na halmashauri ya ujenzi.

Mu mwezi wa 5, 2001 ndugu Guy Pierce wa Baraza Yenye Kuongoza alitoa hotuba ya kumutolea Yehova majengo ya mupya ya biro ya tawi. Mashahidi zaidi ya 2000 wa Malawi walikuwa ku ile hotuba. Wengi kati yao walikuwa wamefanya miaka 40 tangu wabatizwe. Wale ndugu na dada waaminifu walikuwa wamevumilia kwa miaka mingi mateso makali wakati kazi yetu ilikuwa imekatazwa. Walikuwa maskini kimwili lakini matajiri sana kiroho. Na sasa walifurahi kutembezwa mu Beteli yao ya mupya. Kila fasi kwenye walienda mu Beteli walikuwa naimba nyimbo za Ufalme, mu namna ya kuimba ya Afrika, na ile ilifanya ile tukio yote ikuwe yenye kugusa moyo sana kuliko matukio ingine yote yenye nilishakajionea. Ilikuwa ushuhuda wenye kuonyesha kama Yehova anabariki sana wale wenye wanavumilia magumu kwa uaminifu.

Kisha ujenzi wa biro ya tawi kumalizika, nilifurahi sana wakati nilianza kupewa migao ya kuenda kutoa hotuba za kumutolea Yehova Majumba ya Ufalme. Makutaniko mu inchi ya Malawi, ilifaidika na programu ya kujenga haraka Majumba ya Ufalme mu inchi kwenye ndugu hawakukuwa na makuta mingi. Mbele ya pale, makutaniko fulani ilikuwa nakusanyikia mu nyumba zenye zilijengwa na miti ya mikalitusi (eucalyptus). Walitumia viti vya murefu vyenye vilitengenezwa na udongo. Sasa ndugu walitumika sana ili kuchoma matofali yenye walitumia juu ya kujenga Majumba ya Ufalme ya muzuri. Kuliko kutumia kiti ya mutu moya-moya mu Jumba ya Ufalme, ndugu walipendelea kutumia vile viti vyao vya murefu juu vilikuwa na nafasi ya watu wengi!

Nimefurahia pia kuona namna Yehova amesaidia watu wakomale kiroho. Ndugu vijana wa Afrika walinishangaza sana juu walikuwa tayari kusaidia, walijifunza mambo mingi haraka wakati walipewa mazoezi na tengenezo ya Yehova na wakati walipewa kazi mbalimbali. Ile iliwasaidia kutumikia madaraka mingi ku Beteli na mu makutaniko. Zaidi ya ile, makutaniko ilitiwa nguvu na waangalizi wa muzunguko wenye waliwekwa hivi karibuni, wengi kati yao walikuwa walishaoa. Hata kama watu wengi na hata watu wa familia yao walitazamia wazale watoto, wale waangalizi na bibi zao waliamua kutozala juu waweze kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova.

NIMETOSHEKA NA MAAMUZI YENYE NILIKAMATA

Miye na Anne ku Beteli ya Uingereza

Kisha kufanya miaka 52 mu Afrika, nilikuwa na matatizo fulani ya afya. Halmashauri ya Tawi ilipendekeza kama tuende kutumikia Uingereza, na Baraza Yenye Kuongoza ilikubali. Tulihuzunika kuacha mugao wenye tulikuwa napenda sana. Lakini familia ya Beteli ya Uingereza iko natuhangaikia muzuri mu miaka yetu ya uzee.

Niko hakika kama kuacha Yehova aongoze njia yangu njo uamuzi muzuri kuliko maamuzi yote yenye nilishakakamata. Kama ningetegemea uelewaji wangu mwenyewe, sijue kama ile kazi yangu ingenipelekaka wapi. Sikuzote, Yehova alijua mambo yenye nilikuwa nayo lazima ili ‘kunyoosha mapito yangu.’ (Mez. 3:5, 6) Wakati nilikuwa kijana, nilikuwa nafurahia sana kujifunza namna kompanyi kubwa inaweza kufanya kazi. Lakini, tengenezo ya Yehova ilinipatia kazi ya muzuri ya kiroho yenye ilinisaidia nitosheke sana. Kwangu, kumutumikia Yehova kulikuwa na kunaendelea kuwa jambo ya maana sana mu maisha yangu!

^ Historia ya Mashahidi wa Yehova wa Malawi ilitolewa mu Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 1999, uku. 148-223.

^ Kwa sasa Malawi iko na wahubiri 100 000.