Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 28

Ufalme wa Mungu Uko Natawala!

Ufalme wa Mungu Uko Natawala!

“Ufalme wa ulimwengu umekuwa Ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake.”​—UFU. 11:15.

WIMBO 22 Ufalme Unatawala​—Tunasali Ukuye!

KIFUPI YA HABARI *

1. Tuko hakika na jambo gani, na juu ya nini?

 HALI ya dunia leo inafanya ikuwe nguvu kwako kuamini kama mambo itakuaka muzuri? Mu familia za mingi, watu hawapendane tena, watu wengi wanapenda jeuri sana, wanatafuta tu faida zao, na ni wakali. Watu wengi wanaona kama ni nguvu kutumainia wenye mamlaka. Lakini ile yote inaonyesha kama mambo itakuwa muzuri zaidi. Juu ya nini? Juu namna watu wako wanatenda inatimiza kabisa unabii wa Biblia kuhusu “siku za mwisho.” (2 Ti. 3:1-5) Mutu mwenye anawazaka muzuri hawezi kusema kama ule unabii hauko natimia. Kuona namna ule unabii uko natimia kunafanya tukuwe hakika kama Yesu Kristo amekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Kuchunguza tena maunabii ingine yenye imetimia mu miaka ya hivi karibuni kutatia nguvu imani yetu.

Sawa vile sehemu za picha zinafanyiza picha yenye kuwa wazi wakati zinatiwa pamoya, ni vile pia kuhusu maunabii ya kitabu ya Danieli na Ufunuo wakati tunaitia pamoya. Inafanyiza picha yenye iko wazi yenye inatusaidia tujue kama tuko wapi mu kalendari ya Yehova (Ona fungu ya 2)

2. Tutachunguza mambo gani mu hii habari, na kufanya vile kutatusaidia namna gani? (Zungumuzia picha ku jalada.)

2 Mu hii habari, tutachunguza mambo tatu. Kwanza, tutachunguza unabii wenye unatusaidia kujua ni wakati gani Ufalme wa Mungu ulianza kutawala. Pili, tutachunguza maunabii yenye inatusaidia kuelewa kama Yesu ameanza kutawala mbinguni. Na tatu, tutachunguza maunabii yenye kuonyesha namna maadui wa Ufalme wa Mungu wataharibiwa. Tutaona kama wakati tunatia ile maunabii yote pamoya, inafanyiza picha yenye iko wazi yenye inatusaidia tujue kama tuko wapi mu kalendari ya Yehova.

UNABII WENYE UNATUSAIDIA KUJUA NI WAKATI GANI UFALME WA MUNGU ULIANZA KUTAWALA

3. Unabii wenye kupatikana mu Danieli 7:13, 14 unatuhakikishia jambo gani kuhusu Mufalme wa Ufalme wa Mungu?

3 Unabii wenye kupatikana mu Danieli 7:13, 14 unatuhakikishia kama Yesu Kristo atakuwa Mufalme muzuri sana wa Ufalme wa Mungu. Watu wa kila taifa watafurahia ‘kumutumikia,’ na hakutakuwa mutawala mwingine mwenye atakamata nafasi yake. Unabii mwingine wenye unapatikana mu kitabu ya Danieli ulitabiri kama Yesu angeanza kutawala ku mwisho ya kipindi yenye inaitwa nyakati saba. Inawezekana kujua ni wakati gani Yesu alianza kutawala?

4. Fasiria namna Danieli 4:10-17 inatusaidia kujua mwaka wenye Yesu alikuwa Mufalme. (Ona pia maelezo ya chini.)

4 Soma Danieli 4:10-17. “Nyakati saba” ziko na urefu wa miaka 2 520. Ile kipindi ilianza mu 607 M.K.Y. wakati Wababiloni waliondoa mufalme wa mwisho ku kiti ya ufalme ya Yehova mu Yerusalemu. Ile kipindi ilimalizika mu 1914 K.K.Y. wakati Yehova alifanya Yesu, “mwenye kuwa na haki ya kisheria,” kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. *​—Eze. 21:25-27.

5. Kuelewa unabii kuhusu “nyakati saba” kunatuletea faida gani?

5 Kuelewa ule unabii kunatuletea faida gani? Kuelewa unabii kuhusu “nyakati saba” kunatuhakikishia kama Yehova anatimizaka ahadi zake ku wakati yenye kufaa. Yehova aliamuaka wakati yenye angemufanya Yesu kuwa Mufalme, na wakati ilifikaka, akamufanya kuwa Mufalme. Kwa hiyo, tunajua kama atatimiza pia maunabii ingine ku wakati yenye alishakaamua. Bila shaka, siku ya Yehova “haitachelewa!”​—Hab. 2:3.

UNABII WENYE UNATUSAIDIA KUJUA KAMA YESU AMEKUWA MUFALME MBINGUNI

6. (a) Ni mambo gani yenye tumeona ku dunia yenye inaonyesha kama Yesu iko natawala mbinguni? (b) Namna gani unabii wenye kupatikana mu Ufunuo 6:2-8 unahakikisha ile jambo?

6 Karibu na mwisho wa utumishi wake ku dunia, Yesu alizungumuzia matukio fulani yenye ingesaidia wanafunzi wake wajue kama ameanza kutawala mbinguni. Kwa mufano, alizungumuzia vita, njala, na matetemeko ya inchi. Alisema pia kama magonjwa ya kuambukiza itakuwa “mahali pamoja kisha pengine,” sawa vile ugonjwa wa Coronavirus wenye umetokea hivi karibuni. Ile mambo yote ni sehemu ya ile yenye Biblia inaita kuwa “alama” ya kuwapo kwa Kristo. (Mt. 24:3, 7; Lu. 21:7, 10, 11) Zaidi ya miaka 60 kisha Yesu kufa na kurudia mbinguni, alimupatia mutume Yohana uhakikisho mwingine wenye kuonyesha kama ile mambo ingetokea. (Soma Ufunuo 6:2-8.) Na imetokea tangu Yesu akuwe Mufalme mu 1914.

7. Juu ya nini hali iliharibika sana ku dunia wakati Yesu alikuwa Mufalme?

7 Juu ya nini hali iliharibika sana ku dunia wakati Yesu alikuwa Mufalme mbinguni? Ufunuo 6:2 inazungumuzia jambo fulani ya maana. Inaonyesha kama jambo ya kwanza yenye Yesu alifanya kisha kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu ilikuwa kupigana vita. Alipigana na nani? Alipigana na Shetani na mashetani wake. Sura ya 12 ya Ufunuo inaonyesha kama Shetani hakupata ushindi, na yeye na mashetani wake walitupwa ku dunia. Shetani, alianza kumalizia kasirani yake ku wanadamu, na ile ilileta ole ku dunia.​—Ufu. 12:7-12.

Hatufurahiake kuangalia habari za mubaya, lakini kuona namna maunabii ya Biblia iko natimia kunatuhakikishia kama Ufalme wa Mungu uko natawala sasa (Ona fungu ya 8)

8. Kuona namna maunabii kuhusu Ufalme wa Mungu iko natimia, kunatuletea faida gani?

8 Kuelewa ile maunabii kunatuletea faida gani? Mambo yenye iko natokea mu dunia na namna ya watu ya kutenda inapaswa kutusaidia kuelewa kama Yesu amekuwa Mufalme. Njo maana, kuliko kukasirika wakati tunaona watu wanatafuta tu faida zao na wanakosa huruma, hatupaswe kusahau kama matendo yao inatimiza unabii wa Biblia. Ufalme wa Mungu uko natawala! (Zb. 37:1) Na bado, tujue kama mambo itaendelea kuharibika kadiri Armagedoni inakaribia. (Mk. 13:8; 2 Ti. 3:13) Hauone kama tunapaswa kumushukuru Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo juu anatusaidia kuelewa juu ya nini dunia iko vile leo?

NAMNA MAADUI WA UFALME WA MUNGU WATAHARIBIWA

9. Unabii wa Danieli 2:28, 31-35 unatoa maelezo gani juu ya serikali ya mwisho ya ulimwengu, na ni wakati gani ile serikali ilianza kutawala?

9 Soma Danieli 2:28, 31-35. Ule unabii uko natimia leo. Ndoto ya Nebukadneza ilionyesha mambo yenye ingetokea “katika kipindi cha mwisho cha zile siku,” kisha Yesu kuanza kutawala. Serikali ya mwisho ya ulimwengu yenye Biblia ilitabiri iko kati ya maadui wa Yesu ku dunia. Ile serikali inafananishwa na “vikanyangio vya chuma na udongo,” na tayari iko natawala. Ilianza kutawala wakati ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, wakati Uingereza na Amerika zilianza kutumika kwa upatano sana. Sanamu yenye Nebukadneza aliona mu ndoto yake ilionyesha pia karibu mambo mbili yenye ingefanya ile serikali ikuwe tofauti na serikali zingine zenye zilitangulia.

10. (a) Unabii wa Danieli unafanisha serikali ya Uingereza na Amerika na nini, juu ya nini ule ufaninisho unafaa kabisa? (b) Ni hatari gani tunapaswa kuepuka? (Ona kisanduku “ Ufanye Angalisho na Udongo!”)

10 Kwanza, tofauti na serikali za ulimwengu zenye zilitawala zamani, zenye ndoto ya Nebukadneza inazungumuzia, serikali ya Uingereza na Amerika haifananishwe na metali ya nguvu-nguvu sawa vile zahabu ao feza. Lakini, inafananishwa na muchanganyiko wa chuma na udongo. Udongo unafananisha “uzao wa wanadamu,” ao watu wa kawaida. (Da. 2:43, maelezo ya chini) Leo, tunaona waziwazi mambo yenye watu wanafanya wakati wa uchaguzi, namna wanafanya kampanye za kutetea haki zao, wanafanya maandamano ya kupinga serikali, na wanaanzisha matengenezo ya kutetea haki za wafanyakazi, na ile inafanya ikuwe nguvu kwa viongozi wa hii dunia kutimiza mambo yenye wanapenda kufanya.

11. Juu ya nini serikali ya Uingereza na Amerika inatuhakikishia kabisa kama tunaishi wakati ya mwisho?

11 Pili, serikali ya Uingereza na Amerika yenye inafananishwa na miguu ya ile sanamu kubwa njo serikali ya ulimwengu ya mwisho yenye ilitabiriwa na Biblia. Hakuna serikali ingine ya wanadamu yenye itatawala kisha ile. Lakini, Ufalme wa Mungu utaiharibu wakati ya Armagedoni pamoya na serikali zingine zote za wanadamu. *​—Ufu. 16:13, 14, 16; 19:19, 20.

12. Unabii wa Danieli unatupatia ushuhuda gani mwingine wenye unatufariji na kutupatia tumaini?

12 Kuelewa ule unabii kunatuletea faida gani? Unabii wa Danieli unatupatia ushuhuda mwingine wenye kuonyesha kama tunaishi wakati ya mwisho. Zaidi ya miaka 2 500 yenye imepita, Danieli alitabiri kama, kisha Babiloni kutawala, kungetokea serikali ine zenye zingetawala watu wa Mungu. Zaidi ya ile, alionyesha kama kati ya zile serikali ine, serikali ya Uingereza na Amerika njo ingekuwa ya mwisho. Ile inatufariji na inatupatia tumaini kama karibuni Ufalme wa Mungu utaharibu serikali zote za wanadamu, na utatawala dunia yote.​—Da. 2:44.

13. (a) “Mufalme wa munane” mwenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 17:9-12 anafananisha nini, na “wafalme kumi” wanafananisha nini? (b) Namna gani ule unabii umetimia?

13 Soma Ufunuo 17:9-12. Juu Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilitokeza uharibifu mukubwa, jambo fulani ilitokea yenye ilitimiza unabii wa Biblia kuhusu siku za mwisho. Viongozi wa dunia walipenda kuleta amani mu dunia yote. Kwa hiyo, mu Mwezi wa 1, 1920, walianzisha Ushirika wa Mataifa, wenye ulibadilishwa na kuwa Umoja wa Mataifa mu Mwezi wa 10, 1945. Mu Biblia, Umoja wa Mataifa unaitwa “mufalme wa munane.” Lakini, Umoja wa Mataifa haiko serikali ya ulimwengu. Umoja wa Mataifa uko tu na nguvu juu ya serikali zenye zinautengemeza. Biblia inaita zile serikali zote “wafalme kumi.”

14-15. (a) Ufunuo 17:3-5 inaonyesha nini kuhusu “Babiloni Mukubwa”? (b) Leo, wale wenye kuunga mukono dini za uongo wako nafanya nini?

14 Soma Ufunuo 17:3-5. Mu maono, mutume Yohana aliona kahaba, “Babiloni Mukubwa,” mwenye anafananisha dini zote za uongo. Ile maono imetimia namna gani? Kwa miaka mingi, dini za uongo zimetumika kwa upatano kabisa na serikali za dunia na zimetegemeza zile serikali. Lakini, karibuni Yehova atachochea viongozi wa zile serikali ‘watimize wazo lake.’ Matokeo itakuwa nini? Zile serikali, ni kusema, “wafalme kumi” zitashambulia matengenezo ya dini za uongo na kuiharibu.​—Ufu. 17:1, 2, 16, 17.

15 Nini njo inaonyesha kama mwisho wa Babiloni Mukubwa uko karibu? Juu ya kujibia ile ulizo, inaomba kukumbuka kama muji wa zamani wa Babiloni ulilindwa kwa sehemu na maji ya muto Efrati. Kitabu ya Ufunuo inafananisha mamilioni ya watu wenye kuunga mukono Babiloni Mukubwa na “maji” yenye kumulinda. (Ufu. 17:15) Lakini, kitabu ya Ufunuo inaonyesha pia kama ile maji ‘itakauka.’ Ile inaonyesha kama dini za uongo zitapoteza watu wengi wenye kuziunga mukono. (Ufu. 16:12) Leo, unabii wa ufunuo uko unatimia juu watu wengi wameacha dini ya uongo na wameanza kutafuta musaada fasi ingine.

16. Kuelewa maunabii kuhusu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa na kuharibiwa kwa Babiloni Mukubwa kunatuletea faida gani?

16 Kuelewa ile maunabii kunatuletea faida gani? Kuelewa maunabii kuhusu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa na kuona namna watu wengi hawaunge tena mukono dini za uongo kunatuhakikishia kama tunaishi kabisa mu siku za mwisho. Hata kama watu wengi hawaunge tena mukono Babiloni Mukubwa, haiko ile njo itatokeza mwisho wa matengenezo ya dini za uongo. Vile tuliona, Yehova njo atachochea “wafalme kumi,” ni kusema, serikali zenye zinaunga mukono Umoja wa Mataifa, ‘zitimize wazo lake.’ Zile serikali zitaharibu Babiloni Mukubwa kwa gafla, na ile itashangaza sana watu. * (Ufu. 18:8-10) Uharibifu wa Babiloni Mukubwa utatikisa dunia na utaleta magumu. Lakini, kuko mambo mbili yenye itafanya watumishi wa Yehova wafurahi. Kwanza, adui wa Mungu wa miaka mingi, ni kusema, dini za uongo zitakuwa haziko tena, na ukombozi wetu utakuwa karibu sana!​—Lu. 21:28.

USIOGOPE MAMBO YENYE ITATOKEA HIVI KARIBUNI

17-18. (a) Namna gani unaweza kuendelea kutia nguvu imani yako? (b) Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

17 Danieli alitabiri kama “ujuzi wa kweli utakuwa mwingi.” Na ni vile mambo iko leo. Kwa sasa, tunaelewa maunabii yenye inahusu wakati yetu. (Da. 12:4, 9, 10) Kuona namna ile maunabii iko natimia kabisa kunafanya tumuheshimie sana Yehova na Neno yake, Biblia. (Isa. 46:10; 55:11) Kwa hiyo, uendelee kutia nguvu imani yako kwa kujifunza Maandiko kwa bidii, na kusaidia wengine wakuwe na uhusiano muzuri na Yehova. Atalinda wale wote wenye wanamutumainiaka kabisa, na atawapatia “amani ya kudumu.”​—Isa. 26:3.

18 Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia maunabii kuhusu kutaniko ya Kikristo wakati ya mwisho. Sawa vile tutajifunza, ile maunabii pia inaonyesha kama tunaishi mu siku za mwisho. Tutaona ushuhuda mwingine wenye kuonyesha kama Yesu, mwenye kwa sasa njo Mufalme wetu, iko naongoza wafuasi wake waaminifu.

WIMBO 61 Tuende Mbele

^ Tuko naishi mu kipindi ya muzuri sana ya historia! Ufalme wa Mungu umeanza kutawala, vile maunabii mingi ya Biblia ilisemaka. Mu hii habari, tutachunguza maunabii fulani yenye itatia nguvu imani yetu na kutusaidia tuendelee kuwa watulivu na kumutumainia Yehova leo na mu siku zenye ziko nakuya.

^ Ona Somo ya 32 nukta ya 4 mu kitabu Furahia Maisha Milele!, na uangalie ku jw.org video Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala mu 1914.

^ Juu ya kupata habari zaidi kuhusu unabii wa Danieli, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 6, 2012, uku. 14-19.

^ Juu ya kupata habari zaidi kuhusu mambo yenye itatokea hivi karibuni, ona sura ya 21 ya kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala!