Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 30

Unabii wa Zamani Wenye Unakuhusu

Unabii wa Zamani Wenye Unakuhusu

“Nitatia uadui kati yako na ule mwanamuke.”​—MWA. 3:15.

WIMBO 15 Tumusifu Muzaliwa wa Kwanza wa Yehova!

KIFUPI YA HABARI *

1. Yehova alifanya nini kisha tu Adamu na Eva kufanya zambi? (Mwanzo 3:15)

 KISHA tu Adamu na Eva kufanya zambi, Yehova alitoa unabii fulani wa maana wenye ulipatia wazao wao tumaini. Mambo yenye alisema inapatikana mu Mwanzo 3:15.​—Soma.

2. Juu ya nini unabii wenye kupatikana mu Mwanzo 3:15 ni wa pekee?

2 Unabii wenye Yehova alitoa unapatikana mu kitabu ya kwanza ya Biblia. Ni unabii wa pekee juu, kwa njia fulani, vitabu vingine vya Biblia vinahusiana na ule unabii. Sawa vile sehemu yenye kuunganisha kurasa zote za kitabu, maneno ya Mwanzo 3:15 inaunganisha kila kitabu ya Biblia mu ujumbe moya wenye kupatana. Ni kusema Mungu atatuma Mukombozi mwenye ataharibu Shetani na wale wote wenye kumuunga mukono. * Itakuwa jambo ya muzuri sana kwa wale wote wenye kumupenda Yehova!

3. Tutajibia maulizo gani mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutajibia maulizo yenye kufuata kuhusu unabii wenye kuwa mu Mwanzo 3:15: Nani njo wenye kuzungumuziwa mu ule unabii? Ule unabii umetimia nanma gani? Na unatuletea faida gani?

NANI NJO WENYE KUZUNGUMUZIWA MU ULE UNABII?

4. “Nyoka” ni nani, na nini njo inatusaidia kujua vile?

4 Mwanzo 3:14, 15 inazungumuzia “nyoka,” “uzao” wa nyoka, “mwanamuke,” na “uzao” wa mwanamuke. Biblia inatusaidia kutambua kila mumoja wao. * Tuanze na “nyoka.” Nyoka halisi hangeweza kuelewa mambo yenye Yehova alisema mu bustani ya Edeni. Kwa hiyo, hukumu yenye Yehova alisema kuhusu nyoka ilihusu kiumbe fulani mwenye akili. Kiumbe gani? Ufunuo 12:9 inafasiria waziwazi nyoka ni nani. Inaonyesha waziwazi kama “ule nyoka wa zamani” ni Shetani Ibilisi. Lakini, nani njo uzao wa nyoka?

NYOKA

Shetani, Ibilisi, mwenye Ufunuo 12:9 inaita “ule nyoka wa zamani” (Ona fungu ya 4)

5. Uzao wa nyoka ni nani?

5 Wakati Biblia inasema kama watu fulani ni uzao wa mutu fulani, inamaanisha kama wale watu wanafikiri na kutenda sawa vile ule mutu, na ni vile wanaweza kuitwa kuwa watoto wake. Kwa hiyo, uzao wa nyoka ni malaika na wanadamu wenye, sawa vile Shetani, wanapinga Yehova na watu wake. Kati yao, kuko malaika wenye waliacha migao yao mbinguni mu siku za Noa, na pia wanadamu wabaya wenye wanatenda kama Baba yao, Ibilisi.​—Mwa. 6:1, 2; Yoh. 8:44; 1 Yo. 5:19; Yud. 6.

UZAO WA NYOKA

Malaika waovu na wanadamu wenye wanapinga Yehova na watu wake (Ona fungu ya 5)

6. Juu ya nini “ule mwanamuke” hapaswe kuwa Eva?

6 Tuzungumuzie sasa “ule mwanamuke.” Hapaswe kuwa Eva. Juu ya nini? Ona sababu moya tu. Unabii unasema kama uzao wa mwanamuke ‘ungeponda’ kichwa ya nyoka. Vile tuliona, nyoka ni kiumbe wa roho mwenye kuitwa Shetani. Na hakuna mwanadamu mwenye hakamilike, mwenye alitokana na Eva, mwenye angeweza kumuponda Shetani. Sasa, nani njo angeponda Shetani?

7. Vile Ufunuo 12:1, 2, 5, 10 inaonyesha, mwanamuke mwenye kuzungumuziwa mu Mwanzo 3:15 ni nani?

7 Kitabu ya mwisho ya Biblia inatusaidia kujua mwanamuke mwenye kuzungumuziwa mu Mwanzo 3:15 ni nani. (Soma Ufunuo 12:1, 2, 5, 10.) Haiko mwanamuke wa hapa ku dunia. Iko na mwezi ku miguu yake na taji ya nyota 12 ku kichwa yake. Anazala mutoto mwenye haiko wa kawaida kabisa, ni kusema, Ufalme wa Mungu. Ufalme wa Mungu uko mbinguni. Kwa hiyo, ule mwanamuke anapaswa pia kuwa mbinguni. Anafananisha sehemu ya mbinguni ya tengenezo ya Yehova yenye kufanyizwa na malaika waaminifu.​—Gal. 4:26.

ULE MWANAMUKE

Sehemu ya mbinguni ya tengenezo ya Yehova yenye kufanyizwa na malaika waaminifu (Ona fungu ya 7)

8. Nani njo sehemu ya kwanza ya uzao wa mwanamuke, na ni wakati gani alikuwa sehemu ya kwanza ya uzao wa mwanamuke? (Mwanzo 22:15-18)

8 Biblia inatusaidia pia kujua sehemu ya kwanza ya uzao wa mwanamuke ni nani. Ule uzao ulipaswa kutoka mu kizazi ya Abrahamu. (Soma Mwanzo 22:15-18.) Sawa vile unabii ulionyesha, Yesu alikuwa uzao wa ule mwanaume muaminifu. (Lu. 3:23, 34) Lakini, ule uzao ulipaswa kuwa na nguvu kuliko mwanadamu juu ulipaswa kuponda Shetani Ibilisi. Kwa hiyo, wakati Yesu alikuwa na miaka 30 hivi, alitiwa mafuta kupitia roho takatifu ya Mungu. Ni kisha Yesu kutiwa mafuta, njo alikuwa sehemu ya kwanza ya uzao wa mwanamuke. (Gal. 3:16) Kisha Yesu kufa na kufufuliwa, Mungu ‘alimuvalisha taji la utukufu na heshima’ na akamupatia “mamlaka yote mbinguni na duniani,” na pia mamlaka ya ‘kuvunja kazi za Ibilisi.’​—Ebr. 2:7; Mt. 28:18; 1 Yo. 3:8.

UZAO WA ULE MWANAMUKE

Yesu Kristo na wale 144 000 wenye watatawala naye (Ona fungu ya 8-9)

9-10. (a) Ni nani wenye kufanyiza sehemu ya pili ya uzao wa mwanamuke, na ni wakati gani Mukristo anakuwa sehemu ya ule uzao? (b) Tunapenda kuzungumuzia nini sasa?

9 Lakini, kuko sehemu ya pili ya uzao wa mwanamuke. Maneno yenye mutume Paulo aliambia Wakristo Wayahudi na watu wa mataifa wenye kutiwa mafuta inatusaidia kujua wale wenye kufanyiza sehemu ya pili ya uzao wa mwanamuke. Aliwaambia hivi: “Kama ninyi ni wa Kristo, ninyi kwa kweli ni uzao wa Abrahamu, wariti kuhusiana na ahadi.” (Gal. 3:28, 29) Wakati Yehova anatia mafuta Mukristo fulani kupitia roho yake, ule Mukristo anakuwa sehemu ya uzao wa mwanamuke. Kwa hiyo, uzao unafanyizwa na Yesu Kristo na wale 144 000 wenye watatawala naye. (Ufu. 14:1) Wote wanajikaza kufikiri na kutenda sawa vile Baba yao, Yehova Mungu.

10 Vile tumejua wale wenye kuzungumuziwa mu Mwanzo 3:15, tuzungumuzie sasa kwa kifupi namna Yehova ametimiza ule unabii hatua kwa hatua na faida yenye tunapata.

ULE UNABII UMETIMIA NAMNA GANI?

11. Unabii ulimaanisha nini wakati ulisema kama uzao wa mwanamuke ‘ungepigwa kwenye kisigino’?

11 Kulingana na unabii wenye kuwa mu Mwanzo 3:15, Shetani angepiga uzao wa ule mwanamuke “kwenye kisigino.” Ule unabii ulitimia wakati Shetani alichochea Wayahudi na Waroma waue Mwana wa Mungu. (Lu. 23:13, 20-24) Kama mutu anaumia ku kisigino, anaweza kuwa na magumu ya kutembea kwa muda fulani. Vilevile, kwa wakati fulani Yesu hakukuwa na uwezo wa kufanya jambo fulani wakati alikuwa mu kaburi.​—Mt. 16:21.

12. Kichwa ya nyoka itapondwa namna gani na wakati gani?

12 Juu unabii wote wenye kuwa mu Mwanzo 3:15 utimie, Yesu hangepaswa kubakia mu kaburi. Juu ya nini tunasema vile? Juu sawa vile ule unabii unaonyesha, uzao ungepaswa kuponda kichwa ya nyoka. Ile ilimaanisha kama pigo yenye Yesu alipewa kwenye kisigino ilipaswa kupona. Ni kusema alipaswa kufufuliwa. Na ni vile ilikuwa. Siku tatu kisha Yesu kufa, alifufuliwa na kuwa kiumbe wa roho mwenye hawezi kufa. Kwa wakati yenye Mungu ameweka, Yesu atamuharibu Shetani. (Ebr. 2:14) Kristo na wale wote wenye watatawala naye wataharibu maadui wa Mungu, ni kusema, uzao wa nyoka.​—Ufu. 17:14; 20:4, 10. *

ULE UNABII UNATULETEA FAIDA GANI?

13. Utimizo wa Mwanzo 3:15 uko natuletea faida gani?

13 Kama uko mutumishi wa Yehova mwenye amejitoa kwake, utimizo wa Mwanzo 3:15 uko nakuletea faida. Yesu alikuya ku dunia kama mwanadamu. Alionyesha kwa ukamilifu sifa za Baba yake. (Yoh. 14:9) Njo maana kupitia yeye, tumefikia kumujua Yehova Mungu na kumupenda. Tumefaidika pia na mafundisho ya Yesu na muongozo wenye anatolea makutaniko leo. Ametufundisha kuishi mu njia yenye itafanya Yehova atukubali. Na siye wote tunafaidika vile Yesu alipigwa kwenye kisigino, ni kusema, kuuawa. Namna gani? Kisha Yesu kufa, Yehova alimufufua, na alikubali damu ya Mwana wake kuwa zabihu kamilifu yenye “inatusafisha kutoka katika zambi yote.”​—1 Yo. 1:7.

14. Nini njo inaonyesha kama unabii wenye Yehova alitoa katika Edeni haungetimia palepale? Fasiria.

14 Mambo yenye Yehova alisema mu unabii wenye Yehova alitoa katika Edeni ilionyesha kama ule unabii haungetimia palepale. Ingeomba wakati juu mwanamuke atokeze uzao wenye uliahidiwa, juu Ibilisi akusanye wafuasi wake, na juu uadui (ao chuki) ikuwe kati ya vile vikundi viwili. Kuelewa ule unabii kunatusaidia sana juu ule unabii unatuonya kama dunia ya Shetani itachukia watumishi wa Yehova. Yesu pia alipatiaka wanafunzi wake onyo ya kufanana na ile. (Mk. 13:13; Yoh. 17:14) Tumejionea kabisa utimizo wa ile sehemu ya unabii zaidi sana mu miaka 100 yenye imepita. Namna gani?

15. Juu ya nini dunia inatuchukia sana, lakini juu ya nini hatuna sababu ya kuogopa Shetani?

15 Wakati kidogo kisha Yesu kufanywa kuwa Mufalme mu 1914, Shetani alifukuzwa mbinguni. Kwa sasa, amezuiwa ku dunia na anachunga kuharibiwa. (Ufu. 12:9, 12) Lakini, haiko nachunga uharibifu bila kufanya kitu. (Ufu. 12:13, 17) Shetani iko na kasirani sana, na iko namalizia kasirani yake juu ya watu wa Mungu. Njo maana dunia ya Shetani inatuchukia sana kuliko zamani. Hatuna sababu ya kuogopa Shetani na wale wenye kumuunga mukono. Lakini, tuko na uhakika sawa ule wenye mutume Paulo alikuwa nao, mwenye aliandika hivi: “Kama Mungu iko upande wetu, ni nani atatushinda?” (Ro. 8:31) Tunaweza kumutumainia kabisa Yehova juu, sawa vile tumeona, sehemu kubwa ya unabii wenye kuwa mu Mwanzo 3:15 ilishatimia.

16-18. Kuelewa Mwanzo 3:15 kumesaidia namna gani Curtis, Ursula na Jessica?

16 Ahadi ya Yehova yenye inapatikana mu Mwanzo 3:15 inaweza kutusaidia kupambana na jaribu yoyote yenye tunaweza kukutana nayo. Curtis, misionere mu inchi ya Guam, anasema hivi: “Wakati fulani, nimekutana na majaribu na mambo yenye kuvunja moyo yenye imefanya ikuwe nguvu kwangu kuendelea kuwa muaminifu kwa Yehova. Lakini, kufikiri sana juu ya unabii wenye kuwa mu Mwanzo 3:15 kumenisaidia niendelee kumutumainia Baba yangu wa mbinguni.” Curtis anachunga kwa hamu siku yenye Yehova atamaliza magumu yetu yote.

17 Dada wa Bavaria, mwenye kuitwa Ursula, anasema kama kuelewa Mwanzo 3:15 kumemusaidia akuwe hakika kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu. Aliona namna maunabii ingine yote inahusiana na ule unabii, na ile ilimushangaza sana. Anasema pia hivi: “Niliguswa sana wakati nilijifunza namna Yehova alikamata mipango bila kukawia juu wanadamu wasikuwe bila tumaini.”

18 Jessica, wa Mikronesia, anasema hivi: “Ningali nakumbuka vile nilijisikiaka kwa mara ya kwanza wakati nilitambua kama nimepata kweli. Unabii wenye kuwa mu Mwanzo 3:15 ulikuwa unatimia. Ile imenisaidia kukumbuka kama maisha yenye tuko nayo leo haiko njo yenye Yehova alipenda tukuwe nayo. Ule unabii umenisaidia pia nikuwe hakika kama kumutumikia Yehova njo jambo yenye inaweza kunisaidia nikuwe na maisha ya muzuri sasa na hata mu siku zenye ziko nakuya.”

19. Nini njo inatuhakikishia kama sehemu ya mwisho ya unabii wenye kuwa mu Mwanzo 3:15 itatimia?

19 Vile tumeona, Mwanzo 3:15 iko natimia sasa. Uzao wa mwanamuke na uzao wa nyoka vimejulikana waziwazi. Yesu, sehemu ya kwanza ya uzao wa mwanamuke, alipona pigo yenye alipata kwenye kisigino, na kwa sasa iko Mufalme mwenye utukufu na mwenye hawezi kufa. Yehova alishachagua karibu wale wote wenye watatawala na mwana wake mbinguni. Juu sehemu ya kwanza ya ule unabii ilishatimia, ile inatuhakikishia kama sehemu ya mwisho, ni kusema kupondwa kwa kichwa ya nyoka, itatimia pia. Watumishi wa Yehova watafurahi sana wakati Shetani ataharibiwa. Tuendelee kuvumilia mupaka ile wakati ifike. Mungu wetu ni mwenye kutumainika. Atatumia uzao wa mwanamuke juu ya kufanya mambo mingi ya muzuri kwa ajili ya “mataifa yote ya dunia.”​—Mwa. 22:18.

WIMBO 23 Yehova Anaanza Kutawala

^ Hatuwezi kuelewa muzuri Biblia kama hatuelewe unabii wenye unapatikana mu Mwanzo 3:15. Kujifunza ule unabii kunaweza kutia nguvu imani yetu katika Yehova na kunaweza kutusaidia tukuwe hakika kama atatimiza ahadi zake zote.

^ Ona Nyongeza B1, “Ujumbe wa Biblia,” mu Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

^ Ona kisanduku “Wale Wenye Kuzungumuziwa mu Mwanzo 3:14, 15.”