Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 32

Vijana, Muendelee Kufanya Maendeleo Kisha Kubatizwa

Vijana, Muendelee Kufanya Maendeleo Kisha Kubatizwa

“Tuendelee kukomaa katika mambo yote.”​—EFE. 4:15.

WIMBO 56 Acha Kweli Ikuongoze

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni mambo gani ya muzuri yenye tayari vijana wengi wamefanya?

 KILA mwaka, maelfu ya vijana Wakristo wanabatizwa. Ulishabatizwa? Kama ni vile, ndugu na dada zako wa kiroho wanafurahia uamuzi wenye ulikamata, na Yehova pia anafurahi! (Mez. 27:11) Fikiria mambo ya muzuri yenye umefanya mupaka hapa. Kwa mufano, umejifunza Biblia kwa bidii, pengine kwa miaka mingi. Mambo yenye umejifunza imekuhakikishia kama Biblia ni Neno ya Mungu. Zaidi ya ile, umefikia kumujua na kumupenda Muandikaji wa Biblia. Umemupenda Yehova sana mupaka ukafikia kutoa maisha yako kwake na kubatizwa. Umekamata uamuzi muzuri sana!

2. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

 2 Bila shaka, imani yako imejaribiwa mu njia mbalimbali wakati ulikuwa nafanya maendeleo juu ufikie kubatizwa. Lakini, vile utaendelea kukomala, utakutana na majaribu ingine. Shetani atajaribu kukufanya uache kumupenda Yehova na uache kumutumikia. (Efe. 4:14) Usiache ile itokee. Jambo yenye itakusaidia uendelee kushikamana na Yehova na uendelee kuheshimia ahadi yenye ulimutolea ya kumutumikia ni kuendelea kufanya maendeleo, ni kusema, “kusonga mbele kuelekea” ukomavu wa Kikristo. (Ebr. 6:1) Mu hii habari, tutazungumuzia namna vijana wanaweza kufanya maendeleo na kufikia kuwa Wakristo wakomavu.

UNAWEZA KUFANYA NINI JUU UFIKIE KUWA MUKRISTO MUKOMAVU?

3. Wakristo wanapaswa kufanya nini kisha kubatizwa?

3 Kisha kubatizwa, siye wote tunapaswa kufuata shauri yenye mutume Paulo alipatia waamini wenzake mu muji wa Efeso. Aliwatia moyo wakuwe Wakristo ‘wenye kukomaa kabisa.’ (Efe. 4:13) Mu maneno ingine, aliwaambia, ‘Muendelee kufanya maendeleo.’ Paulo alilinganisha maendeleo ya kiroho ya Mukristo na namna mutoto anakomalaka. Wakati mutoto anazaliwa, wazazi wake wanamupendaka na kumufurahia sana. Lakini, hawezi kubakia mutoto milele. Kadiri wakati inapita, anapaswa kuacha “tabia za mutoto.” (1 Ko. 13:11) Ni vile pia kwa Wakristo. Kisha kubatizwa, tunapaswa kuendelea kufanya maendeleo. Tuchunguze basi mapendekezo fulani yenye inaweza kutusaidia kufanya vile.

4. Ni sifa gani inaweza kukusaidia kufanya maendeleo ya kiroho? Fasiria. (Wafilipi 1:9)

4 Umupende Yehova zaidi. Tayari unamupenda Yehova sana. Lakini, unaweza kumupenda zaidi. Namna gani? Mu Wafilipi 1:9, (Soma.) Paulo alitaya sifa moya yenye inaweza kutusaidia kufanya maendeleo. Mu ile andiko, Paulo alisali kama upendo wa Wafilipi “ukuwe mwingi zaidi na zaidi.” Kwa hiyo, tunaweza kumupenda Yehova zaidi. Tunaweza kufanya vile kwa kujikaza kupata “ujuzi wenye hauna makosa na utambuzi kamili.” Kadiri tunafikia kumujua Yehova, ni vile tunamupenda na kufurahia sifa zake na matendo yake. Tamaa yetu ya kumufurahisha inakuwa nguvu, na hatupendi hata kidogo kufanya jambo yenye inaweza kumuhuzunisha. Tunafanya yetu yote ili kujua mambo yenye Yehova anapenda tufanye na namna tunaweza kuifanya.

5-6. Nini inaweza kutusaidia tumupende Yehova zaidi? Fasiria.

5 Jambo yenye inaweza kutusaidia tumupende Yehova zaidi ni kumujua muzuri Mwana wake, mwenye alionyesha sifa za Baba yake kwa ukamilifu. (Ebr. 1:3) Njia ya muzuri zaidi ya kutusaidia tumujue Yesu ni kujifunza habari zenye kuwa mu vitabu ine vya Injili. Kama hauyaanza kusoma Biblia kila siku, inaweza kuwa muzuri uanze sasa kusoma habari kuhusu Yesu. Wakati uko nasoma habari kuhusu Yesu, ukazie uangalifu sifa zake. Ilikuwa mwepesi kuzungumuza naye; alipenda kukamata watoto kidogo mu mikono yake. (Mk. 10:13-16) Alifanya wanafunzi wake wajisikie muzuri; walijisikia hata huru kuambia Yesu mawazo yao. (Mt. 16:22) Yesu aliiga kabisa Baba yake wa mbinguni. Ni mwepesi pia kuzungumuza na Yehova. Tunaweza kuzungumuza naye katika sala. Wakati tunasali, tunaweza kumufungulia moyo wetu. Tuko hakika kama hatatuhukumu juu anatupenda na anatuhangaikia.​—1 Pe. 5:7.

6 Yesu alisikilia watu huruma. Matayo anasema hivi: “Wakati aliona watu wengi akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wenye hawana muchungaji.” (Mt. 9:36) Yehova naye anakuwaka na huruma? Yesu alisema hivi: “Baba yangu mwenye kuwa mbinguni hapendi hata mumoja wa hawa wadogo aangamie.” (Mt. 18:14) Ile inatia moyo sana! Wakati tunafikia kumujua Yesu muzuri zaidi, tunamupenda Yehova zaidi.

7. Kupitisha wakati na ndugu na dada kunaweza kukusaidia kufanya nini?

7 Jambo ingine yenye inaweza kukusaidia umupende Yehova zaidi na ukuwe Mukristo mukomavu ni kupitisha wakati na ndugu na dada zako na kujikaza kuwajua muzuri. Ona furaha yenye wako nayo. Hawahuzunikie uamuzi wao wa kumutumikia Yehova. Uwaombe wakuelezee mambo fulani yenye wamejionea mu kazi ya Yehova. Wakati unataka kukamata uamuzi fulani wa maana, uwaombe mashauri. Kumbuka, “kuko mafanikio kupitia washauri wengi.”​—Mez. 11:14.

Unaweza kufanya nini juu uweze kupambana na fundisho ya mageuzi ku masomo? (Ona fungu ya 8-9)

8. Unaweza kufanya nini kama uko na mashaka juu ya mafundisho fulani ya Biblia?

8 Upiganishe mashaka. Kama vile  fungu ya 2 inaonyesha, Shetani atajaribu kukuzuia kufanya maendeleo ya kiroho. Anaweza kufanya vile kwa kukuchochea ukuwe na mashaka juu ya mafundisho fulani ya Biblia. Kwa mufano, siku fulani unaweza kusoma ao kusikia mawazo fulani kuhusu fundisho ya mageuzi yenye kumuzaraulisha Mungu. Wakati ulikuwa mutoto, pengine haukufikiriaka ile jambo. Lakini, pengine juu sasa umekomala, uko nafundishwa ile jambo ku masomo. Mambo yenye walimu wako wanasema juu ya mageuzi inaweza kuonekana kuwa ya kweli na yenye kusadikisha. Lakini, inawezekana hawayachunguzaka ushuhuda wenye unaonyesha kama kuko Muumbaji. Kumbuka kanuni yenye kuwa mu Mezali 18:17: “Mutu wa kwanza kueleza kesi yake ya hukumu anaonekana kuwa anasema kweli, mupaka wakati mwingine anafika na kumuuliza maulizo.” Kuliko kukubali kila kitu yenye unajifunza ku masomo, chunguza kwa uangalifu mambo yenye Neno ya Mungu inasema. Fanya utafiti mu vichapo vyetu. Zungumuza na ndugu na dada wenye walikuwa naamini fundisho ya mageuzi zamani. Uwaulize ni mambo gani yenye iliwahakikishia kama kuko Muumbaji mwenye anatupenda. Kuzungumuza nao kunaweza kukusaidia uvumbule mambo yenye inahakikisha kama kuko Muumbaji.

9. Habari ya Melissa inakufundisha nini?

9 Dada mwenye kuitwa Melissa alifanya utafiti kuhusu uumbaji na ile ilimusaidia sana apiganishe mashaka yenye alikuwa nayo. * Anasema hivi: “Ku masomo, walimu wanafasiria mageuzi mu namna yenye inafanya ionekane kama ni fundisho ya kweli. Ku mwanzo, sikupenda kufanya utafiti. Niliogopa kama nitafikia kuvumbula mambo yenye inaonyesha kuwa fundisho ya mageuzi ni ya kweli. Lakini nilijiambia kama Yehova hapendi tuamini-amini mambo bila kuwa na ushuhuda. Kwa hiyo, nilianza kufanya utafiti. Nilisoma kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? na broshua Uhai​—Ulitokana na Muumba? na Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?​—Maulizo 5 ya Kujiuliza. Ile njo jambo yenye nilipaswa kufanya kabisa. Nilijiuliza juu ya nini sikufanyaka vile zamani.”

10-11. Nini njo inaweza kukusaidia usiangukie mu uasherati? (1 Watesalonike 4:3, 4)

10 Uepuke mwenendo mubaya. Wakati uko kijana, tamaa ya ngono inaweza kuwa nguvu sana, na wengine wanaweza kukuchochea ufanye uasherati. Ni vile njo Shetani anapenda ufanye. Nini njo inaweza kukusaidia usiangukie mu uasherati? (Soma 1 Watesalonike 4:3, 4.) Wakati unasali, umuambie Yehova namna unajisikia, na umuombe akupatie nguvu. (Mt. 6:13) Ukumbuke kama Yehova anapenda kukusaidia, hapana kukuhukumu. (Zb. 103:13, 14) Biblia pia inaweza kukusaidia. Melissa, mwenye tulishazungumuzia, alikuwa na magumu ya kupiganisha mawazo ya uasherati. Anasema hivi: “Kusoma Biblia kila siku kulinisadia niendelee kupiganisha tamaa zangu za mubaya. Kulinikumbusha kama niko mali ya Yehova na kama niko na lazima ya Yehova mu maisha yangu.”​—Zb. 119:9.

11 Usijaribu kumaliza magumu yako weye peke. Ambia wazazi wako mambo yenye iko nakuhangaisha. Haiko mwepesi kuambia wengine mambo yako ya kipekee, lakini, ni jambo ya maana kufanya vile. Melissa anasema hivi: “Nilisali juu nikuwe na uhodari na kisha niliambia baba yangu magumu yenye nilikuwa nayo. Kisha kufanya vile, nilijisikia muzuri zaidi. Nilijua kama Yehova alinifurahia.”

12. Nini njo inaweza kukusaidia kukamata maamuzi ya muzuri?

12 Uache kanuni za Biblia zikuongoze. Kadiri utaendelea kukomala, wazazi wako watakuachia uhuru wa kujikamatia maamuzi ingine. Lakini, kuko mambo mingi yenye haujue. Nini njo itakusaidia uepuke kufanya makosa yenye inaweza kuharibisha urafiki wako na Yehova? (Mez. 22:3) Dada mwenye kuitwa Kari anafasiria mambo yenye ilimusaidia akamate maamuzi ya muzuri. Alielewa kama Mukristo mukomavu hana lazima ya sheria mu kila hali. Anasema hivi: “Nilikuwa na lazima ya kuelewa kanuni za Biblia, hapana tu sheria.” Wakati uko nasoma Biblia, ujiulize hivi: ‘Hii andiko inanisaidia kuelewa mawazo gani ya Yehova? Iko na kanuni zenye zinaweza kunisaidia kujiendesha muzuri? Kama ni vile, kutumikisha zile kanuni kutaniletea faida gani?’ (Zb. 19:7; Isa. 48:17, 18) Kama unakuwa nasoma Biblia na kutafakari kuhusu kanuni zake, itakuwa mwepesi zaidi kwako kukamata maamuzi yenye itamufurahisha Yehova. Utatambua kama hauna lazima ya sheria mu kila hali juu utaelewa mawazo ya Yehova.

Huyu dada kijana alichagua marafiki wa namna gani? (Ona fungu ya 13)

13. Marafiki wazuri wanaweza kukusaidia namna gani? (Mezali 13:20)

13 Uchague marafiki wenye wanamupenda Yehova. Vile tuliona, mu fungu ya 7, marafiki wenye unachagua wanaweza kukusaidia ukomale kiroho. (Soma Mezali 13:20.) Wakati fulani, dada mwenye kuitwa Sara hakukuwa na furaha. Kisha, kulitokea jambo fulani yenye ilimusaidia akuwe tena na furaha. Sara anasema hivi: “Nilipata marafiki wazuri wakati yenye nilikuwa nao lazima kabisa. Kila juma, miye na dada fulani kijana tulikuwa nakutana juu ya kutayarisha Munara wa Mulinzi pamoya. Rafiki mwingine alinisaidia nianze kutoa maelezo ku mikutano. Juu marafiki walinisaidia, nilianza kufanya funzo ya pekee na kusali kwa ukawaida. Urafiki wangu na Yehova ulianza kuwa nguvu zaidi, na nilianza tena kuwa na furaha.”

14. Namna gani Julien alipata marafiki wazuri?

14 Namna gani unaweza kupata marafiki wenye watakusaidia ufanye maendeleo ya kiroho? Julien, mwenye sasa ni muzee wa kutaniko, anasema hivi: “Wakati nilikuwa mudogo, nilifanya urafiki na wale wenye nilihubiri nao. Walikuwa na bidii, na walinisaidia nione namna kazi ya kuhubiri inaletaka furaha sana. Nilianza kuwa na muradi wa kuingia mu utumishi wa wakati yote. Nilitambua pia kama sikukuwa na marafiki wengi wazuri juu nilikuwa natafuta tu marafiki wa miaka yangu. Kisha, nilifanya pia urafiki na wanabeteli. Mufano wao ulinisaidia nichague mambo ya muzuri ya kujifurahisha, na ile ilifanya nimukaribie Yehova zaidi.”

15. Paulo alipatia Timoteo mashauri gani kuhusu urafiki? (2 Timoteo 2:20-22)

15 Ufanye nini kama unatambua kuwa mutu fulani mu kutaniko haiko rafiki muzuri? Paulo alijua kama watu fulani mu kutaniko ya Kikristo ya karne ya kwanza hawakukuwa naona mambo namna Yehova anaiona. Kwa hiyo, aliambia Timoteo awaepuke. (Soma 2 Timoteo 2:20-22.) Urafiki wetu na Yehova ni wa maana sana. Tumetumika sana juu tukuwe marafiki wa Yehova. Kwa hiyo, tusiruhusu mutu yeyote aharibishe ule urafiki.​—Zb. 26:4.

NAMNA GANI KUJIWEKEA MIRADI KUNAWEZA KUKUSAIDIA UFANYE MAENDELEO YA KIROHO?

16. Unapaswa kujiwekea miradi gani?

16 Ujiwekee miradi yenye inafaa. Ujiwekee miradi yenye itasaidia imani yako ikuwe nguvu na yenye itafanya ukuwe Mukristo mukomavu. (Efe. 3:16) Kwa mufano, unaweza kuamua kukuwa najifunza na kusoma Biblia kwa ukawaida. (Zb. 1:2, 3) Ao unaweza kujaribu kukuwa nasali kwa Yehova mara mingi zaidi na kumufungulia Yehova moyo wako. Pengine unapaswa kuwa muangalifu zaidi kuhusu mambo ya kujifurahisha yenye unachaguaka na namna unatumiaka wakati yako. (Efe. 5:15, 16) Yehova atafurahi wakati ataona namna uko najikaza sana kufanya maendeleo zaidi.

Huyu dada kijana alijiwekea muradi gani? (Ona fungu ya 17)

17. Utapata faida gani kama unasaidia wengine?

17 Utaonyesha kama uko Mukristo mukomavu wakati unasaidia wengine. Yesu alisema: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Utakuwa na furaha sana ikiwa unatumia wakati yako na nguvu yako ya ujana juu ya kusaidia wengine. Kwa mufano, unaweza kujiwekea muradi wa kusaidia ndugu na dada wenye kuzeeka na wenye kuwa na ulemavu fulani mu kutaniko yako. Pengine unaweza kuenda kuwauzia vitu fulani ao kuwasaidia kutumia vyombo vyao vya kielektroniki. Kama uko ndugu, ujiwekee muradi wa kuwa mutumishi wa huduma juu uweze kutumikia zaidi ndugu na dada zako. (Flp. 2:4) Unaonyesha pia kama unapenda wale wenye hawako Mashahidi kwa kuwahubiria habari njema ya Ufalme. (Mt. 9:36, 37) Kadiri inawezekana, ujiwekee muradi wa kumutumikia Yehova mu aina fulani ya utumishi wa wakati yote.

18. Utumishi wa wakati yote unaweza kukusaidia namna gani?

18 Utumishi wa wakati yote unaweza kukupatia nafasi za mingi za kufanya maendeleo ya kiroho. Kazi ya upainia inaweza kukufungulia mulango wa kuhuzuria Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Unaweza kutumikia ku Beteli ao mu kazi ya ujenzi. Dada painia kijana mwenye kuitwa Kaitlyn anasema hivi “Kuhubiri na ndugu na dada wenye uzoefu kulinisaidia sana nikomale kiroho kisha kubatizwa. Mufano wao ulinichochea nijifunze Biblia zaidi na nifanye namna yangu ya kufundisha ikuwe muzuri.”

19. Utapata baraka gani kama unaendelea kufanya maendeleo ya kiroho?

19 Kama unaendelea kufanya maendeleo ya kiroho, utapata baraka nyingi. Hautapoteza miaka yako ya ujana mu kufuatia miradi yenye haina maana. (1 Yo. 2:17) Hautapata huzuni yenye mutu anapataka juu ya kukamata maamuzi ya mubaya. Lakini, utakuwa na mafanikio na furaha ya kweli. (Mez. 16:3) Mufano wako muzuri utatia moyo waamini wenzako, ikuwe vijana ao wazee. (1 Ti. 4:12) Na zaidi sana, utatosheka na utakuwa na amani yenye mutu anapataka juu ya kumufurahisha Yehova na juu ya kuwa na urafiki wa karibu naye.​—Mez. 23:15, 16.

WIMBO 88 Unijulishe Njia Zako

^ Watumishi wote wa Yehova wanafurahiaka sana wakati vijana wanabatizwa. Kusema kweli, kisha wanafunzi wapya kubatizwa, wanapaswa kuendelea kufanya maendeleo ya kiroho. Hii habari itatusaidia siye wote mu kutaniko tuchunguze mambo mbalimbali yenye kijana mwenye anatoka kubatizwa anaweza kufanya juu afikie kuwa Mukristo mukomavu.

^ Majina fulani imebadilishwa.