Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 33

Yehova Iko Naona Magumu Yetu na Iko Tayari Kutusaidia

Yehova Iko Naona Magumu Yetu na Iko Tayari Kutusaidia

“Jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa.”​—ZB. 33:18.

WIMBO 4 “Yehova Ni Muchungaji Wangu”

KIFUPI YA HABARI *

1. Juu ya nini Yesu alimuomba Yehova alinde wanafunzi wake?

 USIKU, mbele ya kifo yake, Yesu alimuomba Baba yake wa mbinguni jambo fulani ya pekee. Alimuomba Yehova alinde wanafunzi wake. Sikuzote Yehova amelinda na kuhangaikia watu wake. Lakini, Yesu alijua kama Shetani angechukia sana wanafunzi wake. Yesu alijua pia kama wangekuwa na lazima ya musaada wa Yehova wakati Shetani angewashambulia.

2. Kulingana na Zaburi 33:18-20, juu ya nini hatupaswe kuogopa magumu?

2 Hii dunia yenye kuongozwa na Shetani inaletea Wakristo wa kweli magumu mingi sana leo. Tunakutana na majaribu yenye inaweza kutuvunja moyo na hata kufanya ikuwe nguvu kwetu kuwa washikamanifu kwa Yehova. Lakini, sawa vile tutaona mu hii habari, hatupaswe kuogopa. Juu ya nini? Juu Yehova iko naona magumu yenye tuko nakutana nayo na kila wakati iko tayari kutusaidia kupambana nayo. Tuchunguze mifano mbili ya Biblia yenye inaonyesha namna Yehova ‘analinda wale wenye kumuogopa.’​—Soma Zaburi 33:18-20.

WAKATI TUNAJISIKIA KUWA PEKE YETU

3. Ni wakati gani tunaweza kujisikia kuwa peke yetu?

3 Hata kama tuko na ndugu na dada wengi mu kutaniko, wakati fulani tunaweza kujisikia kuwa peke yetu. Kwa mufano, vijana wanaweza kujisikia sawa vile hakuna mutu wa kuwasaidia wakati wanaeleza mambo yenye wanaamini mbele ya wanafunzi wenzao ao wakati wanahamia mu kutaniko ya mupya. Wengine kati yetu wanaweza kuwa na huzuni ao kuvunjika moyo na kuwaza kama hawana mutu wa kuwasaidia. Tunaweza kujizuia kuambia wengine namna tuko najisikia juu tunawaza kama pengine hawatatuelewa. Na wakati fulani, tunaweza hata kujiuliza kama kuko mutu mwenye anatuhangaikia kabisa. Kujisikia kuwa peke yetu, hata ikuwe juu ya sababu gani, kunaweza kutufanya tujisikie sawa vile hatuna mutu wa kutusaidia na kunaweza kutuletea mahangaiko. Yehova hapendi hata kidogo tujisikie vile. Juu ya nini tunasema vile?

4. Pengine ni juu ya nini nabii Eliya alisema: “Ni mimi tu ndiye nimebakia”?

4 Fikiria mufano wa mwanaume muaminifu Eliya. Yezebeli alisema kama atamuua. Kwa hiyo, Eliya alikimbia na kujificha kwa zaidi ya siku 40. (1 Fa. 19:1-9) Ku mwisho, wakati alikuwa yeye peke mu pango, alimuambia Yehova hivi: “Ni mimi tu ndiye [nabii mwenye] nimebakia.” (1 Fa. 19:10) Hakukuwa yeye peke; kulikuwa kungali manabii wengine mu inchi ya Israeli. Obadia aliweza kuficha manabii 100 juu Yezebeli asiwaue. (1 Fa. 18:7, 13) Sasa, juu ya nini Eliya alijisikia kuwa peke yake? Pengine aliwaza kama manabii wote wenye Obadia alificha walikuwa wamekufa. Pengine alijisikia kuwa peke yake juu hakuna mutu mwingine mwenye alianza kumutumikia Yehova pamoya naye hata kisha Yehova kuonyesha kama yeye njo Mungu wa kweli ku Mulima Karmeli. Ao pengine aliwaza kama hakuna mutu mwenye anajua kuwa maadui wake wako natafuta kumuua, ao tena aliwaza kama hakuna mutu mwenye anamuhangaikia. Biblia haituambie kabisa juu ya nini Eliya alijisikia kuwa peke yake. Lakini, tunajua kama Yehova alielewa juu ya nini Eliya alijisikia vile na alijua kabisa namna ya kumusaidia.

Wakati tunajisikia kuwa peke yetu, namna Yehova alimusaidia Eliya inaweza kutufundisha nini? (Ona fungu ya 5-6)

5. Yehova alifanya nini juu ya kumuhakikishia Eliya kama haiko peke yake?

5 Yehova alifanya mambo fulani juu ya kumusaidia Eliya. Alimutia Eliya moyo amufasirie. Mara mbili alimuuliza: “Unafanya nini hapa?” (1 Fa. 19:9, 13) Kila mara, Yehova alisikiliza wakati Eliya alikuwa namuambia namna alikuwa najisikia. Yehova alimujibia Eliya kwa kumuonyesha kama alikuwa pale na kama iko na uwezo sana. Tena, Yehova alimuhakikishia kama kuko Waisraeli wengi wenye wangali wanamuabudu. (1 Fa. 19:11, 12, 18) Bila shaka, kisha kumuambia Yehova namna alikuwa najisikia na kusikia jibu ya Yehova, Eliya alitulia. Yehova alimupatia Eliya kazi fulani ya maana ya kufanya. Alimuomba atie Hazaeli mafuta juu akuwe mufalme wa Siria, atie Yehu mafuta juu akuwe mufalme wa Israeli, na atie Elisha mafuta juu akuwe nabii. (1 Fa. 19:15, 16) Wakati Yehova alimupatia ile kazi, alimusaidia akaze akili yake juu ya mambo ya muzuri. Alimupatia pia rafiki wa karibu, Elisha. Yehova anatusaidiaka namna gani wakati tunajisikia kuwa peke yetu?

6. Unaweza kumuambia Yehova nini wakati unajisikia kuwa peke yako? (Zaburi 62:8)

6 Yehova anatuomba tusali kwake. Iko naona magumu yetu, na anatuhakikishia kama iko tayari kila wakati kusikiliza sala zetu. (1 Te. 5:17) Anafurahiaka sana kusikiliza sala za waabudu wake. (Mez. 15:8) Unaweza kumuambia nini wakati unajisikia kuwa peke yako? Umuambie namna uko najisikia, sawa vile Eliya alifanya. (Soma Zaburi 62:8.) Umuambie mahangaiko yako na namna inakufanya ujisikie. Umuombe akusaidie kujua mambo ya kufanya wakati unajisikia kuwa peke yako ao mwenye huzuni. Kwa mufano, wakati unajisikia sawa vile hakuna mutu wa kukusaidia, ao unaogopa wakati uko nahubiri ku masomo, umuombe Yehova akupatie uhodari wenye uko nao lazima juu ujieleze bila woga. Unaweza hata kumuomba hekima ya kukusaidia ufasirie mambo yenye unaamini kwa busara. (Lu. 21:14, 15) Kama umevunjika moyo ao uko na huzuni, umuombe Yehova akupatie nguvu ya kuelezea Mukristo mukomavu namna uko najisikia. Unaweza kumuomba Yehova asaidie ule mwenye utaelezea magumu akusikilize na kukuelewa. Kama unamuambia Yehova namna uko najisikia, unajikaza kuona namna iko najibia sala zako, na kukubali musaada wa wengine, hautajisikia kuwa peke yako.

Unaweza kufanya nini juu uhubiri zaidi na juu uhubiri pamoya na wengine? (Ona fungu ya 7)

7. Mufano wa Mauricio unakufundisha nini?

7 Yehova ametupatia siye wote kazi ya maana ya kufanya. Ukuwe hakika kama anaona na anafurahia mambo yote yenye unafanya mu kutaniko na mu kazi ya kuhubiri. (Zb. 110:3) Kuhubiri sana kunaweza kukusaidia wakati unajisikia kuwa peke yako. Namna gani? Fikiria mufano wa ndugu kijana mwenye kuitwa Mauricio. * Kisha tu Mauricio kubatizwa, rafiki yake mumoja wa karibu sana alianza pole kwa pole kuacha kweli. Mauricio anasema hivi: “Kuona namna alimuacha Yehova kulinifanya nisijitumainie. Nilijiuliza kama nitaweza kuheshimia ahadi yenye nilimutolea Yehova na kama nitaweza kuendelea kuwa mu familia yake. Nilijisikia kuwa peke yangu, na nikawaza kama hakuna mwenye angenielewa.” Nini njo ilisaidia Mauricio? Anasema hivi: “Nilianza kuhubiri sana. Ile ilinisaidia niache kujifikiria na niache kuwa na mawazo ya mubaya. Kuhubiri na wengine kulinisaidia nikuwe na furaha na nisijikie kuwa peke yangu.” Kwa kweli, hata wakati haiwezekane tukuwe uso kwa uso na ndugu zetu mu kazi ya kuhubiri, tunatiwa nguvu wakati tunahubiri nao kupitia barua na kupitia telefone. Ni nini ingine yenye ilisaidia Mauricio? Anasema tena hivi: “Zaidi ya ile, nilitumika sana mu kutaniko. Nilikuwa nafanya yangu yote juu ya kutayarisha na kupitisha vipindi ku mikutano. Kufanya vile kulinisaidia kutambua kama Yehova ananiona kuwa wa maana na kama wengine pia wananiona kuwa wa maana.”

WAKATI TUNAVUNJIKA MOYO

8. Magumu inaweza kufanya tujisikie namna gani?

8 Tunajua kama tutapata magumu mu siku hizi za mwisho. (2 Ti. 3:1) Lakini, magumu fulani inaweza kutufikia wakati yenye hatukuwazia. Bila kutazamia, tunaweza kuwa na magumu ya kupata makuta, tunaweza kuvumbuliwa na ugonjwa fulani wa nguvu sana, ao tunaweza kufiwa na mutu fulani mwenye tunapenda sana. Wakati mambo ya vile inatokea, tunaweza kuwa na mahangaiko na kuvunjika moyo, zaidi sana wakati inaonekana sawa vile magumu yetu iko nafuatana-fuatana ao yote inatokea wakati moya. Lakini, ukumbuke kama Yehova anajua mambo yenye iko nakufikia, na anaweza kukusaidia kuvumilia magumu yoyote.

9. Yobu alipata magumu gani?

9 Fikiria mufano wa mwanaume muaminifu Yobu. Alipata magumu mingi mu wakati kidogo tu. Siku moya, Yobu alipata habari kama wanyama wake fulani wameibwa na wengine wameuawa, na kama watumishi wake na watoto wake wameuawa. (Yob. 1:13-19) Siku kidogo tu kisha pale, wakati Yobu alikuwa angali na huzuni ya mingi, alipigwa na ugonjwa mubaya sana. (Yob. 2:7) Hali yake ilikuwa mubaya sana mupaka akafikia kusema hivi: “Ninachukia maisha yangu; sitaki kuendelea kuishi.”​—Yob. 7:16.

Yehova alimuambia Yobu namna anahangaikia kila kitu yenye aliumba juu Yobu aamini kama Yehova anamupenda na kumuhangaikia (Ona fungu ya 10)

10. Yehova alifanya nini juu ya kumusaidia Yobu avumilie magumu yake? (Ona picha ku jalada.)

10 Yehova alikuwa naona mambo yenye ilikuwa namupata Yobu. Juu Yehova alimupenda Yobu, alimupatia nguvu ya kuvumilia magumu yake na kuendelea kuwa muaminifu. Yehova aliongea na Yobu, alimukumbusha kama iko na hekima sana, na kama anapenda viumbe wake. Yehova alizungumuzia wanyama wengi wenye kushangaza. (Yob. 38:1, 2; 39:9, 13, 19, 27; 40:15; 41:1, 2) Tena, Yehova alitumia kijana muaminifu mwenye kuitwa Elihu juu ya kumutia moyo Yobu na kumufariji. Elihu alimuhakikishia Yobu kama sikuzote Yehova anabariki waabudu wake juu ya uvumilivu wao. Lakini, Yehova alimuchochea pia Elihu amupatie Yobu mashauri fulani. Elihu alimusaidia Yobu aache kujiona kuwa mwenye haki. Alifanya vile kwa kumukumbusha kama hatuko kitu kwa kulinganishwa na Yehova, Muumbaji wa ulimwengu wote. (Yob. 37:14) Pia, Yehova alimupatia Yobu kazi fulani. Alimuambia asali kwa ajili ya marafiki wake watatu wenye walikuwa wamefanya zambi. (Yob. 42:8-10) Namna gani Yehova anatusaidiaka leo wakati tunakutana na magumu?

11. Biblia inatuambia mambo gani yenye inaweza kutufariji wakati ya magumu?

11 Yehova haongeake na siye moja kwa moja sawa vile aliongea na Yobu. Lakini, anaongeaka na siye kupitia Neno yake, Biblia. (Ro. 15:4) Anatufariji kwa kutupatia tumaini. Fikiria mawazo fulani ya Biblia yenye inaweza kutufariji wakati tuko mu magumu. Kupitia Maandiko, Yehova anatuhakikisha kama hakuna kitu, ikuwe magumu ya nguvu, yenye inaweza “kututenganisha na upendo [wake].” (Ro. 8:38, 39) Tena, anatuhakikishia kama “iko karibu na wale wote wenye kumuitia” katika sala. (Zb. 145:18) Yehova anatuambia kama ikiwa tunamutegemea, tunaweza kuvumilia magumu yoyote na hata kuwa na furaha kwa kiasi fulani wakati tuko nateseka. (1 Ko. 10:13; Yak. 1:2, 12) Biblia inatukumbusha kama magumu yetu ni ya wakati kidogo kama tunailinganisha na baraka za milele zenye Mungu anatupatia. (2 Ko. 4:16-18) Yehova anatupatia tumaini ya kama ataharibu chanzo ya magumu yetu yote, ni kusema, Shetani na wale wote wenye wanaiga njia zake za uovu. (Zb. 37:10) Ulishaweka mu akili maandiko fulani ya Biblia yenye kutia moyo na yenye inaweza kukusaidia kuvumilia magumu yenye unaweza kupata wakati yenye kuya?

12. Yehova anapenda tufanye nini juu Neno yake itusaidie kabisa?

12 Yehova anatuomba tupange wakati ya kujifunza Biblia kwa ukawaida na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma. Wakati tunatumikisha mambo yenye tunajifunza, imani yetu inakuwa nguvu zaidi, na tunamukaribia zaidi Baba yetu wa mbinguni. Na ile inafanya tukuwe na nguvu ya kuvumilia magumu. Tena, Yehova anapatia roho yake takatifu wale wenye wanapenda Neno yake, Biblia. Na ile roho inaweza kutupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida” juu tuweze kuvumilia jaribu yoyote.​—2 Ko. 4:7-10.

13. Chakula ya kiroho yenye “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anatupatia inatusaidia namna gani?

13 Kwa musaada wa Yehova, “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anatupatia kwa uwingi habari, video, na nyimbo zenye zinaweza kutusaidia tuendelee kuwa na imani ya nguvu na kuwa macho kiroho. (Mt. 24:45) Tunapaswa kufaidika kabisa na kila kitu yenye Yehova anatupatia kwa wakati yenye kufaa. Hivi karibuni, dada fulani wa Amerika alionyesha shukrani yake kwa ajili ya chakula yote ya kiroho yenye tunapata. Alisema hivi: “Kwa miaka 40 yenye nimemutumikia Yehova, imani yangu imejaribiwa tena na tena.” Alipata magumu fulani ya nguvu sana: Tate (ao kambo) yake mwanaume aliuawa na shofere fulani mulevi, wazazi wake walikufa na ugonjwa fulani hatari, na aligonjwa kansere mara mbili. Nini njo ilimusaidia kuvumilia? Alisema hivi: “Kila mara Yehova amenihangaikia. Chakula ya kiroho yenye ametutolea kupitia mutumwa muaminifu na mwenye busara imenisaidia kuvumilia. Njo maana, sawa vile Yobu, na miye naweza kusema hivi: ‘Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!’”​—Yob. 27:5.

Tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia wengine mu kutaniko? (Ona fungu ya 14)

14. Namna gani Yehova anatumia ndugu na dada zetu juu ya kutusaidia wakati ya magumu? (1 Watesalonike 4:9)

14 Yehova amefundisha watu wake kupendana na kufarijiana wakati ya magumu. (2 Ko. 1:3, 4; soma 1 Watesalonike 4:9.) Ndugu na dada zetu wanamuiga Elihu. Wako tayari kutusaidia tuendelee kuwa waaminifu wakati ya magumu. (Mdo. 14:22) Tufikirie mufano wa Diane. Ndugu na dada mu kutaniko yake walimutia moyo na kumusaidia aendelee kuwa nguvu kiroho kisha bwana yake kupata ugonjwa fulani hatari. Alisema hivi: “Haikukuwa mwepesi. Lakini, tulijionea namna Yehova alitusaidia kwa upendo kabisa mu ile miezi ya magumu. Ndugu na dada mu kutaniko walifanya mambo mingi juu ya kutusaidia. Walitutembelea, walituita ku telefone, walitukumbatia, na ile yote ilitusaidia kuvumilia. Juu sijue kutembeza gari, ndugu na dada walifanya mipango juu nisikose mikutano na juu nisikose kuenda mu mahubiri kadiri ningeweza.” Ni baraka kabisa kuwa mu hii familia ya ndugu na dada wenye upendo!

UMUSHUKURU YEHOVA JUU ANATUHANGAIKIAKA KWA UPENDO

15. Juu ya nini tuko hakika kama tunaweza kuvumilia magumu?

15 Siye wote tutapata majaribu fulani. Lakini, sawa vile tumejifunza hatutakuwa peke yetu hata kidogo wakati tutapata majaribu. Sawa vile baba mwenye upendo, kila siku Yehova anaona magumu yetu. Iko karibu na siye, iko tayari kusikiliza sala zetu za kumuomba musaada, na iko tayari kutusaidia. (Isa. 43:2) Tuko hakika kama tunaweza kuvumilia magumu juu ametupatia kwa ukarimu mambo yote yenye tuko nayo lazima ili tuvumilie. Ametupatia pendeleo ya kusali kwake, Biblia, chakula mingi ya kiroho, na familia ya ndugu na dada wenye upendo juu ya kutusaidia wakati ya magumu.

16. Tunapaswa kufanya nini juu Yehova aendelee kutuhangaikia kwa upendo?

16 Tuko wenye shukrani sana juu tuko na Baba yetu wa mbinguni mwenye iko naona magumu yetu! “Mioyo yetu inashangilia katika yeye.” (Zb. 33:21) Tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani juu ya namna Yehova anatuhangaikia kwa upendo kwa kufaidika kabisa na mipango yote yenye amekamata juu ya kutusaidia. Na siye kuko mambo yenye tunapaswa kufanya juu Mungu aendelee kutuhangaikia. Kwa hiyo, kama tunaendelea kufanya yetu yote juu ya kumutii Yehova na kufanya mambo yenye anakubali, ataendelea kutuhangaikia kwa upendo!​—1 Pe. 3:12.

WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, na Rafiki Yangu

^ Tuko na lazima ya musaada wa Yehova juu tuweze kupambana na magumu yenye tuko nayo leo. Mu hii habari, tutaona kama Yehova anahangaikia watumishi wake. Iko naona magumu ya kila mutumishi wake na anamusaidia kupambana na ile magumu.

^ Majina fulani imebadilishwa.