Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Paulo alipenda kusema nini wakati alijiita kuwa “mutoto mwenye alizaliwa mbele ya wakati wake”? (1 Wakorinto 15:8)

Kulingana na 1 Wakorinto 15:8, Paulo alisema hivi: “Mwisho kabisa alinitokea mimi pia kama vile kwa mutoto mwenye alizaliwa mbele ya wakati wake.” Zamani, tulifasiria kama inaonekana Paulo alikuwa nazungumuzia mambo yenye ilimufikia wakati alipata maono ya Yesu katika utukufu wake wa mbinguni. Ilikuwa sawa vile Paulo alipewa pendeleo ya kuzaliwa ao kufufuliwa, na kupewa uzima wa kiroho mbele ya wakati, ni kusema, miaka mingi mbele ufufuo wa Wakristo watiwa-mafuta kuanza. Lakini, kisha kuchunguza tena ile andiko, inaonekana ni jambo ya lazima kubadilisha namna tulikuwa naielewa.

Kwa kweli, mu ile andiko, Paulo alikuwa nazungumuzia mambo yenye ilitokea wakati aligeuka na kuwa Mukristo. Lakini, alimaanisha nini wakati alisema kama “alizaliwa mbele ya wakati wake”? Kuko mambo mbalimbali yenye pengine alimaanisha.

Pengine alimaanisha kama namna aligeuka na kuwa Mukristo ilitokea haraka na ilileta maumivu. Mara mingi, mutoto mwenye anazaliwa mbele ya wakati, anazaliwaka saa yenye watu hawawazie. Ilikuwa vile pia kuhusu Sauli (mwenye alifikia kuitwa Paulo). Wakati alikuwa naenda Damasko juu ya kutesa Wakristo, hakukuwa nawazia kama angeona maono ya Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa. Kugeuka kwa Paulo na kuwa Mukristo kulimushangaza na kulishangaza pia Wakristo wa mu muji wa Damasko wenye alikuwa napanga kutesa. Zaidi ya ile, mambo yenye ilimufikia, ilimuletea maumivu sana na hata akakuwa kipofu kwa wakati fulani.​—Mdo. 9:1-9, 17-19.

Pengine alimaanisha kama aligeuka na kuwa Mukristo “wakati yenye haifae.” Neno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “mutoto mwenye alizaliwa mbele ya wakati wake” inaweza pia kumaanisha “mutoto mwenye alizaliwa wakati yenye haifae.” Bible de Jerusalem inatafsiri ile andiko hivi: “Ilikuwa sawa vile nilizaliwa wakati yenye hakuna mutu aliwazia.” Wakati Paulo aligeuka na kuwa Mukristo, Yesu alikuwa tayari amerudia mbinguni. Tofauti na wale wenye Paulo alizungumuzia mu maandiko yenye kutangulia, yeye hakuonaka Yesu mbele Yesu aende mbinguni. (1 Ko. 15:4-8) Wakati Yesu alimutokea bila yeye kutazamia, alimupatia Paulo nafasi ya kumuona kisha ufufuo wake, hata kama ile ilionekana kuwa “wakati yenye haifae.”

Pengine alikuwa nazungumuzia kwa unyenyekevu mambo yenye ilimufikia. Watu fulani wenye elimu wanasema kama maneno yenye Paulo alitumia hapa inaweza kusikilika sawa vile alikuwa najizarau. Kama ni vile, ni kusema, Paulo alitambua kama hakustahili pendeleo yenye alipewa. Njo maana, alisema hivi: “Mimi ni mudogo zaidi kati ya mitume, na sistahili kuitwa mutume, kwa sababu nilitesa kutaniko la Mungu. Lakini kwa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu mimi niko kile niko.”​—1 Ko. 15:9, 10.

Kwa hiyo, inaonekana Paulo alikuwa nazungumuzia namna Yesu alimutokea haraka na wakati yenye hakuwazia, namna aligeuka na kuwa Mukristo wakati yenye hakutazamia, ao alimaanisha kama hakustahili kupewa maono yenye kushangaza vile. Ikuwe ni vile ao hapana, Paulo aliona mambo yenye ilimufikia kuwa ya maana sana. Ilimuhakikishia kabisa kama Yesu alikuwa amefufuliwa. Bila shaka, wakati Paulo alikuwa nahubiria wengine kuhusu ufufuo wa Yesu, alizoea kuzungumuzia mambo yenye ilimufikia bila yeye kutazamia.​—Mdo. 22:6-11; 26:13-18.