Ona video zinazopatikana

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Kulingana na kanuni za Biblia zenye kuzungumuzia njia yenye kufaa ya kutumia damu, Mashahidi wa Yehova wako na mawazo gani juu ya matunzo yenye inaomba kutumia damu ya mutu?

Wakati Mukristo anataka kukamata uamuzi kuhusu matunzo yenye inaomba damu yake itumiwe, anapaswa kufikiria mambo yenye Biblia inasema. Hapana mambo yenye yeye mwenyewe anapenda ao yenye munganga anapenda. Ni jambo yenye haihusu watu wengine. Inahusu tu yeye na Yehova.

Yehova, mwenye alitupatia uzima, anakataza kabisa kula damu. (Mwanzo 9:3, 4) Mu Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli wa zamani, alionyesha namna damu inapaswa kutumiwa juu damu ni uzima. Alisema hivi: “Kwa maana uzima wa mwili uko katika damu, na mimi mwenyewe nimeitoa kwenye mazabahu kwa ajili yenu ili mufunike zambi kwa ajili yenu wenyewe.” Sasa mutu alipaswa kufanya nini kama anaua munyama kwa ajili ya chakula? Mungu alisema hivi: “Anapaswa kumwanga damu yake chini na kuifunika kwa mavumbi.” * (Mambo ya Walawi 17:11, 13) Yehova alirudilia ile amri tena na tena. (Kumbukumbu la Torati 12:16, 24; 15:23) Kitabu fulani ya Wayahudi, yenye kuzungumuzia Sheria ya Musa inasema hivi: “Mwisraeli hakupaswa kuweka damu, lakini alipaswa kuimwanga chini juu mutu yeyote asiikule.” Hakuna Mwisraeli mwenye alipaswa kukamata damu, kuiweka, na kutumia damu ya munyama mwingine yeyote, mwenye uzima wake ulitoka kwa Mungu.

Wakati Masiya alikufa, watu hawakulazimika tena kufuata Sheria ya Musa. Lakini mawazo ya Yehova kuhusu damu haiyabadilika. Roho yake iliongoza mitume waambie Wakristo kama wanapaswa ‘kujiepusha na damu.’ Ile ilikuwa jambo nzito. Walipaswa kujiepusha na damu sawa vile tu walipaswa kujiepusha na uasherati ao ibada ya sanamu. (Matendo 15:28, 29; 21:25) Kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, ilianza kuwa kawaida sana kutoa damu na kutiwa damu mu mishipa. Lakini Mashahidi wa Yehova walielewa kama kufanya vile kulipingana na mambo yenye Biblia inafundisha.

Wakati fulani, munganga anaweza kuambia mugonjwa akuye wamutoshe damu na waiweke kwa majuma fulani mbele ya siku ya upasuaji, juu wamutie ile damu kama inakuwa lazima kufanya vile. Lakini, kutoa damu, kuiweka, na kuitia mu mishipa kunapingana na mambo yenye kitabu ya Walawi na Kumbukumbu la Torati inasema. Hatupaswe kuweka damu, tunapaswa kuimwanga chini. Wakati tunaimwanga chini, ni sawa vile tunairudishia Mungu. Ni kweli kwamba hatufuate Sheria ya Musa leo, lakini Mashahidi wa Yehova wanaheshimia kanuni za Mungu zenye kuwa mu ile Sheria, na wanaamua ‘kujiepusha na damu.’ Njo maana hatutoleake watu damu yetu na hatukubali damu yetu iwekwe juu watutie tena ile damu mu mishipa. Tunajua kama damu inapaswa ‘kumwangwa.’ Kupatia watu damu na kuiweka juu itiliwe mu mishipa yetu kunapingana na Sheria ya Mungu.

Kuko matumizi ingine ya damu yenye Biblia haizungumuzie. Kwa mufano Wakristo fulani wamekubali wanganga wachukue sehemu fulani ya damu yao juu ya kuipima, na kisha ile damu inamwangwa. Kuko ingine matumizi ya damu yenye tunapaswa kujiamulia ikiwa tutaikubali ao hapana.

Kwa mufano, kuko ile yenye inaitwa hemodilution, ni kusema wakati wa upasuaji, sehemu fulani ya damu ya mutu inaweza kutiwa mu mashini, kisha damu yenye inabakia mu mwili wake inafanywa kuwa majimaji. Na kisha ile damu yenye ilikuwa mu mashini inarudishwa tena mu mwili wake. Kuko ingine yenye inaitwa récupération du sang épanché, ni kusema, wakati wa upasuaji, damu yenye mugonjwa iko anapoteza, inaingizwa mu mashini, inasafishwa, na kisha inarudishwa tena mu mwili wake. Na kuko ingine aina ya matunzo, yenye damu ya mugonjwa inatiwaka mu mashini yenye kutumika sawa vile moyo, mapafu, ao figo. Na kuko matunzo ingine yenye damu inatiwaka mu aina fulani ya mashini, yenye inagabulaka ile damu mu sehemu mbalimbali, juu ya kutosha ndani sehemu zenye kuwa hatari ao zenye kuharibika. Ao tena damu inaweza kuachanishwa mu sehemu mbalimbali juu sehemu fulani zitiwe fasi ingine mu mwili. Na mu hali fulani, wanganga wanaweza kuchukua sehemu fulani ya damu yetu, kuongeza kitu fulani mu ile damu, na kisha kuiingiza tena mu mwili wetu juu waweze kufanya vipimo fulani. Ao munganga anaweza kuchanga ile damu na dawa na kuirudisha mu mwili wa mugonjwa.

Kuko aina za mingi za matunzo, na wanganga wanaendelea kutokeza aina zingine za matunzo. Haiko kazi yetu kuambia wengine mambo yenye wanapaswa kufanya mu kila hali. Wakati Mukristo iko na lazima ya matunzo, anapaswa kuamua ni aina gani ya matunzo yenye atakubali. Mbele ya kupata matunzo, anapaswa kwanza kuuliza munganga ikiwa damu yake itatumiwa namna gani. Na kisha anapaswa kufuata zamiri yake.

Wakristo wanapaswa kukumbuka kama wamejitoa kwa Mungu na wanapaswa, ‘kumupenda kwa moyo wao wote na kwa nafsi yao yote na kwa nguvu zao zote na kwa akili yao yote.’ (Luka 10:27) Mashahidi wa Yehova wanaona kama ni jambo ya maana sana kumutii Mungu na kuendelea kuwa na uhusiano muzuri pamoja naye. Yehova mwenye alitupatia uzima anatuambia tukuwe na imani katika damu yenye Yesu alimwanga. Biblia inasema hivi: “Kupitia yeye [Yesu Kristo] tunaachiliwa huru kwa njia ya bei ya ukombozi kupitia damu ya huyo, ndiyo musamaha wa makosa yetu.”​—Waefeso 1:7.

[Maelezo ya chini]

^ Profesere Frank Gorman aliandika hivi: “Wakati mutu alimwanga damu chini, alionyesha kama anaheshimia uzima wa ule munyama, na alionyesha kama anamuheshimia Mungu mwenye aliumba ule munyama na kuendelea kutunza uzima wake.”

[Kisanduku/​Picha]

MAULIZO YA KUJIULIZA

Kama damu yangu inatoshwa ndani ya mwili wangu na pengine inaacha hata kutembea mu mwili kwa wakati fulani, zamiri yangu itaona kama ile damu ingali sehemu ya mwili wangu, ao itaona kama inapaswa ‘kumwangwa kwenye udongo’?

Kama wakati ya matunzo sehemu ya damu yangu inatoshwa, narekebishwa, na kurudishwa tena ndani ya mwili wangu, zamiri yangu yenye kuzoezwa na Biblia itani sumbua ao hapana?