Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova wanakubali sehemu za kidogo-kidogo za damu?

Mashahidi wa Yehova wanakubali sehemu za kidogo-kidogo za damu?

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Mashahidi wa Yehova wanakubali sehemu za kidogo-kidogo za damu?

Hii habari ilitolewa kwa mara ya kwanza mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 6, 2000.

Bila kuenda mbali, Mashahidi wa Yehova hawakubali damu. Tunaamini kama sheria ya Mungu kuhusu damu haiwezi kubadilika. Lakini leo, damu inaweza kugawanywa mu sehemu ine kubwa, na zile sehemu ine kubwa zinaweza pia kugawanywa mu sehemu za kidogo-kidogo. Kwa hiyo, Mukristo anapaswa kuamua ikiwa atakubali ao hatakubali sehemu za kidogo-kidogo za damu. Hapaswe tu kufikiria faida ao hatari yenye matunzo fulani itamuletea. Lakini jambo ya maana zaidi yenye anapaswa kufanya ni kutii mambo yenye Biblia inasema na kumufurahisha Mungu.

Mambo yenye Biblia inasema kuhusu damu iko wazi. Tuone basi mambo yenye inaweza kutusaidia tuamue muzuri.

Yehova alimuambia Noa kama damu inapaswa kuonwa kuwa kitu ya pekee. (Mwanzo 9:3, 4) Kisha, sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli ilionyesha kama damu ni takatifu. Ile sheria ilisema hivi: “Kama mutu yeyote wa nyumba ya Israeli ao mugeni yeyote . . . anakula damu ya namna yoyote, hakika nitakunja uso wangu juu ya mutu huyo mwenye anakula damu.” Kama Mwisraeli angekosa kutii ile sheria, angechochea wengine pia wafanye vile. Njo maana Mungu alisema hivi: “Nitamuondoa katikati ya watu wake.” (Mambo ya Walawi 17:10) Miaka mingi kisha pale, wakati mitume na wazee walikuwa ku mukutano Yerusalemu, waliamua kama Wakristo wanapaswa ‘kujiepusha na damu.’ Kujiepusha na damu ni jambo ya maana sana, sawa vile kujiepusha na uasherati na ibada ya sanamu.​​—Matendo 15:28, 29.

Ile wakati, Wakristo walipaswa kufanya nini juu ya kuonyesha kama ‘wanajiepusha na damu’? Wakristo hawakukuwa nakula damu ya mubichi, ao ya kuganda; na hawakukuwa nakula nyamafu. Tena, hawakukuwa nakula chakula yenye iliongezwa damu, sawa vile sosise ya damu. Kula damu mu njia yoyote ingekuwa kuvunja sheria ya Mungu.​—1 Samweli 14:32, 33.

Zamani, watu wengi hawakuona kama kula ao kunywa damu ni makosa. Maneno ya Tertullian, mwenye aliishi mu kipindi kati ya mwaka wa 200 na 300 hivi kisha Kristo, inaonyesha vile. Alionyesha kama watu wa makabila fulani walikuwa nakunywa damu wakati walikuwa nafanya mapatano. Alisema pia kama watu walikuwa nakunywa damu ya “watu wenye waliuawa mu viwanja vya michezo . . . Walikuwa nakunywa damu juu waliwaza kama itaponyesha ugonjwa wa kifafa.”

Wakristo waliona kama kufanya vile ni mubaya, hata kama Waroma walikuwa nafanya vile juu ya kutunza magonjwa. Tertullian aliandika hivi: “Hatutiake hata damu ya wanyama mu chakula yetu.” Juu ya kuona kama mutu fulani ni Mukristo wa kweli ao hapana, Waroma walikuwa namupatia chakula yenye kuwa na damu. Tertullian aliongeza hivi: “Kama Wakristo wanakatala kula damu ya wanyama, unawaza kama damu ya watu njo watakunywa?”

Leo, watu fulani wanawaza kama sheria ya Mungu haikataze kutumia damu mu mambo ya matunzo, ikiwa munganga anasema kama ni lazima kufanya vile. Mashahidi wa Yehova hawapendake kufa. Lakini pia wanapenda kutii sheria ya Mungu kuhusu damu. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunatii sheria ya Mungu mu matunzo yenye inaomba kutumia damu?

Kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, wanganga walianza kutia watu damu sana mu mishipa. Lakini Mashahidi wa Yehova walielewa kama kutia damu mu mishipa kunapingana na sheria ya Mungu, na tungali na ile mawazo mupaka leo. Hata vile, kumekuwa maendeleo mingi mu mambo ya matunzo. Leo, wanganga hawatiake sana watu damu, lakini wanazoea sasa kutia watu sehemu moya kati ya sehemu ine kubwa za damu. Zile sehemu ni (1) chembe nyekundu; (2) chembe nyeupe; (3) vigandisha-damu; na (4) plazma, ni kusema umaji-maji wa damu. Kulingana na hali ya mugonjwa, munganga anaweza kuamua ikiwa atatiwa chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, ao plazma. Juu damu inaweza kugawanywa mu sehemu mbalimbali, inaweza kutumiwa kutunza wagonjwa wengi. Mashahidi wa Yehova wanaamini kama kutiwa damu yenye kuenea, ao kutiwa moya kati ya sehemu zake ine kubwa ni kuvunja sheria ya Mungu. Ile imewasaidia wasipate magonjwa sawa vile hépatite, ao SIDA, yenye mutu anaweza kupata wakati anatiwa damu ya mutu mwingine mu mishipa.

Lakini zile sehemu ine kubwa za damu zinaweza pia kugawanywa mu sehemu za kidogo-kidogo zaidi. Zile sehemu za kidogo-kidogo zinatumiwaka namna gani? Na nini njo inaweza kusaidia Mukristo aamue ikiwa atazikubali ao hapana?

Damu inafanyizwa na mambo mingi sana. Hata plazma, yenye sehemu yake kubwa ni maji, nayo iko na mambo ingine ya mingi. Kwa mufano, iko na proteine yenye kuitwa albimine, proteine za kusaidia damu isiendelee kuvuya, na proteine za kusaidia kupiganisha magonjwa. Wanganga wanaweza kutosha proteine za plazma juu ya kuzitumikisha. Proteine fulani yenye kutoka mu plazma inaweza kutumiwa juu ya kusaidia kuzuia damu isivuye. Kama mutu iko mu hatari ya kuambukizwa ugonjwa fulani, wanganga wanaweza kuomba atobolewe sindano ya gammaglobuline, yenye ilitoshwa mu plazma ya mutu mwenye mwili wake ulishakakuwa na uwezo wa kupiganisha ule ugonjwa. Kuko proteine zingine za plazma zenye wanganga wanaweza kutumia. Lakini ile mifano tu inaonyesha kama inawezekana kugawanya plazma mu sehemu za kidogo-kidogo. *

Sawa tu vile plazma inaweza kugawanywa mu sehemu za mingi za kidogo-kidogo, sehemu zingine kubwa za damu, ni kusema, chembe nyekundu, chembe nyeupe, na vigandisha-damu, zinaweza pia kugawanywa mu sehemu za kidogo-kidogo. Kwa mufano, mu chembe nyeupe munakuwaka sehemu za kidogo-kidogo zenye kuitwa interferons na interleukins, zenye zinaweza kutumiwa juu ya kutunza magonjwa yenye kutokana na virise, zinaweza pia kutumiwa juu ya kutunza kansere. Sehemu fulani za vigandisha-damu zinaweza kutumiwa juu ya kuponyesha vidonda. Na wanganga wanaendelea kutengeneza dawa zingine kwa kutumia sehemu za kidogo-kidogo za damu. Wakati wanganga wanatunza mutu kwa kutumia zile dawa, hawamutie sehemu kubwa za damu. Lakini wanatumia njo sehemu za kidogo-kidogo zenye zilitoshwa mu zile sehemu kubwa za damu. Mukristo anaweza kukubali matunzo yenye inaomba kutumia sehemu za kidogo-kidogo za damu? Yeye peke njo wa kuamua. Biblia haizungumuzie ile aina ya matunzo. Njo maana kila Mukristo anapaswa kutumia zamiri yake juu ya kuamua.

Wakristo fulani wanakatala matunzo yoyote yenye kutokana na damu, hata yenye inaomba kutumia sehemu za kidogo-kidogo za damu, zenye zinaweza kusaidia kupiganisha magonjwa. Vile njo wao wanaelewa amri ya Mungu ya ‘kujiepusha na damu.’ Wanaelewa kama sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli ilisema kama damu inapaswa ‘kumwangwa chini.’ (Kumbumbuku la Torati 12:22-24) Ile sheria iko na uhusiano gani na sehemu za kidogo-kidogo za damu? Juu ya kutengeneza zile dawa za kusaidia kupiganisha magonjwa, na dawa zingine, inaomba kukamata damu na kutumika nayo juu ya kutokeza zile dawa. Wakristo fulani wanakatala zile dawa, sawa vile tu wanakatalaka damu ao sehemu ine kubwa za damu. Juu ya nini? Juu ile damu haikumwangwa. Tunapaswa kuheshimia uamuzi wao.

Wakristo wengine wanakamata uamuzi tofauti. Wanakatala pia kutiwa damu ao sehemu ine kubwa za damu, ni kusema, chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, na plazma. Lakini, wanaweza kukubali munganga awatunze kwa kutumia sehemu za kidogo-kidogo zenye zilitoshwa mu sehemu kubwa za damu. Hata kati ya wale Wakristo, wamoja wanaweza kuwa na mawazo tofauti. Mukristo fulani anaweza kukubali gammaglobuline yenye ilitoshwa mu plazma, lakini anaweza kukatala dawa ingine yenye kutoshwa mu chembe nyekundu ao chembe nyeupe. Sasa, juu ya nini Wakristo fulani wanaona kama wanaweza kukubali sehemu za kidogo-kidogo za damu?

Mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 6, 1990, mulikuwa habari “Maulizo ya Wasomaji Wetu” yenye ilionyesha kama proteine za plazma zinatokaka mu damu ya mwanamuke mwenye mimba na kuingia mu damu ya mutoto wake mwenye kuwa mu tumbo. Kwa hiyo, mama anapitishiaka mutoto wake sehemu za damu zenye zinamulinda asipate magonjwa. Tena, wakati chembe nyekundu za mutoto mwenye hayazaliwa zinazeeka, anazipitishiaka mama yake na mwili wa mama yake unazitoshaka inje sawa vile uchafu. Kwa hiyo, Wakristo fulani wanaweza kuona kama vile sehemu za kidogo-kidogo za damu zinaweza kutoka mu mwili wa mutu na kuingia mu mwili wa mutu mwingine kwa njia ya kiasili, ni kusema wao pia wanaweza kukubali sehemu za kidogo-kidogo za plazma ao za chembe zingine za damu.

Juu kila Mukristo anajiamuliaka ikiwa atakubali ao hapana sehemu za kidogo-kidogo za damu, ile inamaanisha kama haiko uamuzi wa maana? Hapana, ni uamuzi wa maana. Lakini mambo iko wazi. Sawa vile tumeona, Mashahidi wa Yehova wanakatala kutiwa damu na sehemu ine kubwa za damu. Biblia inaambia Wakristo ‘kujiepusha na vitu vyenye vilitolewa zabihu kwa sanamu, na damu, na vitu vyenye vilinyongwa, na uasherati.’ (Matendo 15:29) Lakini, mbele ya kuamua ikiwa tutakubali ao hapana sehemu za kidogo-kidogo zenye zinatoshwa mu sehemu ine kubwa za damu, tunapaswa kufikiri sana na kuomba Yehova atuongoze.

Watu wengi wanakuwaka tayari kukubali matunzo yoyote, hata kama inaweza kuwaletea matokeo ya mubaya. Mara mingi inakuwaka vile wakati wanganga wanatunza mutu kwa kutumia dawa zenye kutokana na damu. Mashahidi wa Yehova wanasamini mambo yenye wanganga wanafanya juu ya kuwatolea matunzo ya muzuri, na wanafikiriaka faida na hatari ya matunzo yoyote. Lakini wakati inaomba kutumia dawa zenye zinatokana na damu, wanafikiriaka sana mambo yenye Mungu anasema na pia urafiki wao na Mungu, mwenye aliwapatia uzima.​​—Zaburi 36:9.

Tuko na mawazo sawa ya muandikaji fulani wa zaburi mwenye aliandika hivi: “Yehova Mungu ni jua na ngao; anatoa wema na utukufu. Yehova hatawaima jambo lolote la muzuri wale wenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu. Ee Yehova . . . , mwenye furaha ni mutu mwenye anakutegemea”!​​—Zaburi 84:11, 12.

[Maelezo ya chini]

^ Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 6, 1978, na wa tarehe 1 Mwezi wa 10, 1994. Kompanyi za kutengeneza dawa zimetengeneza dawa fulani zenye hazitokane na damu zenye zinaweza kutumiwa pa nafasi ya sehemu za kidogo-kidogo za damu zenye zilikuwa natumiwa zamani.

[Kisanduku]

MAULIZO YENYE UNAWEZA KUULIZA MUNGANGA

Kama itaomba ufanyiwe upasuaji ao utumie dawa yenye kutengenezwa na damu, uliza munganga wako hivi:

Wote wenye watanitunza wanajua kama niko Shahidi wa Yehova, na kama hata kutokee nini, sikubali kutiwa damu mu mishipa, na sehemu ine kubwa za damu, ni kusema, chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, ao plazma?

Kama utatunzwa kwa kutumia dawa zenye zilitengenezwa na plazma, chembe nyekundu, ao chembe nyeupe, ao vigandisha-damu, uliza munganga wako hivi:

Ile dawa imetengenezwa kwa kutumia moya kati ya sehemu ine kubwa za damu? Kama ni vile, muko sehemu gani?

Itaomba nitumie kiasi gani ya hii dawa, na nitaitumia namna gani?

Kama zamiri yangu inaniruhusu nikubali hii dawa, kuko hatari gani?

Kama zamiri yangu hainiruhudu kukubali hii dawa, ninaweza kupata matunzo gani ingine?

Kisha kufikiria sana ile jambo, ni wakati gani njo ninaweza kukujulisha uamuzi wangu?