Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Ujitoe kwa Yehova?

Juu ya Nini Ujitoe kwa Yehova?

Juu ya Nini Ujitoe kwa Yehova?

“Usiku huu malaika wa Mungu mwenye mimi ni mali yake.”​—MATENDO 27:23.

1. Wale wenye wanataka kubatizwa wanakuwaka walishafanya mambo gani, na ile inatokeza maulizo gani?

 “ULISHATUBU zambi zako, ulishajitoa kwa Yehova katika sala, na unakubali wokovu wenye anatoa kupitia Yesu Kristo?” Ile ni ulizo moja kati ya maulizo mbili yenye wale wenye watabatizwa wanajibiaka ku mwisho wa hotuba ya ubatizo. Juu ya nini Wakristo wanapaswa kujitoa kwa Yehova? Tutapata faida gani kama tunajitoa kwa Yehova? Juu ya nini mutu hawezi kumuabudu Mungu mu njia yenye inafaa kama hayajitoa kwake? Juu ya kuelewa majibu ya ile maulizo, tunapaswa kwanza kujua maana ya kujitoa kwa Mungu.

2. Kujitoa kwa Yehova maana yake nini?

2 Kujitoa kwa Mungu maana yake nini? Tuone mambo yenye mutume Paulo alisema wakati alizungumuzia urafiki wake na Mungu. Wakati alikuwa na watu wenye alisafiri nao mu mashua yenye ilikuwa napigwa na upepo, alimuita Yehova “Mungu mwenye mimi ni mali yake.” (Soma Matendo 27:22-24.) Wakristo wote wa kweli ni mali ya Yehova. Lakini, ulimwengu wote “unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Wakristo wanakuwa mali ya Yehova wakati wanajitoa kwake katika sala. Wakati wanajitoa, wanafanya naziri. Kisha pale, wanabatizwa.

3. Ubatizo wa Yesu ulionyesha nini, na wafuasi wake wanafuata mufano wake namna gani?

3 Yesu alituachia mufano wakati alichagua kufanya mapenzi ya Mungu. Juu alizaliwa mu taifa ya Israeli ya watu wenye walikuwa wamejitoa kwa Mungu, yeye pia alikuwa amejitoa kwa Mungu. Lakini wakati alibatizwa, alifanya jambo fulani yenye sheria haikuomba mutu afanye. Biblia inaonyesha kama alisema hivi: “Angalia! Nimekuja. . . ili kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.” (Ebr. 10:7; Luka 3:21) Kwa hiyo, wakati Yesu alibatizwa, alionyesha kama anajitoa kwa Mungu juu ya kufanya mapenzi ya baba yake. Wafuasi wake wanafuata mufano wake wakati wanabatizwa. Lakini, tofauti na ubatizo wa Yesu, wakati wao wanabatizwa, wanaonyesha waziwazi kama wamejitoa kwa Mungu katika sala.

Faida ya Kujitoa kwa Mungu

4. Urafiki wa Daudi na Yonatani unatufundisha nini kuhusu kujitoa?

4 Kujitoa kwa Mungu haiko muchezo. Ni jambo nzito, ni zaidi ya kuahidi kama tutafanya jambo fulani. Lakini, tunapata faida gani wakati tunajitoa kwa Mungu? Tulinganishe kujitoa kwa Mungu na kufanya urafiki na mutu fulani. Juu ukuwe na rafiki, inaomba wewe mwenyewe kwanza ukuwe rafiki. Unapaswa kujitoa kabisa, ni kusema unapaswa kujua kama uko na daraka ya kuhangaikia rafiki yako. Daudi na Yonatani wako kati ya watu wenye walikuwa marafiki wa sana, wenye Biblia inazungumuzia. Na hata walipatiana ahadi kama wataendelea kuwa marafiki. (Soma 1 Samweli 17:57; 18:1, 3.) Hata kama ni nguvu kupata marafiki wenye wanashikamana sana vile, mara mingi urafiki unakuwaka nguvu, kama kila mumoja anajitoa kwa mwenzake, ao anaelewa kuwa iko na daraka ya kuhangaikia mwenzake.​—Mez. 17:17; 18:24.

5. Mutumwa angepata faida gani kama angeendelea kuwa mali ya bwana wake, juu bwana wake ni mutu muzuri?

5 Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli ilionyesha mufano mwingine wenye kuonyesha faida yenye mutu anaweza kupata kama anafanya makubaliano na mutu mwingine. Kama mutumwa angependa kuendelea kuwa mali ya bwana wake, angeweza kufanya makubaliano na bwana wake ya kuendelea kumutumikia. Sheria ilisema hivi: “Kama mutumwa huyo anasema hivi kwa mukazo: ‘Ninamupenda bwana wangu, bibi yangu, na wana wangu; sitaki kuwekwa huru, bwana wa mutumwa huyo atamuleta mbele ya Mungu wa kweli. Kisha bwana huyo atamuleta kwenye mulango ao kwenye mwimo wa mulango, na bwana wa mutumwa huyo atatoboa sikio la mutumwa huyo kwa sindano, naye atakuwa mutumwa wa bwana wake maisha yake yote.”​—Kut. 21:5, 6.

6, 7. (a) Wakati watu wanajitoa ili kutimiza mambo fulani, ile iko na matokeo gani ya muzuri? (b) Tuseme nini kuhusu kujitoa kwa Yehova?

6 Ndoa ni mufano mwingine wa uhusiano wenye unaomba watu wajitoe kabisa. Haiko kujitoa ku makubaliano fulani, lakini ni kujitoa ili kuhangaikia mutu fulani. Mwanaume na mwanamuke wenye wanaishi pamoya bila kufunga ndoa, hawana usalama wa kweli na watoto wao pia hawako salama. Lakini, mwanaume na mwanamuke wenye wamefunga ndoa na wenye wanaheshimia kanuni za Biblia, watajikaza kumaliza matatizo yao kuliko tu kuachana.​—Mt. 19:5, 6; 1 Ko. 13:7, 8; Ebr. 13:4.

7 Zamani watu walipata faida kwa kufanya mapatano mu mambo ya biashara na kazi. (Mt. 20:1, 2, 8) Ni vile pia leo. Kwa mufano, tunapata faida wakati tunaandikiana mbele ya kuanza kufanya biashara fulani, ao kuanza kufanya kazi fulani. Kujua kama kuko mambo fulani yenye tunapaswa kutimiza, ni jambo ya maana na inaletaka faida mu urafiki, mu ndoa, na mu kazi. Vilevile, kujitoa kwa Yehova kunaletaka faida! Tuone sasa faida yenye watu walipata zamani wakati walijitoa kwa Yehova na tuone kufanya vile kulimaanisha nini.

Faida Yenye Waisraeli Walipata Juu Walijitoa kwa Mungu

8. Wakati Waisraeli walijitoa kwa Mungu, ile ilimaanisa nini?

8 Waisraeli wote walijitoa kwa Mungu wakati walifanya naziri kwake. Mungu aliwaambia wakusanyike karibu na Mulima Sinai, kisha akawaambia hivi: “Kama mutatii kabisa sauti yangu na kushika agano langu, hakika mutakuwa mali yangu ya pekee kati ya vikundi vyote vya watu.” Kisha watu wote wakajibu hivi: “Mambo yote yenye Yehova amesema, tuko tayari kuyafanya.” (Kut. 19:4-8) Ile kujitoa kwa Yehova, ilimaanisha mambo mingi zaidi ya kuahidi tu kama watafanya mambo fulani. Ilimaanisha kama wanakuwa mali ya Yehova na Yehova aliwatendea kama ‘mali yake ya pekee.’

9. Waisraeli walipata faida gani juu walikuwa wamejitoa kwa Mungu?

9 Waisraeli walipata faida juu walikuwa mali ya Yehova. Yehova alikuwa mushikamanifu kwao na aliwahangaikia sawa vile muzazi anahangaikiaka mutoto wake. Mungu aliwaambia hivi: “Je, mwanamuke anaweza kumusahau mutoto wake mwenye kunyonya ao akose kusikilia huruma mwana wa tumbo lake la uzazi? Hata kama wanamuke hawa wanasahau, mimi siwezi kukusahau hata kidogo.” (Isa. 49:15) Mungu aliwapatia sheria ili iwaongoze, alituma manabii ili wawatie moyo, na malaika ili wawalinde. Mwandikaji fulani wa Zaburi aliandika hivi: “Anamutangazia Yakobo neno lake, na Israeli masharti yake na hukumu zake. Hajafanyia vile taifa lingine lolote.” (Zb. 147:19, 20; soma Zaburi 34:7, 19; 48:14.) Vile Yehova alihangaikia taifa ya Israeli yenye ilikuwa mali yake, ni vile pia atahangaikia wale wenye wanajitoa kwake leo.

Juu ya Nini Tunapaswa Kujitoa kwa Mungu?

10, 11. Tunazaliwaka mu familia ya Mungu? Fasiria.

10 Wakati mutu anafikiria kujitoa kwa Yehova na kubatizwa, anaweza kujiuliza hivi: ‘Siwezi kumutumikia Mungu bila kujitoa kwake?’ Hapana, juu tuko watoto wa Adamu, tunazaliwa na zambi, na kwa hiyo hatuna uhusiano muzuri na Mungu na hatuko mu familia yake. (Ro. 3:23; 5:12) Njo maana juu Yehova atukubali mu familia yake, tunapaswa kujitoa kwake. Tuone juu ya nini.

11 Juu wazazi wetu nao ni watenda-zambi, hawawezi kutupatia uzima mukamilifu. (1 Ti. 6:19) Juu Adamu na Eva walifanya zambi, watoto wao wote hawakuzaliwa mu familia ya Yehova, Baba mwenye upendo na Muumbaji. (Linganisha na Kumbukumbu la Torati 32:5.) Tangu ile wakati, wanadamu wote wamekuwa inje ya familia ya Yehova.

12. (a) Juu hatukamilike, tunapaswa kufanya nini juu tuingie mu familia ya Mungu? (b) Tunapaswa kufanya mambo gani mbele tubatizwe?

12 Lakini, kila mutu anaweza kuomba Mungu amukubali mu familia yake. * Inawezekana siye watenda-zambi tukuwe mu familia ya Yehova? Ndiyo, mutume Paulo aliandika hivi: “Kwa maana, ikiwa wakati tulikuwa maadui tulipatanishwa na Mungu kupitia kifo cha Mwana wake.” (Ro. 5:10) Wakati tunabatizwa, tunaomba Mungu atupatie zamiri ya muzuri juu tukubaliwe naye. (1 Pe. 3:21) Lakini mbele ya kubatizwa, kuko mambo ingine yenye tunapaswa kufanya. Tunapaswa kujua Mungu muzuri, kumutumainia, kutubu, na kubadilika. (Yoh. 17:3; Mdo. 3:19; Ebr. 11:6) Lakini kuko jambo ingine yenye tunapaswa kufanya juu Mungu atukubali mu familia yake. Ni jambo gani?

13. Juu ya nini mutu anapaswa kufanya naziri ya kujitoa kwa Mungu juu astahili kuingia mu familia ya Yehova?

13 Mbele mutu akuwe mu familia ya Yehova, anapaswa kumutolea ahadi yenye kutoka ku moyo. Kusudi tuelewe juu ya nini mutu anapaswa kufanya vile, tufikirie mufano wa baba muzuri mwenye anapendezwa na yatima fulani, na anapenda kumufanya kuwa mushiriki wa familia yake. Lakini, ule baba anajulikana kuwa mutu muzuri. Lakini, mbele ya kukubali ule kijana akuwe mutoto wake, anapenda ule kijana amuahidi jambo fulani. Kwa hiyo, ule baba anasema hivi: “Mbele nikukubali kuwa mutoto wangu, napaswa kujua kama utanipenda na kuniheshimia sawa vile baba yako.” Atakubali tu ule kijana mu familia yake ikiwa ule kijana anamuahidi kuwa atafanya vile. Ile inaeleweka. Haiko vile? Vilevile, Yehova anakubali mu familia yeke wale tu wenye wako tayari kufanya naziri ya kujitoa kwake. Biblia inasema hivi: “Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu.”​—Ro. 12:1.

Kujitoa kwa Mungu Kunaonyesha Kama Tunamupenda na Tuko na Imani

14. Juu ya nini kujitoa kwa Mungu kunaonyesha kama tunamupenda?

14 Wakati tunafanya naziri ya kujitoa kwa Mungu, tunaonyesha kama tunamupenda kabisa. Kwa njia fulani, ile naziri iko sawa vile naziri ya ndoa. Bwana harusi Mukristo anaonyesha kuwa anapenda bibi harusi kwa kufanya naziri kama atakuwa mushikamanifu kwake hata kutokee nini. Ile naziri, haiko tu ahadi yenye unatoa ya kufanya jambo fulani; lakini ni ahadi yenye unatoa juu unapenda mutu. Mwanaume Mukristo anaelewa kama mbele ya kuanza kuishi na bibi yake, anapaswa kwanza kufanya naziri ya ndoa. Vilevile, mbele mutu akuwe mu familia ya Yehova, anapaswa kufanya naziri ya kujitoa kwake. Kwa hiyo, hata kama hatuko wakamilifu, tunajitoa kwa Mungu kwa sababu tunapenda kuwa mali yake, na tuko tayari kufanya yetu yote juu tuendelee kuwa washikamanifu kwake hata kutokee nini.​—Mt. 22:37.

15. Juu ya nini kujitoa kwa Yehova kunaonyesha kama tuko na imani?

15 Wakati tunajitoa kwa Mungu, tunaonyesha kama tuko na imani. Juu ya nini? Kumuamini Yehova kunafanya tukuwe hakika kama kuwa rafiki yake kunatuletea faida. (Zb. 73:28) Tunajua kama wakati fulani haitakuwa mwepesi kutembea pamoya na Mungu juu tunaishi kati ya “kizazi chenye kuharibika na chenye kupotoka.” Lakini tuko na imani kama mungu atatusaidia juu ameahidi kufanya vile. (Flp. 2:15; 4:13) Tunajua kama hatukamilike, lakini tuko hakika kuwa Yehova atatutendea kwa rehema hata wakati tunafanya makosa. (Soma Zaburi 103:13, 14; Waroma 7:21-​25.) Tuko na imani kama Yehova atatubariki kama tunaendelea kuwa waaminifu kwake.​—Yob. 27:5.

Kujitoa kwa Mungu Kunaleta Furaha

16, 17. Juu ya nini kujitoa kwa Yehova kunaletaka furaha?

16 ile tunamutolea maisha yetu. Sawa vile Yesu alisema, “kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Matendo 20:35) Yesu alijionea furaha ya kutoa wakati alikuwa ku dunia. Mara fulani, alikosa hata wakati wa kupumuzika na kula juu tu ya kusaidia wengine wapate barabara yenye inaongoza kwenye uzima. (Yohana 4:34) Yesu alipata furaha juu alijikaza kufurahisha moyo wa Baba yake. Alisema hivi: “Sikuzote ninafanya mambo yenye kumupendeza.”​—Yohana 8:29; Mez. 27:11.

17 Yesu aliambia wanafunzi wake jambo yenye wanapaswa kufanya juu wapate furaha, wakati alisema hivi: “Kama mutu yeyote anataka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe.” (Mt. 16:24) Wakati tunajikana wenyewe, tunamukaribia Yehova zaidi. Hakuna mutu mwengine mwenye anaweza kutupenda sana na kutuhangaikia sana sawa vile Yehova.

18. Juu ya nini kuendelea kufanya mapenzi ya Yehova kunaletaka furaha kuliko jambo ingine yoyote?

18 Kujitoa kwa Yehova na kuendelea kufanya mapenzi yake, kunatuletea furaha kuliko jambo ingine yoyote. Kwa mufano, watu wengi wanatumiaka wakati na nguvu yao juu ya kutafuta makuta, lakini ile haiwaleteake furaha ya kweli. Lakini, wale wenye wanajitoa kwa Yehova wanapataka furaha ya kweli. (Mt. 6:24) Kujua kama wao ni “wafanyakazi pamoja na Mungu” kunawaletea furaha, lakini hawajitoe kwa kazi fulani, wanajitoa njo kwa Mungu wetu mwenye shukrani. (1 Ko. 3:9) Yehova iko mwenye shukrani sana kwa ajili ya mambo yote yenye wanafanya juu ya kumutumikia. Na hata atafanya watumishi wake waaminifu wakuwe tena vijana juu aendelee kuwahangaikia milele.​—Yobu 33:25; soma Waebrania 6:10.

19. Wale wenye wanajitoa kwa Yehova wanapata faida gani?

19 Wakati unatoa maisha yako kwa Yehova, unamukaribia zaidi. Biblia inasema hivi: “Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yak. 4:8; Zb. 25:14) Habari yenye kufuata itaonyesha juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama kujitoa kwa Yehova njo uamuzi wa muzuri zaidi.

[Maelezo ya chini]

^ “Kondoo wengine” wa Yesu watakuwa wana wa Mungu ku mwisho wa utawala wa miaka elfu. Lakini, juu wamejitoa kwa Mungu, wanaweza kumuita “Baba” na wanaweza pia kuonwa kuwa wako mu familia ya Mungu.​—Yoh. 10:16; Isa. 64:8; Mt. 6:9; Ufu. 20:5.

Utajibu Namna Gani?

• Kujitoa kwa Mungu maana yake nini?

• Kujitoa kwa Mungu kunatuletea faida gani?

• Juu ya nini Wakristo wanapaswa kujitoa kwa Yehova?

[Maulizo ya Funzo]

[Picha]

Kuendelea kufanya mapenzi ya Yehova kunaleta furaha ya milele