Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Wanamuke Wanapaswa Kuheshimia Ukichwa?

Juu ya Nini Wanamuke Wanapaswa Kuheshimia Ukichwa?

Juu ya Nini Wanamuke Wanapaswa Kuheshimia Ukichwa?

“Kichwa cha mwanamuke ni mwanaume.”​—1 KO. 11:3.

1, 2. (a) Mutume Paulo aliandika nini juu ya mupango wa ukichwa na juu ya kujitiisha? (b) Tutazungumuzia maulizo gani mu hii habari?

 MUTUME Paulo alisema kama “kichwa cha kila mwanaume ni Kristo” na “kichwa cha Kristo ni Mungu.” (1 Ko. 11:3) Ule njo utaratibu wenye Yehova ameweka. Mu habari yenye kutangulia, tuliona kama Yesu aliona kuwa ni pendeleo kujitiisha kwa kichwa chake, Yehova Mungu, na alifurahia kufanya vile. Tuliona pia kama Kristo njo kichwa cha wanaume Wakristo. Yesu alikuwa natendea watu kwa fazili, kwa upole, kwa huruma, na aliwahangaikia. Wanaume mu kutaniko wanapaswa kutendea wengine vile, zaidi sana bibi zao.

2 Halafu wanamuke? Nani njo kichwa chao? Mutume Paulo aliandika hivi: “Kichwa cha mwanamuke ni mwanaume.” Wanamuke wanapaswa kuona namna gani ile maneno yenye iliongozwa na roho ya Mungu? Mwanamuke anapaswa kujitiisha kwa bwana yake hata kama bwana yake haiko Shahidi? Ile inamaanisha kama mwanamuke hawezi kusema mawazo yake wakati inaomba kukamata maamuzi mu ndoa? Mwanamuke anapaswa kufanya nini juu bwana yake amusifu?

“Nitamufanyia Musaidizi”

3, 4. Mupango wa ukichwa uko na faida gani?

3 Mungu njo alianzisha mupango wa ukichwa. Kisha kumuumba Adamu, Yehova alisema hivi: “Haiko muzuri mwanaume huyu aendelee kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi, akuwe kikamilisho chake.” Kisha Eva kuumbwa, Adamu alifurahi sana kupata musaidizi na mutu wa kuishi naye, na kwa hiyo akasema hivi: “Huyu ni mufupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu.” (Mwa. 2:18-24) Adamu na Eva walikuwa na pendeleo ya kufikia kuwa baba na mama ya wanadamu wote wakamilifu wenye wangeishi milele kwa furaha mu dunia paradiso.

4 Juu wazazi wetu wa kwanza walikosa kumutii Mungu, walipoteza hali ya ukamilifu yenye walikuwa nayo mu bustani ya Edeni. (Soma Waroma 5:12.) Lakini, mupango wa ukichwa uliendelea. Wakati bwana anatumikisha muzuri ukichwa wake, na bibi yake anajitiisha kwake, ndoa inakuwa na furaha. Bibi na bwana wanakuwa na furaha sawa yenye Yesu anakuwaka nayo wakati anajitiisha kwa kichwa chake Yehova. Mbele Yesu akuye ku dunia, ‘alifurahi mbele [ya Yehova] wakati wote.’ (Mez. 8:30) Juu hatukamilike, wanaume hawawezi tena kutumikisha ukichwa wao bila kukosea, na wanamuke hawawezi kujitiisha bila kukosea. Lakini wakati bibi na bwana wanaendelea kujikaza sana, ule mupango wa ukichwa unaleta furaha mu ndoa.

5. Juu ya nini bibi na bwana wanapaswa kufuata shauri yenye kuwa mu Waroma 12:10?

5 Juu bibi na bwana wakuwe na furaha, wanapaswa kufuata hii shauri yenye Biblia inapatia Wakristo wote: “Katika upendo wa kindugu mukuwe na upendo wenye upole kwa mutu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima, mukuwe wa kwanza.” (Ro. 12:10) Tena, bibi na bwana wanapaswa kujikaza sana kufuata hii shauri: “Mukuwe wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyingi, na musameheane kwa kupenda kama vile Mungu kupitia Kristo aliwasamehe ninyi kwa kupenda.”​—Efe. 4:32.

Wakati Bwana Yako Haiko Muamini

6, 7. Kama bibi Mukristo anajitiisha kwa bwana yake mwenye haiko Shahidi, matokeo inaweza kuwa nini?

6 Utafanya nini kama bwana yako haiko mutumishi wa Yehova? Mu ndoa za mingi, bwana njo hakuwake muamini. Kama ni vile, bibi yake anapaswa kumutendea namna gani? Biblia inajibia hivi: “Kwa njia ileile, ninyi bibi, mujitiishe kwa bwana zenu, ili kama kuko wale wenye hawatii lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa bibi zao, kwa sababu wameshuhudia kwa macho yao mwenendo wenu wenye kuwa safi pamoja na heshima kubwa.”​—1 Pe. 3:1, 2.

7 Biblia inaambia bibi aendelee kujitiisha kwa bwana yake mwenye haiko muamini. Mwenendo wake muzuri unaweza kuchochea bwana yake atafute kujua juu ya nini iko najiendesha muzuri vile. Na ile inaweza kufanya bwana yake apende kujifunza Biblia na afikie hata kukubali kweli.

8, 9. Bibi Mukristo anaweza kufanya nini ikiwa bwana yake mwenye haiko muamini habadilike hata kama yeye iko najiendesha muzuri?

8 Halafu kama bwana mwenye haiko muamini habadilike hata kama bibi yake iko na mwenendo muzuri? Biblia inashauria bibi Mukristo aendelee kuonyesha sifa za Kikristo kila wakati hata kama wakati fulani haiko mwepesi kufanya vile. Kwa mufano, 1 Wakorinto 13:4 inasema hivi: “Upendo ni wenye uvumilivu.” Njo maana ni muzuri bibi Mukristo aendelee kujiendesha “kwa unyenyekevu wote na upole, [na] kwa uvumilivu.” Atafanya vile kwa kuendelea kuonyesha upendo na kuvumilia hali yake. (Efe. 4:2). Nguvu ya utendaji ya Mungu, ni kusema roho takatifu, inaweza kutusaidia tuendelee kuonyesha sifa za Kikristo hata wakati haiko mwepesi kufanya vile.

9 Mutume Paulo aliandika hivi: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu”. (Flp. 4:13) Roho takatifu inasaidia bibi Mukristo afanye mambo yenye, kwa nguvu yake tu, hangeweza kufanya. Kwa mufano, wakati bwana yake anamutendea mubaya, anaweza kutafuta kulipisha kisasi. Lakini, Biblia inaambia Wakristo wote hivi: “Musimulipe mutu yeyote uovu kwa uovu. . . . Kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa, ni vile Yehova anasema.’” (Ro. 12:17-19) Tena, 1 Watesalonike 5:15 inatushauria hivi: “Muhakikishe kuwa hakuna mutu mwenye anamulipa mutu yeyote ubaya kwa ubaya, lakini sikuzote mufuatie mambo ya muzuri kwa mutu na mwenzake na kwa wengine wote.” Kwa musaada wa roho takatifu ya Yehova, tunaweza kufanya mambo yenye hatungeweza kufanya kwa nguvu yetu tu. Njo maana tuko na lazima ya roho takatifu juu itupatie nguvu yenye tuko nayo lazima!

10. Yesu alifanya nini wakati wengine walisema ao kumufanyia mambo ya mubaya?

10 Yesu alituachia mufano muzuri mu namna alitendea watu wenye walisema ao kumutendea mambo ya mubaya. 1 Petro 2:23 inasema hivi: “Wakati alikuwa anatukanwa, hakujibu kwa matukano. Wakati alikuwa anateseka, hakuogopesha watu, lakini alijitia katika mikono ya ule mwenye anahukumu kwa haki.” Ujikaze basi kufuata mufano wake. Usikasirike wakati wengine wanakutendea mubaya. Wakristo wote wanapaswa kuwa wenye “huruma yenye upole, na unyenyekevu.” Na hawapaswe ‘kulipa ubaya kwa ubaya.’​—1 Pe. 3:8, 9.

Bibi Ni wa Kubakia Tu Kimya?

11. Wakristo fulani wanamuke watakuwa pia na pendeleo gani?

11 Kujitiisha kwa bwana inamaanisha kama mwanamuke anapaswa kubakia tu kimya mu ndoa, hapaswe kusema mawazo yake kuhusu mambo ya familia ao mambo ingine? Hapana. Wanaume na wanamuke, wote Yehova amewapatia mapendeleo ya mingi. Fikiria pendeleo kubwa sana yenye wale 144 000 wako nayo ya kuwa wafalme na makuhani mbinguni, wakati Yesu atatawala hii dunia. Mu ile hesabu, muko pia wanamuke. (Gal. 3:26-​29) Kwa kweli, Yehova anaheshimisha wanamuke kwa kuwapatia kazi ya maana ya kufanya ili kutimiza kusudi yake.

12, 13. Toa mufano wenye unaonyesha kama wanamuke walikuwa natabiri.

12 Kwa mufano, wakati wa zamani, wanamuke walikuwa natabiri. Andiko ya Yoeli 2:28, 29 ilitabiri hivi: “Nitamwanga roho yangu juu ya kila namna ya mwili, na watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke watatoa unabii. . . . Hata juu ya watumwa wangu wanaume na watumwa wangu wanamukeNitamwanga roho yangu.”

13 Siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33, kisha kuzaliwa kwa Yesu, kati ya wanafunzi 120 wa Yesu, wenye walikusanyika mu chumba ya juu kule Yerusalemu, kulikuwa pia wanamuke. Mungu alimwangia wale wanafunzi wote roho yake takatifu. Njo maana Petro alirudilia maneno yenye nabii Yoeli alitabiri na kuonyesha kama ilihusu wanaume na wanamuke pia. Petro alisema hivi: “Haya ndiyo maneno yenye yalisemwa kupitia nabii Yoeli: ‘Na katika siku za mwisho,’ Mungu anasema, ‘Nitamwanga sehemu ya roho yangu juu ya kila namna ya mwili, na watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke watatoa unabii . . . ; na hata juu ya watumwa wangu wanaume na watumwa wangu wanamuke nitamwanga sehemu ya roho yangu katika siku hizo, na watatoa unabii.’”​—Matendo 2:16-18.

14. Wakati wa mitume, wanamuke walifanya nini juu ya kusaidia kueneza Ukristo?

14 Wakati wa mitume, wanamuke walisaidia sana kueneza Ukristo. Walihubiria wengine juu ya Ufalme wa Mungu na walifanya mambo ingine ili kutegemeza kazi ya kuhubiri. (Luka 8:1-3) Kwa mufano, mutume Paulo alimuita Foibe, “mutumishi wa kutaniko lenye kuwa katika Kenkrea.” Na wakati alitumia Wakristo wenzake salamu, Paulo alitaya majina ya wanamuke wengi waaminifu, sawa vile “Trifaina na Trifosa, wanamuke wenye wanafanya kazi kwa bidii katika Bwana.” Alitaya pia “Persisi, mupendwa wetu, kwa maana mwanamuke huyo amefanya kazi kwa bidii katika Bwana.”​—Ro. 16:1, 12.

15. Wanamuke wanasaidia namna kueneza Ukristo mu siku zetu?

15 Wakati wetu, sehemu kubwa ya watu milioni saba wenye wako nahubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu mu dunia yote, ni wanamuke. (Mt. 24:14) Wengi kati yao ni mapainia, wamisionere, na Wanabeteli. Daudi, mwandikaji fulani wa zaburi, aliimba hivi: “Yehova anatoa amri; wanamuke wenye kutangaza habari njema ni jeshi kubwa.” (Zb. 68:11) Ile maneno ya Daudi imetimia kabisa! Yehova anafurahia mambo yenye wanamuke wanafanya juu ya kuhubiri habari njema na kutimiza mapenzi yake. Kwa hiyo, wakati anaomba wanamuke Wakristo wajitiishe, ile haimaanishe kama wanapaswa tu kubakia kimya.

Wanamuke Wawili Wenye Hawakubakia Tu Kimya

16, 17. Namna gani mufano wa Sara unaonyesha kama wanamuke hawapaswe kubakia kimya mu ndoa?

16 Juu Yehova anapatia wanamuke mapendeleo ya mingi, wanaume wanapaswa pia kutafuta kujua mawazo ya bibi zao mbele wakamate maamuzi ya maana. Ni jambo ya hekima kufanya vile. Biblia inazungumuzia mifano ya wanamuke fulani wenye walisema mawazo yao na kutenda hata kama bwana zao hawakuwauliza mawazo yao. Tuone mifano mbili.

17 Sara, bibi ya Abrahamu, aliendelea kuambia bwana yake afukuze bibi yake wa pili pamoya na mutoto wake, juu walikosa heshima. “Jambo lenye Sara alisema juu ya mwana wake lilimuchukiza sana Abrahamu,” lakini halikumuchukiza Mungu. Yehova aliambia Abrahamu hivi: “Usichukizwe na jambo lenye Sara anasema juu ya kijana huyo na juu ya mutumwa wako mwanamuke. Umusikilize.” (Mwa. 21:8-12) Abrahamu alimutii Yehova, akasikiliza bibi yake Sara, na akafanya mambo yenye Sara alimuomba.

18. Abigaili alifanya nini?

18 Fikiria pia mufano wa Abigaili, bibi ya Nabali. Wakati Daudi alikuwa nakimbia Mufalme Sauli mwenye wivu, alipiga kambi kwa wakati fulani karibu na wanyama wa kufugwa wa Nabali. Daudi na wanaume wake hawakukamata hata kitu moya ya ule mwanaume tajiri, lakini walilinda mali yake. Lakini, Nabali “alikuwa mukali na mwenye tabia mubaya,” na “aliwatukana kwa sauti kali” wanaume wa Daudi. Alikuwa mutu “mwenye hana mafaa yoyote,” na ‘upumbavu ulikuwa pamoja naye.’ Wakati wanaume wa Daudi waliomba kwa heshima chakula kidogo, Nabali alikatala kuwapatia. Abigaili alifanya nini wakati alisikia ile habari? Bila kuambia Nabali, “akakamata haraka mikate mia mbili (200), mitungi mikubwa mbili ya divai, kondoo tano (5) wenye kuchinjwa, vipimo tano vya sea vya nafaka yenye kukaangwa, keki mia moja (100) za zabibu, na keki mia mbili (200) za tini zenye kufinywa-finywa” na akavipatia Daudi na wanaume wake. Abigaili alifanya muzuri? Ndiyo juu Biblia inasema kama “Yehova akamupiga Nabali, na akakufa.” Kisha pale, Daudi akaoa Abigaili.​—1 Sa. 25:3, 14-19, 23-25, 38-42.

‘Mwanamuke Mwenye Atasifiwa’

19, 20. Nini njo inafanya mwanamuke astahili kabisa kusifiwa?

19 Biblia inasifu mwanamuke mwenye anafanyaka mambo vile Yehova anapenda. Kitabu ya Mezali inasifu mwanamuke “mwenye uwezo,” wakati inasema hivi: “Samani yake inapita sana samani ya marijani. Bwana yake anamutumainia katika moyo wake, na hakose kitu chochote chenye samani.” Tena, “anafungua kinywa chake kwa hekima; sheria ya fazili iko kwenye ulimi wake. Anaangalia kazi za nyumba yake, na hakule mukate wa uvivu. Watoto wake wanasimama na kumutangaza kuwa mwenye furaha; bwana yake anasimama na kumusifu.”​—Mez. 31:10-12, 26-28.

20 Nini njo inafanya mwanamuke astahili kusifiwa? Mezali 31:30 inasema hivi: “Uvutio unaweza kudanganya, na uzuri unaweza kupita haraka, lakini bibi mwenye anamuogopa Yehova atasifiwa. Lakini bibi mwenye anamuogopa Yehova atasifiwa.” Mwanamuke mwenye anamuogopa Yehova anaelewa kama ni jambo ya maana sana aheshimie mupango wa ukichwa wenye Yehova ameweka. Biblia inasema “kichwa cha mwanamuke ni mwanaume,” sawa vile “kichwa cha kila mwanaume ni Kristo,” na “kichwa cha Kristo ni Mungu.”​—1 Ko. 11:3.

Uonyeshe Shukrani kwa Ajili ya Zawadi Yenye Mungu Amekupatia

21, 22. (a) Wakristo wenye kuoana wako na sababu gani za kumushukuru Mungu? (b) Juu ya nini tunapaswa kuheshimia mupango wa ukichwa wenye Yehova ameweka? (Ona kisanduku ku ukurasa wa 17.)

21 Wakristo wenye walishafunga ndoa wako na sababu za mingi sana za kumushukuru Mungu! Wanaweza kufurahia maisha pamoya. Zaidi sana wanapaswa kumushukuru Mungu juu ya zawadi ya ndoa kwa sababu inawapatia nafasi ya kutumia maisha yao ili kumutumikia Yehova pamoya. (Rut. 1:9; Mik. 6:8) Juu Yehova njo alianzisha ndoa anajua mambo yenye bibi na bwana wanapaswa kufanya juu wakuwe na furaha. Mujikaze kila siku kufanya mambo vile Yehova anapenda, na ‘shangwe ya Yehova itakuwa ngome yenu,’ hata mu hii dunia yenye inayala magumu.​—Ne. 8:10.

22 Bwana Mukristo mwenye anapenda bibi yake sawa vile anajipenda mwenyewe, atatumia ukichwa wake kwa upendo na kwa fazili. Bibi mwenye anamuogopa Mungu, ataonyesha kama anastahili kupendwa kwa kutegemeza bwana yake na kumuheshimia. Zaidi ya yote, kama bibi na bwana wanafanya vile, ndoa yao itamuletea Yehova utukufu.

Unakumbuka?

• ehova ameweka utaratibu gani kuhusu ukichwa na kujitiisha?

• Juu ya nini bibi na bwana wanapaswa kuheshimiana?

• Bibi Mukristo anapaswa kutendea namna gani bwana yake mwenye haiko muamini?

• Sababu gani bwana anapaswa kuuliza bibi yake mawazo yake mbele akamate maamuzi ya maana?

[Maulizo ya Funzo]

[Kisanduku]

Juu ya Nini Tuheshimie Mamlaka?

Yehova ameamua viumbe wake fulani wenye akili wakuwe na mamlaka, na ameonyesha namna wanapaswa kutumia mamlaka yao. Amefanya vile kwa faida ya malaika na wanadamu. Ile inapatia viumbe wake wenye akili nafasi ya kuchagua kumutumikia kwa amani na umoja.​—Zb. 133:1.

Wakristo watiwa-mafuta wanajitiisha chini ya mamlaka ya Yesu Kristo, juu yeye njo Kichwa chao. (Efe. 1:22, 23) Juu ya kuonyesha kama anaheshimia mamlaka ya Yehova, kisha kipindi fulani “Mwana mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Ule mwenye aliweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, ili Mungu akuwe vitu vyote kwa kila mutu.” (1 Ko. 15:27, 28) Kwa hiyo, siye wote wenye kumutumikia Yehova, tunapaswa pia kuheshimia ukichwa katika familia na katika kutaniko! (1 Ko. 11:3; Ebr. 13:17) Kama tunafanya vile, Yehova atatukubali na kutubariki.​—Isa. 48:17.

[Picha]

Sala inaweza kusaidia bibi Mukristo aonyeshe sifa za Kikristo

[Picha]

Yehova anafurahia mambo yenye wanamuke wanafanya juu ya kuunga mukono kazi ya Ufalme