Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mnara wa Mlinzi Katika Kiingereza Rahisi

Mnara wa Mlinzi Katika Kiingereza Rahisi

Mnara wa Mlinzi Katika Kiingereza Rahisi

TUNAFURAHI kuwajulisha kuhusu kuchapishwa kwa toleo la kwanza la funzo la Mnara wa Mlinzi katika Kiingereza rahisi, toleo hilo litachapishwa wakati uleule pamoja na toleo la kawaida la Kiingereza. Toleo hilo jipya litajaribiwa kwa mwaka mmoja, na ikiwa litasaidia, litaendelea kuchapishwa. Litakuwa na makala au habari za funzo na nafasi ikiruhusu, litakuwa pia na habari nyingine. Tunaamini kwamba gazeti hilo litatimiza uhitaji wa maana wa kiroho kwa ajili ya Mashahidi wengi wa Yehova. Jinsi gani?

Katika nchi kama vile Fiji, Ghana, Kenya, Liberia, Nigeria, Papua New Guinea, na Visiwa vya Solomon, kwa kawaida ndugu zetu wanazungumza Kiingereza. Ingawa huenda ndugu zetu katika nchi hizo wanazungumza lugha nyingine za kienyeji, mara nyingi wanazungumza Kiingereza kila siku katika mikutano ya kutaniko na katika huduma ya shambani. Hata hivyo, Kiingereza wanachozungumza ni rahisi kuliko Kiingereza kinachotumiwa katika vichapo vyetu. Pia, ndugu zetu wengine ni wakimbizi au wamehamia katika nchi ambazo wanalazimika tu kuhudhuria mikutano katika lugha ya Kiingereza. Zaidi ya hayo, hawawezi kuhudhuria mikutano katika lugha yao ya asili.

Habari au makala tunazojifunza kila juma katika Funzo la Mnara wa Mlinzi ndiyo njia kuu inayotumiwa kutusaidia kuendelea kupata chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa. Kwa hiyo, ili kuwasaidia wote wanaohudhuria wafaidike kikamili na habari hiyo, toleo la Kiingereza rahisi litatumia maneno na muundo rahisi wa sentensi. Toleo hilo jipya litakuwa na jalada lililo tofauti. Vichwa vidogo, mafungu, maswali ya kurudia, na picha katika habari za funzo zitakuwa sawa na za toleo la kawaida. Hivyo, wote wanaweza kutumia toleo lolote lile na kushiriki katika Funzo la Mnara wa Mlinzi. Ili kuona tofauti ya maneno katika matoleo hayo mawili, ona mfano ulio hapa chini ambao umetolewa kwenye fungu la 2 la makala ya kwanza ya funzo katika toleo hili.

Tunatumaini kwamba msaada huo mpya utajibu sala za wengi ambao wamemwambia Yehova hivi: “Unifanye nielewe, ili nipate kujifunza amri zako.” (Zab. 119:73) Tuna hakika kwamba wale ambao hawana ujuzi mwingi wa Kiingereza, kutia ndani watoto wadogo ambao wanazungumza Kiingereza, wataweza kujitayarisha vizuri kwa ajili ya Funzo la Mnara wa Mlinzi kila juma. Tunamshukuru sana Yehova kwa sababu ‘anaupenda ushirika mzima wa akina ndugu,’ na hivyo anamtumia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kutayarisha chakula cha kiroho kwa wingi.—1 Pet. 2:17; Mt. 24:45.

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova