Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unafurahia “Pendeleo la Kutoa” kwa Moyo Mwema?

Je, Unafurahia “Pendeleo la Kutoa” kwa Moyo Mwema?

Je, Unafurahia “Pendeleo la Kutoa” kwa Moyo Mwema?

WAKRISTO wa kwanza katika Filipi walijulikana sana kwa sababu ya roho yao nzuri ya kutoa michango ili kutegemeza ibada safi. Katika barua yake iliyoongozwa na roho ya Mungu, mutume Paulo aliwaandikia yafuatayo: ‘Namushukuru Mungu wangu sikuzote kila mara ninapowakumbuka ninyi katika dua zangu zote kwa ajili yenu nyote, ninapoendelea kutoa dua yangu kwa shangwe, kwa sababu ya muchango ambao mumeutoa kwa ajili ya habari njema tangu siku ya kwanza mupaka sasa.’ (Flp. 1:3-5) Bila shaka, mutume Paulo alikumbuka wakati Lidia na watu wa nyumba yake walipobatizwa na namna alivyowakaribisha yeye na wenzake kwa kuwakaza wabaki katika nyumba yake.—Mdo. 16:14, 15.

Muda mufupi baadaye, washiriki wa kutaniko jipya la Filipi walimutumia Paulo mara mbili vitu alivyohitaji. Wakati huo Paulo alikuwa Thesalonika kwa majuma fulani pamoja na Wakristo wenzake wa huko. Thesalonika ilikuwa kwenye umbali wa karibu kilometa 160 na Filipi. (Flp. 4:15, 16) Miaka michache baadaye, ijapokuwa Wafilipi na ndugu wengine wa huko Makedonia walikuwa katika taabu na ‘umasikini mukubwa,’ waliposikia kwamba Wakristo huko Yerusalemu walikuwa wenye kuteswa na kwamba walikuwa katika uhitaji, wao walipenda kuwasaidia. Paulo alishuhudia kwamba hilo lilipita uwezo waliokuwa nao. Pia aliandika: “Waliendelea kutuomba kwa kusihi sana wapate pendeleo la kutoa.”—2 Kor. 8:1-4; Rom. 15:26.

Miaka kumi hivi baadaye, kisha Wafilipi kukubali Ukristo, waliendelea kuonyesha roho ya kutoa. Waliposikia kwamba Paulo alikuwa katika gereza huko Roma, walimutuma Epafrodito aliyefanya kilometa 1,287, akisafiri kupitia inchi kavu na bahari ili kumupelekea mutume Paulo vitu alivyohitaji. Ni kweli kwamba Wafilipi walipenda kumusaidia Paulo ili aendelee kuhubiri na kuwatia ndugu moyo, hata ikiwa alikuwa katika gereza.—Flp. 1:12-14; 2:25-30; 4:18.

Leo, Wakristo wa kweli wanaona kuwa pendeleo kutegemeza kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Wanatoa wakati wao, nguvu zao, na mali yao ili kazi ya Ufalme iendelee. Kisanduku kinachofuata kinaonyesha njia mbalimbali za kutoa michango ili kutegemeza kazi ya kuhubiri.

[Sanduku katika ukurasa was 22, 23]

NJIA MBALIMBALI ZA KUTOA MICHANGO

MICHANGO KWA AJILI YA KAZI YA KUHUBIRI ULIMWENGUNI POTE

Wengi wanachunga ao wanachukua katika mushahara wao kiasi fulani cha feza ambacho wanatia ndani ya visanduku vya michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote.

Kila mwezi, makutaniko yanatuma feza hizo kwenye biro ya Mashahidi wa Yehova inayopatikana katika inchi yao. Katika inchi yetu, michango ya kujipendea inaweza kutumwa moja kwa moja kwa “Association Les Témoins de Jéhovah.” Sheke za benki zinazotumiwa kwenye adresi iliyoonyeshwa hapo juu zinapaswa kuonyesha kwamba zitalipwa kwa “Association Les Témoins de Jéhovah.” Michango inaweza kuwa pia vitu kama vile pete ao biju na vitu vingine vyenye bei. Unapaswa kutuma barua fupi pamoja na michango hiyo ili kuonyesha kwamba ni zawadi unayotolea sosaiti.

KUKOPESHA SOSAITI FEZA

Unaweza kukopesha “Association Les Témoins de Jéhovah” feza kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Wakati utahitaji feza zako, sosaiti itakurudishia feza hizo bila kukuongezea faida yoyote. Ili kupata habari zaidi unaweza kutumia namba hii ya telefone: 0998 189 791 ao 081 555 1000

MIPANGO MINGINE INAYOHUSU MICHANGO

Kuna njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Njia hizo zinatia ndani:

Asiranse: Unaweza kuandika kwamba “Association Les Témoins de Jéhovah” ndiyo itachukua feza zako za asiranse ao za pansio. Ili kufanya hivyo mutu anapashwa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili ajue jinsi ya kufanya.

Akaunti za Benki: Mutu anaweza kutuma zawadi yake kwa kutia feza katika akaunti ya benki ya “Association Les Témoins de Jéhovah.” Ili kufanya hivyo mutu anapashwa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili ajue namba ya akaunti kupitia hiyo atatuma zawadi yake.

Nyumba ao Parcelle: Unaweza kuitoa kuwa zawadi. Unaweza kuendelea kuishi katika nyumba hiyo mupaka utakapokufa. Mbele ya kutolea sosaiti zawadi kama hiyo unapashwa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ya inchi yenu.

Zawadi: Ni mupango wa kutoa feza ao vitu vingine ili viwe mali ya shirika fulani linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova. Yule anayependa kutoa zawadi ili kutegemeza kazi ya Ufalme, anapashwa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria kuhusiana na zawadi ambayo anapenda kutolea “Association Les Témoins de Jéhovah.”

Testama: Shirika la Association Les Témoins de Jéhovah” linaweza, kupitia testama, kuachiwa uriti wa mali ao feza. Mbele ya kufanya testama hiyo mutu anapashwa kwanza kupashana habari na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria.

Usemi “mipango mingine inayohusu michango” unaonyesha kwamba ili mutu afanye michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango fulani kamili. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotamani kutoa michango ili kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri ulimwengu pote iendelee. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa ao kama uriti mutu anapokufa. Kisha kusoma broshua hiyo na kushauriana na washauri wao wa mambo ya kisheria ao kodi, watu wengi wamesaidia kutegemeza kazi yetu ya kuhubiri na wanatoa misaada ulimwenguni pote na kupunguziwa kodi wanapofanya hivyo. Ikiwa unapenda kupata broshua hiyo unaweza kuiomba kwenye biro ya tawi.

Ili kupata habari zaidi, unaweza kuzungumuza na biro ya tawi. Unaweza pia kutuma barua kupitia adresi ya B.P. 634, Limete-Kinshasa, ao kuita kwa njia ya telefone kwa kutumia adresi iliyo hapa chini ao unaweza kuzungumuza na biro ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika inchi yenu.

Biro ya tawi

“Association Les Témoins de Jéhovah” no 75, 13ème Rue, Industriel, Limete-Kinshasa, République Démocratique du Congo.

Telefone: 0998 189 791 ao 081 555 1000