Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa uangalifu habari zilizozungumuziwa hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Basi, ona ikiwa unaweza kujibu maulizo yanayofuata:

• Olivétan alikuwa nani, na kwa nini tunapendezwa na kazi aliyofanya?

Ni Pierre Robert, Mfaransa aliyeitwa Olivétan. Wakati wa marekebisho ya kidini katika karne ya 16, alitafsiri Biblia katika Kifaransa. Alitumia neno “mwangalizi” pahali pa “askofu” ao “kutaniko” pahali pa “kanisa.” Mahali pengi, alitumia jina la Mungu “Yehova.”—9/1, ukurasa wa 18-20.

• Mungu alimaanisha nini alipowaambia Walawi: “Mimi ni fungu lako”?

Kila kabila la Israeli lilipokea sehemu ya nchi, lakini “fungu” la Walawi lilikuwa Yehova. (Hes. 18:20) Hawangerithi sehemu fulani ya nchi, lakini walipewa pendeleo la pekee la utumishi. Hata hivyo, Yehova aliendelea kutosheleza mahitaji yao ya kimwili ya lazima. Leo, wale walio na pendeleo la kuendeleza faida za Ufalme wanaweza kuwa hakika kwamba Yehova atatosheleza mahitaji yao ya kimwili.—9/15, ukurasa wa 7-8, 13.

• Namna gani tunajua wakati ambapo muji wa Yerusalemu ulianguka katika mikono ya Wababiloni?

Wanahistoria wa kale, wanatoa maelezo yenye kupingana kuhusu wafalme wa Babiloni na utawala wao. Lakini, wasomi wanakubali kwamba Koreshi II, alipata ushindi juu ya Babiloni katika 539 K.W.K., tarehe ya msingi. Wayahudi waliwekwa huru, na walifika katika nchi yao katika mwaka wa 537 K.W.K. Biblia inasema kwamba walifanya miaka 70 uhamishoni. Kwa hiyo, muji wa Yerusalemu ulipaswa kuanguka katika 607 K.W.K. (2 Nya. 36:21, 22; Yer. 29:10; Dan. 9:1, 2)—10/1, ukurasa wa 26-31.

• Ni nini linaloweza kumusaidia Mkristo aamue ikiwa aina fulani ya tafrija ni yenye faida ao hapana?

Ili kujua ikiwa aina fulani ya tafrija ni yenye faida na yenye kupendeza machoni pa Mungu, ni vizuri kujiuliza: Inatia ndani nini? Nitaendelea na tafrija hiyo mpaka wakati gani? Nitashirikiana na nani huko?—10/15, ukurasa wa 9-12.

• Kwa nini ni vibaya kutoa mimba?

Machoni pa Mungu, uhai ni mtakatifu na anaona kiini-tete kuwa kiumbe hai. (Zab. 139:16) Kutoa mimba ni tendo la kuua. Katika Sheria ya Musa mutu alipaswa kutoa hesabu ikiwa angemuumiza mtoto aliyekuwa tumboni. (Kut. 21:22, 23)—11/1, ukurasa wa 6.

• Namna gani habari iliyo kwenye Methali 7:6-23 inatusaidia tuepuke kutazama ponografia?

Andiko hilo linatuelezea kuhusu kijana mumoja aliyepitia barabara, mahali panapojulikana vema kwamba mwanamuke kahaba anaishi. Kahaba huyo akamushawishi. Leo, ni lazima tuepuke mahali katika internet palipo na picha za kuamusha tamaa za ngono, na ni lazima tutafute musaada wa Mungu katika sala mbele hata ya kufungua internet mahali panapoonyesha mambo ya ponografia.—11/15, ukurasa wa 9-10.

• Namna gani tunajua kwamba dunia haitaangamizwa katika 2012?

Kwa sababu ya kalenda ya zamani ya Wamaya, watu fulani wanafikiri kwamba dunia itaangamizwa katika 2012. Lakini hilo haliwezekani, kwa kuwa Yehova aliiumba dunia ili ikaliwe. Biblia inasema kwamba dunia itadumu milele. (Mhu. 1:4; Isa. 45:18)—12/1, ukurasa wa 10.

• Ni waandishi gani wa Biblia ambao walikuwa kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K.?

Inaonekana kwamba waandishi 6 wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo walikuwepo. Mitume watatu walikuwepo—Mathayo, Yohana, na Petro. Ndugu wawili wa Yesu walikuwepo pia—Yakobo na Yuda. Na inaelekea pia kwamba kijana Marko alikuwepo.—12/1, ukurasa wa 22.