Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kufanya Mabadiliko Katika Maisha Kumeniletea Baraka Nyingi

Kufanya Mabadiliko Katika Maisha Kumeniletea Baraka Nyingi

Kufanya Mabadiliko Katika Maisha Kumeniletea Baraka Nyingi

James A. Thompson Anaeleza maisha yake

Nilizaliwa Amerika ya kusini mwaka wa 1928, wakati huo sheria ya ubaguzi wa rangi kati ya weusi na wazungu ilikuwa ikitawala. Kuivunja kungemufanya mutu afungwe ao aazibiwe vikali.

WAKATI huo katika sehemu mbalimbali huko Amerika, Mashahidi wa Yehova weusi na wazungu hawakuchangana; kila wamoja walikuwa na makutaniko yao, mizunguko yao, na wilaya zao. Katika mwaka wa 1937, baba yangu alipendekezwa kuwa mutumishi wa kutaniko (leo muratibu wa baraza la wazee) katika kutaniko la weusi huko Chattanooga, Tennessee. Ni Henry Nichols aliyekuwa mutumishi wa kutaniko la wazungu.

Ninakumbuka nilipokuwa kijana, nilikuwa kwenye veranda usiku, na nilikuwa nikisikiliza mazungumuzo ya Baba na Ndugu Nichols. Ijapokuwa sikuelewa kila jambo, nilifurahia kuwa pembeni ya Baba yangu, wote wawili walipokuwa wakizungumuzia jinsi ya kuhubiri vizuri zaidi katika hali hizo.

Mwanzoni mwa mwaka wa 1930, familia yetu ilipatwa na musiba. Mama alikufa, akiwa na miaka 20 tu. Baba aliendelea kutuchunga, dada yangu Doris, mwenye miaka 4 na mimi miaka 2 tu. Hata ikiwa Baba alikuwa amebatizwa hivi karibuni, alifanya maendeleo mazuri ya kiroho.

Mifano Iliyonisaidia Katika Maisha

Mwaka wa 1933, Baba alikutana na dada mumoja mwenye sifa nzuri anayeitwa Lillie Mae Gwendolyn Thomas, na kisha muda kidogo wakaoana. Wote wawili walituwekea mufano muzuri wa kumutumikia Yehova kwa uaminifu.

Mwaka wa 1938, makutaniko yaliombwa kuunga mukono azimio lililoonyesha kwamba wazee wanapaswa kutiwa na makao makuu, Brooklyn, New York, kuliko kufanya vote katika kutaniko. Ndugu fulani huko Chattanooga walisita kukubali badiliko hilo, lakini Baba alisema waziwazi kwamba anapaswa kuunga mukono mabadiliko hayo ya kitengenezo. Mufano wake wa ushikamanifu, na jinsi mama alivyomutegemeza kwa moyo wote, vimenisaidia mupaka leo.

Ubatizo na Utumishi wa Wakati Wote

Mwaka wa 1940, kutaniko letu lililipia gari ili kusafiri kwenye mukusanyiko uliofanywa huko Detroit, Michigan. Ni wachache tu katika gari letu ndio waliobatizwa huko. Wengine walijiuliza kwa nini sikubatizwa, kwa kuwa nilianza kuhubiri nilipokuwa na miaka mitano na nilikuwa na bidii katika mahubiri.

Waliponiuliza niliwajibu, “Sijaelewa vizuri kabisa maana ya ubatizo.” Baba alisikia yale niliyosema na akashangaa. Kuanzia wakati huo, alijikaza sana ili kunisaidia nielewe maana ya ubatizo. Miezi 4 baadaye, tarehe 1 mwezi wa 10, 1940 nilibatizwa katika ziwa ndogo inje ya Chattanooga, ilikuwa siku yenye baridi sana.

Nilipokuwa na miaka 14, nilianza kufanya upainia wakati wa mapumuziko ya masomo. Nilihubiri katika miji midogo huko Tennessee na katika miji mikubwa karibu na Georgia. Nilikuwa nikiamuka asubuhi sana, kutia chakula katika mukoba, na kwenda kuchukua gari ao treni pa saa 12 ya asubuhi ili kwenda katika eneo, na kurudi saa 12 ya mangaribi. Mara nyingi chakula kilimalizika mbele ya wakati. Ijapokuwa nilikuwa na feza, singeweza kuingia katika duka ili kununua chakula kwa kuwa nilikuwa mutu mweusi. Wakati fulani nilijaribu ili ninunue kreme ya baridi, lakini nilifukuzwa. Kwa fazili, mwanamuke mumoja muzungu aliniletea kreme moja.

Nilipoanza masomo ya juu, vyama vya kugombania haki ya watu viliongezeka upande wa Kusini. Vyama kama vile NAACP (Chama cha Kitaifa kwa Ajili ya Maendeleo ya Weusi) kilitia wanafunzi moyo wafanye maandamano ili kupigania haki yao. Tuliombwa tuwe washiriki wa vyama hivyo. Masomo mengi ya weusi, kutia ndani masomo yetu, yalikusudia wanafunzi wote wawe washiriki wa vyama hivyo. Walinikaza “nitegemeze watu wa rangi yangu.” Lakini nilikataa, nilikuwa nikiwaelezea kwamba Mungu hana ubaguzi na hapendelee watu wa rangi fulani na kuchukia wa rangi nyingine. Kwa hiyo ninamutegemea Mungu kwa kuwa ni yeye atamaliza hali za ukosefu wa haki.—Yoh. 17:14; Mdo. 10:34, 35.

Muda mufupi kisha kumaliza masomo, nilihamia katika muji wa New York. Mbele ya kufika huko, nilibaki kwanza Philadelphia, Pennsylvania, ili kuonana na marafiki niliokutana nao kwenye mukusanyiko wakati uliopita. Mahali hapo nilihuzuria mikutano katika kutaniko lililokuwa la kwanza kuchanganya wazungu na weusi. Wakati wa ziara yake katika kutaniko hilo, mwangalizi mwenye kusafiri alinichukua pembeni na kunielezea kwamba nitakuwa na mugawo kwenye mukutano unaofuata. Hivyo nikaamua kubaki hapo.

Kati ya marafiki niliokutana nao katika Philadelphia kulikuwa dada mumoja kijana anayeitwa Geraldine White—baadaye nilimwita Gerri. Alikuwa na ujuzi mwingi wa Biblia na alikuwa na ufundi wa kuzungumuza na watu katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba. Jambo lililonipendeza zaidi ni kwamba alikuwa pia na muradi wa kuwa painia. Tulioana tarehe 23 mwezi wa 3, 1949.

Tunaalikwa kwenye Masomo ya Gileadi

Kusudi letu lilikuwa kuhuzuria Masomo ya Gileadi na kutumikia kama misionari katika inchi ya kigeni. Tulifurahi kubadili hali zetu ili tustahili kuhuzuria masomo hayo. Kisha muda mufupi, tulilazimika kuhamia Lawnside, New Jersey; kisha tukahamia Chester, Pennsylvania; na mwishowe katika Atlantic City, New Jersey. Huko Atlantic City, tulitimiza matakwa ya kuhuzuria Masomo ya Gileadi, kwa kuwa tulikuwa tumeoana kumepita sasa miaka miwili. Lakini tulipojaza ombi tuliambiwa tungojee kwanza. Kwa nini?

Mwanzoni mwa miaka ya 1950, vijana wengi wanaume waliandikishwa katika jeshi ili kwenda kupigana vita huko Korea. Biro ya kuandikisha vijana huko Philadelphia iliwachukia Mashahidi kwa sababu ya musimamo wao wa kutounga mukono upande wowote. Mwishowe, mwamuzi alinijulisha kwamba shirika la upelelezi la Amerika (FBI) linakubali musimamo wangu. Kwa hiyo, tarehe 11 mwezi wa 1, 1952, Mahakama ilinitolea kikaratasi 4-D ili kuniruhusu niendelee kutumika kama mweneza-injili.

Mwezi wa 8 mwaka huo, mimi na Gerri tulipokea mwaliko wa kuhuzuria darasa la 20 la Masomo ya Gileadi iliyoanza mwezi wa 9. Wakati wa masomo, tulitazamia kutumwa katika inchi ya kigeni. Dada yangu Doris, alitumwa Brazili kisha kuhuzuria darasa la 13 la Gileadi. Gerri na mimi tulishangaa kupata mugawo katika muzunguko—tulitembelea makutaniko fulani ya weusi kusini mwa muji wa Alabama! Hilo lilituvunja moyo kwa kiasi fulani, kwa kuwa tulipenda mugawo wa inchi ya kigeni.

Kutaniko la kwanza tulilotembelea lilikuwa katika Huntsville. Tulipofika, tulienda kwa dada mumoja, mahali tulipopangishwa. Tulipokuwa tukishusha vitu vyetu, tulimusikia akisema kwenye telefone: “Watoto wamefika.” Kila mumoja wetu alikuwa na miaka 24, na tulionekana vijana sana. Muda wote tuliopitisha katika muzunguuko huo, tuliitwa kwa jina hilo la kutania.

Mara nyingi upande wa kusini uliitwa Eneo la Biblia kwa kuwa watu wengi huko waliheshimu sana Biblia. Kwa hiyo tulikuwa tukianzisha mazungumuzo kwa kutumia mambo haya matatu:

(1) Maelezo mafupi kuhusu hali za ulimwengu.

(2) Suluhisho ambalo Biblia inatoa.

(3) Yale ambayo Biblia inatuomba tufanye.

Kisha tulimutolea mutu kichapo fulani cha kumusaidia kujifunza Biblia. Kwa kuwa njia hiyo ya kuhubiri ilikuwa na matokeo mazuri, mwaka wa 1953 nilipewa hotuba kwenye mukusanyiko wa New World Society huko New York. Katika hotuba hiyo nilionyesha mambo hayo matatu.

Katika mwaka huo, nilitiwa kuwa mwangalizi wa wilaya ili kutumikia mizunguko ya weusi upande wa Kusini. Eneo letu lilianzia Virginia mupaka Florida na mbali upande wa mangaribi, Alabama na Tennessee. Waangalizi wenye kusafiri wanapaswa kujiambatanisha na hali. Kwa mufano, mara nyingi tuliishi katika nyumba ambazo hazikuwa na maji ndani, wala choo wala mahali pa kuogea. Kwa kuoga tulitumia robinet iliyokuwa nyuma ya mafiga kwa kuwa hiyo ndiyo ilikuwa sehemu ya nyumba iliyokuwa na joto!

Tatizo la Ubaguzi wa Rangi

Kutumikia sehemu ya Kusini kuliomba kujitayarisha na kuwa werevu ili upate kitu ulichohitaji. Weusi hawakuruhusiwa kupeleka mavazi yao kwenye nyumba za kusafisha mavazi kwa mashine. Gerri alipopeleka mavazi huko, alisema kwamba mavazi ni ya “Madame Thompson.” Wengi walifikiri kwamba Gerri alikuwa mutu wa kazi na kwamba “Madame Thompson” ndiye alikuwa mama wa nyumba. Wakati waangalizi wa wilaya walikuwa wakionyesha watu filme La Société du Monde Nouveau en action, niliita maduka kupitia telefone na kusema waniwekee televizyo kubwa ya “Bwana Thompson.” Kisha, nilienda kwenye duka na kuchukua televizyo hiyo. Tulikuwa watu wenye adabu na hivyo kwa ukawaida tulihubiri kwa amani.

Kulikuwa ubaguzi wa aina nyingine, kati ya watu wa Kusini na wa Kaskazini. Wakati fulani gazeti moja lilisema kwamba James A. Thompson, Jr., wa Watchtower Bible and Tract Society ya New York atatoa hotuba kwenye mukusanyiko. Watu fulani waliposoma habari hiyo walifikiri kwamba nilitoka New York, na makubaliano yetu ya kutumia jumba la masomo yakavunjwa. Kwa hiyo nikaenda kuonana na wasimamizi wa masomo hayo na kuwaeleza kwamba nilisomea Chattanooga. Kwa hivyo, tukaruhusiwa kufanya mukusanyiko wetu.

Ubaguzi wa rangi ulichacha katikati ya miaka ya 1950; wakati fulani kulikuwa mauaji. Katika 1954, Mashahidi fulani walikasirika kwa sababu wasemaji weusi hawakupewa hotuba kwenye mikusanyiko fulani ya wilaya. Tulitia ndugu zetu weusi moyo kuwa wavumilivu. Mukusanyiko uliofuata nilikuwa na hotuba. Baadaye, ndugu wengi weusi wa Kusini walipewa hotuba kwenye mikusanyiko.

Baada ya muda, jeuri iliyotokana na ubaguzi katika sehemu ya Kusini ilipunguka, na polepole makutaniko yakawa na washiriki wazungu na weusi. Hilo liliomba wahubiri fulani wabadilishwe makutaniko, pia iliomba kubadili maeneo ya makutaniko, kubadili madaraka ya ndugu wanaosimamia kazi. Watu fulani, weusi na wazungu, hawakufurahia mupango huo mupya. Hata hivyo, wengi hawakuwa na ubaguzi, kama Baba yetu wa mbinguni. Kwa kweli, wengi walikuwa marafiki wa karibu ijapokuwa walikuwa wa rangi tofauti. Familia yetu ilijionea jambo hilo katika miaka ya 1930 na 1940 nilipokuwa mutoto.

Mugawo Mupya

Katika mwezi wa 1, 1969, mimi na Gerri tuliombwa kwenda Guyana, Amerika ya Kusini, na tulikubali kwa furaha. Tulienda kwanza Brooklyn, New York, ili kupata mazoezi ya kusimamia kazi ya kuhubiri katika Guyana. Tulifika huko mwezi wa 7, 1969. Kisha miaka 16 katika kazi ya kusafiri, haikuwa vyepesi kufanya kazi ya kubaki nafasi moja, ilikuwa ni mabadiliko makubwa. Gerri alipitisha wakati mwingi katika mahubiri akiwa misionari, nami nilitumika kwenye biro ya tawi.

Nilifanya kila kazi, kutengeneza bustani, kushugulika na vichapo kwa ajili ya makutaniko 28 na pia kuandikiana na makao makuu Brooklyn. Nilitumika saa 14 ao 15 kila siku. Mimi na Gerri tulikuwa na kazi ngumu, lakini tulifurahia mugawo wetu. Tulipofika Guyana, hesabu ya wahubiri ilikuwa 950; leo kuna wahubiri zaidi ya 2,500.

Ijapokuwa tulipendezwa na hali ya hewa, matunda na mboga ya majani ya huko, jambo lilitotufurahisha zaidi ni kuona kwamba watu wanyenyekevu walio na hamu ya ukweli wa Biblia wanajifunza kuhusu Ufalme wa Mungu. Mara nyingi Gerri alikuwa akiongoza mafunzo ya Biblia 20 kwa juma, na wengi tuliojifunza nao waliendelea mupaka kubatizwa. Wengine wao wakawa mapainia, wazee wa makutaniko, na hata misionari kama sisi.

Matatizo ya Afya

Mwaka wa 1983, wazazi wangu katika Amerika walihitaji musaada. Doris, Gerri, na mimi tulikutana ili kuzungumuzia jambo hilo. Doris, ambaye alikuwa ametumikia kwa muda wa miaka 35 kama misionari huko Brazili, aliamua kurudi ili kuchunga wazazi, kuliko sisi wamisionari wawili kurudi, ndivyo alivyofikiri. Tangu kifo cha wazazi, Doris amebaki Chattanooga na anatumikia akiwa painia wa pekee.

Mwaka wa 1995, nilipatwa na magonjwa ya kansa ya prostate, kwa hiyo nililazimika kurudi Amerika. Tulikaa Goldsboro, Carolina ya Kaskazini, kwa kuwa mahali hapo palikuwa karibu na familia yangu katika Tennessee na familia ya Gerri katika Pennsylvania. Sasa ninajisikia vizuri kidogo, na sisi ni mapainia wa pekee wasiotimiza saa za mapainia kwa sababu ya kuwa wazaifu kimwili, katika kutaniko la Goldsboro.

Ninapofikiri kuhusu miaka zaidi ya 65 katika utumishi wa wakati wote, ninamushukuru kabisa Yehova kwa kuwa ametubariki mimi na Gerri kwa kufanya mabadiliko ili kumutumikia. Maneno haya ya Daudi ni ya kweli kabisa: ‘Kwa mutu mushikamanifu, [Yehova] atatenda kwa ushikamanifu’!—2 Sam. 22:26.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Baba yangu na Ndugu Nichols waliniachia mufano muzuri

[Picha katika ukurasa wa 4]

Mwaka wa 1952, mimi na Gerri, tayari kwa ajili ya Gileadi

[Picha katika ukurasa wa 5]

Kisha Gileadi, mugawo wetu ulikuwa muzunguko katika sehemu ya Kusini

[Picha katika ukurasa wa 6]

Mwaka wa 1966, waangalizi wenye kusafiri na wake zao tayari kuhuzuria mukusanyiko wa wilaya wa wazungu na weusi

[Picha katika ukurasa wa 7]

Kazi ya umisionari katika Guyana ilikuwa yenye kufurahisha